JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

Ukosefu wa ajira ,ajira ,ajira na kunyima haki,uonevu ni chanzo cha kuibuka kwa vikundi vya kigaidi duniani,Note my words
Ni kweli ajira ndiyo huchochea vijana kuwa occupied na mambo ya maendeleo na kutojihusisha na mambo ya uvunjifu wa sheria, lakini kitendo walichokifanya hao vijana ni cha hatari sana, huenda wangeenda mbali na hata kufanya mapinduzi ya kumpindua raisi.
 
Dhana ya uasi ni pana sana na ipo kimkakati sana.
Tushukuru Mungu kuwa amani nchini imetamalaki na hakuna wala dalili za uasi nchini kwetu.

Siyo kwamba madhara hayapo kwenye uamuzi huu, yapo hata kama hayaonekani moja kwa moja.
 
Vijana hao, hawajawahi kulipwa chochote,walikuwa wanapewa chakula na malazi tu. Wengi ni kidato cha sita kutoka mikoa ya kanda ya ziwa, wameishi na kufanya kazi ikulu ya Dodoma kwà zaidi ya miaka miwili,leo wanafukuzwa bila hata kupewa nauli ya kwenda makwao
Inasikitisha na kuumiza sana Mkuu. Jasho lao halitokwenda bure. Mungu anawaona waliowadhulumu Vijana wale. Eti fanyeni kazi kwa bidii kisha Ujenzi wa Ikulu utakapomalizika basi mtaajiriwa kwenye Vikosi mbali mbali vya Majeshi yetu. Leo wamekuwa Waasi?? Au kwakuwa kazi yao imeisha??
 
Vijana hao, hawajawahi kulipwa chochote,walikuwa wanapewa chakula na malazi tu. Wengi ni kidato cha sita kutoka mikoa ya kanda ya ziwa, wameishi na kufanya kazi ikulu ya Dodoma kwà zaidi ya miaka miwili,leo wanafukuzwa bila hata kupewa nauli ya kwenda makwao
Kwa tetezi nasikia wamefanya kazi zaidi ya miaka 3+, wamejenga Chamwino, Ukuta wa Mererani, majengo ya magereza Ukonga, ndio walio ratibu wizi wa kura na usimamizi wa uchaguzi 2020 na n.k, pia waliahidiwa baada ya kumaliza shughuli zote hizo watapewa ajira jeshini lakini baadae upepo ukageuka na ndio maana walifanya mandamano kwenda Chamwino.

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Kuna mfumo wa maisha ambao kuuvunja ni vigumu! Ni awamu ya marehemu Magufuli watu kutoka familia za "kawaida" waliweza kuajiliwa usalama wa taifa, JWTZ, TRA, BOT na kadhalika.
Enzi zetu zikitangazwa nafasi za Polisi au Jeshi unashangaa watu kutoka Dar es salaam, Moshi, nk wanakuwa wazaliwa wa Kwimba!
"...aliyenacho ataongezewa na asiye nacho hata kile kidogo alichonacho atanyanganywa..."
 
Kwa tetezi nasikia wamefanya kazi zaidi ya miaka 3+, wamejenga Chamwino, Ukuta wa Mererani, majengo ya magereza Ukonga, ndio walio ratibu wizi wa kura na usimamizi wa uchaguzi 2020 na n.k, pia waliahidiwa baada ya kumaliza shughuli zote hizo watapewa ajira jeshini lakini baadae upepo ukageuka na ndio maana walifanya mandamano kwenda Chamwino.

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Kama waliandamana baada ya kugeukwa, hiyo ni sahihi kabisa.

Hata hivyo, ndio wajifunze kuwa CCM sio wema.
 
Hata watumishi wote waliokuwa wameshauriwa ikulu na mwendazake mtasikia wametimuliwa wote wameshauriwa wengine wapya wa dini ile
 
Meko alitoa ahadi ya kuwaajiri Kwa Mhemuko. Kumbe kiuhalisia Jeshi halikuwa limejipanga kuwaajiri..
 
“Tunasikitika kufuta mikataba ya vijana 854 wa JKT kutokana na kufanya vitendo vya uasi.”Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania - Jenerali Venance Mabey
----------

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jen. Venance Mabeyo amesema wamefuta mikataba ya Vijana 854 wa JKT ambao ni miongoni mwa walioahidiwa kupewa ajira kwa kujenga Ikulu, Chamwino na hii ni kutokana na Vijana hao kufanya uasi kwa kugoma na kuandamana kwenda Ikulu.

via @ayotv


Mytake ; Gharama kubwa zilizotumika kuwaandaa hao vijana ili kuja kulitumikia taifa zinarejeshwa vipi?
Ngoja kwanza vuguvugu hili liishe na ionekane hakuna msukumo uliyowapekea wafanye hivyo ila ni kweli kama wanavyodai basi mama Samia anaweza kuwaonea huruma na kuwarudisha kwani toka raisi aingie madarakani kuna tetesi za kuwepo baadhi ya watu wasiyo waaminifu kutaka kuleta fujo, na nadhani ilimpelekea hata mama Samia mwenyewe kusema na kunukuliwa kuwa "huyu aliyesimama hapa ndiye raisi". Hivyo hivi vitu tusivione ni kama kuwanyanyasa hao vijana lakini nidhamu na utii wa sheria lazima ufuatwe.
 
Siwafundishi kazi, bali naamini taalamu yenu inawataka mfanye hivyo na si kuishia kupata taarifa za upande mmoja tu kwa maana ya maelezo ya viongozi wa Jeshi na serikali tu bila kuwahoji Vijana waliofukuzwa.

Wateendeni haki hawa vijana ili umma uweze kuwahukumu kwa haki maana teyari wameshaitwa waasi(sifa mbaya sana katika Jamii na kila watakokwenda).

Mazingira ya kufukuzwa hawa vijana, kwa mtazamo wangu, hayana tofauti na mazingira ya wale vijana waliofukuzwa UDOM na hayati Magufuli mwaka 2017.

Yangu ni hayo tu.
[emoji848]hivi wakisharudi Nani atawaajiri wakati tayari ni waasi?
 
Kwa kichapo walichopata hawatakuja kusahau, nasikia walikomaa wanataka kwenda msata kuhenya hapo washamgomea Mbuge wanataka onana na Samia tu, zikaletwa karandinga haya pandeni mwende msata kufika msata MP Kama wote wanawasubiria, wakapata kipigo heavy na kusafirishwa makwao.
Vijana wameonesha ushujaa wa Hali ya juu Sana, tutegemee kuona mabadiliko siku zijazo kuhusu ili swala, sela Mbovu za mwenda zake zimeharibu vijana, zimetukosesha nguvu za kiume.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa tetezi nasikia wamefanya kazi zaidi ya miaka 3+, wamejenga Chamwino, Ukuta wa Mererani, majengo ya magereza Ukonga, ndio walio ratibu wizi wa kura na usimamizi wa uchaguzi 2020 na n.k, pia waliahidiwa baada ya kumaliza shughuli zote hizo watapewa ajira jeshini lakini baadae upepo ukageuka na ndio maana walifanya mandamano kwenda Chamwino.

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Ukifuatilia vizuri maelezo ya mabeyo,anasema Kama wangekuwa ni askari wangefikishwa mahakamani,swali ni je, Kama sio askari wanaitwaje waasi?
Kama sio askari wamezuiliwaje kuandamana?
 
Back
Top Bottom