Pre GE2025 John Heche: Nitamuunga Mkono Tundu Lissu, na nitagombea Umakamu Mwenyekiti CHADEMA

Pre GE2025 John Heche: Nitamuunga Mkono Tundu Lissu, na nitagombea Umakamu Mwenyekiti CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Natamani
1. Lissu - Mwenyekiti
2.Heche - M/mwenyekiti
3. Lema - Katibu mkuu
Thubutuuu!! Chadema ni SACCOS YA KICHAGA, hatuwezi kukubali saccoss yetu itekwe na wanyaturu!
 
  • Mshangao
Reactions: K11
Hapa ccm utawakuta wanaongea peke yao barabarani ,dadeki
Kwani hao siyo viongozi wa Chadema kwa Sasa? LISSU makamu mwenyekiti, Lema alikuwa mbunge na akawa mwenyekiti wa kanda, hali kadhalika Heche.
Waliifanya nini CCM zaidi ya wao kukashfiana wakigombea madaraka?
 
Kwa maelezo haya inaonyesha unaamini huu uchaguzi utaigawa Chadema ila tambua lengo la uchaguzi sio hilo ila hilo linaweza kutokea kulingana na uchaguzi utakavyoendeshwa.

Kiufupi hali kama hii inasaidia kukuza demokrasia ndani ya chama hivyo haipaswi kuogopwa.
Lengo halikuwa hilo lakini jinsi kampeni zilivyofanywa zimeacha vidonda vingi. Unadhani, Mbowe akishindwa, yeye na wafuasi wake watakuwa na moyo ule ule wa kukitumikia chama chao baada ya Mbowe alivyochafuliwa? Au Lissu, akishindwa, wafuasi wake hawataamini kuwa aliibiwa ushindi hata kama utaendeshwa kwa uwazi 100% na kusimamiwa na malaika? Mimi ndio maana hizi lugha za " kama uchaguzi utakuwa wa haki na uwazi " naona ni hatari sana maana zinapanda mbegu ya doubt. Huu ni uchaguzi wa CDM lakini CCM wameshiriki kikamilifu bila kificho.

Bahati mbaya CDM imeingia na kunasa katika mtego waliowekewa. Kwenye hili namlaumu Lissu. Inaelekea Heche anaamini chanzo ni Wenje. Sijui kwa nini anaamini hivo. Labda ni kwa yeye kutia nia ya kugombea umakamu uenyekiti.

Amandla...
 
Chama kinatakiwa kuwa na resources zake na si kutegemea resources za mtu binafsi.
Resources zipi? Vyama vya siasa si vizuri katika kufanya biashara. Vinafanikiwa pale tu vikiwa vyama dola. CCM ilikuwa na Sukita ikafa. Viwanja walivyopata bure ni mzigo tu. Bila support ya serikali isingekuwa hapa ilipo.

Vyama vyote vya siasa vinategemea sana michango. Mchango wa Musk, familia ya Koff katika chaguzi za Marekani uko wazi.Katika demokrasia taasisi na mashirika yanachangia vyama ambavyo wanaona vitawasaidia.

Kwetu watu wengi wanasita kuchangia vyama vya upinzani kwa kiasi kinachohitajika kwa uwazi. Watu wanachangia matukio lakini si uendeshaji.

Hapa ndipo uwezo wa Mbowe wa fund raising ulionekana. Naamini kuna matajiri wenzake wengi walikuwa wanamchangia kwa sababu ya mahusiano yao binafsi. Sidhani kama watafanya hivyo hivyo kwa mtu ambae wakikosana tu atawaanika hadharani.

Amandla...
 
Nilitarajia Mbowe angemuachia chama Heche. Lisu sidhani kama ana qualities za kiuongozi. Ni bulldozer kama Magufuli na akipata uenyekiti atawaburuza CHADEMA hadi wakome ubishi.
 
Heche anapoteza muda. Mbowe ni chaguo la wapiga kura wa CHADEMA hakuna namna anaweza kushindwa na Lissu ambaye ni adui wa demokrasia na kirusi ndani ya chama rafiki CHADEMA. Sisi wanaCCM tunamuunga mkono Mbowe.


Shetani alimwambia Yesu ,ukinisujudia nitakupa pesa zote za DP World na utashinda uchaguzi uwe juu ya miliki na fahari zote za Dunia.

Yaani shetani alitaka apigiwe magoti na Mwana wa Mungu ili ampe mambo yote yenye kuleta anasa na fahari za dunia. Yesu akakataa kumsujudia shetani.

Hata Yuda alihongwa pesa ili amsaliti Yesu .

Mbowe na CCM watagawa pesa nyingine.
 
Wakuu mmesikia huko? John Heche rasmi ametangaza kumuunga mkono Tundu Lissu na atagombea Umakamu Mwenyekiti wa Chama.

Heche ameongeza "Mimi Mbowe kwangu ni Baba wa Kisiasa, amenilea na hamheshimu sana. Tunakwenda kwenye uchaguzi na tutakushinda katika uchaguzi huu. Mimi namuunga mkono Tundu Lissu na nimeamua kuchukua Fomu ili nikamsaidie Mwenyekiti kujenga Chama chetu. CHADEMA ni tegemeo la wananchi. Kwa rafiki yangu Wenje, tumefika hapa kwa sababu yako."
View attachment 3193009
Pelekeni Pampasi Black house huko mtu atahar....................shaaaaaaaa
 
Heche anapoteza muda. Mbowe ni chaguo la wapiga kura wa CHADEMA hakuna namna anaweza kushindwa na Lissu ambaye ni adui wa demokrasia na kirusi ndani ya chama rafiki CHADEMA. Sisi wanaCCM tunamuunga mkono Mbowe.
Kama mnamuunga mkono Mbowe hadharani maana yake mnataka wanaCDM wasimpe kura, maana yake mtu wenu ni Lissu.
 
Resources zipi? Vyama vya siasa si vizuri katika kufanya biashara. Vinafanikiwa pale tu vikiwa vyama dola. CCM ilikuwa na Sukita ikafa. Viwanja walivyopata bure ni mzigo tu. Bila support ya serikali isingekuwa hapa ilipo.

Vyama vyote vya siasa vinategemea sana michango. Mchango wa Musk, familia ya Koff katika chaguzi za Marekani uko wazi.Katika demokrasia taasisi na mashirika yanachangia vyama ambavyo wanaona vitawasaidia.

Kwetu watu wengi wanasita kuchangia vyama vya upinzani kwa kiasi kinachohitajika kwa uwazi. Watu wanachangia matukio lakini si uendeshaji.

Hapa ndipo uwezo wa Mbowe wa fund raising ulionekana. Naamini kuna matajiri wenzake wengi walikuwa wanamchangia kwa sababu ya mahusiano yao binafsi. Sidhani kama watafanya hivyo hivyo kwa mtu ambae wakikosana tu atawaanika hadharani.

Amandla...
Kama anakopata hela Mbowe ni siri au hakufahamiki hiyo ni hatari kuliko kutokuwa na pesa.
 
Wakuu mmesikia huko? John Heche rasmi ametangaza kumuunga mkono Tundu Lissu na atagombea Umakamu Mwenyekiti wa Chama.

Heche ameongeza "Mimi Mbowe kwangu ni Baba wa Kisiasa, amenilea na hamheshimu sana. Tunakwenda kwenye uchaguzi na tutakushinda katika uchaguzi huu. Mimi namuunga mkono Tundu Lissu na nimeamua kuchukua Fomu ili nikamsaidie Mwenyekiti kujenga Chama chetu. CHADEMA ni tegemeo la wananchi. Kwa rafiki yangu Wenje, tumefika hapa kwa sababu yako."
View attachment 3193009
Dj lete maneno

Siasa zimepata watu sahihi sasa
 
Kamanda mbona kama unamtakia heri Kamanda John Heche kinyonge! Nilikuambia last time CHADEMA imegawanyika sehemu mbili kwenye huu uchaguzi, na ulinibishia. Ila ukweli ndiyo huu sasa.
Ndani ya mioyo, fikra na nafsi za wana Chadema wote wanajua Lissu ndie mleta mabadiliko ya kweli ndani ya Chama.
 
Back
Top Bottom