Uchaguzi 2020 Kamanda Mambosasa: Mbowe na wenzake kushtakiwa kwa makosa ya ugaidi, walipanga kulipua vituo vya mafuta

Aliyeshikiliwa anayezungumziwa katika uzi huu ni nani?
Hao si tumeongea na wamevunja sheria ambazo wao wenyewe walizitunga bungeni? Kama zilikuwa hazifai miaka 15 ya Mbowe alipokuwa Bungeni kwa nini hakuzipinga? Hawa ni wasanii tu.
 
Niwekee sheria inayopiga marufuku kuandaa maandamano bila kibali.

Usiniambie mambo ya video. Sijakuomba video mimi.
Mkuu sina hiyo sheria kwa sasa lakini hiyo sheria ipo hata wewe unaweza kuitafuta. Hizo sheria zipo nchi zote duniani zinatumika.
 
Mkuu sina hiyo sheria kwa sasa lakini hiyo sheria ipo hata wewe unaweza kuitafuta. Hizo sheria zipo nchi zote duniani zinatumika.
Achana naye, leo anajifanya hajui kuna sheria inayotaka aombe kibali polisi masaa 48 kabla. Uzuri kutokujua sheria siyo kinga
 
Mimi nimeshajiandaa na vijana wenzangu kama 70 hivi. Mabali na sisi Coaster kumi na mbili toka maeneo mengine ikiwemo Arusha ziko njiani muda huu
Hivi utani wako huu utaisha lini,
 

Wana intelligence gani hao, upumbavu mtupu
 
Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam ACP Lazaro Mambosasa amesema wanawashikilia watu kadhaa wakiwemo viongozi watatu wa CHADEMA...
Ni tuhuma au ni kweli? wanawashikilia kwa tuhuma au wanawashikilia kwamba ni kweli wana njama za kupanga hayo yasemwayo... hiyo kesi ya Mambo sasa imeharibika tayari hata kabla haijafika mahakamani ya nini kukimbilia kwemye media? hii huitwa trial by media na wataachiwa huru tu.. usumbufu mwingine usio wa maana
 
Wangewaacha tu makamanda, unaweza kukuta hata ambao wangeandamana wasingefika 10, hapa wanakuza mambo tu.
Mbona Lisdu alivyorudi waliandamana wakachoka wakarudi makwao ?
 
Nimecheka sana. Lakini mfano wako unamaana kazi ya Polisi si kuzuia kosa lisitendeke bali wasubiri kosa litendeke ndio waingie kazini. Ni sawa na kusubiri watu wajenge kando ya mto ndio uende kubomoa nyumba zao, badala yaa kuweka ulinzi kabla ili waharifu wasifanye huo uharifu. X😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…