Kijana kamkimbia mchumba wake alietaka kumuoa baada ya kujua kwao kuna walemavu ni sawa?

Kijana kamkimbia mchumba wake alietaka kumuoa baada ya kujua kwao kuna walemavu ni sawa?

Hujafa Hujaumbika .....huku kwetu Kuna maza jirani yake kulikuwa na Albino ......so yule Kwa yule maza wale watoto albino wakija pale kwake kucheza ....

Wakila chakula ...vyombo alikuwa anavitenga + kutupa

At the end of the day....naye kapata mimba ....kuzaa mtoto ni albino

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Bado ana utoto huyo
Anajua anapoenda kuoa sasa
Au yeye anaijua kesho yake
Haya mambo hutokea ghafla sana bila kupanga

Asije jikuta yeye katika familia yao ndio anakuwa wa kwanza kupata ulemavu.

Kumcheka au kumdharau mlemavu ni jambo baya sana na malipo yake huwa ni ya haraka sana.

Ukiwa mzima shukuru.
 
Binafsi mimi naona kijana kakosea, hakuwa sahihi, mkasa huu hapa nawapeni.

Kuna kijana mdogo wa kiume miaka 26 tupo nae kazini alikuwa kwenye uchumba na binti wa miaka 22, wote ni wasomi binti kamaliza degree mwaka jana.

Kijana alikuwa tayari kabisa mwezu huu kwenda kujitambulisha nyumbani kwa binti ili amuoe.

Wiki 3 ziliyopita kijana alipata safari ya kikazi kwenye mkoa anakotokea huyo binti, alikaa huko kama wiki hivi

Huko alipofika na kuamua kuchagua malazi ni mitaa karibu na nyumbani kwa huyo binti, katika kujichanganya na wakazi wa hapo akitoka kazini aliulizia kama wanamfaham mzee wa binti akaongezea na maelezo ya ziada, wakamwambia ni mtaa huo huo tu na wanaijua familia ya hapo.

Kijana ikabidi aanza kukamua intelejensia, akagundua kuwa pale nyumbani kwa binti kuna wanafamilia wawili wana matatizo ya kutosikia vuzuri na kuna mwengine huwa yupo ndani tu ana matatizo ya akili tangu mdogo.

kuna wawili wengine hawana shida wamesoma na wana kazi na biashara zao.

Kijana akamkimbia mwenzake na kumuweka wazi kwamba anampenda lakini anachukua tahadhari hawezi kurisk kumuoa sababu ndoa bila watoto ni ngumu na anahofia alichokigundua kwenye familia anayotokea huyo binti, aloimwambia kwamba mtu yeyote anaweza kupata mtoto mlemavu lakini anahofia kwamba uwezekano wa kupata mtoto mlemavu utaongezeka zaidi wakipata mtoto kwa kuhofia binti kabeba genes / genetics zinazoweza kuleta mtoto mwenye ulemavu (alimficha sababu ya ziada kwamba anahofia kuna mambo ya mila / ushirikina yanayoweza kurithika kwa watoto),

Alimwambia binti wanaweza kuwa na mahusiano mengine ila si kwenye kupata watoto, Binti hakumwelewa kabisa ikawa ndio mwisho hapo.

Je, ni sawa ?
Hajafanya jambo sahihi, siku zote ulemavu unaweza kusababishwa na changamoto zingine za kiafya hasa wakati wa kujifungua

Kuna baadhi ya huduma ukichelewa kuzipata kipindi cha ujauzito au wakati mzazi anajifungua inaweza kupelekea mtoto kupata athari katika afya yake au hata kupoteza maisha

Hivyo hii sio kigezo sana, ila kwenye imani ya kishirikina unapaswa uwe na imani na uamini, hupaswi kufunga ndoa na mtu asieamini na mshirikishe Mungu naye atavunja hizo imani za kishirikina

Mwisho, nimeshuhudia baadhi ya walemavu wa kuzaliwa wakipata watoto wazima wa afya na nimeona pia watu ambao hata familia zao hata ukoo hamna mlemavu hata mmoja pande zote mbili, lakini isivyo bahati wakazaa mlemavu na kuishia kukisia na kupiga ramli inawezekana kwa mababu na mababu walikuwepo walemavu kitu ambacho ni senseless


lolote linaweza kutokea na Mungu ndio muweza wa yote, mtangulize daima katika kila kitu.
 
Pole sana mkuu,

Hapa changamoto kubwa huwa ni pesa, Yaani pesa isipokuwepo mzazi anaweza fanya maamuzi magumu sana pesa ipatikane
Hakika. Na inapokua haipatikan hali huwa hailezek vile una feel.
Mtoto anateseka ..matibabu huwez mudu na we kila ukimuona ule uchungu kwakwel no one can tell ukaelewa
 
Haya mambo hutokea ghafla sana bila kupanga

Asije jikuta yeye katika familia yao ndio anakuwa wa kwanza kupata ulemavu.

Kumcheka au kumdharau mlemavu ni jambo baya sana na malipo yake huwa ni ya haraka sana.

Ukiwa mzima shukuru.
Kabisa
Niliwahi simuliwa story
Jamaa alimkataa mtoto albino
Matokeo yake yeye akaanza kupata ule ugonjwa vitiligo ukubwani ukasambaa mwili mzima
 
Mbona ni wewe mkuu ..
Acha unyanyapaa.. Oa.
 
Pole mkuu, mama yake anaongea na kusikia vizuri?
Ila kuna familia nyingine jamani sikieni tu. Niliwahi kuwa karibu na familia moja ya mke na mumuwe ambao ni wasomi wazuri tu na wana kazi nzuri. Shida ilikuwa kwenye watoto. Walikuwa na watoto wanne na wote walikuwa na maumbo kama mazombi hivi. Yaani wakati wa kuzaliwa, wanazaliwa vizuri kabisa, wakiwa watoto wazuri mno. Na wanakua vizuri kabisa kuanzia kuzaliwa mpaka miaka minne. Wakifikisha miaka minne wanaanza kupata mabadiliko. Maumbo yanaanza kubadilika, miguu inajipinda na maumbo yao yanageuka wanakuwa kama ndondocha au mazombi. Pia akili nazo zinabadilika wanakuwa kama mazuzu. Yaani walikuwa wanatia huruma kweli kweli watoto wazuri wanne wote wakageuka kuwa mazombi. Hakuna maombi ambayo hakupitia na hospital pia. Hospital alimbiwa wana kasoro kwenye gene zao na jambo walilorithi. Nikajakusikia baadae walijafariki wote.
 
Kabisa
Niliwahi simuliwa story
Jamaa alimkataa mtoto albino
Matokeo yake yeye akaanza kupata ule ugonjwa vitiligo ukubwani ukasambaa mwili mzima
Hivi inatokeaje mtu akatae mtoto wake? Ninavyopenda watoto mimi... da.
 
Kosa alilolifanya Ni kumwambia( kuropoka) kwa Nini anaachana naye, angetafuta tu njia ya kuachana naye tu kiaina kwa ustaarabu bila binti kujua, Hata wazee wa zamani walikuwa wanafuatilia familia ya mtu mnaetaka Kuoana nae, Kama familia Ina changamoto walibadili maamuzi na ilisaidia Sana kuepusha changamoto mbalimbali.
Umenikumbusha baba yangu alikua anasisitiza ukipata mchumba umwambie mapema achunguze ukoo wake maana kuna magonjwa ya kurithi, tabia za kuhama vizazi, laana za ukoo na mambo muhimu kuchunguza kabla ya ndoa.
 
Ila kuna familia nyingine jamani sikieni tu. Niliwahi kuwa karibu na familia moja ya mke na mumuwe ambao ni wasomi wazuri tu na wana kazi nzuri. Shida ilikuwa kwenye watoto. Walikuwa na watoto wanne na wote walikuwa na maumbo kama mazombi hivi. Yaani wakati wa kuzaliwa, wanazaliwa vizuri kabisa, wakiwa watoto wazuri mno. Na wanakua vizuri kabisa kuanzia kuzaliwa mpaka miaka minne. Wakifikisha miaka minne wanaanza kupata mabadiliko. Maumbo yanaanza kubadilika, miguu inajipinda na maumbo yao yanageuka wanakuwa kama ndondocha au mazombi. Pia akili nazo zinabadilika wanakuwa kama mazuzu. Yaani walikuwa wanatia huruma kweli kweli watoto wazuri wanne wote wakageuka kuwa mazombi. Hakuna maombi ambayo hakupitia na hospital pia. Hospital alimbiwa wana kasoro kwenye gene zao na jambo walilorithi. Nikajakusikia baadae walijafariki wote.
Jamani, hadi huruma.
Kwa nchi za wenzetu hizi shida wanazigundua tangu mtoto akiwa tumboni. Wanafanya genetic testing kama kuna tatizo wewe mwenyewe utaamua uendeleze ujauzito au lah.

Rafiki yangu yupo Marekani huko kaolewa. Akawa mjamzito akafanyiwa hivo vipimo akaambiwa mtoto wake ana shida kuna mawili mimba itaharibika au baada ya kujifungua mtoto hatamaliza masaa 24. Akawabishia akaamu kuendeleza ujauzito japo walikuwa wanamsumbua kila mara kumshauri atoe.

Kweli alibeba ile mimba full term akajifungua na kweli yule mtoto hakumaliza hata masaa manne akafariki. Aliumia sana.
 
Kwa useful was story hii inaonyesha dhahiri muhusika ni wewe. But naona ni sahihi tunashauriwa kufanya ata vipimo ili kupunguza chances za magonjwa ya kurithi pia kama circle cell, magonjwa ya akili n.k. Kama unaona dhahiri kuna hatari hakuna haja ya kujiingiza. Nashangaa mabinti wanaoolewa na Manara wakimuona kabisa ni Albino. Wanaxhojisifia kwamba Manara anazaa watoto weusi, hawajui kwamba Manara anagenes za Ualbino kwa hiyo ata kama yeye hatozaa watoto Albino kizazi kitarudu kwa wajukuu wake na kusabahisha majutto.
 
Hajafanya jambo sahihi, siku zote ulemavu unaweza kusababishwa na changamoto zingine za kiafya hasa wakati wa kujifungua

Kuna baadhi ya huduma ukichelewa kuzipata kipindi cha ujauzito au wakati mzazi anajifungua inaweza kupelekea mtoto kupata athari katika afya yake au hata kupoteza maisha

Hivyo hii sio kigezo sana, ila kwenye imani ya kishirikina unapaswa uwe na imani na uamini, hupaswi kufunga ndoa na mtu asieamini na mshirikishe Mungu naye atavunja hizo imani za kishirikina

Mwisho, nimeshuhudia baadhi ya walemavu wa kuzaliwa wakipata watoto wazima wa afya na nimeona pia watu ambao hata familia zao hata ukoo hamna mlemavu hata mmoja pande zote mbili, lakini isivyo bahati wakazaa mlemavu na kuishia kukisia na kupiga ramli inawezekana kwa mababu na mababu walikuwepo walemavu kitu ambacho ni senseless


lolote linaweza kutokea na Mungu ndio muweza wa yote, mtangulize daima katika kila kitu.
Mkuu ww unaonekana unaelewa sana haya mambo ya magonjwa ya kurithi..Nami naomba niulize hapa. Hivi ukoma(leprosy) nao pia huwa ni ugonjwa wa kurithi, genetically?
 
Back
Top Bottom