Kijana ukihitaji kuoa chagua mke kutoka kwenye familia ya kipato cha kati

Kijana ukihitaji kuoa chagua mke kutoka kwenye familia ya kipato cha kati

Ukiridhika naye oa, yaani ujihakikishie kwenye uzuri, dini, familia yake, na ukwasi wake
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((تُنْكَحُ الْمَرْأَةُ لأَرْبَعٍ: لِمَالِهَا وَلِحَسَبِهَا وَجَمَالِهَا وَلِدِينِهَا. فَاظْفَرْ بِذَاتِ الدِّينِ تَرِبَتْ يَدَاكَ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwanamke huolewa kwa sababu nne; Kwa mali yake, nasaba yake [ukoo], uzuri wake na Dini yake. Tafuta mwenye Dini ubakie salama)).[Al-Bukhaariy na Muslim] (yaani usiharibikiwe katika maisha yako).

Chagua Mwenye Dini kisha mengine utayatazama. Ukipata mwenye Dini kisha ana uzuri unaoupenda sawa na ni muhimu, ana dini kisha ana nasaba nzuri sawa, ana dini kisha ni mkwasi sawa. Ana vyote vinne ni kheri juu ya kheri. Lakini Dini ndio kwanza kisha mengine. Chagua/tafuta mwenye Dini. Tuwe makini kwa hili ndugu yangu. Allah atusaidie.
 
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((تُنْكَحُ الْمَرْأَةُ لأَرْبَعٍ: لِمَالِهَا وَلِحَسَبِهَا وَجَمَالِهَا وَلِدِينِهَا. فَاظْفَرْ بِذَاتِ الدِّينِ تَرِبَتْ يَدَاكَ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwanamke huolewa kwa sababu nne; Kwa mali yake, nasaba yake [ukoo], uzuri wake na Dini yake. Tafuta mwenye Dini ubakie salama)).[Al-Bukhaariy na Muslim] (yaani usiharibikiwe katika maisha yako).

Chagua Mwenye Dini kisha mengine utayatazama. Ukipata mwenye Dini kisha ana uzuri unaoupenda sawa na ni muhimu, ana dini kisha ana nasaba nzuri sawa, ana dini kisha ni mkwasi sawa. Ana vyote vinne ni kheri juu ya kheri. Lakini Dini ndio kwanza kisha mengine. Chagua/tafuta mwenye Dini. Tuwe makini kwa hili ndugu yangu. Allah atusaidie.
Amiin
 
Tatizo ni ile life cycle ndo inatutenga sisi masikini na wale was uchumi wa kati, matokeo yake tunabaki kuoana na Hawa Hawa masikini wenzetu .... Ila asikuambie mtu kuoa/ kuolewa na mtu anaetoka kwenye familia ya kimaskini ni shida Sana ( umasikini ni laana tuikatae kwa nguvu zote)
 
Sheria moja inasema kuwa ikitokea kama unatokea kipato cha chini au cha Kati , jitahidi wakati wakumchagua mtu wako asiwe wa level ya chini endapo ukiwa level ya chini...

Ikitokea upo level ya juu chagua ya chini lengo ni usisumbuke na matokeo ya siku za usoni
 
Faida ya kwanza unapunguza wategemezi watu, watakao kuwa wanakulilia shida zao mara kwa mara
Ni kweli mkuu lakini wewe umegusa upande mmoja na upande wa pili huja gusa, ukio au kuolewa kwenye familia ya masikini ni ngumu sana kufanikiwa maishani ila ukiolewa au kuoa kutoka familia yenye uchumi wakati kuna vitu hauta Kutana navyo mfano, kuwatumia wazazi pesa za kujikimu kila mwezi, kusomesha, kuwajengea wazazi, kwakifupi kuombwa ombwa pesa na ndugu na utakuwa miaka yote ni kutumia pesa zako kuwatoa ndugu kwenye umasikini na kitu hicho ni kigumu
 
Sio kweli. Tajiri, mtu kati na maskini wote wanahitaji pesa. Tena wenye pesa wanahitaji pesa kubwa zaidi. Michango mikubwa mikubwa.
Maskini wanahitaji buku 10, buku 30, buku 50. Ukifikisha laki, unaabudiwa.
Familia zenye pesa au kipato cha kati sasa! Dah!
Watu wenye pesa sio wa mchezo mchezo!
Inaonekana kwa akili yako umejiandaa kuwa tegemezi au kuwa maskini.
Sio kweli ukioa mwanamke kwao ni kipato cha kati huwezi kusikia ana fanya maendeleo kwao kwasababu kwao wazazi wake walishafanya maendeleo na uwezi kumsikia akisema mshahara wake ana somesha ndugu zake wala kuwa jengea nyumba wazazi wake wala kumsikia akisema mtoto wa dada wala wakaka anakuja kukaa naye ili kumsomesha, na wazazi wake kuja kuja nyumbani kwake ni ngumu sana.
 
Kuna mambo mengine ni kujitakia wakuu. Awe mwanamke toka kipato cha chini au cha juu au cha kati ishu ni kuwa na misingi binafsi ya wewe na maisha ya familia yako. Mimi sijaoa ukoo au familia nimemchukuwa mwanao awe mke wangu sio kuja lea familia yao kwangu maana mimi pia nina hitaji kujiendeleza kulea familia yangu na yeye etc. so swala la kusema nita pigwa mizinga wajipange kabisa siwezi endekeza kujibebesha matatizo yalio nje ya uwezo wangu.
Kuna vitu tuna endekeza wenyewe mwisho tuna kuja laumu. siwezi pata binti mzuri na elewana nae niogope kuoa kisa kipato cha chini ni uongo. kama yeye ndio ana lelea familia yake hapo sawa nikimchukuwa ntakuwa nimewa haribia mipango yao ila kama wana subiri aolewe ndio waje tatua matatizo yao hawata amini aseeeh.
maana swala kama la ugeni sipokei timu kwangu aje mmoja tena kwa taarifa na mda maalum sio kuhamia. na wakisha juwa kuwa niko makini kwa hilo hawa wezi kuja nivamia kizembe zembe. so tujifunze kuwa na mipaka katika maisha yetu ya kila siku sio kila jambo ubebe tu kisa ndugu au familia mwisho ndio mana hatuendelei tuna zidi tengeneza familia tegemezi na zakivivu wakiamini ata kuja mtu kuwa okoa.
 
Back
Top Bottom