Kim Jong-Un aagiza muuza filamu kupigwa risasi hadharani

Kim Jong-Un aagiza muuza filamu kupigwa risasi hadharani

May 30, 2021 by Global Publishers

kim.jpg

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Lee, ameuwawa kwa kufyatuliwa risasi pamoja na familia yake huko Wonsan Korea ya Kaskazini baada ya kukamatwa akiuza Cd na Pamoja na Flash ambazo zilikuwa na filamu kutoka nchi Jirani ya Korea ya Kusini.

Lee pamoja na familia yake walipigwa risasi uwanjani mbele ya watu 500, ikiwa ni fundisho kwa watu wengine wanaouza filamu kutoka nje.

Kiongozi wa taifa hilo Kim Jon Un alipiga marufuku kuangalia filamu za nje kwa kuhofia nchi kuingia kwenye utamaduni wa nchi za magharibi.

Taarifa zinaseama watu zaidi ya 20 wamekamatwa kwa kosa hilo la kuuza filamu na Muziki na wanatarajiwa kuhumiwa kwani wameunja sheria za nchi hiyo.

Aidha unaweza kufungwa miaka saba jela kwa kosa kutotoa taarifa za mtu anayeuza filamu na Cd za Muziki kwa polisi.
Huyu mwamba aje awe Rais tz japo mwezi 1 tu maana Wizara ya fedha watu wanajilipa posho tu bila mpangilio na hawana cha kufanywa.
 
Yaani huko hata ukishikwa na chochote tu ni kifungo
Huko ni balaa hata waamdishi wa habari toka nje wanabanwa haswa

Kuna mengi huko ila nashangaa sijui kiduku alimpendea nini Rodman
Huyo Rodman ni rafiki yake mpendwa walikutana na Kim akiwa anasoma USA
 
Pia inasemekana nchi hii inaongoza duniani kwa mabalozi wake kuto Rudi nyumbani baada ya kumaliza muda wake.Kwani wafikapo ughaibuni wanashangaa mambo yalivyo na kujikuta wameingia sayari nyingine.
Ukiwa Korea kas mambo yafuatayo NI mwiko kuyafanya:-
1.kutumia Google
2.kutumia mtandao wowote wa kijamii
3.kuangalia tv yoyote ya nje,wao Wana Chanel zao 3 basi.
4.kukutwa na biblia
5.kutopiga au kuharibu kura,kumbuka mgombea ni mmoja ambaye ni Rais wa Sasa.
6.kuingia mji mkuu Piyong'ayang ni lazima uwe na kibali.Walioruhusiwa kuishi huko ni matajiri na watu waiifu kwa serikali.
Ukikiuka Sheria hizi adhabu yake kuimudu ni vigumu.
Kama kumbukumbu zangu ziko sawa,huko hata Corona haikufika
Sasa si watu watoroke tu au nayo shida?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Huyu jamaa ni mbwa kabisa. Tatizo wameshindwa kumuua.
Najuta kusomea JUCHE IDEA YAO. Inafundisha mambo magumu sana na ya kikatili
 
Tanzania iliruhusu NOrth Korea kufundisha Juche Ideology, nami ni mmojawapo niliipata. Ila nashukuru sijaenda Korea
 
Jamaa aliwahi kumuua mjomba wake kabisa,kwa kula rushwa,akatupwa kwenye mbwa wakali ambao hawakupewa chakula wiki nzima ,ili mjomba wake in awe kitoweo .mwamba katili sana
 
Alafu kuna kima walikuwa wakisema rip ni dikteta.

Kama wangekuwa huko wasingethubutu hata kufikiria udikteta wa kim.

Wewe umeona wapi mtu anathubutu kumtukana dikteta hadharani.
 
May 30, 2021 by Global Publishers

kim.jpg

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Lee, ameuwawa kwa kufyatuliwa risasi pamoja na familia yake huko Wonsan Korea ya Kaskazini baada ya kukamatwa akiuza Cd na Pamoja na Flash ambazo zilikuwa na filamu kutoka nchi Jirani ya Korea ya Kusini.

Lee pamoja na familia yake walipigwa risasi uwanjani mbele ya watu 500, ikiwa ni fundisho kwa watu wengine wanaouza filamu kutoka nje.

Kiongozi wa taifa hilo Kim Jon Un alipiga marufuku kuangalia filamu za nje kwa kuhofia nchi kuingia kwenye utamaduni wa nchi za magharibi.

Taarifa zinaseama watu zaidi ya 20 wamekamatwa kwa kosa hilo la kuuza filamu na Muziki na wanatarajiwa kuhumiwa kwani wameunja sheria za nchi hiyo.

Aidha unaweza kufungwa miaka saba jela kwa kosa kutotoa taarifa za mtu anayeuza filamu na Cd za Muziki kwa polisi.
Taarifa ambazo base yake ni magharibi wala tusitegemee kuwa ni reliable info.

Hakuna kitu kama hiko DPRK
 
Duh,na mijananchi ya huko imekaa tu hata haindamani kupinga,yaani uhai uondokw kwa kosa la hivyo kweli,huyo dogo ni zaidi ya sheitwan aisee
Hakuna mtu anataka kuzikwa na matundu ya risasi mwili mzima.

Hata wewe usingethubutu kama ungethubutu ungeandama peke yako nchi nzima.
 
Back
Top Bottom