Kinachoendelea Kigoma kuibua wachawi ni udhalilishaji, upuuzi na uchonganishi

Kinachoendelea Kigoma kuibua wachawi ni udhalilishaji, upuuzi na uchonganishi

Narudia tena ni Udhalilishaji, Upuuzi, Ushenzi, Uchonganishi na Utapeli.

Nimefika mkoa wa Kigoma Tokea Majuzi nilicho Kikuta huku Sielewi Huku ninchi Nyingine au ni Tanzania hii hii !

Kuna kitu kinaitwa  KAMCHAPE, hawa wapuuzi nani kawaleta, Hili kweli nani kalipa Baraka kufanyika karibu mkoa mzima wa Kigoma?

Kinachofanyika Ni Udhalilishaji na Uchonganishi kwa jamii.

Kwanza Wanachangisha Tsh 5,000 kila kaya kwa lazima sio ombi.

Kisha Wanapita kila nyumba Eti wanatoa Uchawi na wachawi! Tena utake usitake lazima.

Wakifika kwako wanasema hapa kuna uchawi Lazima uchapwe kisha unanyolewa Nywele Mbele ya umati wa watu kisha kunyweshwa Kile wanachoKiita Dawa hautakuwa mchawi tena!

Nimefuatilia kinachofanyika pale ni Mazinga Ombwe na Kujipatia Pesa kwa Utapeli!

Wakati Yakifanyika hayo Kijiji Jirani, Nyie mnaanza jiandaa na kama mwenyekiti hata Wakaribisha hao watu au kuchangisha hizo pesha kila kaya naye Anajumuishwa kwenye Kundi moja la Wachawi !

Kuna vitu vya Ajabu sana Vinafanyika mpaka nimeshikwa na Butwaa. Nimeuliza nikaambiwa Serikali Ndio Imeruhusu hili Lifanyike Mkoa mzima kweli?

Mbona Sioni Dodoma na Mbeya Kwanini Kigoma?

Kwasasa zoezi limepamba Moto Vijiji vya Nyarubanda, Kalinzi, Mukigo, Muhinda, Nyaruboza, Rukoma, Igalula, Mgambo, Katumbi, Kalya Nk.

Huko kumechafukwa hali ni mbaya na lisipofanyiwa kazi na kuacha litaleta shida kwa watu


Pia soma
- Mfahamu 'Kamchape' mkamata wachawi na shughuli zake kwa ujumla kutokea hapa Mkoani Kigoma
Ma ccm yakiona hivyo yanafurahi, jinsi wananchi walivyowajinga na mazuzu!
 
Hayo mapembe,watu wao wanayachombia usiku. I'll
Kuna mama mmoja mtu mzima mwenye umri mkubwa kuweza kuitwa bibi alichanjwa chale kwa lazima eti uchawi wake ukose nguvu akitaka kuloga. Mama wa watu alivuja damu njingi. Ilikuwa kila nyumba wakipita zingine wanasema hakuna uchawi na zingine wanasema kuna uchawi, wanafukua sehemu fulani ya nyumba wanaibuka na kitu kama pembe ya myama wanasema ni uchawi, mwenye nyumba anakamatwa na kuchanjwa chale kwa lazima
 
Hii yote ni sababu watu hawaendi makanisani Kwenye ibada bali wanakubali udanganyifu na shoti kati
Makanisani kwenye,kuna baadhi ya madhehebu,ya kitapeli tu.
 
Kwamba hao wataalamu hawana familia au mahitaji yao binafsi?
Hizo pesa hua wanachukua hao waganga uchwara na wasaidizi wao Ila wao wanakula pakubwa.

Ni utapeli tu kama ulivyo utapeli mwingine hakuna zaidi na hakuna mchawi wanaweza kumtoa kwa usanii wao zaidi ni kudhalilishana tu.
Jambo usilolielewa ni vyema ukasalia kimya kuliko kulizungumzia!
 
💔So kitabu Cha dini kikisema magonjwa yote ni mapepo nenda kaombewe we unaacha kwenda hospital...dunia imeendelea saa hivi unabidi uache Mila za kitoto na za kijinga
Mila za kitoto na za Kijinga...! Sema watu wengine wana Amini vitu usivyoamini....!

Kuna Nchi kama South Africa, unakuta wanaamini uwepo wa Mungu, wanasali na kuomba kwa namna yao, lakini hawaamini kuhusu Yesu, na wana sababu zao wakikupa unabaki kusema kila mtu wacha aamini anachoamini.

Mfano huwa wanaomba kwa Mungu kupitia Mizimu yao, ukiwauliza kwa nini wanachanganya mizimu na Mungu, wanakwambia Yesu mwenyewe ni Mzimu, aliishi na kufa zamani, kwa nini nimtumie Yesu kumfikia Mungu, wakati nina Ndugu zangu walishatangulia...!?
 
Naandika haya, nikiwa nimeshikwa na butwaa kubwa kwa Taifa langu Tanzania. Hapa Kigoma, limeibuka kundi la watu wanaojiita Kamchape. Watu hawa wanajitambulisha kuwa wanatoa watu uchawi. Hivyo wanazunguka vijiji kwa vijiji, kuwatoa uchawi hao wanaowaita ni wachawi. Ajabu ni kwamba, wanalazimisha watu kuwapa hela, la sivyo unapigwa na kuitwa Mchawi. Mpaka sasa nimeona watu kadhaa, ambao wamepata majanga hayo kwa kupigwa, kunyang’anywa mali zao na fedha wakiwemo viongozi wa dini. Kuna wakati nililazimika kumpeleka mtu Hospitali baada ya kupigwa vibaya kwa kuwa alikataa kutoa hela. Habari za Kamchape zimesambaa karibu Kigoma nzima, lakini hakuna jitihada zozote za kuwazuia watu hawa.

Mambo yanayofikirisha kuhusu Kamchape

  • Watu hawa wanajisifu kuwa wanatambulika serikalini, je Wametumwa na nani?
  • Kwa nini Serikali mkoa wa Kigoma haichukui hatua za dhati za kuzuia watu hawa, je wamewashindwa au na wao ni waamini wa mambo hayo?
  • Ikiwa hali hii ikiachwa iendelee tutakuwa na taifa la namna gani? Yaani mtu anapewa shutma za uchawi, na kupigwa au kunyang’wanywa mali. Maafa yatakuwa mengi sana na chuki itatawala Taifa
  • Nahuzunika kwa Taifa langu, nchi niipendayo kwa kuendekeza imani hizi za kishirikina na kutengeneza chuki na maafa kwa jamii.
 
Hao jamaa inatakiwa wapate mtu mmoja mwenye akili timamu akawashitaki watalipishwa hela hawatakaa wasahau!.. hiyo ni Moja kati ya fursa sema wanafanyiwa hivyo wamelala tu.. ingalikuwa Mimi sahivi tayari navibunda kadhaa mfukoni mwangu..😋
 
Back
Top Bottom