binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 11,201
- 28,642
Mimi nimeacha kabisa kununua nguo, viatu na handbags online. Ptuuu Wabongo ni waongo rangi imewekwa filter, size za uongo, hata hand bag kwanini mtu asiweke hata rula kama kipimo. Unaagiza handbag kubwa kinakuja kidunchu cha kuchezea watoto.Hakuna biashara pasua kichwa kama kuuza nguo na viatu online.
hahahahahaUnaagiza handbag kubwa kinakuja kidunchu cha kuchezea watoto.
Kila mmoja hupewa bei yake wanacheki dp yako tu. Hawana bei mojaMimi huwa siwaelewi wale wauzaji wa vitu mitandaon anaweka picha za bidhaa zake alafu bei anakuambia nenda dm, sielewag wana maana gani naona hawapo serious na kazi.
Hivi hakuna tester kama perfumes ambapo unakuwa na za kujaribu tuSisi wauza urembo unakuta mdada anataka wanja anachagua mmoja anautest halafu anarudisha anachukua mpya ambao haujaguswa ndio ananunua ule aliotest anakuachia .Hii tabia wanafanya hata kwa bidhaa nyingine pia .
Wewe ni mnoma sana hadi bando la simu yako unatumia njia za panya.Ukiwa hivi vitu vizuri hutatumia mkuu,au utakuwa unaingia gharama sana ili kuvitumia.
Mimi nikiona kitu kinauzwa nikakipenda wala sijiulizi mara mbili mbili,namshukuru Mungu sijawahi kung’atwa japo nakiri udhaifu sina subira ya kuanza kuchunguzana na seller kama nachunguza mchumba,hivi kuna mwamba nimemtumia 35K aniunge bundle la Voda inaenda week ya tatu kimya uzuri bado yupo responded nikimuuliza anajibu smoothly na pia ni biashara tuliwahi kuifanya ndo maana sina wasi sana.
Feedback toka kwa wateja wengine ni muhimu..maana hata aliexpress na nk huko unakuta watu wameweka reviews zao kibao...Jiwe gizani
Wasumbufu wameguswa hapo juu
Ukiona blue ticks kwenye whatsap yangu unaweza ukaacha kabisa online business
Mtu anakuja na screenshot yenye bei Halafu anakuuliza bei gani?
Umeandika location anauliza unapatikana wapi
Picha umeweka anaomba picha zaidi
Wengine wanaomba mpaka feedback kutoka Kwa wateja wengine [emoji119]
Uko Mbeya Sumbawanga?Me nko mbeya na huu ni mwaka wa 7 nanunua bidhaa online...nikisha kuamini,hata mzgo uwe wa mil 5 nakutumia
Hununui kwa wabongo bila shaka....Me nko mbeya na huu ni mwaka wa 7 nanunua bidhaa online...nikisha kuamini,hata mzgo uwe wa mil 5 nakutumia
Tatizo wafanyabiashara wa online bongo hamuaminiki kwahiyo muendelee kuvumilia tu watu wanapohoji kujiridhishaYaani chief watu wanakuuliza maswali ambayo yana majibu kwenye description tena umeyapanga very clear.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Mbona hata physical ni hivyo hivyo tu, siye wauza genge anakuja bidada anaminyaminya nyanya halafu ananunua biringanya.
Hahah it's all about business mkuu.Wewe ni mnoma sana hadi bando la simu yako unatumia njia za panya.
Msumbufu wa leo ni mteja wa kesho au ni balozi bila malipo. Kuna jamaa mmoja alinieleza kilichomtokea, alifika mteja dukani kidogo amwambie ondoka ila uvimilivu na huduma yake ilimpa biashara nzuri sana.Elimu ya customer care mkuu unamaanisha nini kuweza kuvumilia ujinga wa wengine..
Ili kupunguza maswali unaweka maelezo yote yaliyoshiba tena kwa msisitizo ili mtu akija inbox basi aje kama mnunuzi. kama sio mnunuzi ni alipite tu tangazo.
Sumbawanga ni RUKWA sio mbeyaUko Mbeya Sumbawanga?
aah sawa ile mikoa mipya, okSumbawanga ni RUKWA sio mbeya
Wateja wengine ni wasumbufu sababu ya kulizwa.Yaani chief watu wanakuuliza maswali ambayo yana majibu kwenye description tena umeyapanga very clear.
Kwa kuongezea.Wauzaji pia sio waaminifu.. ndo maana wateja tunakua na maswali mengi ili kujiridhisha na huduma mkuu..
Imagine kuna mzgo nmeagiza kutoka dar tangu J3 ya wiki iliyopita, ila cha ajabu mpaka leo muuzaji hajautuma.
Uaminifu wenu ni ZERO