Kuona Maiti ikizikwa na Manispaa kumenitafakarisha sana maisha yetu hapa duniani

Kuona Maiti ikizikwa na Manispaa kumenitafakarisha sana maisha yetu hapa duniani

Siwezi sikitika mtu kuzikwa na manispaa, siwezi sikitika mtu kukosa watu wa kumzika. Nasikitika mtu akifa tu, akishakufa mumzike kwa helicopter au toroli bado amekufa.

Mumzike kwenye jeneza au kwenye mkeka, amekufa. Na mazishi mazuri hayampi nafasi ya kwenda mbinguni wala kumuepusha na moto.

Kwangu mimi nikiona mtu anasikitika na kulilia maiti kuzikwa na manispaa huwa namuona weak, na taifa halijengwi na watu wa mioyo dhaifu kama huyo. Mkiwa vitani comrade akafa si lazima mbebe mwili kurudisha nyumbani kama logistics haziruhusu. Yani tuhangaike kubeba majeruhi kutoka frontline kisha tuhangaike kubeba miili ya waliokufa? Kama hakuna ceasefire ya kuchukua deceased mnachukua dogtags na vitambulisho ila miili mnazika ukouko frontline.

Nikienda sehemu kutafuta, sina ndugu wala jamaa nikatangulia ghafla bila yeyote kujua ni sahihi sana nizikwe na manispaa. Hakuna haja ya kutia huruma kwenye hilo
Wamarekani waendapo vitani wana msemo maarufu sana, 'Dead or alive, we will always be back home'.

Na wafafanya kila namna, mwanajeshi aliyefia katika uwanja wa vita anarudishwa nyumbani. Shushushu aliyeuwawa wakati wa kutimiza majukumu yake, hata ipite miaka mingapi, watapeleleza wajue ni wapi mwili wa mpambanaji wao ulizikwa.

Watafukua hata kama ni mabaki, kisha kuipeleka nyumbani kuzikwa kiheshima.

Sawa, ameshafariki na hana faida tena, lakini maisha yake yalikuwa na maana hapo kabla.

Taifa halijengwi na watu wenye roho mbaya. Halijengwi na watu wasio na hofu. Taifa linajengwa na watu waliostaarabika.

Uwe na asubuhi njema.
 
Kuna siku nilikuwa Mwananyamala Hospital hao jamaa na Manispaa wakaja kuchukua maiti..aisee ilikuwa imeharibika inavyoonyesha kwa sababu ya harufu ila kilichonishangaza ni jinsi alivyowekwa kwenye gari..yaani alitupwa tu kama box vile.

All in all mtu akifa amekufa..azikwe vizuri asizikwe vizuri hilo halina maana sana.
 
Upande wangu mwezi June mwaka huu nilihudhuria mazishi ya ndugu mmoja aliyefariki huko DSM akaletwa kuzikwa huko kwao nilipokuwepo kama mgeni tu. Yule ndugu aliniuma kwakweli maana alizikwa na Serikali ya mtaa imagine.

Ndugu walikuwepo na wachungaji + mashehe ila hawakuhusika katika kumzika kwa sababu ya Kwanza toka akiwa kijana hakua akishiriki ibada ya kanisa wala msikiti japo alikuwa anafahamika kama mkristo.

Iliniuma aiseee yaani hata ile sala au dua ya mwisho hakusaliwa, yaani kama tumefukia mbwa aliyegongwa na gari.
Pole.
Lakini haijalishi umezikwaje kama mtu akifa ameshakufa. Hizo taratibu ni kwaajili yetu sisi tuliobaki...kujifariji tu lakini haina maana yoyote kwa marehemu.
 
Inakuaje mtu kukosa ndugu serikali ijiangalie kwa hilo. Ni mauzembe tu. Science ilisha advance ila sisi bado tupo nyuma. Lililokubwa hapa ni ndugu za maiti wawe na taarifa kwamba jamaa yao kashaondoka ulimwenguni ili wasibaki njia panda.
 
Mwananyamala hospital hata kama hukupenda kuweka wazi jina la hospital husika... Je nimepatia?

Kwa bahati mbaya Serikali haina muda wa kufanya utambuzi wa DNA ili walau waondolewe kwenye kundi la waliopotea wasitafutwe zaidi na ndugu zao.
Serikali imechelewa kidogo.

Inapaswa kuwa na database ya DNA ya wananchi wake wote. Kuanzia wanaozaliwa mpaka utu uzimani.

Hii itasaidia sana katika utambuzi na usalama wa raia wake. Hata pia katika swala zima la usalama.
 
Wamarekani waendapo vitani wana msemo maarufu sana, 'Dead or alive, we will always be back home'.

Na wafafanya kila namna, mwanajeshi aliyefia katika uwanja wa vita anarudishwa nyumbani. Shushushu aliyeuwawa wakati wa kutimiza majukumu yake, hata ipite miaka mingapi, watapeleleza wajue ni wapi mwili wa mpambanaji wao ulizikwa.

Watafukua hata kama ni mabaki, kisha kuipeleka nyumbani kuzikwa kiheshima.

Sawa, ameshafariki na hana faida tena, lakini maisha yake yalikuwa na maana hapo kabla.

Taifa halijengwi na watu wenye roho mbaya. Halijengwi na watu wasio na hofu. Taifa linajengwa na watu waliostaarabika.

Uwe na asubuhi njema.
Kila mwanajeshi wa Marekani amesajiliwa na anajulikana alipo na wazazi wake na ndugu wanajua company yake na ilipo deployed. Marekani ndio nchi yenye logistics kubwa zaidi duniani, ina bases zaidi ya 50 pande zote za dunia ila bado wanazika uko uko frontline wakikosa uwezo wa kuchukua maiti. Baada ya miaka ndio wanasaini bill ya kufukua miili na kuirudisha.

Haya wewe unasimamia mortuary ya hospitali. Miili haijachukuliwa na yeyote, utakaa na hizo miili miaka mingapi? Mortuary ikijaa hospital ijenge nyingine au? Sasa kwani mortuary imekuwa cemetery.
Ukiachana na kuzikwa na manispaa option nyingine ipi, wabebe mwili walete nyumbani kwako muubatize jina la ukoo mzike kwa kupiga kilio?

Nchi halijengwi na mama huruma au baba huruma bila kuzingatia uhalisia
 
Ya Moto Sana
Unaweza ukapooza kaka. Sijaja hapa kutafuta attention kwa yeyote asiyenifahamu.

Nenda Mwananyamala Hospital, muite mlinzi yeyote aliyekuwa zamu Jumapili saa sita au saba kasoro mchana.

Muulize hili tukio. Alafu endelea na maisha yako.
 
Siwezi sikitika mtu kuzikwa na manispaa, siwezi sikitika mtu kukosa watu wa kumzika. Nasikitika mtu akifa tu, akishakufa mumzike kwa helicopter au toroli bado amekufa.

Mumzike kwenye jeneza au kwenye mkeka, amekufa. Na mazishi mazuri hayampi nafasi ya kwenda mbinguni wala kumuepusha na moto.

Kwangu mimi nikiona mtu anasikitika na kulilia maiti kuzikwa na manispaa huwa namuona weak, na taifa halijengwi na watu wa mioyo dhaifu kama huyo. Mkiwa vitani comrade akafa si lazima mbebe mwili kurudisha nyumbani kama logistics haziruhusu. Yani tuhangaike kubeba majeruhi kutoka frontline kisha tuhangaike kubeba miili ya waliokufa? Kama hakuna ceasefire ya kuchukua deceased mnachukua dogtags na vitambulisho ila miili mnazika ukouko frontline.

Nikienda sehemu kutafuta, sina ndugu wala jamaa nikatangulia ghafla bila yeyote kujua ni sahihi sana nizikwe na manispaa. Hakuna haja ya kutia huruma kwenye hilo
Unaonekana ni jitu katili sana, huko unakosemea kujenga nchi, ni nchi gani hii unayoiongelea?,soma hili still facing the barrel of UMASIKINI, MARADHI,UJINGA na sasa cousin wao Rushwa, huku lingusenguse hatuna maji Safi na salama hadi leo!,niambie hiyo vita ya kujenga nchi inapigwana wapi Nami nikajiunge
 
Kila mwanajeshi wa Marekani amesajiliwa na anajulikana alipo na wazazi wake na ndugu wanajua company yake na ilipo deployed. Marekani ndio nchi yenye logistics kubwa zaidi duniani, ina bases zaidi ya 50 pande zote za dunia ila bado wanazika uko uko frontline wakikosa uwezo wa kuchukua maiti. Baada ya miaka ndio wanasaini bill ya kufukua miili na kuirudisha.

Haya wewe unasimamia mortuary ya hospitali. Miili haijachukuliwa na yeyote, utakaa na hizo miili miaka mingapi? Mortuary ikijaa hospital ijenge nyingine au? Sasa kwani mortuary imekuwa cemetery.
Ukiachana na kuzikwa na manispaa option nyingine ipi, wabebe mwili walete nyumbani kwako muubatize jina la ukoo mzike kwa kupiga kilio?

Nchi halijengwi na mama huruma wenye poor thinking capacity
Nimezungumzia swala lolote la kuwabakisha Mortuary?

Ambacho sikuona ni sawa ni namna maziko yao yanavyofanyika Mkuu. Wala si swala la kuwatoa humo ili wengine wapate nafasi.

Mtu asitupwe kama boksi wakati wa kupakizwa. Walau asitiriwe na Sanda. Wanapozikwa pachimbwe vizuri. Hayo si mauaji ya halaiki kwamba wazikwe kwa pamoja.

Duh!. Hayo ya poor thinking capacity yametokea wapi tena?
 
Unaweza ukapooza kaka. Sijaja hapa kutafuta attention kwa yeyote asiyenifahamu.

Nenda Mwananyamala Hospital, muite mlinzi yeyote aliyekuwa zamu Jumapili saa sita au saba kasoro mchana.

Muulize hili tukio. Alafu endelea na maisha yako.
Ninapachukia Mwananyamala Hospital ,Nina hasira mno na wale wafanyakazi wanaosimamia maiti pale, kwangu ni washenzi ila ninaandaa push back against them, always nimezaliwa hivyo na nitakufa hivyo
 
Siwezi sikitika mtu kuzikwa na manispaa, siwezi sikitika mtu kukosa watu wa kumzika. Nasikitika mtu akifa tu, akishakufa mumzike kwa helicopter au toroli bado amekufa.

Mumzike kwenye jeneza au kwenye mkeka, amekufa. Na mazishi mazuri hayampi nafasi ya kwenda mbinguni wala kumuepusha na moto.

Kwangu mimi nikiona mtu anasikitika na kulilia maiti kuzikwa na manispaa huwa namuona weak, na taifa halijengwi na watu wa mioyo dhaifu kama huyo. Mkiwa vitani comrade akafa si lazima mbebe mwili kurudisha nyumbani kama logistics haziruhusu. Yani tuhangaike kubeba majeruhi kutoka frontline kisha tuhangaike kubeba miili ya waliokufa? Kama hakuna ceasefire ya kuchukua deceased mnachukua dogtags na vitambulisho ila miili mnazika ukouko frontline.

Nikienda sehemu kutafuta, sina ndugu wala jamaa nikatangulia ghafla bila yeyote kujua ni sahihi sana nizikwe na manispaa. Hakuna haja ya kutia huruma kwenye hilo
Una bwabwaja tu ujinga!
 
Unaonekana ni jitu katili sana, huko unakosemea kujenga nchi, ni nchi gani hii unayoiongelea?,soma hili still facing the barrel of UMASIKINI, MARADHI,UJINGA na sasa cousin wao Rushwa, huku lingusenguse hatuna maji Safi na salama hadi leo!,niambie hiyo vita ya kujenga nchi inapigwana wapi Nami nikajiunge
Acha upumbavu mama huruma wewe. Ukatili unao wewe na familia yako, nenda Mwananyamala ujitie wewe ndio ndugu wa hao marehemu ulipie na bills wanazodaiwa ukazike uko Lingusenguse kijijini kwenu.

Mnataka hospitali ifanyeje na maiti hazijachukuliwa. Aliyekwambia hospitali ni makaburini nani? Mortuary ni sehemu ya kuhifadhi miili kwa muda, sio kuzika humo. Kama mwili hauchukuliwi ni sahihi kuzikwa na manispaa. Mbona akili ndogo inahitajika kuelewa hii
 
Unaweza ukapooza kaka. Sijaja hapa kutafuta attention kwa yeyote asiyenifahamu.

Nenda Mwananyamala Hospital, muite mlinzi yeyote aliyekuwa zamu Jumapili saa sita au saba kasoro mchana.

Muulize hili tukio. Alafu endelea na maisha yako.

Mwananyamala iko mkoa gani
 
Acha upumbavu mama huruma wewe. Ukatili unao wewe na familia yako, nenda Mwananyamala ujitie wewe ndio ndugu wa hao marehemu ulipie na bills wanazodaiwa ukazike uko Lingusenguse kijijini kwenu.

Mnataka hospitali ifanyeje na maiti hazijachukuliwa. Aliyekwambia hospitali ni makaburini nani? Mortuary ni sehemu ya kuhifadhi miili kwa muda, sio kuzika humo. Kama mwili hauchukuliwi ni sahihi kuzikwa na manispaa. Mbona akili ndogo inahitajika kuelewa hii.
Mkuu unachobishania wala hukifahamu. Huenda ukatili uliojijengea unakamata na ufahamu wako wa kushindwa kuelewa kinachozungumziwa.

Kilichonisikitisha ni namna ndugu zetu wanavyositiriwa wakati wa kupelekwa mazikoni. Wanatupwa kama boksi. Hawaulazi hata kistaarabu.

Hakuna hata sanda ya kuwasitiri. Wanatupwa kwenye shimo moja. Kwako ni sahihi?
 
Back
Top Bottom