Kurejea kwa Elia F. Michael, CHADEMA iwe makini

Kurejea kwa Elia F. Michael, CHADEMA iwe makini

Ni hivi boss, hao wanasiasa wanaweza kufanya watakacho na kwenda watakako, ila pia hawana haki ya kupata imani yetu pindi wanapokwenda tofauti na matakwa yetu. Kama ww unataka kuvumilia wanachotaka wanasiasa wasio na misimamo, hiyo ni haki yako. Huyo Lowassa unayemtaja sio kila mtu alikubaliana na uhuni ule, na nina hakika upuuzi kama ule hautakaa urudiwe.

Tunasema ccm haina ushawishi sio kwamba haina kabisa, bali haina ushawishi iliokuwa nao huko mwanzo, na haina uwezo wa kuwa nao tena zaidi ya kutegemea vyombo vya dola. Na
huko kushinda sio kwa ushawishi bali ni kwa nafasi yao ya kumiliki dola. Hivi leo ccm ikitumia huo ushawishi unaotaka tuamini inao, inahitajika chaguzi mbili tu kuiweka ccm pembeni. Hii sio rocket science bali ni uhalisia wa kibinadamu. Ufahamu CCM sio chama cha kizazi hiki bali ni cha kizazi kilichopita, ndio maana inatumia nguvu kubwa kubaki madarakani kuliko ushawishi.

Kuitisha maandamano sio lazima ufanikiwe mara moja kulingana na nature ya watu ilivyo. Ilitakiwa kusiwe na vitisho kisha uje na ushuhuda kuwwa watu wamegoma kujitokeza. Ila kupanda mbegu ya kuandamana iko siku itazaa matunda. Huko Egypt, Sudan, Zimbabwe nk walitawaliwa kibabe zaidi ya miaka 30 wakiwa wanaogopa kuandamana, ila ilifika siku hofu iliondoka na leo tawala zile za wababe ni historia.

Hiyo join the chain inasuasua maana wachangiaji ni watu waliopigika na hawana uwezo wa kutoa, isitoshe haikuwa deni bali ni jambo la hiyari. Kodi yenyewe tu ya nchi watu wanadaiwa kisheria inakuwa mbinde kutoa, ndio itakuwa huo mchango wa hiyari?
sio mimi boss, unakosea unvyojibu kama vile mimi ndio nashawishika na hao wanasiasa..Hapa nazungumzia wananchi walivyo, wananchi wengi uelewa wao ni mdogo kuhusu kuchanganua utapeli na ukweli

Mfano hilo la Lowassa, baada ya Chadema kumsimamisha Lowassa ikawa ndio uchaguzi wenye ushindani zaidi kwa CCM ambapo walipata kura nyingi na wabunge wengi zaidi, japo Lowassa anafahamika ni fisadi na hakuwa hata na sera za maana, hili linakupa picha akili za wananchi zipo vipi kuhusu kujua uwongo wa wanasiasa, na sio siasa tu, hata kwenye dini,au mpira huko

Pointi hapa sio kutetea Chadema kuchukua watu kama Lowassa , ila ni kuwa pragmatic ama utaishia tu kudumaa, mtu kama hana historia chafu sana, na alikuwa mwanachama mzuri mwenye ushawishi tu eneo alilokuwepo kabla ya kuhama, kumpokea haina ubaya, ukizingatia na siasa za awamu ya 5 zilivyokuwa...Sasa mkitaka watu pure mtaishia kuwa kakikundi kadogo tu ka mtandaoni
 
Kosa kubwa Sana chadema kupokea watu aina hii. Bora ya hata covid-19 ni bora wapokelewe na sio hao waunga juhudi
 
Hapa ndipo upinzani mnapojidanganya
Huyu si miongoni mwenu
Ukisoma alichoandika utagundua jambo
Ni mnafiki mchafuzi mharibifu
* Akae mbali na viongozi
Eti abebe briefcase ! Huyu ni wa kufanana na akina musiba
Endeleeni kujidanganya
Arudi kufanya nini? Akaanzishe chama chake mrundi huyu

Arudi ila cheo kwa sasa hapana, kuanzisha chama ni utashi wake. Kama ni wabaya hata sasa ndani ya chama wapo. Huu ni mtazamo wangu, I stand to be corrected.
 
Wapokeeni....

Acheni siasa za chuki na hasama....

Vijana wenu hao....wapokeeni wawapigie kazi.......

#Siempre JMT 🙏
 
Nashauri akutane na Mbowe nadhani atafunguka mambo mengi sn, pia Mbowe ni mtu mwenye hekima na busara sn
Hekima na busara hizi hapa eeee?!!!
2991488_images_7.jpeg
 
sio mimi boss, unakosea unvyojibu kama vile mimi ndio nashawishika na hao wanasiasa..Hapa nazungumzia wananchi walivyo, wananchi wengi uelewa wao ni mdogo kuhusu kuchanganua utapeli na ukweli

Mfano hilo la Lowassa, baada ya Chadema kumsimamisha Lowassa ikawa ndio uchaguzi wenye ushindani zaidi kwa CCM ambapo walipata kura nyingi na wabunge wengi zaidi, japo Lowassa anafahamika ni fisadi na hakuwa hata na sera za maana, hili linakupa picha akili za wananchi zipo vipi kuhusu kujua uwongo wa wanasiasa, na sio siasa tu, hata kwenye dini,au mpira huko

Pointi hapa sio kutetea Chadema kuchukua watu kama Lowassa , ila ni kuwa pragmatic ama utaishia tu kudumaa, mtu kama hana historia chafu sana, na alikuwa mwanachama mzuri mwenye ushawishi tu eneo alilokuwepo kabla ya kuhama, kumpokea haina ubaya, ukizingatia na siasa za awamu ya 5 zilivyokuwa...Sasa mkitaka watu pure mtaishia kuwa kakikundi kadogo tu ka mtandaoni

Ni kweli wananchi hawana uelewa, ila sio kwa wingi huo unaousema ww. Huyo Lowassa hakupata kura kama yeye, bali alipata kura nyingi maana alikuwa cdm, na kwa taarifa yako cdm wangemsimamisha Dr. Slaa wangepata kura zaidi. Isitoshe Lowassa hakupokelewa na kupewa nafasi ya kugombea na wafuasi wa cdm, bali genge dogo la viongozi kwa maslahi yao binafsi. Juu ya wananchi kuchanganua utapeli tumeona wananchi kukifanyika midahalo na mikutano mbalimbali hupata uelewa wa kutosha. Kama 2010-2015 walielewa ina maana sasa hivi ndio wamekuwa wajinga?

Sina popote ninapokataa mtu kupokelewa regardless aliondoka vipi, ila ninachokataa ni mtu kurejea na kupewa tena cheo au nafasi ya kugombea. Anaweza kukaa nje ya nafasi za uongozi sio chini ya miaka mitano chini ya uangalizi kabla ya kuaminiwa tena.
 
Hawa vijana waliondoka CHADEMA wenyewe kwa kununuliwa baada ya kushawishiwa , huku wengine wakihamia ccm baada ya vitisho, yeyote anayeogopa vitisho vya watawala hafai kwenye siasa za upinzani.

Ninatambua msululu wa wasaliti wanaoomba kurejea CHADEMA, wakiwemo Wakuu wa Wilaya wawili ambao wako tayari kuachia vyeo na kurudi walikotoka (Haifamiki walichokisahau), Bali naitahadharisha sana Chadema kuwa makini inapowapokea watu hawa , ni kweli kwamba mtaji wa chama cha siasa ni watu, Lakini ni lazima WATU HAO WAWE BINADAMU.

View attachment 2176348
Haka kanyigu kabishi sana.
 
Hawa vijana waliondoka CHADEMA wenyewe kwa kununuliwa baada ya kushawishiwa , huku wengine wakihamia ccm baada ya vitisho, yeyote anayeogopa vitisho vya watawala hafai kwenye siasa za upinzani.

Ninatambua msululu wa wasaliti wanaoomba kurejea CHADEMA, wakiwemo Wakuu wa Wilaya wawili ambao wako tayari kuachia vyeo na kurudi walikotoka (Haifamiki walichokisahau), Bali naitahadharisha sana Chadema kuwa makini inapowapokea watu hawa , ni kweli kwamba mtaji wa chama cha siasa ni watu, Lakini ni lazima WATU HAO WAWE BINADAMU.

View attachment 2176348
Tatizo lako unasiasa za chuki, wewe unavyosema walinunuliwa, kutishiwa au kushawishiwa haya nambie, sasa hivi wanarudi chadema je wamefika bei? mewashawishi au mmewatisha? Mwache mtu atumie uhuru wake na hiyo ndio Democracia.
 
Kiukweli huyu kijana siyo kwamba alihama chama kwa kupenda,zipo tetesi kuwa alitishwa! Wakati anashiriki uchaguzi wa marudio jimbo la Buyungu kufuatia kifo cha Bilago MP alishinda lakini matokeo yakabadilishwa harafu akalazimishwa kuyakubali.
Kwa muktada huo mimi nadhani kijana aruhusiwe kurudi kundini bila masharti.
 
Arudi ila cheo kwa sasa hapana, kuanzisha chama ni utashi wake. Kama ni wabaya hata sasa ndani ya chama wapo. Huu ni mtazamo wangu, I stand to be corrected.
Asirudi
Hawa wapo kimaslahi zaidi
Hawana uchungu na Taifa
Mnawapokea wa nini?
Biblia inasema ' mtatangatanga hata lini?
Chagua kuwa moto au vuguvugu

The guy anaonekana kabisa yupo kwa mission maalum
Action speaks louder
Hamuoni tunachoona

Asipewe hata hii promo
Ni trash

Mtayakumbuka maneno haya
Walikuja akina Sumaye wapo wapi
Kosa si kufanya kosa kosa ni kurudia kosa
 
Asirudi
Hawa wapo kimaslahi zaidi
Hawana uchungu na Taifa
Mnawapokea wa nini?
Biblia inasema ' mtatangatanga hata lini?
Chagua kuwa moto au vuguvugu

The guy anaonekana kabisa yupo kwa mission maalum
Action speaks louder
Hamuoni tunachoona

Asipewe hata hii promo
Ni trash

Mtayakumbuka maneno haya
Walikuja akina Sumaye wapo wapi
Kosa si kufanya kosa kosa ni kurudia kosa

Tunaheshimu mawazo yako, ila Sumaye hakuwa mwanacdm bali alikuwa mzee mwanaccm aliyeondoka ccm kwa kuzira na kupata hifadhi ya muda mfupi. Ni tofauti na Elia ambaye ni kijana na alikuwa mwanacdm. Cheo siafiki apewe, ila kubeba briefcase za viongozi na kupanga viti wakati wa mikutano, ni sehemu ya kitubio chake.
 
Back
Top Bottom