Kusomesha watoto sana, ni njia ya kujiongezea upweke huko uzeeni

Kusomesha watoto sana, ni njia ya kujiongezea upweke huko uzeeni

Unaiandika kama mtu ambaye hajasoma au ambaye hujapata exposure yoyote kuna umri unafika pesa c chochote zaidi ya watu nyumbani tulikuwa 17 kipindi nakuwa, nyumba ilikuwa na vyumba 9 Leo hii kabaki Bibi na dada yake na mfanyakazi na mtoto WA mjomba ana kila kitu pesa gari mashamba analimisha na anapata mazao kibao Tu Ila kila siku anataka wajukuu wake akakkae nawo Ila ndyo ivyoo ata ujipange VIP kuna umri utafika utaitaji watu wa Kula nawo meza, kucheka nawo, na kujifariji hasa pale unapoumwa ndyo maana wahindi au waarabu wengi wanakaa kama familia wengi tunaona kama ushamba Ila lile ni Jambo jema sana kwenye kutunza wazee wenu
Uko sahihi
 
Kuhitaji mtoto akufariji ni kukosa kujipanga vizuri katika maisha.

Umeshindwa kujiwekea akiba ya uzeeni? umeshindwa kujipanga kupata mwenza wa kuwa naye uzeeni?

Unazaa mtoto, unamsomesha, anakua mkubwa, na yeye inakuwa zamu yake ya kuzaa na kusomesha akipenda. Mwache naye aishi maisha yake, akiamua kusaidia wazazi sawa, akiamua kuwa busy na maisha yake sawa.

Wewe baba au mama unayehitaji sana mtoto wako aache ku focus kwenye familia anayoianzisha, halafu a focus sana kwako wewe mzazi, ni mbinafsi na umeshindwa kujipanga na maisha yako mwenyewe ya uzeeni.

Nimeona hii tabia ya wazazi kuwatumia watoto wao kama mbadala wa mfumo wa mafao ya uzeeni, au wazazi kudai matunzo uzeeni kwa sababi waliwalea watoto wakiwa wadogo. Huu ni ubinafsi wa hali ya juu.
Hii ni akili ya kitoto sana.upendo unazidi kushuka siku zinavyozidi.ilawewe ukiugua na kuwa kilema kabisa ukafilisika unataka mzazi aendelee kukulea mpaka kifo chako?
 
Ni kweli,hiyo situation imetokea kwa bi mkubwa wangu mara baada ya sisi watoto wake kuwa na maisha yetu na kuishi mbali na nyumbani na mzee kufariki. Tunajitahidi kumtafutia watu wa kukaa naye ambao ni wafanyakazi na watoto wa ndugu ila changamoto zimekuwa Ni nyingi hivyo hujikuta anabaki mwenyewe.Hii imenifanya nifikiri sana maisha yangu yatakavyokuwa baada ya watoto wangu wote kuondoka nyumbani na kwenda kujitegemea.
Ili kukabiliana na hii hali nimeamua kuanzisha vitega uchumi ndani ya eneo langu la makazi maana ninaishi kwenye mojawapo ya majiji hapa nchini.Kati ya hivyo vitega uchumi nitafungua ofisi ambayo itanifanya nikutane na watu Mara kwa mara na hizo ofisi nyingine nitazipangisha hivyo muda mwingi nitakuwa na communicate na watu.Ikifika muda nikawa mzee sana kiasi Cha kushindwa kutoka hata nje ya nyumba basi watoto wangu itabidi wabebe jukumu la kujua nitaishije maana nitakuwa nimepoteza nguvu na uwezo wa kufikiri.
Ukiwa na familia na ukawaza kwa mapana hayo mambo lazima uyaone.mfano mm nimeshajua chanzo Cha kwa nn watoto wa kiume huwatelekeza wazazi wao wa kiume na kumjali mama yao.wakipiga cm inaanzia kwa mama kwanza .nikajiuliza kama mm nafanya hv Ina maana na mm nitafanyiwa na watoto wangu.hvyo nilibadilisha mfumo wa maisha kuwa rafiki wa watoto wangu na kuwatekelezea mahitaji Yao kalibu 80% nawapatia mm mwenyewe Moja kwa Moja sio kumpatia mama Yao.
 
Solution ni kuchelewa kuzaa mtoto wa mwisho ,au kuchukua wajukuu kuishi nao au watoto wa ndugu ,pia watoto hata kama wameshakua na familia zao wajitahidi kua karibu na wazazi wao ikiwemo kwenda kuwatembelea mara kwa mara hata kuwajulia hali pia inasaidia kuwaondolea upweke.

Ni kweli upweke upo kukaa bila uzao wako karibu,ndio mana ndoa inayokosa mtoto lazima iwe na migogoro sababu ya upweke ,watoto wanasaidia kuchangamsha nyumba.
 
Somesha ila zaa katika interval fulani itakayokufanya muishi na katoto kenu ka mwisho muda mrefu mpaka kufikia kaoe mnakuwa mmeshafariki
[emoji23][emoji23] mawazo hayo mda huo yanatoka wapi, ? Mnakua mnawaza kuzaa tu
 
Tena nyinyi wazazi wa kizazi hiki ambao watoto wenu mnawapeleka wakakulie kwenye vituo vya Day Care kisa nyie mpo busy kutafuta pesa ndio mjipange kisawasawa. Msipojipanga vizuri na wao lazima wawapeleke kwenye elderly centers.
Ndio janga lijalo!
 
Hii ni akili ya kitoto sana.upendo unazidi kushuka siku zinavyozidi.ilawewe ukiugua na kuwa kilema kabisa ukafilisika unataka mzazi aendelee kukulea mpaka kifo chako?
Kwanza kabisa, umewanyanyapaa watoto kwa kauli yako "hii ni akili ya kitoto sana".

Watoto mara nyingine wana mawazo mazuri sana, mpaka hapo umejionesha unaishi kwa kukariri.

Upendo ni pamoja na kujua kwamba watoto nao wana maisha yao na hawakuzaliwa ili kutumikia wazazi wao.

Kila mtu anatakiwa ajiandae kujitosheleza kwa maisha ya uzeeni, familia iwe na option ya kumsaidia au kutomsaidia.

Hizi habari za kuzaa kama investment ili watoto wakusaidie baadaye, kwa hali ama mali, ni mfumo wa ujima.

Kwa sababu, inawezekana kabisa mtoto wako akatangulia kufa kabla yako.

Sasa mtoto akifa kabla yako atakuhudumiaje uzeeni?

Watu wa familia waachiane uhuru, bila kunyanyapaa mtu.

Mtu akitaka kusaidia wazazi, sawa. Mtu asipokuwa na uwezo wa kusaidia wazazi, sawa. Mtu akiwa na uwezo wa kusaidia wazazi halafu asisaidie, sawa.

Watu wasaidiane kwa sababu wanataka kusaidiana, si kwa sababu kuna wajibu, au kwa sababu wanalipa fadhila za kulelewa na wazazi, au wanaweka kitegauchumi kwa watoto ili waje wawasaidie baadaye.

Hiyo ni biashara, hiyo si familia.
 
Yasije yakatokea kama yale ya Arusha......mzee kafungiwa ndani, hapewi chakula siku nyingi, mpaka kaanza kula haja yake. Yote hiyo mtoto anataka kurithi. Anyway, yote ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu.
 
Wazazi wengi, wanajitahidi sana kusomesha watoto wao ili huko mbeleni wawe na maisha mazuri au wasiwe tegemezi.

Watoto wakishahitimu, uanzisha maisha yao, kwa kujitegemea pamoja na kuwa mbali na wazazi wao; wakuoa wataoa, na wakuolewa wataolewa.

Changamoto inayojitokeza, ni wazazi kubaki wenyewe, na kukosa watu wa kuwafariji pale wanapohitaji faraja. Wengi hubaki na vijana wakazi, ambao kwa namna moja au nyingine hawawezi kuumaliza msongo wa mawazo wa wahusika.

Uzee ni umri unaohitaji kuwa karibu sana na uzao wako, kwa kufurahi pamoja na kupeana faraja; ingawa wazee wengi hawapati hiyo fursa kutokana na uzao wao kuwa mbali nao, hii inawapelekea kujutia uzao wao.

Wenzetu wa Asia wamejaribu kudhibiti hii hali, kwa kuishi na uzao wao kwenye boma moja, lengo kuu ni kudhibiti hali ya upweke huko uzeeni.​

Karibuni wakuu, kwa maoni.
Labda uchelewe kuzaa ndio utaishi na watoto mpk uzeeni wako karibu
 
Yasije yakatokea kama yale ya Arusha......mzee kafungiwa ndani, hapewi chakula siku nyingi, mpaka kaanza kula haja yake. Yote hiyo mtoto anataka kurithi. Anyway, yote ni majaliwa ya Mwenyezi Mungu.
Kwani watoto si ni baraka?🤣au imekuaje tena?
 
Kuhitaji mtoto akufariji ni kukosa kujipanga vizuri katika maisha.

Umeshindwa kujiwekea akiba ya uzeeni? umeshindwa kujipanga kupata mwenza wa kuwa naye uzeeni?

Unazaa mtoto, unamsomesha, anakua mkubwa, na yeye inakuwa zamu yake ya kuzaa na kusomesha akipenda. Mwache naye aishi maisha yake, akiamua kusaidia wazazi sawa, akiamua kuwa busy na maisha yake sawa.

Wewe baba au mama unayehitaji sana mtoto wako aache ku focus kwenye familia anayoianzisha, halafu a focus sana kwako wewe mzazi, ni mbinafsi na umeshindwa kujipanga na maisha yako mwenyewe ya uzeeni.

Nimeona hii tabia ya wazazi kuwatumia watoto wao kama mbadala wa mfumo wa mafao ya uzeeni, au wazazi kudai matunzo uzeeni kwa sababi waliwalea watoto wakiwa wadogo. Huu ni ubinafsi wa hali ya juu.
Mbona hujamuelewa Kiranga? Yeye kaongelea upweke na faraja, hayo mambo yakunipanga sijui nini....
umeleta wewe na hii inapaswa kuwa maada nyingine. Ukiweza anzisha.
 
Mbona hujamuelewa Kiranga? Yeye kaongelea upweke na faraja, hayo mambo yakunipanga sijui nini....
umeleta wewe na hii inapaswa kuwa maada nyingine. Ukiweza anzisha.
Hata hayo ya upweke na faraja mbona nimeyaandika, hujasoma?

Na upweke ni matokeo ya kushindwa kuwa na hobby, mwenza, marafiki.
Ni tatizo unalolisababisha wewe mwenyewe unayejisikia upweke.

Sasa utasemaje upweke utenganishwe na kushindwa kujipangia maisha vizuri?

Mtu aliyejipangia maisha yake vizuri atakuwa na tatizo la kuwa na marafiki wengi, kuwa anatafutwa na watu wengi, kuwa ana hobby nyingi, kuwa ana mambo mengi ya kufanya,.

Yani, mtu huyu tatizo lake litakuwa ni kuchagua afanye nini, aonane na nani, aende wapi, ili awe productive zaidi, ili apumzike zaidi.

Mtu huyu hawezi kuwa na tatizo la upweke.

Watu wengi wanapata tatizo la upweke kwa sababu hawajui kupanga maisha yao ya uzeeni yatakuwaje.

Mtu anayejua kupanga maisha yake hata akiumwa vibaya na akiwa hana uwezo, hawezi kuwa na upweke, atapambana au kukubali hali yake tu kwa kuelewa "the human condition".

Sio kusumbua watu wengine kwa upweke wake.
 
Ukimfuatilia mtoa mada, unaweza kuishi na wanao kama mifugo.

Wasisome shule, wakae nawe nyumbani mnatizamana mpaka unakuwa mzee, ili uwatumie kama vitu vya kukufariji usiwe mpweke.

Yani kama unafuga ng'ombe ili upate maziwa au nyama!

What a selfish and medieval way of thinking.
 
Back
Top Bottom