Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Barua ya kujiuzuku kumnusuru bosi na maswahiba utaiandikaje?
Rais A.H Mwinyi alipoandika barua kutokana na mauaji ya Watu hakuwa na kosa. Mwinyi hakuagiza wala hakuwa na ufahamu wa kilichotokea. Katika kuonyesha kwamba serikali inajali alijiuzulu.
Kujiuzulu kwa mwinyi kulimuondolea Rais mzigo kwasababu kinyume chake ingalikuwa tabu.
Barua inaandikwaje? Soma barua ya A.H. Ipo mtandaoni.
Hata ukisema "mimi sina makosa, ila najiuzulu kwa kuinusuru serikali kutoka kwenye matatizo yanayohusiana na mimi kuwapo serikalini" tayari unanuka, tayari umejiweka katika matatizo ya kukufanya uwe untenable. Kuna calculations fulani umekosea hapo.
Hapana , ndiyo maana A.H. Mwinyi alirudi na kuwa Rais wa Zanzibar na Tanzania chini ya Uongozi ulioshuhudia anguko lake. Timu nzima ya kupitisha majina akiwemo RC wa Shinyanga Peter Kisumo ilikuwa ile ile.
Walijua hakutenda, aliwajibika.
Caesar's wife must be above suspicion.
I agreed
Kuhusu Kikwete.
Kwanza kabisa mna uhakika gani Kikwete alikata jina la Lowassa? Kwa uamuzi wake tu. Hizi habari zina uhakiki gani? Was Kijwete realky that powerful?
Kuna habari kutoka kwa 'privy' na mtando mzima. Kumbuka mtandao ulikuwa na watu wengi
Habari zinatoka ''horse's mouth'

Kuna circumstancial evidence pia kuhusu nguvu ya Kikwete
Rais SSH anasema wakati wanachagua nani awe VP baada ya Magufuli kuteuliwa, kamati kuu iliitwa.

Rais Samia anasema, ''sisi tulikaa nje tukinywa chai na biskuti wakati vingunge wameingia na kujifungia' Vingunge si Kamati kuu ni JK na watu wachache sana. Maana yake ni kwamna hata CC haikuwa na nguvu

Pili, unakumbuka ' ...Tunaimani na Lowassa''. Ilikuwa dhahiri wajumbe wa NEC walikuwa na taarifa za nini kimetoke.
Magufuli akathibitisha kwa kusema ''.... walioimba ningewatimua siku hiyo' akionyesha nguvu ya Mwenyekiti.

Tatu, mwaka 1995 Mkapa alipomshinda JK, ilisemwa kura ''hazikutosha'. hii ilikuwa lugha laini tu, tunajua Mwenyekiti wakati huo akiwa na Nyerere walimtaka Mkapa. Unaweza kuona nguvu ya Mwenyekiti kama Kikwete

Nne, Mkapa anathibitisha alitumwa na Nyerere kwenda kwa mzee Kitwana Kondo. Nyerere ndiye alimshawishi achukue Form, tunajua the rest is history
Pili,

Chama kinapeleka vipi mbele jina la mtu aliyejiuzulu kwa kashfa kubwa ya rushwa na kutoa angalau optics kwamba ama ameshiriki moja kwa moja katika hiyo rushwa, ama ameshindea kusimamaia wizara rushwa hiyo isitokee?

Yani chama badala ya kujikita kwenye ilani na kampeni, kianze kumsafisha mgombea na ku explain kwa nini mgombea alijiuzulu, huku wapinzani wakimpiga mawe kwamba huyu ni mla rushwa aliwahi mpaka kujiuzulu kwa rushwa?

Kwa nini chama kichague mgombea huyo wakati kina wagombea wengine ambao hawana wingu hilo la kashfa ya rushwa na wanaweza kuanza kampeni moja kwa moja bila kuhitaji kusafishwa?
Hapa ndipo pana hoja nzuri sana. Suala ninaloongelea si kukubalika au kutokubalika kwa Lowassa.
Wala siongelei na sikubali kuwa alidhulumiwa Urais.

Ninachosema hapa ni kwamba alidhulumiwa taratibu. Chama kina sifa za mgombea na zinajulikana.
Ikiwa ENL alikuwa hana sifa, Chama kilimpa vipi Form ya kugombea? Chama kiliridhika alikuwa na sifa!

Pili, taratibu zinasema mwenye kura nyingi atasonga mbele. Iwe Kikwete au kundi lote liliondoa jina lake si kwa kukosa kura bali kwa fikra zao, hiyo ni dhuluma. Kikwete au kundi hilo wangemzuia kwa kukosa sifa, na kwa kukosa kura. Kukata jina lake kwa utashi na si taratibu ni dhuluma

Nipo kwenye rekodi, sijawahi kumkubali ENL na hata juzi niliandika machache mazuri na mengi mabaya yake.
Hata hivyo hatuwezi kuacha kusema dhulma aliyofanyiwa! na katikati ya dhulma yupo Kikwete in so many ways.
 
Kupanic ni nini? Unahakikishaje hapa mtu ka panic na hapa anaandika kwa passion tu hajapanic?

Unajuaje wewe unapoona mtu ka panic, mwenzako hajapiga chafya tu kwa reflex action ila wewe nyoronyoro unaona amepanic?

Nimepanic vipi, wapi, kwa sababu gani, unajuaje nimepanic na si wewe uliye panic kusema nime panic?

How do you know you meet the requisite wattage to make me panic and that you are not just flattering yourself by thinking that you could make me panic?

Tutajuaje kuwa hutumii gia ya kuniambia "umepanic" kukimbia mazungumzo haya na kukimbia kujibu hoja na maswali nilliyoyaleta?

Mtu yeyote anayetaka kukimbia maswali anaweza kusema "Umepanic". Kwa nini tusikuchukulie kama mtu anayekimbia maswali kwa gia ya kusema "umepanic"?

You rest your case? Do you even know what a case is?
Nimehakikisha kwasababu umeandika kwa kukosea grammar kulikojirudia zaidi ya mara moja. No editing at all.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Rais A.H Mwinyi alipoandika barua kutokana na mauaji ya Watu hakuwa na kosa. Mwinyi hakuagiza wala hakuwa na ufahamu wa kilichotokea. Katika kuonyesha kwamba serikali inajali alijiuzulu.
Kujiuzulu kwa mwinyi kulimuondolea Rais mzigo kwasababu kinyume chake ingalikuwa tabu.
Barua inaandikwaje? Soma barua ya A.H. Ipo mtandaoni.

Hapana , ndiyo maana A.H. Mwinyi alirudi na kuwa Rais wa Zanzibar na Tanzania chini ya Uongozi ulioshuhudia anguko lake. Timu nzima ya kupitisha majina akiwemo RC wa Shinyanga Peter Kisumo ilikuwa ile ile.
Walijua hakutenda, aliwajibika.

I agreed

Kuna habari kutoka kwa 'privy' na mtando mzima. Kumbuka mtandao ulikuwa na watu wengi ''horse's mouth'
Kuna circumstancial evidence pia kuhusu nguvu ya Kikwete

Rais SSH anasema wakati wanachagua nani awe VP baada ya Magufuli, kamati kuu iliitwa. Rais Samia anasema, ''sisi tukaa nje tukinywa chai na biskuti wakati vingunge wameingia na kujifungia' Vingunge si Kamati kuu ni JK na watu wachache sana. Maana yake ni kwamna hata CC haikuwa na nguvu

Pili, unakumbuka ' ...Tunaimani na Lowassa''. Ilikuwa dhahiri wajumbe wa NEC walikuwa na taarifa za nini kimetoke.
Magufuli akathibitisha kwa kusema ''.... walioimba ningewatimua siku hiyo' akionyesha nguvu ya Mwenyekiti.

Tatu, mwaka 1995 Mkapa alipomshinda JK, ilisemwa kura ''hazikutosha'. hii ilikuwa lugha laini tu, tunajua Mwenyekiti wakati huo akiwa na Nyerere walimtaka Mkapa. Unaweza kuona nguvu ya Mwenyekiti kama Kikwete





Hapa ndipo pana hoja nzuri sana. Suala ninaloongelea si kukubalika au kutokubalika kwa Lowassa.
Wala siongelei na sikubali kuwa alidhulumiwa Urais.

Ninachosema hapa ni kwamba alidhulumiwa taratibu. Chama kina sifa za mgombea na zinajulikana.
Ikiwa ENL alikuwa hana sifa, Chama kilimpa vipi Form ya kugombea? Chama kiliridhika alikuwa na sifa!

Pili, taratibu zinasema mwenye kura nyingi atasonga mbele. Iwe Kikwete au kundi lote liliondoa jina lake si kwa kukosa kura bali kwa fikra zao, hiyo ni dhuluma. Kikwete au kundi hilo wangemzuia kwa kukosa sifa, na kwa kukosa kura. Kukata jina lake kwa utashi na si taratibu ni dhuluma

Nipo kwenye rekosi, sijawahi kumkubali ENL na hata juzi niliandika machache mazuri na mengi mabaya yake.
Hata hivyo hatuwezi kuacha kusema dhulma aliyofanyiwa! na katikati ya dhulma yupo Kikwete in so many ways.
Haya mengi tumeyagusia awali kwenye uzi

Inaonekana mfumo mzima wa kuteua mgombea CCM una usiri na matatizo mengi.

Ndiyo maana kuna habari hata Kikwete alikuwa victim wa mifumo hii 1995.

Mfumo ni opaque kiasi kwamba ni vigumu kumlaumu Kikwete beyond reasonable doubt, hapa tunapata maneno mengi ya hearsay na innuendo.

Kwangu mimi, the bottom line ni kwamba, Lowassa, kwa kukubali kujiuzulu, alikuwa amejitengenezea doa la narrative kwamba yeye ni mla rushwa kukubalika.

Hii ilikuwa ni "shooting oneself in the foot before starting a marathon".Especially kwenye nfumo wa ki sniper ambao hauna fairness na watu wanaweza kukatana kirahisi. Kama aliona hana kosa angekomaa tu mpaka aondolewe uwaziri mkuu na ku pull a Mrema on them kwa kutumia kuondolewa huko.

By resigning, he took the wind out of his sails himself.
 
Nimehakikisha kwasababu umeandika kwa kukosea grammar kulikojirudia zaidi ya mara moja. No editing at all.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

That's all? Mtu akikosea kuandika tu, ka panic?

Watu hawakosei kwa kuandika kwa kasi kwenye simu?

Mtu akiandika kwa kasi kwenye simu ka panic?

You are making a dictionary logical fallacy here.

Kukosea grammar au kukosea spelling?

Mimi nakosea spelling kila post na narudia ku edit. Natumia simu.

Kama unataka kuwa secretary wangu kunionesha wapi nimekosea, karibu.
 
That's all? Mtu akikosea kuandika tu, ka panic?

Watu hawakosei kwa kuandika kwa kasi kwenye simu?

Mtu akiandika kwa kasi kwenye simu ka panic?

You are making a dictionary logical fallacy here.

Kukosea grammar au kukosea spelling?

Mimi nakosea spelling kila post na narudia ku edit. Natumia simu.

Kama unataka kuwa secretary wangu kunionesha wapi nimekosea, karibu.
Sasa mbona kwangu hukurudia ku edit? Hata nami naandika kwa simu but sikosei mara nyingi kama ilivyo kwako.

Mimi ni mkulima, sijasomea secretarial course. Anyway, endelea na wengine.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Sasa mbona kwangu hukurudia ku edit? Hata nami naandika kwa simu but sikosei mara nyingi kama ilivyo kwako.

Anyway, endelea na wengine.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Ninekuuliza wapi? Hujaonesha.

Inawezekana wewe hu interact na watu wengi kama mimi, hivyo kumsahau mtu si rahisi.

Inawezekana mimi na interact na watu wengi sana, hivyo, kukusahau mtu kama wewe ni rahisi.

Naona umeshindwa hoja, unakosoa muandiko, na hata huo muandiko hujaonesha wapi.
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Hata salimu ahamed salimu naye atasema alidhulumiwa Haki yake. Uongozi unatoka kwa Mungu na siyo kwa Mwanadamu. Hakuna mwenye haki miliki ya Urais wa nchi hii wala wakusema kuwa mimi ndiye nilistahili kuwa Rais wakati fulani. Huo ni ujinga na utoto. Mtoa mada najuwa hajakomaa akili na anaandika kwa kutumia hisia za uvyama badala ya kuwaza nje ya boksi.
 
Hayo mambo ya kuwa Rais kwa kupitia urafiki wao, siyo hoja ya msingi. Hoja ya msingi, ni roho ya dhuluma aliyo nayo Kikwete.

Hata kama tukisema kuwa Lowasa alipojiuzulu ilimkera Kikwete, lakini kwa nini Kikwete aamue kudhulumu haki yake? Alitumia madaraka yake kulikata jina la Lowasa licha ya kwamba wajumbe wengi na wanachama wengi wa CCM walikuwa wakimtaka Lowasa.

Hiyo haitoshi, umemkata jina kwenye chama ambacho wewe ni mwenyekiti wake, ameondoka, amepigiwa kura na wananchi, ameshinda uchaguzi, bado unadhulumu umma wote wa Watanzania kuongozwa na mtu waliyemtaka. Hivi wewe ni mtu wa namna gani? Zanzibar nako akamtumia Jecha kudhulumu haki ya Maalim Seif. Halafu leo, kwa unafiki mkubwa anasema eti marehemu aliendelea kuwa rafiki yake siku zote. Wewe unayaamini hayo?
Acha umbumbumbu wako. Unaposema alishinda ni alishinda katika uchaguzi upi na kwa ushahidi upi? Tatizo umeandika mada kwa kutumia hisia badala ya kutumia akili.
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
kama hujui historia nyamaza ile ndege ya kwenda dodoma ililipwa na rostam aziz,pia unajua wizi ambao marehemu aliufanya?
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Magufuli aliko kwenye tanuru la moto wa mkaa wa mawe
 
Lowassa na Rostam Azizi wlitaka kufanya ujanja...wakashindwa kujua kuwa Jakaya ni mtoto wa mjini. Akapindua meza. The rest is known.

Ngosha Mzilamkende akaona Jakaya boya...akamsogeza Lowassa, naye akamleta Rostam Azizi. Ngosha akajenga urafiki na wahuni wamualika kuzindua kiwanda pale Morogoro. Haikupita mwezi, tukatangaziwa msiba!
 
Ninekuuliza wapi? Hujaonesha.

Inawezekana wewe hu interact na watu wengi kama mimi, hivyo kumsahau mtu si rahisi.

Inawezekana mimi na interact na watu wengi sana, hivyo, kukusahau mtu kama wewe ni rahisi.

Naona umeshindwa hoja, unakosoa muandiko, na hata huo muandiko hujaonesha wapi.
Au ulikuja ku edit baada yangu kukujibu, basi mimi nilipoona tu yale makosa yako ya kiuandishi na kukujibu sikurudi tena kule juu kutazama maendeleo yako, nikaendelea na maisha mengine.

Hapa hoja wala sio tatizo, tatizo nilipokusoma kwa namna ulivyoandika nikaona huyu mtu kama ningekuwa karibu yake angenichapa makofi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
CCM Wana taratibu zao na yeye ndio alikuwa mwenyekiti wa hicho kikao, kilichomkataa EL ni taratibu za CCM wenyewe ndani ya vikao vyao sio JK.

toka 1995 ninasikia upinzani umeshinda na umeibiwa kura, Watanzania wengi bado ni wajinga ndio maana CCM inashinda maana wengi wanaamini katika CCM. 2015 binafsi nikipiga kura Kwa mara ya kwanza na kura yangu ilienda kwa JPM maana niliamini kwa JPM na ilivyokuwa kwa Watanzania wengi 2015 madai yako EL alishinda na kuconclude alidhulumiwa hayana mashiko zaidi ya "hearsay" maana hakuna chombo huru kilichothibisha hili.
Acha uongo kikwete alikuja na majina kwenye mfuko wa shati mpaka nchimbi na sophia simba wakamwambia kikwete sio utaratibu inaonekana ulikua mdogo sana 2015
 
Sasa, kama Lowassa alimwambia Kikwete anataka kujiuzulu, Kikwete akakataa, lakini Lowassa akalazimisha kujiuzulu, huoni Lowassa kajitakia mwenyewe kupigwa chini kwa kulazimisha kujiuzulu?

Ulitegemea vipi Kikwete aendelee ku support mbio za Urais za Lowassa baada ya Lowassa mwenyewe kulazimisha kujiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond?

Yani ulitaka Kikwete ampigie kampeni ya urais Lowassa aliyeshindwa Uwaziri Mkuu kwa kashfa?

Huoni kwamba Lowassa ndiye aliyemsaliti Kikwete hapo kwa kulazimisha kujiuzulu na kumuachia manyanga Kikwete, wakati labda alihitajika kupambana akiwa upande wa serikali?

Mtu aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu kutokana na msukosuko wa kashfa, unajuaje akipata urais na kupata msukosuko wa kashfa hatajiuzulu tena?

Lowassa alipewa mtihani wa uongozi, akashindwa. Kikwete akaona huyu kashindwa, twende na wengine.

Hata mimi ningemshangaa sana Kikwete kama angempigia kampeni Lowassa kwa sababu ni rafiki yake tu.
Naona tunajichanganya tu, mkasa mzima wa Richmond ulishawekwa hapa JF kitambo nabulieleza mkasa mzima jinsi BT alivyousuka nanjumba bovu kumwangikia ENL. Sidhani kama aliomba nadhani mshambulizi yalimzidi ikabidi abwage manyanga. Akasema tatizo ni 'PM. PPP ENL
 
Back
Top Bottom