Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Changamoto kubwa ninayoiona binafsi siyo kuunganisha mitaji."Tunaungana kufanya nini? " This is Critical question we need to have its answer before we do anything!

Tukisoma maelezo yanaeleweka kiurahisi shida itakuja kwenye operation mtu kuweka pesa yake afu angojee 30% ya faida yake siyo kesi. Huu ni sawa na mfumo wa HISA tuwe makini je, tunawekeza wapi na nani watasimamia hii business? Na je, tunaelewa mfumo wa uendeshaji wa pesa na sheria zake. Isije kuishia kuwa DESI.
 
Hii nimeipenda sana, Nina mpango wa kuanza hii biashara hapa Morogoro.
Vp mkuu ulishaanza
Kwanza Weka Aibu Pembeni Maana Itakurudisha Nyuma. Angalia kama Upo Jirani na Shule, Vyuo au Njia Ambazo watu huwa wanapita au kukusanyika kwa Wingi. Fanya Mpango uwe Freelancer wa Mitandao yote ya cm, uwe una kazi ya kusajili line, kutengeneza special number, ku renew line, kuuza vocha n.k.

fight upate mwamvuli mf wa voda, chonga meza ya mbao ya kishkaji na kiti cha mbao, au kama vipo home vifanye viwe vya ofisi .

Ongea na Muuza magazeti jirani na wewe, akufanyie mpango nawe uwe wakala, tengeneza stand ya wavu ya chuma ambayo kwa ubavuni na juu kidogo utaweza kutenga eneo la kuweka pipi, biskuits, karanga, hankerchiefs, pen n.k

Tafuta Deli, tengeneza Maji na Juice za kupima, weka na barafu uwe unafaya biashara zako eidha jiran na maeneo ya njia panda, karibu na shule/vyuo, jirani na maeneo ya sokoni au kwenye mikusanyiko ya watu. Pia waweza omba nafasi mbele ya duka mfano la nguo ukaweka biashara yako huku ukawa unamlipa 500-1000 mwenye frem kila siku.

hapo nimekadiria upo home, friji lipo, blender, kiti meza pia unaweza vitoa home. otherwise gharama za mtaji zinaweza fika hata laki 2 au 3.

Mm nimewaza hayo, Mengine utajiongeza mwenyewe depending na mazingira uliopo. Kila la kheri.
 
Mi naona kama upo dar (namzungumzia huyo Dada wa miaka 24) kutembeza/kuuza shanga na hereni kwa akina mama. Inalipa sana. Dadangu aliwahi kuifanya na ikampa pesa za kunisomesha kidato cha 5&6 private school. Ukiwa na aibu hutaifanya
 
Ndio maana nataka kujua ni biashara zipi zinazowezekana kwa hio hela ili nichague
Kuuza karanga, kuuza maji barabarani, kuuza vocha stendi ya mabasi, kufungua genge la vitu mvhanganyiko stendi, biashara za mtaji huo ni nyingi sana, suala ni wewe tu kuamua na kusnzs
 
nitafanyia kazi wazo lako
na vipi bei naweza nikapata kwa sh ngapi
Hili swali limetia najisi kabisa hata biashara unayotaka kufanya. Kilichotakiwa ni ww kuuliza maeneo ya kufungia mzigo sio bei. Bei ni ww kufanya survey na kuomba punguzo.
 
Kua muwazi ni jambo Jema dogo, ila sasa yakupasa kueka wazi details like uko wapi,mjini au kijijini? Unapoishi ni kwako au umepanga? Hii itatusaidia kukushaur ww.

Kwa mfano uko kijijini na unaishi kwenu na Kuna eneo ambalo unaeza fuga kuku wa kienyeji huku unafanya shughuli nyingine kupata pesa ya kuwalishia kuku.

Kama uko mjini let's say Dar, unaeza tafuta kakijiwe ukaanza kukaanga chips kwa Huo mtaji Mdogo ulionao, unaeka chips na unadamka asbh unaanza kukaanga mihogo kwa ajili ya breakfast, saa nne tunaanza menya viazi kiasi kwamba saa tano chips tayar.

Kua msafi na wajali Wateja, naamini hadi umejiunga Jf Basi hata kama hujasoma sana lkn una uelewa mkubwa. Tumia akili yako kua mbunifu.

Katika kufanya yote usimwangalie mtu au kuwaza fulani atakuonaje, cha msingi zingatia unataka Kufika wapi.

Kukutia moyo tu, mm nlishauza chips nkiwa na degree moja lengo likiwa kupata mtaji wa kufungua kampuni ya ujenzi, nliuza for only one year huku nikilima na kufuga broilers ambao pia Nlikua nkiwakaanga hadi Miguu na vichwa vyao (vigondi) na kukamua utumbo wa kuku bila aibu, nliwauza masista duh na braza men kibao bila kujali tena kwa kuwaheshimu.

Boda Boda na dereva bajaji walikua wakiniagiza na kuntumikisha Lakini nliwaheshimu kwasababu ni Wateja, ktk kufanya hiyo kazi sikuwahi kuiwazia degree yangu hata chembe zaid ya kuwazia nataka Kufika wapi.

Baada ya mwaka mmoja nlianza usajili wa kampuni na baadae Mungu akanjalia nkavuna alizeti gunia 156 nkauza kila gunia elfu 54.

Nlitamani niendlee na chips Lakini nkaona hapana ngoja nkaitendee Haki ile degree. Ila kulima sijaacha had wa leo. Namshukuru Mungu ya Jana Si ya Leo.

Nimekupa kidogo tu ili usife moyo na uamini kila kitu kinaezekana
Mkuu, kwasasa umejiajiri au umeajiriwa??
 
Tengeneza kipato cha Ziada Kwa kupata kitabu maalumu kitakacho kufanya ujue kutengeneza bidhaa mbali mbali muhimu za viwamdani nyumbani kwako na uweze kujiajiri. Kitabu hicho utakipata Kwa bei ya TSh.5,000 tu! Katika email au whatsup yako. Nipigie au whatsup 0762208190 AU 0718978295. Utachagua unacho taka kujiajiri kitaalam kupitia kitabu hicho.
Nahitaji icho kitabu 0718459870
 
Habari za humu
Naomba msaada wa mawazo nipo kijijin na nataka nianze biashara na nina mtaji wa laki tano je naweza kufanya biashara gan????? MAJIBU PLIZ
 
Kwanza Weka Aibu Pembeni Maana Itakurudisha Nyuma. Angalia kama Upo Jirani na Shule, Vyuo au Njia Ambazo watu huwa wanapita au kukusanyika kwa Wingi. Fanya Mpango uwe Freelancer wa Mitandao yote ya cm, uwe una kazi ya kusajili line, kutengeneza special number, ku renew line, kuuza vocha n.k.

fight upate mwamvuli mf wa voda, chonga meza ya mbao ya kishkaji na kiti cha mbao, au kama vipo home vifanye viwe vya ofisi .

Ongea na Muuza magazeti jirani na wewe, akufanyie mpango nawe uwe wakala, tengeneza stand ya wavu ya chuma ambayo kwa ubavuni na juu kidogo utaweza kutenga eneo la kuweka pipi, biskuits, karanga, hankerchiefs, pen n.k

Tafuta Deli, tengeneza Maji na Juice za kupima, weka na barafu uwe unafaya biashara zako eidha jiran na maeneo ya njia panda, karibu na shule/vyuo, jirani na maeneo ya sokoni au kwenye mikusanyiko ya watu. Pia waweza omba nafasi mbele ya duka mfano la nguo ukaweka biashara yako huku ukawa unamlipa 500-1000 mwenye frem kila siku.

hapo nimekadiria upo home, friji lipo, blender, kiti meza pia unaweza vitoa home. otherwise gharama za mtaji zinaweza fika hata laki 2 au 3.

Mm nimewaza hayo, Mengine utajiongeza mwenyewe depending na mazingira uliopo. Kila la kheri.
mi pia nimejifunza kitu asee
 
Back
Top Bottom