Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

habar za midaa hii wana jamvi?
Nimeona nyuzi nyingi zikiwa na maswali mengi yakiusiana na BIASHARA GANI ZA KUFANYA KWA MTAJI MDOGO..
Bhaaaasi kwa wale wabishi,wavumilivu na wasiokata tamaa,msio ogopa biashara za kudharaulika angalau tunaeza peana mwanga jinsi ya pa kuanzia.

Kwa kifupi mimi ni kijana wa miaka 29 nimezaliwa kwenye maisha ya kishuani huko Arusha ila nilifukuzwaga nyumbani toka 2006.Hapo ndo nilipopata changamoto za kufanya biashara za mitaji midogo.
Katika biashara nilizowai kufanya zote nilifanikiwa.

AINA ZA BIASHARA
1:KULENGA NGUO ZA KIKE KUUZA VYUONI
2:KUUZA PIPI,MAJI YA KANDOROO NA SIGARA(Nyakati maalum)
3:MATOFALI YA KUCHOMA
4:KUUZA DAGAA LA KUOSHA
5:BANDA LA CHIPSI
6😛LAYSTATION(KUCHEZESHA MAGEMU)

Nyingine nashindwa kuziorodhesha kutokana na kupitwa na wakati.
Sitaweza kuchambua zote ila nitaanza kuchambua moja kwa sasa.

JE WEWE UNAWEZA KUUZA PIPI,MAJI YA KUFUNGA(Kandoroo enzi zile) NA SIGARA KIPINDI CHA SABA SABA AU NANE NANE?(SIKU 7/8 ZA MAFANIKIO)
Nilipewa wazo toka kwa house boy aliyefukuzwa hom miaka mingi.lilikua wazo gumu kwangu tokana na maisha niliyokulia ila nilijikaza nikafanya.

NILIANZA NA MTAJI WA ELFU 70(MOROGORO)
niliazima meza mbili kwa ajili ya kuwekea pipi,nilikodisha ice box mbili kwa ajili ya barafu,nilinunua ndo 8 za maji,nililipa kitambulisho cha mfanya biashara ili kupunguza gharama za kulipa kila nikiingia langoni mwa uwanja wa nane nane.

Nilinunua vifuko vya kufungia maji vya kutosha.nilinunua chujio kubwa. katika hii biashara maji ndo yalinipa pesa nyingi
Ndoo ya maji sh 100

Sikumbuki mahesabu yote kwa uhakika ila siku ya kwanza niliuza maji elfu 9 ikiwa kandoro moja ni tsh 50 wakati biashara ya pipi na sigara ikisua sua,siku ya pili niliuza maji ya elfu 12 biashara ilienda vizuri lakini ugumu maji yaliisha sikua na uwezo wa kufunga huku nikiuza biashara ya pipi.jion yake nikamualika mshikaj(house boy)usiku tukafunga maji mengi sana.siku ya tatu tuliuza elfu 24.

JION YA SIKU YA 3
Nilipata moyo sana nikaanza kuona faida ya biashara niliyokua naidharau.
Basi tukapata wazo la kuwaajiri vijana wanne kutoka kitaa usiku tunafunga maji.asubuh mpaka jion tunafanya biashara ya kuuza tu.pamoja na kufunga maji mengi sana.biashara ya pipi na sigara nayo ikachanganya sana.

Hakika mpaka inafika tarehe 5 tulikua tunauza mpaka maji laki mwaka huo Mungu alijalia jua lilikua la maana.maajabu ni tarehe sita saa 6 mchana maji yote yameisha na watu wanataka tuwauzie hata kwa glasi. Hapo ndo tulipopiga pesa wadau. Zile cooler box zilikua na kitu kama kabomba. Tukazijaza maji na barafu tukanunua na vikombe 10.

Sisi kazi yetu ilikua ni kujaza barafu na maji tu.kila glas ya maji sh 100. Uongo dhambi kama kuibiana lazima siku hiyo niliibiwa sana ila sikujali. Usiku wa tarehe nane tulilewa sana na vijana wangu.asubuh ya tarehe 9. Ndio nikapiga mahesabu nimebaki na laki 8.

Nikagawa laki 2 nikabaki na sita. Pipi zilizobaki nikaziuza kwa bei ya jumla kwa muuza duka elfu 50 tukasambaratika tarehe 10.

Nia ni kutaka kukutia moyo kama kweli unania. Pia changamoto zilikua ni nyingi sana. Mfano sehemu ya kupanga meza zilikuwa zinapangishwa kwa zaidi ya mtu mmoja. Mwenye nguvu ndiye anafanya biashara.
Nawasilisha
 
nimependa sana kujituma kwako...vipi kuhusu hii biashara ya playstation mkuu,inatoa kweli?
 
Habari!

Hii ni mahususi kwa wale wanaohitaji kufanya biashara, sio wanaofanya biashara.
Njia panda,mahala salama pa kutafakari upande upi uelekee ama uufate. Nimechagua leo kushare nanyi ndugu zangu kwa kile kidogo, na kesho siku yakuanza mfungo ianze vema.

Haihitaji shule kufanya hili, inahitaji dhamira, kuamka na kufanya. Waweza kuwa na mapesa mengi ama kidogo sana..

(1) Tafuta laki 3 TU ama ukiwa na pesa zaidi sio mbaya, ni nzuri zaidi.

(2) Tafuta simu ya android, hata window phones poa

(3) Tenga muda wa kutembelea mitandao hii:

a.AliExpress.com - Online Shopping for Electronics, Fashion, Home & Garden, Toys & Sports, Automobiles from China.

b.Manufacturers, Suppliers, Exporters & Importers from the world's largest online B2B marketplace-Alibaba.com

c.ebay.com

NB: Hapa masoko ya kwenye mitandao ni miiingi sana lakini for beginners anzia hapa, 1 step at a time, pia apa hakikisha unaspend almost siku 14 kuipitia hii mitandao kwa kina, usijipe moyo kwa siku moja tu kwamba aah niisha umaliza kuupitia, mind u; The more u get involved to them the more new things about them you will learn.

(4)Tenga muda wa kushare urafiki na watu wako wa karibu ata kama ulikuwa huna tabia io,sasa unahitaji watu katika biashara yako,maana wao ndio wateja wa kile utakacho anza uza,pokea watu wote... Hudhuria vikao vya harusi ata kama huna mchango wa kuchangia,uwepo wapo ni muhimu zaidi kuliko ile pesa,nenda kuswali kwa jumuia sio ndani kwako pekee,kama msikitini,kanisani n.k

(5)Jiunge na magroup kupitia hiyo android phone yako either katika WhatsApp, viber, instagram n.k laweza kuwa group la ulio soma nao,group la kazini kwenu,group la washkaji wanywa pombe,group lolote ata wewe waeza kubuni waunge tu ata watu 7 kwa siku

(6)Jiunge na facebook na magroup yalioko umo,yatakusaidia...

Itaendelea...
nimevutiwa sana na hii thread sema ni.ya mda.sijui kama.bado kutakuwa nafasi kwa group la whasap
 
habar za midaa hii wana jamvi?
Nimeona nyuzi nyingi zikiwa na maswali mengi yakiusiana na BIASHARA GANI ZA KUFANYA KWA MTAJI MDOGO..
Bhaaaasi kwa wale wabishi,wavumilivu na wasiokata tamaa,msio ogopa biashara za kudharaulika angalau tunaeza peana mwanga jinsi ya pa kuanzia.

Kwa kifupi mimi ni kijana wa miaka 29 nimezaliwa kwenye maisha ya kishuani huko Arusha ila nilifukuzwaga nyumbani toka 2006.Hapo ndo nilipopata changamoto za kufanya biashara za mitaji midogo.
Katika biashara nilizowai kufanya zote nilifanikiwa.

AINA ZA BIASHARA
1:KULENGA NGUO ZA KIKE KUUZA VYUONI
2:KUUZA PIPI,MAJI YA KANDOROO NA SIGARA(Nyakati maalum)
3:MATOFALI YA KUCHOMA
4:KUUZA DAGAA LA KUOSHA
5:BANDA LA CHIPSI
6😛LAYSTATION(KUCHEZESHA MAGEMU)

Nyingine nashindwa kuziorodhesha kutokana na kupitwa na wakati.
Sitaweza kuchambua zote ila nitaanza kuchambua moja kwa sasa.

JE WEWE UNAWEZA KUUZA PIPI,MAJI YA KUFUNGA(Kandoroo enzi zile) NA SIGARA KIPINDI CHA SABA SABA AU NANE NANE?(SIKU 7/8 ZA MAFANIKIO)
Nilipewa wazo toka kwa house boy aliyefukuzwa hom miaka mingi.lilikua wazo gumu kwangu tokana na maisha niliyokulia ila nilijikaza nikafanya.

NILIANZA NA MTAJI WA ELFU 70(MOROGORO)
niliazima meza mbili kwa ajili ya kuwekea pipi,nilikodisha ice box mbili kwa ajili ya barafu,nilinunua ndo 8 za maji,nililipa kitambulisho cha mfanya biashara ili kupunguza gharama za kulipa kila nikiingia langoni mwa uwanja wa nane nane.

Nilinunua vifuko vya kufungia maji vya kutosha.nilinunua chujio kubwa. katika hii biashara maji ndo yalinipa pesa nyingi
Ndoo ya maji sh 100

Sikumbuki mahesabu yote kwa uhakika ila siku ya kwanza niliuza maji elfu 9 ikiwa kandoro moja ni tsh 50 wakati biashara ya pipi na sigara ikisua sua,siku ya pili niliuza maji ya elfu 12 biashara ilienda vizuri lakini ugumu maji yaliisha sikua na uwezo wa kufunga huku nikiuza biashara ya pipi.jion yake nikamualika mshikaj(house boy)usiku tukafunga maji mengi sana.siku ya tatu tuliuza elfu 24.

JION YA SIKU YA 3
Nilipata moyo sana nikaanza kuona faida ya biashara niliyokua naidharau.
Basi tukapata wazo la kuwaajiri vijana wanne kutoka kitaa usiku tunafunga maji.asubuh mpaka jion tunafanya biashara ya kuuza tu.pamoja na kufunga maji mengi sana.biashara ya pipi na sigara nayo ikachanganya sana.

Hakika mpaka inafika tarehe 5 tulikua tunauza mpaka maji laki mwaka huo Mungu alijalia jua lilikua la maana.maajabu ni tarehe sita saa 6 mchana maji yote yameisha na watu wanataka tuwauzie hata kwa glasi. Hapo ndo tulipopiga pesa wadau. Zile cooler box zilikua na kitu kama kabomba. Tukazijaza maji na barafu tukanunua na vikombe 10.

Sisi kazi yetu ilikua ni kujaza barafu na maji tu.kila glas ya maji sh 100. Uongo dhambi kama kuibiana lazima siku hiyo niliibiwa sana ila sikujali. Usiku wa tarehe nane tulilewa sana na vijana wangu.asubuh ya tarehe 9. Ndio nikapiga mahesabu nimebaki na laki 8.

Nikagawa laki 2 nikabaki na sita. Pipi zilizobaki nikaziuza kwa bei ya jumla kwa muuza duka elfu 50 tukasambaratika tarehe 10.

Nia ni kutaka kukutia moyo kama kweli unania. Pia changamoto zilikua ni nyingi sana. Mfano sehemu ya kupanga meza zilikuwa zinapangishwa kwa zaidi ya mtu mmoja. Mwenye nguvu ndiye anafanya biashara.
Nawasilisha
Kwaiyo saiv wewe tajiri
 
Sina mishemishe na nimemaliza chuo nursing ila mambo ya ajira siyaelewi ila ninakakimtaji kama laki 3 iv je nifanye biashara gani wadau life la kitaa gum eti.
 
Back
Top Bottom