Kwanini January Makamba unakataa kutambua nguvu na juhudi za hayati Magufuli kwenye JNPP?

Kwanini January Makamba unakataa kutambua nguvu na juhudi za hayati Magufuli kwenye JNPP?

Ni raia wenye level gani ya elimu?..

Usilete mambo ya hoyahoya hapa.
Nyie elimu yenu SI ni ya kifisadi kwani kuna kingine mnajua?
Ni bola ya hao wanaoshangilia maana ndio mnawaibia kodi wanazolipa.
 
Mataga mnahangaika sana, hamkai mkatulia kabisa
 
Ukweli lazima usemwe,kuna tatizo gani kutambua juhudi za hayati Magufuli kwenye mradi huu wa umeme (JNPP),hasa kwenye hotuba zenu?

Wazo lilikuwa la Mwalimu Nyerere ,akashindwa,awamu zilizofuata kuanzia ya pili mpaka ya NNE,hawakuwa na habari na mradi huo,waliupa kisogo.

Hayati Magufuli kwa nguvu kubwa na ujasiri usio na shaka akaamua kutekeleza wazo hilo.
Miongoni mwa waliohujumu juhudi hizi ni waziri wa sasa wa nishati, January Makamba kwa kisingizio cha uharibifu wa mazingira,ikapelekewa kuondolewa baraza la mawaziri.

Leo hotuba ya mkurugenzi mkuu Maharage Chande na waziri wake wamejificha kwenye kichaka cha mipasho ,hasa waziri Makamba.

Nijielekeze kwenye usanii wa waziri kutambua juhudi za watangulizi kwenye ujenzi wa bwawa hilo,katengeneza zawadi za kutambua michango ya mzee Mwinyi na Jakaya,wana mchango gani ikiwa mradi waliupa kisogo?
Makamba junior kawapa medal za kinafiki sana,hata wao wamejisikia aibu sana kupewa medal za ushiriki wao wa mradi wakati hawajashiriki hata kidogo.

Huyu kijana ndio awaza kuwa rais wa hii nchi.tuna hasara kubwa kama taifa.

Nimpongeze rais Samia kwa kujaribu kuusema ukweli kuhusu kazi kubwa ya hayati Magufuli katika kufanisha mradi huu.

Kumekuwa na ka syndicate kupoteza Juhudi za hayati Magufuli kwa kuzimeza kijumla jumla na wasiostahili .moja wapo ni hilo tukio la kinafiki la kutambua mchango wa bwawa wakati si washiriki.

Namalizia kwa kumwambia waziri Makamba na walio nyuma yake kwamba watanzania hawadanganyiki tena , Magufuli aliwafumbua macho.

Huu mchezo wa kujaza vijana mitandaoni kumdhihaki, mmeona leo jinsi likitajwa jina lake makofi na shangwe kama lote.

Nikiashiria kwamba kimwili hatuko naye ila kifikra tukonae,acheni majungu dhidi ya marehemu.
hata wasipomtaja, kivuli chake kitawatesa sana
 
Hata mjifiche vipi kwenye mwanga mtaonekana tu na maguo yenu meusi.
Unapigania nn? Legacy? Watu angalau wenye akili ni wale wanaopigania katiba mpya huko field hawa wa legacy kulilia JPM atajwe tajwe kwenye hotuba ni wajinga tu maana nchi sio ya wafu hii, ni ya walio hai.
 
SSH haweka "legacy" yoyote hadi sasa zaidi ya kuendeleza miradi aliyoifanyia maamuzi ya utekelezaji na kuyasimamia km elimu bila malipo, kuboresha huduma za afya na elimu, ujenzi wa miundo mbinu ya usafishaji nchi kavu, majini na angani, nishati, maji na hata kuhamisha makao makuu ya nchi.

Tusubiri "diplomasia ya uchumi" kama itakuwa ndio "legacy" ya SSH
Nyerere peke yake aliweka legacy kwa kuwa rais wa kwanza. Umejiuliza kwanini JPM aliitwa jina lake kama rais wa tano baada ya watangulizi wake kupewa tuzo zao?.

Alikuwa ni rais wa tano hivyo alifanya kazi vyema kwa kutumia misingi ya wanne waliomtangulia. SSH anaendeleza pale walipomuachia watano waliomtangulia, na huyo wa saba ataendeleza pale atakapoachiwa na sita waliomtangulia.
 
Nafasi ipo...Unaweza kuvaa rubega na kuwa hunter kama huwezi kulamba asali na hutaki kuwapiga vijembe wanaomkashifu marehemu.
Huko ni kuwa kama ngamia kuficha uso mchangani !!!!

The point is this will be the generation which will be remembered as the stupidest by the coming generations yaani ni wafujaji wachoyo, wapuuzi (wakati tuna knowledge and we can do better)

Bora kina chief Mangungo wa Msovero they did not know better....
 
Huko ni kuwa kama ngamia kuficha uso mchangani !!!!

The point is this will be the generation which will be remembered as the stupidest by the coming generations yaani ni wafujaji wachoyo, wapuuzi (wakati tuna knowledge and we can do better)

Bora kina chief Mangungo wa Msovero they did not know better....
Acha kuteseka. Generation ikumbukwe na nani? We angalia iwapo watoto na wajukuu zako watakukumbuka kwa kuwaachia urithi. Unadhani nani atakaa akumbuke generation? Hii ni genetation ya ngapi kwani na wanaotakiwa kuikumbuka ni kina nani? Generation ya kina Nyerere inakumbukwa sababu ya uhuru, muungano n.k baada ya hapo ni kuendeleza walipoishia unless usimamie katiba mpya ipatikane useme sisi tulipigania katiba, kinyume na hapo pigania watoto na wajukuu au teseka for nothing.
 
Acha kuteseka. Generation ikumbukwe na nani? We angalia iwapo watoto na wajukuu zako watakukumbuka kwa kuwaachia urithi. Unadhani nani atakaa akumbuke generation? Hii ni genetation ya ngapi kwani na wanaotakiwa kuikumbuka ni kina nani? Generation ya kina Nyerere inakumbukwa sababu ya uhuru, muungano n.k baada ya hapo ni kuendeleza walipoishia unless usimamie katiba mpya ipatikane useme sisi tulipigania katiba, kinyume na hapo pigania watoto na wajukuu au teseka for nothing.
Selfish reply
 
hata wasipomtaja, kivuli chake kitawatesa sana
Waafrika wengi, hususan wabongo, siasa zao haziwezi kuvuka personalities. Hawawezi abstract thinking, critical thinking, logical thinking, sometimes thinking period.

Ndiyo maana hapa tunajadili watu badala ya sera.

Hili ni moja ya matatizo yanayoendeleza umasikini Africa.

Watu hawawezi kujadili sera. Hawawezi data driven conversations tu.

Ukiweka mjadala wa faida na hasara za Hydro Electric Dams, watu wajadili kisomi, wajadili kwa data, wajadili kwa logic, waongee kuhusu current trends and research, waongee mambo ya mazingira na maendeleo, waongee kuhusu climate change and the future of H.E.P, ni watu wachache sana watachangia kwa muktadha huo.

Ukosefu wa elimu na ukosefu wa utashi unatu cost.

Ukiweka habari za kuchambana team Makamba na team Magufuli, angalia watu watakavyochambana hapo.

Kwa sababu wabongo wengi ni wavivu wa kusoma, hawana data, hawawezi kuchambua mambo kisomi.

Wanachoweza wao kwa kiasi kikubwa ni kutukanana, kuchambana, maongezi yasiyo na data wala logic. Hapo utawakuta sana.
 
Nyerere peke yake aliweka legacy kwa kuwa rais wa kwanza. Umejiuliza kwanini JPM aliitwa jina lake kama rais wa tano baada ya watangulizi wake kupewa tuzo zao?.

Alikuwa ni rais wa tano hivyo alifanya kazi vyema kwa kutumia misingi ya wanne waliomtangulia. SSH anaendeleza pale walipomuachia watano waliomtangulia, na huyo wa saba ataendeleza pale atakapoachiwa na sita waliomtangulia.
Mmh,uongo mwingine bhana
 
Selfish reply
EXactly. Au unapendelea wale wa kukupigania haki zako kama mwenyekiti ili uje hapa umsifie na fake id huku yeye kanyolewa kipara? Inasemekana kajiamulia zake kulamba asali na yeye.
 
Ukweli lazima usemwe,kuna tatizo gani kutambua juhudi za hayati Magufuli kwenye mradi huu wa umeme (JNPP),hasa kwenye hotuba zenu?

Wazo lilikuwa la Mwalimu Nyerere ,akashindwa,awamu zilizofuata kuanzia ya pili mpaka ya NNE,hawakuwa na habari na mradi huo,waliupa kisogo.

Hayati Magufuli kwa nguvu kubwa na ujasiri usio na shaka akaamua kutekeleza wazo hilo.
Miongoni mwa waliohujumu juhudi hizi ni waziri wa sasa wa nishati, January Makamba kwa kisingizio cha uharibifu wa mazingira,ikapelekewa kuondolewa baraza la mawaziri.

Leo hotuba ya mkurugenzi mkuu Maharage Chande na waziri wake wamejificha kwenye kichaka cha mipasho ,hasa waziri Makamba.

Nijielekeze kwenye usanii wa waziri kutambua juhudi za watangulizi kwenye ujenzi wa bwawa hilo,katengeneza zawadi za kutambua michango ya mzee Mwinyi na Jakaya,wana mchango gani ikiwa mradi waliupa kisogo?
Makamba junior kawapa medal za kinafiki sana,hata wao wamejisikia aibu sana kupewa medal za ushiriki wao wa mradi wakati hawajashiriki hata kidogo.

Huyu kijana ndio awaza kuwa rais wa hii nchi.tuna hasara kubwa kama taifa.

Nimpongeze rais Samia kwa kujaribu kuusema ukweli kuhusu kazi kubwa ya hayati Magufuli katika kufanisha mradi huu.

Kumekuwa na ka syndicate kupoteza Juhudi za hayati Magufuli kwa kuzimeza kijumla jumla na wasiostahili .moja wapo ni hilo tukio la kinafiki la kutambua mchango wa bwawa wakati si washiriki.

Namalizia kwa kumwambia waziri Makamba na walio nyuma yake kwamba watanzania hawadanganyiki tena , Magufuli aliwafumbua macho.

Huu mchezo wa kujaza vijana mitandaoni kumdhihaki, mmeona leo jinsi likitajwa jina lake makofi na shangwe kama lote.

Nikiashiria kwamba kimwili hatuko naye ila kifikra tukonae,acheni majungu dhidi ya marehemu.
Ni kweli Mwendazake ana mchango wake Ila sio kweli kusema Awamu ya 4 iliupa kidogo mradi.

Awamu ya 4 ilikuwa ianze utekelezaji Ila Kama unavyojua ubinafsi wa Mwendazake kila kitu alipindua na kuanza upya anavyojua yeye ili apate sifa Kama individual.

Alibadilisha reli,Bandari ya bagamoyo na huu mradi ambao tayari MoU ilikuwa imesainiwa.
Screenshot_20221222-091015.png
Screenshot_20221222-090909.png
 
Back
Top Bottom