Kwanini January Makamba unakataa kutambua nguvu na juhudi za hayati Magufuli kwenye JNPP?

Kwanini January Makamba unakataa kutambua nguvu na juhudi za hayati Magufuli kwenye JNPP?

Ukweli lazima usemwe,kuna tatizo gani kutambua juhudi za hayati Magufuli kwenye mradi huu wa umeme (JNPP),hasa kwenye hotuba zenu?

Wazo lilikuwa la Mwalimu Nyerere ,akashindwa,awamu zilizofuata kuanzia ya pili mpaka ya NNE,hawakuwa na habari na mradi huo,waliupa kisogo.

Hayati Magufuli kwa nguvu kubwa na ujasiri usio na shaka akaamua kutekeleza wazo hilo.
Miongoni mwa waliohujumu juhudi hizi ni waziri wa sasa wa nishati, January Makamba kwa kisingizio cha uharibifu wa mazingira,ikapelekewa kuondolewa baraza la mawaziri.

Leo hotuba ya mkurugenzi mkuu Maharage Chande na waziri wake wamejificha kwenye kichaka cha mipasho ,hasa waziri Makamba.

Nijielekeze kwenye usanii wa waziri kutambua juhudi za watangulizi kwenye ujenzi wa bwawa hilo,katengeneza zawadi za kutambua michango ya mzee Mwinyi na Jakaya,wana mchango gani ikiwa mradi waliupa kisogo?
Makamba junior kawapa medal za kinafiki sana,hata wao wamejisikia aibu sana kupewa medal za ushiriki wao wa mradi wakati hawajashiriki hata kidogo.

Huyu kijana ndio awaza kuwa rais wa hii nchi.tuna hasara kubwa kama taifa.

Nimpongeze rais Samia kwa kujaribu kuusema ukweli kuhusu kazi kubwa ya hayati Magufuli katika kufanisha mradi huu.

Kumekuwa na ka syndicate kupoteza Juhudi za hayati Magufuli kwa kuzimeza kijumla jumla na wasiostahili .moja wapo ni hilo tukio la kinafiki la kutambua mchango wa bwawa wakati si washiriki.

Namalizia kwa kumwambia waziri Makamba na walio nyuma yake kwamba watanzania hawadanganyiki tena , Magufuli aliwafumbua macho.

Huu mchezo wa kujaza vijana mitandaoni kumdhihaki, mmeona leo jinsi likitajwa jina lake makofi na shangwe kama lote.

Nikiashiria kwamba kimwili hatuko naye ila kifikra tukonae,acheni majungu dhidi ya marehemu.
Sukuma gang muda wenu umeisha, Tanzania imeshakombolewa na Mungu kutoka utawala wa giza. Fanya kazi kuendesha maisha yako badala ya kulialia na mambo yasiyokusaidia
 
Mwinyi na Kikwete walitafuna nchi hii tu hakuna Cha maana walichoacha kama alama ya kuwatambua. Sasa wanakula matunda ya waliofanya ya maana. Hao maraisi waliotangulia mbele za haki ndo walifanya mambo makubwa.

Nyerere aliacha vitu vingi hadi Leo vipo. Viwanda, viwanja vya ndege, vyuo vikuu, barabara, nk

Mkapa kaacha; Uwanja wa BMkapa, Hospitali ya BMkapa, Chuo Kikuu dodoma, nk

Magufuli; Standa ya Magufuli, Magufuli City Dodoma, Masoko, Ikulu dodoma, SGR, Bwawa la Nyerere, Vivuko,

Kikwete kajenga jengo la CCM makao makuu hana Cha kukumbukwa nacho alikuwa mzururaji tu.

Mwinyi aliuza sehemu ya Tanzania kwa waarabu wa loliondo.
 
Mpuuzi huwa hana hoja,matusi ni mtaji wake,wewe ni mpuuzi
Umedandia kwa mbele ngoja nokuweke 👇
20221219_095038.jpg
 
Ni kweli Mwendazake ana mchango wake Ila sio kweli kusema Awamu ya 4 iliupa kidogo mradi.

Awamu ya 4 ilikuwa ianze utekelezaji Ila Kama unavyojua ubinafsi wa Mwendazake kila kitu alipindua na kuanza upya anavyojua yeye ili apate sifa Kama individual.

Alibadilisha reli,Bandari ya bagamoyo na huu mradi ambao tayari MoU ilikuwa imesainiwa.View attachment 2454681View attachment 2454682
Mipango mingi mikubwa ya nchi huwa inaanzia katika awamu moja, na kutekelezwa na awamu nyingine.

Hii si Tanzania tu, dunia nzima katika nchi za kidemokrasia ambazo marais wanakaa miaka 5-10, mara nyingi mipango inayoonekana kufanikiwa na rais mmoja inakuwa imeanzia awamu moja au mbili nyuma.

Hapo utaona Brazil Luiz Inácio Lula da Silva anasifiwa sana, lakini mipango hii ilikuwapo tangu kipindi cha Fernando Henrique Cardosso.

Namsoma rais Mwinyi hapa katika kitabu chake "Mzee Rukhsa: Safari ya Maisha Yangu", anaelezea kuwa watu waliona uchumi kwenda kufunguliwa kama ni maamuzi ya serikali ya rais Mwinyi, kumbe sera hizi zilianza tangu miaka ya mwisho ya urais wa Nyerere.

Marekani tumeona Trump akichukua credit kwa sera za kuanzia tangu miaka ya Obama.

Ndiyo maana mimi naona kushadadia watu ni ujinga. Kwa sababu hawa watu kazi zao zimechanganyikana sana, kama maji ya ndoo yaliyoingiwa na mkojo.

Sasa maji ya ndoo yakishaingiwa na mkojo, huwezi kusema "haya maji ya upande huu safi, hayajaingiliwa na mkojo, naweza kunywa". Si rahisi kutenganisha.

Ndiyo maana watu walioendelea wakaweka kitu kinaitwa "collective responsibility". Ndiyo maana Mkapa akamkaripia Magufuli akamwambia asiseme "serikali ya Magufuli" aseme "serikali ya CCM".

Ila, watu wengi wanapenda sana kushabikia watu, kuliko kuchambua sera.

Hapo ndipo mwisho wa uwezo wao labda. Maana kuchambua sera kunataka kazi ya kusoma, kuchakata data, kufikiri, na wengi hawawezi kazi hii.
 
Leo wananchi wamewaonesha JPM ni nani mioyoni mwao, mwanasiasa unayetaka anguko lako kisiasa simama jukwaana umponde JPM mbele ya wananchi, huku mitandaoni wamejaza vijana na mimultiple accounts kila uchao kumdhihaki, 2025 sio mbali.
Labda kama unahubiri kwa wananchi wasiyojielewa aka Wanyonge kama wewe, ila kwa wananchi wanaojielewa na wenye pesa hawana habari na huyo muuaji wanu
 
Mipango mingi mikubwa ya nchi huwa inaanzia katika awamu moja, na kutekelezwa na awamu nyingine.

Hii si Tanzania tu, dunia nzima katika nchi za kidemokrasia ambazo marais wanakaa miaka 5-10, mara nyingi mipango inayoonekana kufanikiwa na rais mmoja inakuwa imeanzia awamu moja au mbili nyuma.

Hapo utaona Brazil Luiz Inácio Lula da Silva anasifiwa sana, lakini mipango hii ilikuwapo tangu kipindi cha Fernando Henrique Cardosso.

Namsoma rais Mwinyi hapa katika kitabu chake "Mzee Rukhsa: Safari ya Maisha Yangu", anaelezea kuwa watu waliona uchumi kwenda kufungukiwa kama ni maamuzi yabserikali ya rais Mwinyi, kumbe sera hizi zikianza tangu miaka ya mwisho ya urais wa Nyerere.

Marekani tumeona Trump akichukua credit kwa sera zikuzianza tangu miaka ya Obama.

Ndiyo maana mimi naona kushadadia watu ni ujinga. Kwa sababu hawa watu kazi zao zimechanganyikana sana, kama maji ya ndoo yaliyoingiwa na mkojo.

Sasa maji ya ndoo yakishaingiwa na mkojo, huwezi kusema "haya maji ya upande huu safi, hayajaingiliwa na mkojo, naweza kunywa". Si rahisi kutenganisha.

Ndiyo maana watu walioendelea wakaweka kitu kinaitwa "collective responsibility". Ndiyo maana Mkapa akamkaripia Magufuli akamwambia asiseme "serikali ya Magufuli" aseme "serikali ya CCM".

Ila, watu wengi wanapenda sana kushabikia watu, kuliko kuchambua sera.

Hapo ndipo mwisho wa uwezo wao labda. Maana kuchambua sera kunataka kazi ya kusoma, kuchakata data, kufikiri, na wengi hawawezi kazi hii.
Wenye akili kisoda wafuasi wa Jiwe sidhani Kama watakuelewa..

Jiwe anatekeleza miradi Nchi iko paralysed Ila SSH anatekeleza miradi Wala Hakuna vilio Vya kipumbavu
 
Nimekuambia unless unapigania KATIBA mengine yote ni muendelezo wa waliyofanya wengine na hayana cha kukumbukwa. UNATESEKA SANA HAHAHA.
Kwamba Kenya na Katiba Mpya wamemaliza matatizo yao ? Pili unaona dunia kwa mafungu mimi naangalia dunia as a Unit.. Nchi zote na ninaposema generation hii simaanishi Tanzania tu bali dunia nzima kwa ujumla - Unaweza ukasema we shit where we eat..., tunajiona tupo civilized ila ni waharibifu watupu...; ndio maana nikatoa mfano wa hunters and gatherers (unaweza ukasema walikuwa hawapo civilised) ila ngoja nikuonyeshe msemo wa a generation past alafu uniambie who was brighter ?

Only when the last tree has been cut down, the last fish been caught, and the last stream poisoned, will we realize we cannot eat money.”

Ila the saddest truth ni kwamba the coming generations are the ones to pay the price.....,
 
Back
Top Bottom