Lema: Bodaboda imekuwa ni ajira ya Laana

Lema: Bodaboda imekuwa ni ajira ya Laana

Godbless Lema wa Chadema....
View attachment 2534970

Kwamba bodaboda ni kazi ya laana! Sawa tumekusikia! Ebu tuambie kama umeona hao ni laana! Ina maana kwamba hata abiria wao nao ni laana kubwa zaidi. Maana wao ndio wanaowawezesha hao bodaboda kuweza kujiendesha kutokana na malipo wanayowalipa. Na ikumbukwe kwamba wananchi wengi wa kipato cha kati na cha chini ndio wanaonufaika na huduma hii ya bodaboda nchini Tanzania. Na pia ikumbukwe kwamba kwa hapa nchini Tanzania, hilo tabaka pia ndio ambalo linashiriki siasa katika kiwango cha upigaji kura kwenye chaguzi mbalimbali.

Je, Lema unamaanisha hata wapiga kura wa nchi hii nao wamelaaniwa? Pia tuambie... kama bodaboda ni laana nchi hii. Inakuwaje mnaowatumia kwenye shughuli zenu zote za kisiasa nchini? Je, mnaitumia laana ili kupata political mileage toka kwao?

#Lema na #Chadema njooni hapa mtutajie nchi ya Afrika ambako hakuna bodaboda! Na mnapowaita bodaboda laana, ni kazi ipi mmewaandalia ambayo ni mbadala wa hiyo laana! Msiishie kuchonganisha wananchi huku mkiwa hamna lolote la mbadala vichwani. Mfano mzuri ni hapo #Kenya kwa Rutto, aliwaahidi Paradiso kwa kujiita "Hustler"... Nenda leo Kenya au angalia media zao na uone kinachojiri huko...
Yaani imekuwa wimbo hoja muhimu ya Lema haitajwi lakini minor issue ya bodaboda ndiyo inawasumbua. Chukueni tukio zima la kuondoka kwake na kisha kurudi sababu ni zipi tujadili.
Bodaboda hawakumkimbiza au kumrudisha lema! This is very minor, hence, it needs no discussion men!
 
Hello!

Naona Lema ameanza kwa gia ya matusi kwa wanaojiita bodaboda. Lema amesema bodaboda sio kazi ila ni laana.

Hivi hizi si ni dharau kwa vijana wa bodaboda? Yaani watu wanaendesha familia kwa kazi hiyo halafu anakuja mtu anawadharau na kutukana eti wamelaaniwa?

Nyie wafuasi wa CHADEMA mnaposhabikia watu muwe mnajitambua. Hawa kina Lema wamekuwa wabunge hapo Arusha miaka 10, waliwafanyia nini cha maana?

Ujinga kama huu wa CHADEMA ndio kina Ruto walikuwa wanawadanganya Kenya badala yake hakuna cha maana anafanya; ameongeza tax, ameondoa ruzuku kwenye mafuta maisha yako juu, anakopa na alisema hatokopa, anaomba misaada ya chakula hadi Ukraine, mfumuko wa bei ndio usiseme nk.

Ujinga kama huu wa upinzani ulifanyika hata Malawi, kawaulize Wamalawi kama kuna nafuu wamepata, the likes ya Zambia.

Ukiwasikiliza CHADEMA huwa wanaota ila hawana strategy ya kile wanachoota, uje uwaulize watawatoa vipi Watanzania kwenye umaskini kama wanavyodai wakati hawana hata sera inayoeleweka.

Toka nimeanza kuwasikiliza CHADEMA zaidi ya Katiba Mpya na mambo ya Majimbo hakuna jipya, maana hizo political tools sio nyenzo za kuondoa watu kwenye umaskini.

Mwisho, ukiwasikiza ACT Wazalendo unaona content ila ukiwasikiza CHADEMA unaona ulalamishi na kuorodhesha matatizo ya Watanzania bila suluhisho.

Watanzania stukeni mnafanyiwa ngazi za kutengenezea watu maisha.

 
Ndivyo mnavyodanganyana na vipro pagan da uchwara. Tuambie ni sera gani za CCM ambazo ni bora kuliko hao Unapodai hawana sera.
Mimi sio mpenzi wa CCM kwanza wewe jibu tu hoja CHADEMA Wana sera zipi juu ya Hili Taifa waaminiwe na wananchi?
 
Lema ni mjumbe wa kamati kuu, anachokisema kwenye mikutano yake ya hadhara hatupaswi kuyapuuza, kamati kuu ya chama chetu cha Chadema ndio chombo chenye kutengeneza mipango yote ikiwemo mikakati ya chama kushinda uchaguzi, kwahiyo anapongea mjumbe wa kamati kuu kama Lema, Msigwa nk tunapaswa kumsikiliza kwa makini.

Lema amewananga bodaboda akisema sio kazi, ni kazi ya laana, amefika mbali akidai kazi hiyo imesababisha vijana wengi kuwa vilema.

Jamaa kweli ni mwehu sana ingawa namshabikia sana, hivi Lema hajui kuwa ajali za magari zimesababisha vifo na vilema wengi kama lilivo jina lake? Mbona kuna watu wana mwaka wa 20 huu wanaendesha bodaboda na hawajahi kupata ajali?

Ajali ni mipango ya mungu, hivi wanasiasa wa chadema mnaokwenda kwenye majimboni kuongea na wananchi wenu mtajibu nini mkiulizwa hoja ya Lema, mjumbe wa kamati kuu kuwa bodaboda sio kazi.

Chadema itoke hadharani na kueleza kuhusu hoja hiyo vinginevyo lema rudi Canada aliko mke ukainjoy conjugal rights
 
Lema ni mjumbe wa kamati kuu, anachokisema kwenye mikutano yake ya hadhara hatupaswi kuyapuuza, kamati kuu ya chama chetu cha Chadema ndio chombo chenye kutengeneza mipango yote ikiwemo mikakati ya chama kushinda uchaguzi, kwahiyo anapongea mjumbe wa kamati kuu kama Lema, Msigwa nk tunapaswa kumsikiliza kwa makini.

Lema amewananga bodaboda akisema sio kazi, ni kazi ya laana, amefika mbali akidai kazi hiyo imesababisha vijana wengi kuwa vilema.

Jamaa kweli ni mwehu sana ingawa namshabikia sana, hivi Lema hajui kuwa ajali za magari zimesababisha vifo na vilema wengi kama lilivo jina lake? Mbona kuna watu wana mwaka wa 20 huu wanaendesha bodaboda na hawajahi kupata ajali?

Ajali ni mipango ya mungu, hivi wanasiasa wa chadema mnaokwenda kwenye majimboni kuongea na wananchi wenu mtajibu nini mkiulizwa hoja ya Lema, mjumbe wa kamati kuu kuwa bodaboda sio kazi.

Chadema itoke hadharani na kueleza kuhusu hoja hiyo vinginevyo lema rudi Canada aliko mke ukainjoy conjugal rights
Nikajua umeambatanisha na press release ya CDM toka kwa katibu kua kama CDM huo ndio msimamo wao!! Kumbe hakuna ni muendelezo wa thread za kitoto toka kwa wachunga ng'ombe wazee wa legacy!!!
 
Hebu acheni upumbavu.
Unapoongelea bodaboda unaongelea value chain ya motorcycle industry yoote kwa ujumla.
Kuna viwanda vinavyotengeneza bike kuna makampuni na mawakala wanaonunua hizo bike kutoka viwandani, pia kuna wauzaji na wakopeshaji wanaouza bike kwa rejareja.

Kuna mabosi wanaonunua bike na kuwapa vijana ambao ndio wanafanya biashara ya bodaboda pia kuna wauzaji spares na mafundi wa bike.

Hivyo unaposema bodaboda ni kazi laana unakua umehusisha watu wote waliokwenye mnyororo wa thamani wa industry ya bodaboda.
 
Hoja zao mbofu mbofu kweli!
Yaani wanatembelea na ile Doctrine ya kiinjili. Gospel!

A Gods intervention
 
A must read

The Transactional Context of Psychological Normality.

Jeremiah 26:2-7

The Industrial Revolution: The conflict between English and Irish Workers etc etc

Lema na CHADEMA ni vibaraka wa mabeberu.

Hawana sera za kuuza, wanahubiri injili...."The angry white man" mentality!
 
Mkuu, usiifanye hii kuwa ajenda kuu. By the way kabla Adam na Hawa hawajalaaniwa, walikuwa hawafanyi kazi yoyote.
Mungu aliwapa assignments ndogo ndogo kama vile ya kutunga majina ya wanyama na ndege.
Siku walipolaaniwa, Adam akaambiwa kwa jasho utakula.
Kwa hiyo unaweza kuona kuwa kufanya kazi ni laana. Ni matokeo ya binadamu kulaaniwa na Muumba wake.
Wastaafu wenye pensheni ambao kwa sasa hawali kwa jasho ndio baadhi ya binadamu ambao wamevuka 'mstari wa laana' kwa vile hawali tena kwa jasho...
 
Hii ni muda mchache uliopita. Sasa mnadhani vijana wangapi nchi nzima wanakumbana na haya madhila siku ya leo?
Screenshot_20230304-134730_Twitter.jpg
 
Hii ni muda mchache uliopita. Sasa mnadhani vijana wangapi nchi nzima wanakumbana na haya madhila siku ya leo?View attachment 2536796
halafu mapoyoyo ya ccm yakiambiwa bodaboda ni kaz ya laana yanapayuka payuka haya wafuas wa lumumba nenden kwa huyo kijana aliyegongwa mumuulize kama kaz ya bodaboda anaifurahia na kama haifurahii bas ni kaz ya laana
 
A must read

The Transactional Context of Psychological Normality.

Jeremiah 26:2-7

The Industrial Revolution: The conflict between English and Irish Workers etc etc

Lema na CHADEMA ni vibaraka wa mabeberu.

Hawana sera za kuuza, wanahubiri injili...."The angry white man" mentality!
yani chadema iwe vibaraka wa mabeberu huku mamayenu wa ccm anaenda kukopa kwa mabeberu kila siku had deni limefika trillion 76, kama hujui mamayenu ccm na mamayenu ndio mawakala ya mabeberu ndio maana mnakimbilia kukopa huko kila siku wapuuz kabisa.
 
Mimi sio mpenzi wa CCM kwanza wewe jibu tu hoja CHADEMA Wana sera zipi juu ya Hili Taifa waaminiwe na wananchi?
Hata mimi siyo mapenzi wa Chadema. Pia ushasema Chadema hawana sera. Sasa kwa nini unaniuliza tena kuhusu sera zao.
 
Wasubiri ajira ama
Marekani kila mwaka inapeleka maelfu ya wahitimu wake wa vyuo vikuu katika nchi za ulimwengu wa 3 kwa ajili ya kujitolea kwa mkataba miaka isiyopungua miwili, huku wakilipwa posho ya kujikimu.

Baada ya hiyo miaka miwili, wanarudidi nchini mwao kwa ajili ya kuajiriwa. Sisi nchini mwetu kuna sekta kibao za serikali zina upungufu wa watenda kazi! Lakini serikali inashindwa kutoa ajira za kujitolea kwa wahitimu wake.

Badala yake, wako tayari kufanya matumizi yasiyo na ulazima wowote ule, na mwisho wa siku wahitimu wa vyuo vikuu baadhi yao wanaishia kuwa bodaboda.
 
Ukiwasikiliza CHADEMA huwa wanaota ila hawana strategy ya kile wanachoota, uje uwaulize watawatoa vipi Watanzania kwenye umaskini kama wanavyodai wakati hawana hata sera inayoeleweka.

Toka nimeanza kuwasikiliza CHADEMA zaidi ya Katiba Mpya na mambo ya Majimbo hakuna jipya, maana hizo political tools sio nyenzo za kuondoa watu kwenye umaskini.
Nimekaa karibu dakika mbili tatu nikitafuta maneno ya kuandika juu ya maneno haya uliyoweka hapa katika hii mistari michache niliyonyanyua kwenye bandiko lako.

Ninakubaliana na wewe bila ya kupinga chochote hapo.
Ila, huenda tofauti inayoweza kuwepo kati yako na mimi juu ya swala hili ni kwamba ni uamini wangu kuwa niko tayari kuunga mkono chama kingine chochote kinachoonekana kuwa na uwezo wa kuwaondoa CCM madarakani kwa sasa, bila kujali chama hicho kimejitangaza kufanya mambo gani kikiwa na madaraka.
Kwa hiyo, kwa upande wangu, kukitokea kupiga kura leo, nitawapa CHADEMA kura yangu ili wawaondoe CCM madarakani. Wakishafanya hivyo, tunaanza mwanzo mpya wa kuwaza ni chama kipi kinachosimamia zaidi maslahi ya waTanzania.

Hii ndiyo 'bottomline' niliyoifikia katika kutafuta uhuru wa nchi yetu toka kwa mkoloni mpya CCM.

Sera za CHADEMA hazinipi matumaini hata kidogo kuhusu hatma ya Tanzania na wananchi wake. Wakiweza kutufanyia hiyo kazi ya kuwaondoa CCM, tutawashukuru; lakini baada ya hapo, kama hawana msimamo mwingine kuhusu sera zao, tunaachana nao njia.
 
Back
Top Bottom