Lissu: Watoto wangu wote ni raia wa Marekani

Lissu: Watoto wangu wote ni raia wa Marekani

Nyie wapuuz mnaofisi ipi majengo ya serikali mliyoyageuza ofisi za lumumba ndo mnaona mnaofis ndio maana uzezeta hautawaisha na chadema ikishika madaraka jiandaeni kujibu kesi za uhujumu uchumi kwa mali za umma.
Chadema ilishapoteza muelekeo
 
Brother unayajua machafuko?.

Hakuna Chama cha siasa kinacholeta machafuko duniani, maisha magumu ya raia ndio huleta machafuko....vingine ni njia tu za kupitia..

sijui umri wako, lakini jitahidi sana kupambania ndugu zako watanzania wanaoteseka na maamuzi ya hovyo ya wanasiasa unaowatetea ambao ndio chanzo cha umasikini huu unaouona lwa mamilioni ya watanzania.

Mataifa yote yaliyoendelea duniani yanajivunia kuwa na vijana wenye akili, wabunifu, wanaohoji na kufanya kazi kwa bidii, wanaosoma na kuelimika, wenye uwezo wa kupambana kokote duniani.

Think Gentle mike, Tanzania is for Tanzanians not for fool cartel....
 
Brother Watanzania wana kila sababu ya kupambana na CCM kutokana na ujinga mwingi ambao chanzo chake ni wanasiasa waliopewa/kujitwalia mamlaka ya kuongoza Watanzania..

Kaa chini fikiri vizuri, Tafuta nauli tembeatembea duniani, kutana na watu tofauto tofauti wa mataifa tofauti vijana, wazee, watoto halafu fananisha na nchi yako uone tofauti ~ UTAAMUA MWENYEWE.

Machafuko yataletwa na CCM maana wanalazimisha kutumia nguvu kwenye dunia inayoendeshwa kwa akili nyingi na facts, Nguvu inafika mahala zinashindwa na hao mnaotumia nguvu kwao na propaganda wanachoka taratibu na time ya liwalo na liwe itafike ambapo watu watakuwa tayari kujitoa sadaka kwa manufaa ya kizazi kijacho..

Hakuna aliye tayari kuona vitukuu au wajukuu waje waone baba/babu alikuwa mpumbavu....

Viongozi wajinga, wapumbavu, wanafiki, wachawi nk kizazi chao kilishapita duniani hapa toka 1800's, its time for clever and intelligent society...
 
Yaani jamaa yangu huoni huu ujinga wooote unapambana na CDM ambayo haina athari yeyote kubwa kulinganisha na maamuzi mabovu ya watawala...

Huoni shida ya umeme, huoni shida ya maji, huoni miundombinu mibovu, huone elimu mbovu inayozalisha vijana wapumbavu, huoni huduma mbovu za Afya, huoni shida ustawi wa jamii namatokeo yake taifa linakuwa na vijana wa hovyo (malaya,wazinzi, walevi, machawa, mashoga), Huono tatizo la ajira na hakuna anayejali.. matatizo ni mengi sana unawaza kumaliza server ya JF...

too sad kwako brother, kesho jumapili nenda kanisani kama wewe ni christian kamwambie Mungu akusamehe na akupe wepesi wa kuona maovu pamoja na kutetea wengi wanaoteseka...
 
Mimi sijazungumzia habari za uteuzi
Hata jpm mlimjaza ufitini hvhv leo hii mwenzenu anaoza chato ; chawa ni wabaya sana pengine bila ufitini wenu kajpm kawatu kangekuwa madarakani mpk leo ila chawa kama chawa ni watu wabadi sana.
 
Ndugu zangu siku zote Mwenyezi Mungu hamfichi Mnafiki ,Kwa miaka mingi viongozi wa chadema wamekuwa wakiwaita na kuwabatiza watanzania majina mbalimbali mfano utasikia wanasema watanzania Ni waoga,wajinga ,wamekosa Elimu n.k,Mara nyingi kukitokea mapinduzi ya kiraia kwa baadhi ya serikali za nchi fulani zinazokuwa zimeshindwa kusikiliza wananchi wake unakuta viongozi wa chadema wakitamani na kutoa maneno ya kutaka machafuko yatokee hapa nchini.

Sasa Imefahamika wazi kupitia Tundu Lisu kiongozi wa chadema wa ngazi ya juu kabisa akitamka kupitia mdomo wake ambao siku zote Hauna breki wala kuchagua maneno ya kutamka kuwa watoto wake Ni raia wa Marekani, Ndugu zangu kumbe ndio maana chadema imekuwa ikitaka kuona umwagikaji wa damu hapa nchini kwa kuwa wanajuwa kuwa wao na familia zao hawataathirika na chochote,kumbe wanafahamu kuwa Damu za familia zao zitakuwa salama,kumbe wanafahamu kuwa hakuna mtoto wao au mwana familia wao atakayebakia na kilema Wala upofu Wala majeraha Wala njaa Wala kuvunjwa miguu kwa kuwa wanafahamu kuwa wao siyo raia wenye uzalendo na nchi hii hata ikichafuka na kutiririsha Damu Kama chemichemi za maji jangwani zaidi ya kuhitaji madaraka tu hata kwa kushirikiana na shetani

Hii ndio sababu kumbe chochote kinachofanywa na serikali hii wanakibeza kwa kuwa wanajuwa watoto wao wanapata huduma Bora huko kwingine,Ndio maana wakiona mama yetu mpendwa mama Samia akitoa Elimu bure Hadi kidato Cha sita au kuwapa mikopo wanafunzi wote wa Elimu ya juu wenye sifa wao wanabeza,wanadharau ,wanatoa maneno ya kumkatisha Tamaa Mh Rais kwa kuwa wanajuwa watoto wao wanapata huduma bora huko nchi za magharibi na kwamba wanatamani watoto wa watanzania wazeeke bila Elimu Wala ujuzi,wanataka watoto wa watanzania wawe wanyonge,wajinga mbele za watoto wao,wanataka watanzania wasijitambue ili waje wawatumie kuleta machafuko hapa nchini kwetu

Ndio maana wakiona mama yetu na Rais wetu mpendwa mama Samia akijibidisha kujenga vituo vya Afya kila sehemu wao hawapendi kwa kuwa wanajuwa watoto wao wakiumwa hawatatibiwa hapa nchini kwa kuwa watakwenda huko nchi za magharibi na bima zao kubwa kubwa,hawataki kuona watanzania wakipata huduma Bora za kiafya,hawataki kuona watanzania wakipata maji Safi na salama kwa kuwa wanatamani waone watanzania wakihangaiika na magonjwa ya matumbo mpaka wapoteze ufahamu ili waje wasimame majukwaani kuwahamasisha watanzania waibomoe nchi yao kwa mikono yao

Ndio maana wakiona Rais wetu akiwainua wakulima wananuna na kumbeza kwa kuwa Wao chedema wanatamani wakulima wasilime na wakumbwe na njaa na hata kufa na njaa,wanatambua kuwa huwezi kumuongoza mwenye njaa Ndio sababu wanatamani watanzania wawe na njaa ili waje wasimame hadharani kuwatumia watanzania kuchinjana.ndio sababu ya kupandikiza chuki kwa watanzania dhidi ya serikali yao,ndio sababu wakati wote wamekuwa wakitoa maneno yenye sumu ili kuwamezesha watanzania waichukie serikali yao,ndio sababu wakati wote maombi yao yamekuwa ni kutaka kuona serikali ikishindwa ili ichukiwe na watanzania,Ndio sababu kuna wakati wamewahi kusema kuwa nchi haitatawalika

Chadema hawapendi kusikia habari za mama kutoa maelfu ya ajira kwa vijana takribani elfu 42, kwa kuwa wanataka kuona vijana wakihangaiika mitaani Kama vibaka kusudi wawatumie kubeba hasira na sumu mioyoni mwao ya kuvuruga amani ya nchi yetu kwa kuwa wanajuwa watoto wao wapo ulaya na familia zao na wao wenyewe watakimbilia huko halafu wawe wanarusha picha mitandaoni kwa makubwa zao,Hakika chadema Ni vibaraka, Ni wasaliti wa nchi yetu ,wapo Tayari kwa lolote ilimradi tu wapate madaraka,wanachoomba wao Ni machafuko tu yatokee ili watafute njia ya mkato

Kibaya zaidi Ni kuwa safu ya uongozi ya Chadema nidhaifu Sana kwa Sasa na iliyopoteza matumaini na kujikatia Tamaa,imejikatia Tamaa yakutwaa Dola kwa njia ya kidemokrasia,imepoteza ushawishi kwa watanzania,haionyeshi matumaini ya kesho,Hakuna anayeiunga mkono,imebaki Ni mkusanyiko wa watu waliokata na kujikatia Tamaa ndio maana wanaona njia fupi ni kama Ile aliyoitangaza Lisu uchaguzi uliopita ili watanzania waandamane mitaani wakati huo yeye Anayo tiketi ya kukimbia nchini na kajificha ubalozini

Watanzania Tumeshayajuwa ya sirini na dhamira ya Chadema,wamejiumbua wao wenyewe,Ndio hasara ya kuwa na kiongozi mropokaji Kama Tundu Lisu,Tusiwape nafasi chadema ya kuharibu Taifa letu kwa kuleta machafuko na kupandikiza chuki miongoni mwetu,wao hawatakuwepo hapa nchini na Wala hawataumia kwa chochote,Tusiwaunge mkono,Tuwapuuze na kuwadharau kwa lolote watamkalo maana hawana Nia nzuri na Taifa letu

Ushauri kwa Idara yetu ya usalama wa Taifa(TISS) Ni kuhakikisha wanakuwa chonjo na nyendo zote za viongozi wa chadema katika safari zao za nje ya nchi,wasiruhusu mapesa yakaingia kiholela hapa nchini ambayo yakaja kufadhili mipango Yao miovu,wawe makini na kufuatilia matamshi yao ,wasiwaruhusu wakapandikiza mbegu za chuki kwetu watanzania,Tumeona siku za hivi karibuni wakijaribu kutaka kupandikiza mbegu ya ukanda na ukabila Kama kete ya kupata uungwaji mkono ambao walisha upoteza muda mrefu

Watanzania Tuendelee kumuunga mkono mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani katika kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe,Nadhani tumeshatambua kwanini Chadema ipo msitari wa mbele kupinga juhudi za mh Rais,Tumeshatambua ni kwa kuwa hawana uchungu na sisi watanzania Bali wanaombea tuteseke ili waje watutumie kufanikisha ajenda zao, Tusiwape nafasi hiyo. Tuwe bega kwa bega na Rais wetu na Tusikubali watimize malengo yao kupitia mikono yetu,Tulipende Taifa letu na Tulipiganie kwa nguvu zote,Ni Rahisi kulibomoa Taifa kuliko kulijenga na kuliinua mpaka tulipo nalo hapa penye amani utulivu na usalama,Tukumbuke watu wengi wanatuonea wivu watanzania kwa namna tulivyo na mshikamano, hivyo tusije jiroga tukavuruga amani yetu tuliyo nayo

Mwisho tukumbuke kuwa matatizo yetu tutayatatua sisi wenyewe kwa kushirikiana na serikali yetu,matatizo na kero ndogondogo Tuwe wavumilivu na wenye subira wakati serikali yetu ikiendelea na juhudi na jitihada za kukabiliana nazo.serikali yetu ipo kazini muda wote na Rais wetu tunaona akifanya kazi usiku na mchana kututumikia watanzania.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
Limeweka na namba ya cm haya ndio machawa yanayoishi kupitia ufitini na rushwa sasa hiyo namba ya cm ni yanini ili uitwe Kwenye kamati za uchaguzi na wizi wa kura?
 
Back
Top Bottom