Lupaso, Mtwara: Rais Mstaafu, Hayati Benjamin William Mkapa azikwa kwa Heshima
Salaam Wakuu,

Leo ni siku ya Kwanza kati ya Tatu ya kuuaga Mwili wa Aliyekuwa rais wa Tanzania Benjamin Wiliam Mkapa katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar Es Salaam.

Tutaendelea kujuzana kile Kinachojiri.

Stay tuned.



=====

UPDATES:

======

View attachment 1517152View attachment 1517154
0910hrs: Mwili wa Marehemu upo Njiani kutoka Hospitali ya Jeshi Lugalo kuelekea Uwanja wa Uhuru Temeke. Ambapo kazi hii inaongozwa na Jeshi la Ulinzi (JWTZ).

Mwili ukifika Uwanja wa Taifa, kutakuwepo na Misa itakayoongozwa na Askofu Tercius Ngalekumtwa.

0935hrs: Msafara wa Mwili wa rais Mstaafu Mkapa, bado upo njiani kutokea Jeshini Lugalo Kawe Dar Es Salaam kupitia barabara ya Hassan Mwinyi, Katikati ya Mji hadi Temeke.
View attachment 1517174
Kila Sehemu Msafara unapopita, Wananchi wamejipanga barabarani kuaga na kutoa heshima zao za mwisho.

0945hrs: Mwili Wa Marehemu Mkapa ndo unaingia Viwanja vya Uhuru Temeke
View attachment 1517216
View attachment 1517194
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Mama Anna Mkapa, akiwa tayari kwenye Uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kushiriki Misa na kuuaga mwili wa Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa
View attachment 1517195
Rais Magufuli na Makamu wa Rais Samia Suluhu wakiwa tayari wamewasili katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki Misa na kuaga mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.
View attachment 1517197
1000hrs: Mwili wa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa ukishushwa kutoka katika Gari maalum ndani ya Uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kuanza kwa misa ya kumuaga.

WAKATI HUO HUO;
View attachment 1517198
Vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakiendelea na shughuli ya ujenzi wa kaburi atakwamozikwa Rais Mstaafu, Marehemu Benjamin Mkapa.

Kiongozi huyo atazikwa kijijini kwao Lupaso, mkoani Mtwara, Julai 29 mwaka huu.

Shughuli za kuuaga mwili wake zinaendelea Dar es Salaam.

1140HRS: Ibada ya kuaga Mwili wa rais Mstaafu Benjamin Mkapa inaelendelea Uwanja wa Uhuru.

MSEMAJI WA FAMILIA: RAIS MKAPA ALIKUTWA NA MALARIA

William Erio, Msemaji wa familia amesema Rais Mstaafu Benjamini Mkapa alipatwa na Malaria Jumatano na akalazwa na kuanza matibabu

Siku ya alhamisi alikuwa anaendelea vizuri, na akaendelea kufuatilia uchaguzi wa kura za maoni uliokuwa unaonyesha mubashara

Baada ya muda, aliinuka alitaka kutoka, alivyoinuka akarudi kukaa na akainamisha kichwa, na akathibitika amefariki kwa mshituko wa moyo, ‘Cardiac arrest’

Msemaji wa familia amewataka watu kuheshimu ukweli huo, na sio kuzusha mambo yasiyo na ukweli kwenye mitandao.

KASEMA;

"Nitoe shukrani kwa Serikali kwa ambavyo wamekuwa pamoja nasi na kushughulikia msiba huu na wanavyoendelea kushughulikia, tunawashukuru kwa uamuzi wa kuanza shughuli ya kuaga kwa Misa Takatifu, tunawashukuru Maaskofu kwa kukubali kuendesha Misa”- William Urio,

“Mzee Mkapa alikuwa hajisikii vizuri akaenda Hospitali akaonekana alikuwa na Malaria akaanza matibabu akalazwa Jumatano,Alhamisi mchana aliendelea vizuri nilikuwa nae hadi saa mbili alikuwa anaangalia Live ya chaguzi za wagombea Ubunge Viti Maalum CCM”-

“Mzee Mkapa Alhamisi usiku baada ya kutazama LIVE ya chaguzi Viti Maalum akasikiliza taarifa ya habari, baadaye aliinuka akitaka kutoka akakaa akainamisha kichwa, walipokuja kumpima wakathibitisha kuwa amefariki, sababu ya kifo cha Mzee Mkapa ni mshtuko wa moyo”-

“Chanzo cha kifo cha Mkapa alipata mshtuko wa moyo, tumeona ni vizuri tuliseme hili kwasababu kumeanza kuwa na manenomaneno kila Mtu akijifanya Nabii katika mitandao ya kijamii na kwingine, tumuenzi Mzee wetu aliyetangulia mbele za haki kwa kuukubali ukweli huo"


View attachment 1517651View attachment 1517650
PICHA: Kutoka Uwanja wa Uhuru DSM ambako imefanyika Misa Takatifu ya kuuaga mwili wa Marehemu Mzee Mkapa kisha Watanzania mbalimbali kupata nafasi ya kupita karibu na Jeneza na kutoa heshima zao za mwisho, haya ndio matukio mbalimbali ya picha uwanjani.

Hivi kuna mtu anafatiliaga mazishi ya haya majamaa kweli?

Kama ulikuaga haupo kwenye mioyo ya wananchi bwana,ndio mtatumia mabajeti na maguvu meeengi kuomba wananchi waje,of which,you have failed..huwezi lazimisha watu!
 
Amechelewa misa kaamua asije kabisa hadi mda wa kuzika
Sasa inawezekanaje yeye Jiwe, akiwa ndiye "main character" wa tukio zima la leo ndiye achelewe?

Hivi si nyinyi mliamua jana kutowaruhusu viongozi wa Chadema, wasiingie uwanja wa Uhuru, kwa madai ya kuwa ni watovu wa nidhamu, kwa kutozingatia protokali?
 
Poleni kwa msiba mzito wa Rais wetu mstaafu.

Nimekuwa nikizunguka hapa na pale katika mkusanyiko huu wa kumuaga mzee Mkapa wananchi wamekuwa wakijadiliana mbona Rais Magufuli hayupo.

Hakuna hata taarifa kama yupo njian ama amepata dharura za majukumu?

Jana Rais Magufuli aliwasili mkoani Mtwara salama kabisa na kwenda kupumzika.

Natoa pole kwa rais Magufuli najua anapitia hali ngumu ya msiba huu. Sisi wananchi wako tunakupa shime uzishinde hali ngumu. Daima tupo pamoja.

Updates:

Rais Magufuli aanza safari rasmi ya kutoka Mtwara. Muda wowote atawasili.
 
Poleni kwa msiba mzito wa Rais wetu mstaafu.

Nimekuwa nikizunguka hapa na pale katika mkusanyiko huu wa kumuaga mzee Mkapa wananchi wamekuwa wakijadiliana mbona Rais Magufuli hayupo.

Hakuna hata taarifa kama yupo njian ama amepata dharura za majukumu?

Jana Rais Magufuli aliwasili mkoani Mtwara salama kabisa na kwenda kupumzika.

Natoa pole kwa rais Magufuli najua anapitia hali ngumu ya msiba huu. Sisi wananchi wako tunakupa shime uzishinde hali ngumu. Daima tupo pamoja.

Updates:

Rais Magufuli aanza safari rasmi ya kutoka Mtwara. Muda wowote atawasili.
Bado kuna ka umbali mtwara to Lupaso labda atumie choppa ije itue hapo msibani
 
Salaam Wakuu,

Leo ni siku ya Kwanza kati ya Tatu ya kuuaga Mwili wa Aliyekuwa rais wa Tanzania Benjamin Wiliam Mkapa katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar Es Salaam.

Tutaendelea kujuzana kile Kinachojiri.

Stay tuned.



=====

UPDATES:

======

View attachment 1517152View attachment 1517154
0910hrs: Mwili wa Marehemu upo Njiani kutoka Hospitali ya Jeshi Lugalo kuelekea Uwanja wa Uhuru Temeke. Ambapo kazi hii inaongozwa na Jeshi la Ulinzi (JWTZ).

Mwili ukifika Uwanja wa Taifa, kutakuwepo na Misa itakayoongozwa na Askofu Tercius Ngalekumtwa.

0935hrs: Msafara wa Mwili wa rais Mstaafu Mkapa, bado upo njiani kutokea Jeshini Lugalo Kawe Dar Es Salaam kupitia barabara ya Hassan Mwinyi, Katikati ya Mji hadi Temeke.
View attachment 1517174
Kila Sehemu Msafara unapopita, Wananchi wamejipanga barabarani kuaga na kutoa heshima zao za mwisho.

0945hrs: Mwili Wa Marehemu Mkapa ndo unaingia Viwanja vya Uhuru Temeke
View attachment 1517216
View attachment 1517194
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Mama Anna Mkapa, akiwa tayari kwenye Uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kushiriki Misa na kuuaga mwili wa Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa
View attachment 1517195
Rais Magufuli na Makamu wa Rais Samia Suluhu wakiwa tayari wamewasili katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki Misa na kuaga mwili wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.
View attachment 1517197
1000hrs: Mwili wa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa ukishushwa kutoka katika Gari maalum ndani ya Uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kuanza kwa misa ya kumuaga.

WAKATI HUO HUO;
View attachment 1517198
Vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakiendelea na shughuli ya ujenzi wa kaburi atakwamozikwa Rais Mstaafu, Marehemu Benjamin Mkapa.

Kiongozi huyo atazikwa kijijini kwao Lupaso, mkoani Mtwara, Julai 29 mwaka huu.

Shughuli za kuuaga mwili wake zinaendelea Dar es Salaam.

1140HRS: Ibada ya kuaga Mwili wa rais Mstaafu Benjamin Mkapa inaelendelea Uwanja wa Uhuru.

MSEMAJI WA FAMILIA: RAIS MKAPA ALIKUTWA NA MALARIA

William Erio, Msemaji wa familia amesema Rais Mstaafu Benjamini Mkapa alipatwa na Malaria Jumatano na akalazwa na kuanza matibabu

Siku ya alhamisi alikuwa anaendelea vizuri, na akaendelea kufuatilia uchaguzi wa kura za maoni uliokuwa unaonyesha mubashara

Baada ya muda, aliinuka alitaka kutoka, alivyoinuka akarudi kukaa na akainamisha kichwa, na akathibitika amefariki kwa mshituko wa moyo, ‘Cardiac arrest’

Msemaji wa familia amewataka watu kuheshimu ukweli huo, na sio kuzusha mambo yasiyo na ukweli kwenye mitandao.

KASEMA;

"Nitoe shukrani kwa Serikali kwa ambavyo wamekuwa pamoja nasi na kushughulikia msiba huu na wanavyoendelea kushughulikia, tunawashukuru kwa uamuzi wa kuanza shughuli ya kuaga kwa Misa Takatifu, tunawashukuru Maaskofu kwa kukubali kuendesha Misa”- William Urio,

“Mzee Mkapa alikuwa hajisikii vizuri akaenda Hospitali akaonekana alikuwa na Malaria akaanza matibabu akalazwa Jumatano,Alhamisi mchana aliendelea vizuri nilikuwa nae hadi saa mbili alikuwa anaangalia Live ya chaguzi za wagombea Ubunge Viti Maalum CCM”-

“Mzee Mkapa Alhamisi usiku baada ya kutazama LIVE ya chaguzi Viti Maalum akasikiliza taarifa ya habari, baadaye aliinuka akitaka kutoka akakaa akainamisha kichwa, walipokuja kumpima wakathibitisha kuwa amefariki, sababu ya kifo cha Mzee Mkapa ni mshtuko wa moyo”-

“Chanzo cha kifo cha Mkapa alipata mshtuko wa moyo, tumeona ni vizuri tuliseme hili kwasababu kumeanza kuwa na manenomaneno kila Mtu akijifanya Nabii katika mitandao ya kijamii na kwingine, tumuenzi Mzee wetu aliyetangulia mbele za haki kwa kuukubali ukweli huo"


View attachment 1517651View attachment 1517650
PICHA: Kutoka Uwanja wa Uhuru DSM ambako imefanyika Misa Takatifu ya kuuaga mwili wa Marehemu Mzee Mkapa kisha Watanzania mbalimbali kupata nafasi ya kupita karibu na Jeneza na kutoa heshima zao za mwisho, haya ndio matukio mbalimbali ya picha uwanjani.
 
Samahani kama mwananchi natamani kufahamu na kujua kama marehemu rais wa awamu ya tatu alikuwa na familia yaani watoto.

Kwa sababu toka msiba uko Dar hadi unagika kijijini kuzikwa sijabahatika kusikia wala kuwaona wanaoitwa watoto wa marehemu Mkapa.

Naomba mwenye ufahamu anisaidie
 
Watanzania wenzangu nimesikitishwa jinsi shughuli ya kumuaga shujaa wetu na muasisi wa wa Tanazania mpya baada ya ile ya Mwl Nyerere.,Ndugu Mkapa. Nahisi watu wa potokali hawajui au kwa makusudi hawakutaka kuwapa watanzania nafasi ya kumuaga Mh Mkapa.

Jna ilikuwa siku ya kumuaga Mh Mkapa kitaifa, nilitegemea kuona makundi mali mbalimali, watu mashuhuri , wasomi wanasiasa jamii ya kimataifa na hata wanafamifilia wakipewa nafasi ya kutoa hotuba za kumuenzi na kuelezea maisha ya Mh. Mkapa. lakini tumeshuhudia mtu mmoja tu akiongea yani raisi Magufuli. Je magufuli anawakilisha mawazo ya watu wote kuhusu hayati Mkapa. Pia maombolezo yametawa;iwa na Ibada kwa kiasi kikubwa , si jambambo kumfanyia ibada, lakini naona imezidi kama vile mkapa alikuwa Kasisi. Ibada hizo zimechukua nasi amboyo ingetumika kuwapa nafasi wanachi kumzungumzia mheshimiwa mkapa.
 
Mkuu, hukusikia Wasifu uliosomwa na Profesa Kabudi jana? Hayati Mkapa ana watoto wawili. Kujionyeshaonyesha, labda, si hulka yao. RIP Mzee Mkapa!
 
Umewaona sasa mkuu au bado?

Maana kama unafuatilia misa Lupaso wala huhitaji utambulisho. Walifanikiwa kumrithi sio tu ufupi ila mpaka miwani zao.

Wewe utakuwa kizazi cha JK, unadhani kila mtoto wa mkubwa ni sampuli ya Riz1.
 
Wafuasi wa cdm wanaopinga pinga kila kitu nadhan mmejifunza kitu lupaso mna kazi sana kuwanyakua hao wapiga kura. Nyomi kama lote
 
Back
Top Bottom