Maeneo yenye baridi la kufa mtu Tanzania

Maeneo yenye baridi la kufa mtu Tanzania

Kwema Wadau!

Mwaka huu DSM kumekuwa na Hali ya hewa ya baridi ambayo imenikumbusha Maeneo yenye hatari kubwa Kwa upande wa baridi.
Watu wengi ambao hawajazunguka hii nchi wanafikiri Arusha na Moshi pekee ndio yenye baridi ya kufa mtu, Kama nawe ni mmoja wapo basi umekosea kabisa, yapo Maeneo ukifika unaweza kukimbia siku hiyohiyo.

Maeneo hayo ni Kama ifuatavyo;

1. Njombe!
Kwa Tanzania hakuna kama Njombe, ukianzia Makete, ludewa, Makambako, huko ukienda ujipange.
Huko ni baridi mwanzo mwisho😃😃.
Yaani ukifika msimu wa baridi ndio Hali unazidi kuwa ngumu.

Arusha na Moshi hapa wakasome Kwanza, Kwanza baridi Yao ni yamsimu, ingawaje yapo baadhi ya Maeneo Kama Rombo huko nako kuna baridi lakini haifikii hayo Maeneo hapo.

Nyumba zote za Maeneo ya Mkoa wa njombe na Iringa zina madirisha ya vioo na Dari za mbao kuepusha baridi kuingia lakini bado utaisikia tuu na lazima ufunike Yale mablanket makubwa.

2. Iringa, hasa wilaya Mufindi, Mafinga.
Mafinga na Makambaku ni pua na mdomo, Hali ya hewa zinafanana. Baridi mwanzo mwisho. Yaani miezi yote 12 baridi lipo, sema kuna kipindi linapungua lakini kipindi cha kiangazi baridi lake ni Sawa na kipindi cha baridi la baadhi ya mikoa Kama Pwani, na Dar, Dodoma, Singida, tabora n.k

3. Arusha.
Wakati mwingine watu waarusha baridi Lao wanadhani ndio linaongoza Tanzania lakini kimsingi sivyo, wao wanaweza kushika nafasi ya tatu wakichuana na Kilimanjaro.

4. Kilimanjaro, hasa Maeneo ya Moshi, Rombo, Moshi vijijini, Hai, Usangi, Chome, Suji, Tae n.k
Baridi la Maeneo ya marangu ukipanda Mlima Kilimanjaro nalo ni Kali, lakini haliumizi Kama lile baridi la Mafinga, au njombe huko.

5. Tanga, Lushoto.
Milima ya usambara imechangia Kwa kiasi kikubwa kuifanya wilaya ya lushoto na Maeneo ya karibu yanayozunguka Maeneo hayo.

6. Mbeya, Maeneo ya Mbeya Mjini, Rungwe, na Tukuyu kuelekea Kyela,
Baridi la Mbeya ni Kali ingawaje linamsimu wake..

7. Ruvuma
Ukaribu wa Songea na mkoa wa njombe ni Kama ilivyo Kwa ukaribu wa Moshi na Arusha.

Sehemu hizo Kwa hapa Tanzania kama unataka kujua nini maana ya baridi basi fika sehemu hizo, ingawaje yapo Maeneo mengine ya Mikoa Kama Morogoro Kama Turiani, na Maeneo ya Singer na Rukwa.

Nawasilisha
Mbona umepasahau na Manzese Dar es Salaam na kwenyewe kuna Baridi hakuna Mfano.
 
Niliwahi kuishi Mahenge Mkoani Morogoro, nako si haba kwa baridi. Tena ni ya mwaka nzima haina msimu.
 
Mleta mada na washirika wako naona bado hamjakanyaga Sumbawanga na inaonesha wengi hamjui hali ya kule. Msimamo ni huu hapa

1. Njombe
2. Iringa
3. Mbeya
4. Sumbawanga
5. Arusha

Tembeeni jamani
 
Sehemu zenye bardi ni
1.Njombe hasa makete
2.Ruvuma hasa mbinga
3. Mufindi iringa
4.Mbeya
5. Rukwa eg Sumbawanga
6.Manyara ( Kateshi ) & some part of Singida
7. Arusha & na baadhi ya maeneo ya Kilimanjaro eg Rombo, Sanya juu
8. Lushoto Tanga
9.Kigoma ndani ndani huko
 
Naona mnaitajataja Arusha kwa dharau ila wenyewe wenye uzoefu na baridi wanasema baridi ya Mbeya haichomi, niko na mzaliwa wa Mbeya hapa Karatu anatamani kurudi kwao.

Hata watu wa Arusha hawajui km Karatu kuna baridi la hatari, njooni mfanye utalii wa ndani mkasimulie.
 
Umesahau kuiweka tanga...lushoto
Na sehemu za korogwe huko milima ya usambara mzee huko juu sahv
Ni giza kuna wakati inagonga mpaka 7,8

Ova
 
Baridi ya Njombe ukitaka Kuoga maji unachemsha Maji ya moto halafu unachemsha Mengine ya Vuguvugu kwa ajiri ya kupoozea ndio uoge sasa....😂😂
 
Joto halipo Dar tu
Hata Moro Kuna mazao kibao yanalimwa na yanawahi kukomaa sababu ya joto.

Baridi ya Njombe ukitaka Kuoga maji unachemsha Maji ya moto halafu unachemsha Mengine ya Vuguvugu kwa ajiri ya kupoozea ndio uoge sasa....😂😂
Mimi nipo Njombe na kila siku naoga maji ya baridi. Asubuhi hii nimeoga maji ya baridi najisikia vizuri sana. Ni kujiendekeza tu kuoga maji ya moto
 
Nimeishi Mufindi, Mbeya na Arusha,
Kuhusu Njombe na Mufindi wala sina shaka ndizo sehemu zinazoongozoea kwa baridi.

Baridi ya Mbeya ikifika mwezi wa 6 huwa ni kali kiasi kuliko ya Arusha.

List iwe hivi

1.Njombe
2.Iringa
3.Mbeya
4.Arusha
Njombe
Marangu
Mbeya
Iringa
Arusha
°°°°°°°°°°°°
 
Kimsingi njombe ndio alfa na omega kwa mikoa ya baridi hapa nchini.


Best place kwangu kuishi ni mikoa ya ukanda wa pwani na kanda ya ziwa.

Baridi siliwezi kabisa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom