Maharage Chande aondolewa TANESCO, apelekwa TTCL. Gerson Msigwa awa Katibu Mkuu Wizara ya Michezo
Kazi inaendelea kwa baraka nyingi...[emoji120]

Eeh Mwenyezi Mungu tutunzie Samia wetu ,aamen aamen[emoji120]
 
Enzi za magufuli hao waliobadilishwa taasisi wasingepelekwa taasisi zingine wakashindwe na huko, wangewekwa kando wajitathimini kama wanafaa tena kupata uteuzi. Huyu wa TANESCO ndiyo kabisa angepumzishwa ajitafakari kama anaweza kuongoza shirika jingine ikiwaTANESCO ilimshinda
 
Hapo watu washatajirika na kuseti mipango ya utajiri wa maisha na watoto wao.Then wanapelekwa kwengine kuweka mazingira....Tutakuja tu kusikia Tukio huko Jikoni panapopikwa hayo Maharage
 
Naona Kikeke au Kitenge akipewa nafasi ya usemaji ila hasa hasa anaweza kupewa Kitenge kwa sababu amesimama sanana udhalimu wa Liliondo akifanya coveragw kubwa sana kuwafunika wauaji.
Nimekaa pale
Mtu darasa la saba kama Kitenge apewe kitengo kweli?
 
𝑨𝒍𝒊𝒍𝒊𝒇𝒂𝒏𝒚𝒂 𝑺𝒉𝒊𝒓𝒊𝒌𝒂 𝒍𝒂 𝒖𝒎𝒆𝒎𝒆 𝑻𝒂𝒏𝒛𝒂𝒏𝒊𝒂 𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒍𝒂 𝒉𝒐𝒗𝒚𝒐. 𝑺𝒂𝒔𝒂 𝒂𝒎𝒆𝒉𝒂𝒎𝒊𝒔𝒉𝒘𝒂 𝒌𝒘𝒊𝒏𝒈𝒊𝒏𝒆 𝒊𝒍𝒊 𝒂𝒌𝒂𝒇𝒂𝒏𝒚𝒆 𝒚𝒂 𝒉𝒐𝒗𝒚𝒐!
 
Ikitokea kapewa Kitenge nitaamini kwamba hili taifa limeoza kwa kiwango cha mwisho kabisa na kwamba hakuna namna ya kulirekebisha zaidi ya mapinduzi.

Itakuwa ni dharau kubwa sana.
Watakuwa wametudharau sana watanzania.
 
Sababu ni private sector na marketing strategy ya sehemu kama DSTV mchoro wake hutoka kwa makaburu, hizi sub offices zinakuwa zinafuata tu...
Lakini dstv tz iko chini ya mbongo
Na inaendeshwa vzr tu
Ttz mashirika ya umma ni mtihani sana

Ova
 
Salim usela umezidi alafu pia Hangaya hamkubali kivile maana interviews zake nyingi akiwa anamuhoji pale BBC zilikuwa zinamfanya madam aonekane mweupe kichwani na mwisho wa interview alikuwa anafura kweli kweli
Ile kuhusu katiba[emoji23][emoji23]
Eti watanzania wanasema wametaka katiba mpya
Wamekuambia wewe?[emoji1787]
 
𝑨𝒍𝒊𝒍𝒊𝒇𝒂𝒏𝒚𝒂 𝑺𝒉𝒊𝒓𝒊𝒌𝒂 𝒍𝒂 𝒖𝒎𝒆𝒎𝒆 𝑻𝒂𝒏𝒛𝒂𝒏𝒊𝒂 𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒍𝒂 𝒉𝒐𝒗𝒚𝒐. 𝑺𝒂𝒔𝒂 𝒂𝒎𝒆𝒉𝒂𝒎𝒊𝒔𝒉𝒘𝒂 𝒌𝒘𝒊𝒏𝒈𝒊𝒏𝒆 𝒊𝒍𝒊 𝒂𝒌𝒂𝒇𝒂𝒏𝒚𝒆 𝒚𝒂 𝒉𝒐𝒗𝒚𝒐!
Ngoja tuone kama umeme hauta katika katika tena.
 
This is the huge Public deceiving ( shame kwa SHH), ivi kweli mtu kama Maharage kaharibu sehemu then anateuliwa tena sehemu kweli? Kweli jameni?

Kwamba kwa watanzania zaidi ya 20million wenye uwezo na sifa hawaonekani mpaka aliyeharibu point A kuhamishiwa point B kweli? Kweli SHH?

This proves the fact kwamba , Maharage alitumwa kukwapua na kahamishiwa TTCL akaharibu then aje na wazo la kubinafsisha, CCM ni zaidi ya ukoo wa Panya.

Huyu mwamba yangefanyika mawili kama angekuwa kwenye nchi zenye viongozi na uongozi, sio hawa wachumia tumbo,

Mosi, astaafishwe for the public interests

Pili, afunguliwe mashtaka maana tuhuma zake zinathibitika vizuri tu.


Haya yote yana mwisho.
Mwache akaonyeshe uwozo wake pengine kulikua na external influence ya aliyemweka ie makamba, kwa vile Sasa kamaminiwa na rais Moja kwa Moja ataonyesha uwezo.
 
Aisee hii kali kabisa. Ila Kwa nionavyo Mimi.
1. Wizara ya Nishati arudishwe Muhongo.
2. Maharage Chande hata kama uraiani tunaona hajafanya vizuri Ila ndani Tanesco aliwanyoosha Sana wezi. Yaani zile njia za wizi zote alikomesha na Shirika hata mahesabu yake yakaanza kuwa mazuri. Na ninajua kwa kuwanyoosha basi wafanyakazi wakaanza kuhujumu ili aonekane hawezi. Ninakuhakikishia Leo wafanyakazi wa Tanesco watafanya sherehe kwa kuwa fursa za ulaji zitarudi. Yaani walibanwa. Mfano wafanyakazi ofisi za kanda, mikoa na Wilaya walikuwa ni wengi na hakuna KAZI ya maana. Yaani kuajiriwa tu kinansmnanamna unaenda tu kukalia viti vya Tanesco kunywa chai na supu na kupiga umbeya. Huo ukawa mzigo mkubwa Sana kwenye payroll mana unakuwa na wafanyakazi wengi ambao hata hawahitajiki. Kwenye emergency na call ndiyo walipiga mno mno na ndiyo akaweka one call centre. Na wako smart kugawa majukumu kwa zone au ofisi husika ila nako wakawa wanafanya kwa hujuma kutekeleza matatizo ya umeme yaliyokuwa Yana repotiwa centre. Yaani unakuta taarifa ya emergence imeletwa say Tanesco Kurasini lakini warakaa siku hata 3 hawaendi kwenye tukio. Mfano mmoja Mimi binafsi nilipiga simu call centre kuhusu nguzo ya umeme ilivyokuwa hatarini kuanguka. Hakika hawakufika mpaka ikaanguka na ikawagharimu Sana. Niliporudi call centre kuwajulisha walishangaa Sana maana taarifa walishapewa Tanesco Kurasini Ila haikutekelezwa kwa siku 7. Yaani ni kama kulikuwa na kamgomo baridi hivi ili kukwamisha utendaji wa Maharage Chande.

Ila pia hata kama ameondolewa tatizo la umeme halitakwisha kamwe. Kuna hujuma nyingi mno. Hivi.mnajua kuna wauza majenereta? Hivi mnajua kuna fisadi mmoja god father wa Mwezi Mosi anamiliki kampuni ya gas tunazotumia kupikia na mambo mengine?. Ambaye ndiye alikuwa anampa kazi Mwezi Mosi kupigia kampeni gas yake nyumba kwa nyumba? Haya mambo ni magumu kuliko mnavyofikiria mtaani kwetu huku.
Mambo yamekuwa si mambo. Mungu tunusuru tuko kwenye lindi la mahangaiko mengi Sana. Yaani tumesongwa na mambo mengi mno.
Yaani nimechoka Sana Mimi Zogwale.
 
DSTV hilo nalo shirika jamani.Kishirika kidogo,halafu offers zake sio basic needs kwa binadamu. Unaweza ukawa hauna DSTV na maisha yakaenda safi tu.Ila Tanesco hakuna mbadala. Halafu Umeme ni moja ya ni basic needs nchini .
Mwambie hata DSTV Iko hoi bin taaban. Ilikuwa kidogo tu ifungwe
 
Back
Top Bottom