Makamu wa Rais Dkt. Mpango apiga marufuku Polisi kufunga Barabara kwenye Misafara
Nadhani ujamuelewa.

Kuna magari yanasimamishwa muda mrefu hata masaa 4 wakati hata msafara aujaanza kuondoka.

Kuna siku nilishangaa tulisimamishwa kwenye highway kwa masaa 2 sababu ya mwenge wa uhuru alafu mwenge wenyewe ulikuwa unatokea kwenye barabara ya vumbi unakwenda kama mita 500 kutoka kona ya barabara ya vumbi kuingia kwenye highway hadi kwenye jengo nadhani kulikuwa na uzinduzi.

Wale askari niliwashangaa sana, nikasema uwezo wao wa kufikiri na kufanyakazi ni finyu.
 
Halafu kanichefua alipochomekea eti "mtoto wa masikini Mpango anapita" hawa watu ndo maana miaka na miaka bado wametuweka utumwani maana hawana akili wala utashi wa kuchukia umasikini. Mtu kujiita maskini anaona sifa sana alale kwenye nyumba ya tembe basi.
Huo ni unafiki wao wa kutukana masikini
Kama amesema hivyo basi ni msemo wa kukejeli masikini

Wakati mwingine mnawapuuza hata wakisimama mnatawanyika tu
Hizo ndio zao ooh mtoto wa masikini
Wanajua umasikini ni laana na wanatuchora tu
Ana umasikini gani si atembee kwa miguu sasa
 
Mtoa mada, ulitaka kujenga hoja mzuri,
Ila ulivyochomekea ishu ya barakoa na njanjo nimekudharau Sana!
Lini Taifa lilizuia watu wasivae barakoa na wasipate chanjo?
Nani alikamatwa na polisi kwa kutafuta barakoa yake au chanjo yake?
Unataka uveshwe barakoa kwa nguvu ndio uone kuwa serikali haizuii kuvaa barakoa!
Je, serikali inakamata watu kuwavesha kondom?
Wangapi wameshakufa kwa Ukimwi?

Watu walivaa barakoa na watu walichanja!


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani Mzee Filipo kabla ya kuongea hoja yake, alitakiwa aulizane na wataalamu wa usalama kwa nini wanataka barabara iwe wazi, na jinsi gani yeye akiwa anataka kupita sehemu, basi apite kwa wakati aliowaahidi Polisi. Kuliko achelewe na apite nje ya ratiba aliyoahidi wana usalama, halafu alalame

Zile confidence za enzi za corona kukataa chanjo na kuacha kuvaa barakoa, tuliona matokeo yake, pia taifa lina kumbukumbu ya ajali ya Edward Moringe Sokoine, taifa haliko tayari kurudia makosa.

Kiongozi mwizi wa kura akifa hakuna tatizo lolote boss.
 
Nadhani ujamuelewa.

Kuna magari yanasimamishwa muda mrefu hata masaa 4 wakati hata msafara aujaanza kuondoka.

Kuna siku nilishangaa tulisimamishwa kwenye highway kwa masaa 2 sababu ya mwenge wa uhuru alafu mwenge wenyewe ulikuwa unatokea kwenye barabara ya vumbi unakwenda kama mita 500 kutoka kona ya barabara ya vumbi kuingi kwenye highway hadi kwenye jengo nadhani kulikuwa na uzinduzi.

Wale askari niliwashangaa sana, nikasema uwezo wao wa kufikiri na kufanyakazi ni finyu.

Mkuu hakuna askari hapa Tanzania, kuna robot zilizovaa nguo za polisi.
 
Halafu kanichefua alipochomekea eti "mtoto wa masikini Mpango anapita" hawa watu ndo maana miaka na miaka bado wametuweka utumwani maana hawana akili wala utashi wa kuchukia umasikini. Mtu kujiita maskini anaona sifa sana alale kwenye nyumba ya tembe basi.
Dokta wa uchumi anazeeka na umasikini, tena akiwa kiongozi namba mbili wa kitaifa, Waziri wa miaka mingi
 
Mnapoiambia Dunia kuwa TANZANIA ni kisiwa Cha AMANI, Huwa mnamaanisha nini?

Kiongozi wa wananchi akipita spidi ni 120. Yaani anakimbizwa Kasi kuzidi AMBULANCE ya kuwahisha wagonjwa.!!!!

Jiji kama Mwanza kuzuia Kwa 4hrs Si sawa.

Viongozi wa Nchi MASKINI wanalindwa kuliko msafara wa kusafirisha PESA.

Hii Si sawa.
Nchi Ina amani, lakini haiondoi ukweli kwamba Mdude Nyagali alishawahi kuahidi mitandaoni kwamba ana hamu ya kujilipua kama Al-Qaeda au Al-Shaabab, na kwamba anatafuta timing tu
 
Nadhani Mzee Filipo kabla ya kuongea hoja yake, alitakiwa aulizane na wataalamu wa usalama kwa nini wanataka barabara iwe wazi, na jinsi gani yeye akiwa anataka kupita sehemu, basi apite kwa wakati aliowaahidi Polisi. Kuliko achelewe na apite nje ya ratiba aliyoahidi wana usalama, halafu alalame

Zile confidence za enzi za corona kukataa chanjo na kuacha kuvaa barakoa, tuliona matokeo yake, pia taifa lina kumbukumbu ya ajali ya Edward Moringe Sokoine, taifa haliko tayari kurudia makosa.
Kwahyo unataka kusema yeye kaongea bila kuyajua yote hayo?!
 
Nadhani Mzee Filipo kabla ya kuongea hoja yake, alitakiwa aulizane na wataalamu wa usalama kwa nini wanataka barabara iwe wazi, na jinsi gani yeye akiwa anataka kupita sehemu, basi apite kwa wakati aliowaahidi Polisi. Kuliko achelewe na apite nje ya ratiba aliyoahidi wana usalama, halafu alalame

Zile confidence za enzi za corona kukataa chanjo na kuacha kuvaa barakoa, tuliona matokeo yake, pia taifa lina kumbukumbu ya ajali ya Edward Moringe Sokoine, taifa haliko tayari kurudia makosa.
Hujui ulisemalo ngoja nikusamehe tu
 
Tuna mambo ya hovyo sana.

Nchi hii, kwa kiasi kikubwa, umaskini unachangiwa na Serikali na watendaji wake.

Serikali haioni thamani ya muda. Kuna wakati nakumbuka nilikuwa Mwanza. Saa 9 alasiri tumesimamishwa Nyegezi kupisha msafara wa Waziri Mkuu. Muda huo wa saa 9, Waziri Mkuu alikuwa Shinyanga. Halafu alipotoka Shinyanga akasimama Misungwi kuwasalimia wananchi.

Mwanza alifika saa 12.30 jioni
Yaani zaidi ya masaa 3 wananchi wamesimamishwa eti kupisha msafara wa Waziri Mkuu.

Fikiria watu wamesimamishwa tokea Nzega mpaka Mwanza. Ni watu elfu ngapi. Kama watu ni watu 10,000 shughuli zao zimesimama, na kama kila mmoja anaingiza sh 20,000 kwa saa, ina maana ni sawa na 20,000 x 3 x 10,000 = 600,000,000. Hiyo ni kwa siku 1 na kwa kiongozi mmoja. Bado kuna Rais, Makamu wa Rais, siku hizi mpaka makamanda wa polisi wakipita mnasimamishwa. Kwa mwaka, mambo haya ya ajabu yanaliingizia Taifa hasara kiasi gani?

Nadhani tatizo kubwa ni uwezo mdogo wa Polisi wa kufikiri na kupanga. Kinachofanyika hakistahili kuwa hivyo. Uwekwe utaratibu ambao utazuia kuwasimamisha wananchi zaidi ya nusu saa kupisha misafara ya viongozi wa kitaifa.

Huu upuuzi haupo kwenye mataifa yaliyoendelea. Sisi maskini tuliotakiwa kuutumia muda vizuri zaidi, ndiyo tunaoongoza katika kutothamini muda. Umaskini wa kichwani unatufanya kuwa maskini wa kila kitu, isipokuwa kuzaliana..
Nakaziaaaa
 
Nadhani ujamuelewa.

Kuna magari yanasimamishwa muda mrefu hata masaa 4 wakati hata msafara aujaanza kuondoka.

Kuna siku nilishangaa tulisimamishwa kwenye highway kwa masaa 2 sababu ya mwenge wa uhuru alafu mwenge wenyewe ulikuwa unatokea kwenye barabara ya vumbi unakwenda kama mita 500 kutoka kona ya barabara ya vumbi kuingi kwenye highway hadi kwenye jengo nadhani kulikuwa na uzinduzi.

Wale askari niliwashangaa sana, nikasema uwezo wao wa kufikiri na kufanyakazi ni finyu.
Umaskini wa akili inaigharimu sana Afrika.
 
Dokta wa uchumi anazeeka na umasikini, tena akiwa kiongozi namba mbili wa kitaifa, Waziri wa miaka mingi
Inashangaza sana mkuu, mtu ana uhakika wa kuhudumiwa yeye na familia yake, kwa kodi zetu mpaka anakufa,

Leo anajiita mtoto wa masikini? Hata kama alizaliwa katika familia masikini, ina maana muda wote aliofanya kazi, tena msomi wa PhD, alishindwa kuondoa umaskini kwao?

Kuitwa masikini, au mnyonge sio sifa nzuri hata kidogo,

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Mimi niseme tu kuwa nchi hii kila kitu ni ku exaggerate. Kuanzia dini(ulokole) ni kukuza mambo tu tofauti na uhalisia na maandiko, magonjwa(Afya) , Ushoga/Usagaji na hata suala la Usalama ni too much exaggerated tofauti na uhalisia. Yaani ni kutiana hofu tu kuwa kuna tatizo kuuuuuubwa. Ndio maana mnaweza kusimama masaa manne kusubiri msafara.
 
Dokta wa uchumi anazeeka na umasikini, tena akiwa kiongozi namba mbili wa kitaifa, Waziri wa miaka mingi
Mshahara haumfanyi mtu kuwa tajiri, labda awe mwizi.

By being employed, you will never become rich. Because what makes someone rich is the profit. If you are employed, profit and loss go to your employer. You right is only your wage. Unless your convert your wage into capital so that you generate profit.

Dr. Mpango kama hafanyi biashara yoyote, na hajawekeza kqenye mradi wowote, na siyo mwizi, ni sahihi kuwa siyo tajiri. Na asiye tajiri ni maskini.
 
Back
Top Bottom