Makonda ajibu tuhuma za kumpiga risasi Tundu Lissu. Asema Lissu ana matatizo ya akili, aende Milembe

Makonda ajibu tuhuma za kumpiga risasi Tundu Lissu. Asema Lissu ana matatizo ya akili, aende Milembe

Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu, leo akiwa anawasilisha ripoti yake ya miezi 6 ya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Makoa ameamua kujibu mapigo.

Kama mtakumbuka, wiki chache nyuma Lissu alimtuhumu Makonda kuhusika na jaribio la kumuua lililofanyika mwaka 2017.

Akiongea na wanahabari leo, Makonda amekana kuwa hakuhusika na shambulio la Lissu na kuongeza kuwa Lissu kwa sasa anapitia msoto mkali sana wa kisiasa na anamtumia yeye kama ngazi ya kurudi kwenye siasa.

"Kaka angu Tundu Lissu nimemsikia hata mimi lakini kwa hali aliyonayo siwezi kumshangaa. Na nafarijika kuona kwamba ameniona nafaa kumsaidia kujenga career yake ya kisiasa kwenye taifa letu, Na mimi sitaki kumjibu kwa sababu nikimjibu ntamuaibisha kaka yangu yangu"

"Watu wa Clouds wakirudi nyuma siku ya tukio watakumbuka hata siku tukio linatokea mimi nilikuwa Dar Es Salaam uwanja wa mnazi mmoja tulikuwa na kampeni ya matibabu. Kwa hiyo hata sehemu ya tukio sikuwepo"

"Ushauri pekee ambao ningewapa nyie wanahabari, mjitahidi sana kuangalia mtu mnayemuhoji yupo katika wakati gani. Na kwa kuwa alisemea Dodoma nilitegemea mumuombe apite Milembe aone kama yuko sawa au"
Pia ajibu zile tuhuma za wale wamarekani walio sema asije akaenda kwaoaana ni muuaji na mtesi wa maisha ya watu
 
Kwa hili, ni kwa wasio na akili pekee wanaweza kumsikiliza na kisha kumwamini mtu huyu ambaye facial expression yake, maneno yake ni purely yako under the influence ya ujanja ujanja wa kishetani tu..!!

Bora angenyamaza au angejibu kwa kifupi tu, "siyo kweli, sihusiki kwa lolote juu ya shabulio hilo"

Lakini maelezo yake mengi yasiyoeleweka kwa wenye akili, ndiyo yanayom - expose zaidi yeye na serikali yote na hususani jeshi la polisi kwa kushindwa kuchunguza tukio hilo baya kabisa kwa vusingizio vya kipuuzi na kijinga tu...

Dhambi kubwa ya serikali ya CCM na hususani Jeshi la Polisi ni kukataa kutenda wajibu wanapaswa kuutenda. Na mshahara wa dhambi ni MAUTI siku zote. Hakika watakufa tu hawa...!!

Na polisi hawachunguzi kwa sababu wahusika ndio hawa kina Makonda (ma-boss wao) ambao leo wako madarakani na wana abuse madaraka huyo kuyatumia kama koti la kujifunika ili kulinda dhambi na uhalifu huu...

Lakini siku watayapoteza tu madaraka haya na Mungu kuwapa watu wengine na ndiyo itakuwa mwisho wa hilo koti lao hilo la ulinzi (madaraka ya kiserikali) walilolivaa kulinda dhambi na uovu wao dhidi ya binadamu (evil against humanity)....

Nawahakikishia leo kwamba hawa watakuja kufia jela au watakuja kunyongwa hadharani hadi wafe kwa dhambi zao hizi...!!

Kama wana akili wangeacha janja janja yao hii na badala wawe wanyenyekevu na kujua kuwa yupo aliye mkuu kuliko wao na ndiye huyo aliyewapa madaraka hayo kwa kusudi maalumu....

Unyenyekevu unspaswa uambatane na toba kwa watubia makosa na dhambi zao hizi ili Mungu wa mbinguni awarehemu na kuwasamehe ili siku wakinyang'anywa madaraka hayo ya kiserikali, waweze kuishi kwa amani..

Mungu hadhihakiwi eti...

Mwenye kusikia na asikie
 
Kiaje mkuu?
Sasa Trump Serikali yake ilimtaja kama mtu hatari Kwa maisha ya watu na kumpiga ban na akaondoahwa uongozini,

Trump arudi tena, mamlaka hazina budi kumtosa tena ,

Na hapo ndipo kiwewe chake kinapoanzia.
 
Sasa Trump Serikali yake ilimtaja kama mtu hatari Kwa maisha ya watu na kumpiga ban na akaondoahwa uongozini,

Trump arudi tena, mamlaka hazina budi kumtosa tena ,

Na hapo ndipo kiwewe chake kinapoanzia.

Nimekuelewa hapo mkuu.

Na huyu Secretary of state mpya aliyechaguliwa na Trump ndo kichaa kabisa

Ngoja tuone mkuu
 
Mimi nafikiri Watanzania wanaomuamini huyu Zerobrain BASHITE ndiyo wapumbavu. Waache waendelee kutumika. Mtu aliyeshindwa hata kupata D mbili kwenye NECTA hawezi kuwa na fikra chanya. Ukiangalia tu sura ya Bashite na alivyojaza msambwanda hakuna namna anaweza kuwa na akili kichwani

Mkuu mbona una hasira sana.
 
wamuulize kuhusiana na ile issue ripoti ya nape dhidi yake.
Kwani crip hiyo iliwahi kutolewa mahali?

Maana nakumbuka alipokuwa njiani kwenda kukisanua, akawahiwa na mitutu ya bunduki njiani.

Hajakaa sawa, fukuza na uwaziri mazima.
Sasa ni lini ilisomwa, au ilivuja?
 
  • Thanks
Reactions: al1
Makonda anadai tarehe 7 SEPT 2017 hakuwepo Dodoma, alikuwa Dar Es Salaam. Sasa inabidi tupate majibu yasiyo na shaka kama ni kweli, au uongo.
Akosokekane Ikulu iliyo ndani ya mkoa wake ambako boss wake (Rais wake) alikuwa na shughuli maalumu ile ya kupokea ripoti ya makinikia...?

Hivi wewe unadhani ni shughuli gani ambayo ni muhimu zaidi ambayo RC wa DSM siku hiyo alikuwa anaifanya ndani ya mkoa wake huku aliyempa huo u - RC akiwa na kazi maalumu na muhimu ndani ya mkoa wake siku hiyohiyo huku viongozi wote muhimu wa kitaifa Jaji Mkuu, Spika wa Bunge, IGP, CDF, mawaziri, ma - DCs na ma - RCs wa mikoa mingine wakiwa pale...?

Hivi mnawezaje kudanganywa na kudanganyika kirahisi hivi na mtu huyu asiye na utu wala akili kabisa ya kuongea uongo huu huku dunia nzima ikimtazama..??
Makonda anaweza kuwa amehusika, lakini sio lazima kwamba alikuwepo Dodoma. Pia Makonda anaweza kuwa alikuwepo na hakuhusika. Na anaweza kuwa alikuwepo Dodoma, na alihusika...
Haya ni mawazo yako na ni mtazamo wako...

Lakini, jaribu kutumia circumstancial evidences na mlolongo wa matukio mabaya kumhusu kisha umpe hukumu yake..

Rafiki bangusule, ushahidi wa kimazingira kwa tukio hili, unamfunga na kumlalia huyu jamaa kila kona. Ni bora angekaa kimya kama alivyokuwa ameamua kukaa kimya kuliko kupanua mdomo wake kujitetea kwa uzushi na uongo...!
Vilevile Makonda anaweza kuwa alikuwa Dar Es Salaam, ktk shughuli zake kama RC,
Ndugu, are you really thinking straight kweli...?

Aalikwe wapi na nani siku hiyo wakati boss wake Rais alikuwa na shughuli maalumu Ikulu ndani ya mkoa wake na viongozi karibu wote na baadhi ya RCs wenzake wakiwa wako pale..?

Mwaliko wowote kiprotokali kwa siku hiyo ulikuwa uwe surpassed na tukio la ikulu alikokuwa boss wake akifanya kazi hiyo muhimu ya kitaifa.....

Nakushauri tu kuwa, fikiri vizuri na kamwe usikubali kudanganyika na uongo huu toka kwa mtu huyu ambaye ameshakomaa kutenda uovu kwa kutumia madaraka yake vibaya (abuse of power) kwa kiasi cha kuwa sugu na kukosa hata tone la aibu..!
na baadae akapanda ndege kwenda Dodoma kuwahi "shughuli" ya Tundu Lissu.
Haa haa😁😁😁..

Sasa hapa umesema ukweli wako. Hata hivyo aliwahi tukio la Tundu Lissu wapi? Akiwa hospitalini au asubuhi kabla hajapigwa risasi? Funguka tukuelewe...
KInachotakiwa ni ushahidi usiokuwa na mashaka.
Kwanini msingemwambia awaoneshe hiyo tiketi ya ndege aliyopanda siku hiyo wakati mnamuuliza mawali huko Arusha leo? Na alipanda ndege ya shirika gani, ATCL au Precision ili tukafukue kwenye data base..?
 
Anamaanisha pia Pompeoz alikuwa na matatizo ya akili kumpiga ban ya kuingia states of....?
 
Back
Top Bottom