Either Jamii Forums ina watu wengi wasiotumia akili au Kuna tatizo mahali. Hivi nikianzisha kampuni hewa au mradi wa kitapeli lakini ikawa huko nyuma nilisoma na mtu ambaye kwasasa ni Waziri au kiongozi serikalini, kwenye uzinduzi wa kampuni yangu feki nikamualika huyo rafiki au msela wangu awe mgeni rasmi lakini yeye Kama yeye. Na yeye bila kujua au vyovyote akahudhuria na suti kubwa na mapicha kibao. Ikija kugundulika baadae kampuni ni ya kitapeli serikali inahusikaje!???... Kuna mtu aliwahi kuifungulia kesi Qnet!?. Kwamba katapeliwa na serikali ilizindua!??.... HAPANA. Matapeli wengi huwatumia watu maarufu au viongozi wakubwa kuwaaminisha watu kuwa wapo salama. Hata Moshi kwa Sabaya walimu walihamasika baada ya kuona yule kiongozi wa serikalini yupo Qnet na ndo anayewashawishi. Kama umewahi kumtembelea tapeli yeyote anayeaminika hata bongo huwezi kukosa picha ukutani aliyopiga na Mkapa, Kikwete hata Kenyatta. Kuna mzee mmoja tapeli wa kimataifa anaishi Kijitonyama niliwahi kuingia kwake nikakuta kapiga picha na Clinton na ni miaka ya 2001, technology ilikuwa haijakuwa kivile na isingeweza kuwa Photoshop. Nilimuogopa sana, na wengi walilia sana.Mkubali mkatae Watanzania wengi ni WAPUMBAVU na wabishi. Wakishapigwa wanarudi kuilalamikia serikali. Hivi unauziwa saa dola 2000($2000) na unakubali!??.. kisa kazindua Kigwangala!??.. ni akili au matope?!?.. na unaambiwa ili ela yako irudi mpaka utafute MAFALA wengine nao wanunue saa $2000 ndo uanze kupata $200 kwa aliyejiunga, ela yako itarudi lini kwa uchumi wa mtanzania??!, Na mnaomsapoti mleta mada wote ni WAPUMBAVU vilevile.