babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 14,478
- 18,341
Hawa watoto watafika miaka 18 wakute mama yao na hela na wao wamechoka sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapana si unaona mfano hapa ada ni kwa mwaka. Bima kwa mwaka matumizi ni kwa mwezi.Sio kwa mwaka bwana, sio kwamba ni zote kulwaajili ya kuwalea hadi miaka 18??
Haya maisha hayana mwenyewe unaweza kuanza vizuri ukamaliza vibaya kabisa hajawahi tokea.. hii mbilinge inanikumbusha stori ya samson na delila.. so sad
Mahakama imeeleza kuwa uamuzi wa kiasi halisi kinacholipwa lazima ufanywe kwa kuzingatia njia na hali ya maisha ya baba. Mawasilisho na viambatanisho vinadhihirisha kuwa kabla ya kifo cha marehemu alikuwa akitoa kiasi kilichoombwa kutokana na uwezo na hadhi yake. Marehemu alikuwa baba mzazi wa watoto walioitwa.
Mahakama pia imesema kuwa Mwombaji ametaja biashara nyingi kuwa ni ushahidi wa mapato yanayotokana na biashara inayohusishwa na mirathi, hata hivyo watu aliyowaomba matunzo mbele ya mahakama ni wasimamizi wa mali za marehemu.
Mapato yanayotokana na mirathi ya marehemu si mali ya walalamikiwa pekee bali ni mali ya mirathi ambayo imeshughulikiwa mbele ya Mahakama ya Mirathi. Waliyohojiwa wangekuwa baba mzazi wa watoto Mahakama ingewashikilia vinginevyo.
Kwa kuwa hakuna ubishi kwamba mhojiwa kwa nafasi yake ya wasimamizi wamewajibika kuwakimu watoto mahitaji ya msingi, wanapaswa kuendelea na malezi ya watoto kulingana na uwezo na nafasi zao.
Pia, suala la pili la uamuzi ni suala la malimbikizo na amri inayowataka walalamikiwa kutoa matunzo kwa watoto waliotajwa hadi watimize umri wa miaka 18. Ni ukweli kwamba Sheria ya Mtoto ilitungwa ili kuhudumia ustawi wa mtoto. Hata hivyo, tangu awali ni lazima ieleweke kwamba usimamizi wa mali ya marehemu sio jukumu la kudumu.
Kutokana na maelezo ya pande zote, hakuna ubishi kuwa katika shauri la mirathi namba 39 la mwaka 2019 walalamikiwa waliotajwa waliteuliwa kuwa wasimamizi wa mirathi ya marehemu Dk. Reginald Abrahaman Mengi.
Kwa mujibu wa kifungu cha 109 cha mirathi na usimamizi wa Sheria ya Mali majukumu ya wasimamizi ni kukusanya na kusambaza mali za marehemu kwa warithi halali. Jukumu hilo linaisha mara baada ya wasimamizi kuwasilisha hesabu. Mapato ambayo mwombaji anaomba kutunza watoto wake hadi watimize umri wa miaka 18 yakitoka katika mirathi ya marehemu ambapo walalamikiwa ni wasimamizi tu na sio wamiliki.
Kesi ya uthibitisho ni mbele ya mahakama kuu kwa hivyo mahakama ya watoto sio mahakama inayofaa kwa mwombaji kuomba maombi haya. Kadhalika, mahakama hii haiwezi kuwaamuru walalamikiwa kama wasimamizi wa mali za marehemu walipe malimbikizo kutokana na jinsi marehemu alivyokuwa akitunza watoto wake enzi za uhai wake.
Marehemu alikuwa akitoa mahitaji ya watoto wake kwa vile alikuwa baba mzazi wa watoto waliotajwa, na njia na namna zake zilifanikisha mipango yake. Waliohojiwa si wazazi wa watoto, wao ni walezi tu na wasimamizi wa mali za marehemu.
Zaidi ya hayo, kwa kuwa kuna kesi zinazoendelea za mirathi ambazo zote zinalenga kuhakikisha mirathi ya marehemu inagawiwa kwa haki kwa warithi halali, ni vyema mwombaji kupeleka maombi yake mbele ya mahakama ya mirathi na siyo mahakama ya watoto.
Sio kwa mwaka bwana, sio kwamba ni zote kulwaajili ya kuwalea hadi miaka 18??
Hapana si unaona mfano hapa ada ni kwa mwaka. Bima kwa mwaka matumizi ni kwa mwezi.
Yaani hapo ni kwa mwaka na nyingine zinatoka kila mwezi.
Mfano ulioitoe siyo sahihi,mwenyekiti wa makampuni lazima awe ni majority shareholder wa kampuni na Kwa hivyo Mengi alikuwa anamiliki share nyingi za IPP ndo maana akawa mwenyekiti.Azam ni Mali za Bakhresa na meneja niwajiriwa wa mshahara tu.Mengi hakuwa mwajiriwa bali mmiliki mwenye hisa nyingi zaidi ya wengine kwenye makampuni ya IPP.Jackie anashindwa kujua kuwa Mengi haikuwa mmiliki wa Kampuni yeyote, Mengi alikuwa mwenyekuti wa makampuni ya IPP
Ni sawa na mke wa meneja wa Azam aende kudai urithi kwa watoto wa Bakhresa.
Hiyo Changi anakesi ya kughushi Hari ya mirathi
Tofautisha kuzaa na kuoa, tunachosema angezaa hata na wanawake mia kama angetaka, no problem, shida ni kuoaBila mengi kuzaa na jack.
Mali zake zilikuwa zinahama kwenye blood line yake miaka isiyozidi 20 mbele.
Kuzaa na jack mengi hajakosea kabisa. Maana watoto wake wa mwanzo walikuwa hawataki kuoa wala kuzaa na wameshafika miaka 50 wote. Sasa wakifariki mali zingeenda kwa nani?
Wao hawaombi mali za baba yao, bali wanaomba gawio la mazao ya mali za baba yao, wangekuwa wanakula tu mali si zingeshaisha? Na wanaofanya kazi ya kuzisimamia ili zizalosje ndio wanafanya ugawaji unaohimilika ili mtaji (mali) zisije zikakataSiyo anawaomba ni mali ya baba yao na wana hizo haki
Nyingi kwako wewe usiekua nazo wenye nazo hizo zote zinaandikwa kwenye kikaratasi kidogo tu na kuhifadhiwa kwenye kadiKumbe ana taka pesa nyingi hivo na hamsemi mnasiri nyie
Wewe kwako unaona kubwa ila Mzee Mengi hizo alikua anazimudu na aliwahudumia..Yaani ni shilingi za Kitanzania MILIONI MIA SABA THEMANINI NA TANO, LAKI NANE ELFU TISINI NA MIA TISA SITINI bila senti. (785,890,960/=)
Aisee!
Kwani kabla ulikua unajua anatumia million ngapi kwa mwezi? Kuna watu wanatumia hio 15 kwa mwezi cha mtoto yaan ni ndogo, watu wanakung'uta 100 hadi 150 kwa mwezi wewe unashangaa 15 cha mtoto hio usishangae sanaInfact yeye hana mchango wowote. Hao watoto ni kitega uchumi chake. Matumizi million 15 kwa mwezi jamani. Hao watoto wanakula dhahabu?
Dah kwa kweli mali kuwa nazo ni shida pia
Mahakama imeeleza kuwa uamuzi wa kiasi halisi kinacholipwa lazima ufanywe kwa kuzingatia njia na hali ya maisha ya baba. Mawasilisho na viambatanisho vinadhihirisha kuwa kabla ya kifo cha marehemu alikuwa akitoa kiasi kilichoombwa kutokana na uwezo na hadhi yake. Marehemu alikuwa baba mzazi wa watoto walioitwa.
Mahakama pia imesema kuwa Mwombaji ametaja biashara nyingi kuwa ni ushahidi wa mapato yanayotokana na biashara inayohusishwa na mirathi, hata hivyo watu aliyowaomba matunzo mbele ya mahakama ni wasimamizi wa mali za marehemu.
Mapato yanayotokana na mirathi ya marehemu si mali ya walalamikiwa pekee bali ni mali ya mirathi ambayo imeshughulikiwa mbele ya Mahakama ya Mirathi. Waliyohojiwa wangekuwa baba mzazi wa watoto Mahakama ingewashikilia vinginevyo.
Kwa kuwa hakuna ubishi kwamba mhojiwa kwa nafasi yake ya wasimamizi wamewajibika kuwakimu watoto mahitaji ya msingi, wanapaswa kuendelea na malezi ya watoto kulingana na uwezo na nafasi zao.
Pia, suala la pili la uamuzi ni suala la malimbikizo na amri inayowataka walalamikiwa kutoa matunzo kwa watoto waliotajwa hadi watimize umri wa miaka 18. Ni ukweli kwamba Sheria ya Mtoto ilitungwa ili kuhudumia ustawi wa mtoto. Hata hivyo, tangu awali ni lazima ieleweke kwamba usimamizi wa mali ya marehemu sio jukumu la kudumu.
Kutokana na maelezo ya pande zote, hakuna ubishi kuwa katika shauri la mirathi namba 39 la mwaka 2019 walalamikiwa waliotajwa waliteuliwa kuwa wasimamizi wa mirathi ya marehemu Dk. Reginald Abrahaman Mengi.
Kwa mujibu wa kifungu cha 109 cha mirathi na usimamizi wa Sheria ya Mali majukumu ya wasimamizi ni kukusanya na kusambaza mali za marehemu kwa warithi halali. Jukumu hilo linaisha mara baada ya wasimamizi kuwasilisha hesabu. Mapato ambayo mwombaji anaomba kutunza watoto wake hadi watimize umri wa miaka 18 yakitoka katika mirathi ya marehemu ambapo walalamikiwa ni wasimamizi tu na sio wamiliki.
Kesi ya uthibitisho ni mbele ya mahakama kuu kwa hivyo mahakama ya watoto sio mahakama inayofaa kwa mwombaji kuomba maombi haya. Kadhalika, mahakama hii haiwezi kuwaamuru walalamikiwa kama wasimamizi wa mali za marehemu walipe malimbikizo kutokana na jinsi marehemu alivyokuwa akitunza watoto wake enzi za uhai wake.
Marehemu alikuwa akitoa mahitaji ya watoto wake kwa vile alikuwa baba mzazi wa watoto waliotajwa, na njia na namna zake zilifanikisha mipango yake. Waliohojiwa si wazazi wa watoto, wao ni walezi tu na wasimamizi wa mali za marehemu.
Zaidi ya hayo, kwa kuwa kuna kesi zinazoendelea za mirathi ambazo zote zinalenga kuhakikisha mirathi ya marehemu inagawiwa kwa haki kwa warithi halali, ni vyema mwombaji kupeleka maombi yake mbele ya mahakama ya mirathi na siyo mahakama ya watoto.
Gari bovu haliwezi kukokotwa na gari bovu. Siku zote gari bovu hukokotwa na gari Zima!Ndio maana mimi na umri wangu na kustaafu kwangu mabinti nawaogopa sana,wao wanawaza pesa tu sio mapenzi.
Yaani binti awe mzuri vipi au akae uchi mm napita tu maana najua hii ni hatari kwa maisha yangu ya sasa na yajayo.
Wastaafu tutulie njia kuu au tutafute wazee wenzetu,tukihangaika na hawa mabinti wa mwendokasi imekula kwetu mazima tukiwa hai au kaburini.
Washua mkisha zeeka msioe hawa wanawake wachanga hususani hawa wanao angalia panapo fuka moshi mtasababisha uzao wenu uteseke na kusumbuana na kurogana saana. Mkisha zeeka wazee wetu tafuteni wa bibi wenzenu.
MsimtishieDada yetu anahangaika na wachaga. Asijeshangaa watoto wakagezwa imbecile.
Hapo ndipo falsafa ya Goldigger inapojidhihirisha. Yeye hata nusu tu ya hio 700M anaweza kuitoa???Kama baba yao yupo yes. Sasa anawaomba watu ambao si wazazi wa hao watoto. Yeye kama mzazi ana uwezo wa kutoa hizo pesa ?Tuanzie hapo kwanza.