Mamilioni ya pesa anayotaka Jackline Mengi kwa ajili ya malezi ya watoto wake haya hapa!

Mamilioni ya pesa anayotaka Jackline Mengi kwa ajili ya malezi ya watoto wake haya hapa!

Ila kwaajili ya kulea watoto hao wawili hadi miaka 18, ni kawaida

Maana yake yani hiyo gharama ya hao watoto hadi wafike miaka 18, hao watoto shule wanazosoma, safari zao na life style zao pengine hicho kiasi ni kidogo kwa hadi wafike miaka 18, maana tukumbuke jinsi pesa inapoteza thamani
Hujaelewa,
Hizo mil 700+ Ni kila mwaka,
Soma vizur hiyo table aloweka mtoa mada
 
come on hela haifiki hata 1B madafu ndo awe tajiri namba moja Africa? Hawi tajiri namba moja TZ let alone Africa. Hiyo ni hela ya nyumba za watu tu hapo DSM.

Kiuhalisia hii hela ni ndogo sana kumuachia spouse wako mwenye watoto wako wawili wakati Mengi alikua na net worth ya over 500M USD zaidi ya 100B madafu.
Uelewe mada,
Hiyo pesa mil 700+ Jack anaomba kupewa kila mwaka, bado claims zake hazimake sense.
 
Washua mkisha zeeka msioe hawa wanawake wachanga hususani hawa wanao angalia panapo fuka moshi mtasababisha uzao wenu uteseke na kusumbuana na kurogana saana. Mkisha zeeka wazee wetu tafuteni wa bibi wenzenu.
Au kuwe na makubaliano kabla ndoa haijafungwa.

Yaani Binti ajue kabisa atapata nini na zisiingiliane na mali za kifamilia.. Kama ni nyumba basi Wanunue Kiwanja wajenge kabla Binti kutia saini cheti cha ndoa.
 
Au kuwe na makubaliano kabla ndoa haijafungwa.

Yaani Binti ajue kabisa atapata nini na zisiingiliane na mali za kifamilia..kama ni nyumba basi Wanunue Kiwanja wajenge kabla Binti kutia saini cheti cha ndoa.

Mwenye mali ndio anaamua kuhusu mali zake ale na nani? Watoto hawana nguvu kwa mwenye mali
 
Mwenye mali ndio anaamua kuhusu mali zake ale na nani? Watoto hawana nguvu kwa mwenye mali
Ni sawa lakini kumbuka umetafuta hizo mali ukiwa na amani ya moyo kutoka familia, Mke na Watoto...sasa iweje mali zije kuwa zako peke yako?.

Kama inapaswa kuwa hivyo basi iandikwekabla ya ndoa kwamba mali yote itakuwa ni ya Baba, Mama na Watoto mtakuwa wasindikizaji tu.
 
Kitakachotokea mbeleni ni vifo tata kwa yeyote atakayeendelea kukaza fuvu.
 
Kula starehe mkuu, ujibane kisa nini?
Unaacha mali zitunze familia yako ukifa lkn anatokea ndugu yako kusikojulikana anawapoka mali wanabaki maskini....

Kwa niliyoyashuhudia familia nyingi sana wazazi walikua matajiri watoto wanavyoishi sasa hivi bora usiwaachie hata sh 100.
Sheria ya Tz haitambui ndugu kama mrithi rasmi wa mirathi endapo kama mke/mume,watoto,na wazazi wa marehemu wapo hai na ndio wenye haki ya kurithi mali otherwise marehemu mwenyewe aandike wosia na kugawia mali hao ndugu zake.

Tunadekeza sana ndugu kwenye kurithi mali ndio maana wengine wanaweka makalio chini kusubiria ndugu zao wafe wapate kurithi mali za bure.
 
Au kuwe na makubaliano kabla ndoa haijafungwa.

Yaani Binti ajue kabisa atapata nini na zisiingiliane na mali za kifamilia.. Kama ni nyumba basi Wanunue Kiwanja wajenge kabla Binti kutia saini cheti cha ndoa.
Mm navyojua na kuamini. Mali ambayo mke kaikuta haimhusu. Nadhani labda nakosea ila naamini mke wa kwanza alichokitafuta na mumewe hakipaswi kurithiwa na watoto wa mke mwingine labda kitakacho patikana pale baada ya mke huyo mdgo kuolewa. Simple au kuna sheria inaweza kuniondolea huu mtazamo wangu.?
 
Sasa tajiri si kafa
Huyo mwanamke anataka kuua kila kitu kila mtu afe kivyake.
Walai hao watoto mpaka wafike hiyo miaka 18 watambue ufyolo aliofanya mama yao halafu wakute hamna kitu.
Sijui
Kafa lakin kaacha hizo kampuni pesa bado ipo
 
Maisha yao huenda hiyo hela inafika. Ila kitaa huku hela nyingi sana hiyo
Kwanza muulize Kama kwao walikuwa wanatumia Bei gani. Ila bana wanawake wa kwetu. Akishakiwa mzuri ama anatongozwa tongozwa Basi atataka mjukuu wa Trump amuoe na huku yeye Hana anachomuongezea Mana Kama kufaki kila mtu anatoa kiungo Chake. Ila wanaume siku tukiwa waerevu Kama wanawake yaani watapata shida mno.

Ujue wao wanaocheza mno na probability game of so called life. They don't gamble blindly or depends on chance/lucky.

Yaani Wana calculate risks so wanafanya perfect speculation zile probability of their odds are in their side yaani tayari wanapokuwa na edge ya ku win in relationship. Remember the rule of the jungles/valleys,forest/oceans those who have edge must survive during chaos.


Yaani wao wanapiga ama wanafanya calculated risks na ukifanya kalkuletedi risk iyo sio loss kumbuka.


They don't trade their life blindly like us men who are sexual desire driven by nature.

Yaani wanafanya their decisions without being influenced emotionally wanatumia their rational brain to trade their life with so called mwanaume.


Sie tunafanya decision emotionally influenced especially sex emotions na hizi Zina nguvu kinyama yaani zinamzidia mwanaume.

Pia kumbuka na yeye anawaza how she will fit in her peers akiwa anakutambulisha kwao sie we don't care we're pure gamblers who should head to Las Vegas but wao Wana head to wall Street to make calculated gamble/bet.



Lazima ucheki na wewe utapata Nini kwake sio you uchi Mana Kama Ni uchi hata mnyama anao.

Binafsi wakati napiga hesabu za kuoa eti nioe anajua kukaa kwa sofa na kubonyeza remote Hana ujuzi wa maisha Ni no.


Mana sikuwa influenced na ngono. Na ndio Mana kulikuwaga na wanachuo Kama wawili na date na wao Ile second year nikawaambia kuwa nimedisco ili niwaone reaction yao kweli mmoja alichomoa so nikajua kuwa mission accomplished. Tunafungua nashangaa nikiwa cafeteria anajileta kwangu tukiwa tunakula.



Please wanaume do calculated risk katika mahusiano iwe win win situation.
Je, ukikwama hata milioni 50 utazipata kwake kweli ama inakuwaje. Mwingine ukimfungulia hata biashara hawezi endesha.


Sie huwa tunabeba mizoga smt anakupa huduma ambazo unaweza ukazipata at any time anywhere.



I can say that female can be good traders in wall Street they can't be sheep or 🐖 since those are slaughtered by bulls and bears.


Trade your time well and you'll reap reward.



Sasa huyu kabla ya hapo alikuwa ameshapanda hata ndege kweli ama aliunganishiwa na pimp kwa mzee. Yeye anataka kuvuruga huu utajiri ama biashara alizoacha mzee zaidi ya hapo akipewa atakuwa anahonga be ten.


Yaani waafrik kweli jamani Kuna sehemu tulikosea sio bure. Mie naombea ipp na kampuni alizoanzisha mzee ziendelee zitoea Ajira kwa vijana wa kitanzania jamani Ila Sasa hii ke inataka kuvuruga.


Yaani viushoia bana. Jamani oeni kwenu ama watu wa karibu hebu cheki hii Mali ama pesa yote hii inaenda kupotea kwa chasaka Sasa angeoa home hii mali si ingesaidia dada mama baba babu zetu wa upande wa home kwetu. Mana akipata hii pesa atasaidia ndugu zake kunyanyuka kusoma kuwafungulia biashara Sasa huoni Kama unaenda kufaidisha Koo zingine ama kabila zingine.


Wewe unaoa unaishi na ndugu wa mkeo Kama wawili watatu Sasa huoni Kama unanyanyua Koo ama kabila lingine si Bora ungekuwa unalisha ng'ombe wa kwenu wanenepe na wakue wazaliane.


Mana ukikutana na mchaga mwenzake hata USA atakusaidia Kama ndugu yako kuliko ukikutana na mburundi mhutu ama kyasaka Kama vyasaka wengine. Oeni nyumbani. Ukifa Mali unaiacha uchagani.




Unapoa unasaidia kupunguza njaa kwao na ke Mana mamkwe bamkwe shemeji Kuna namna watakutumia Kama daraja kunyanyuka Sasa Ni kwa Nini usipende kwenu wakutumie Kama daraja wakanyanyuka kuliko unaenda kunyanyua watu wengine ambao baada ya kizazi Cha tatu Cha kwako watasahauliana na hakuna kinachowaunganisha kwa pamoja.



Jamani oeni karibukaribu Kama mtt wa shangazi mjomba mamdogo bamdogo mbona waarabu wanaona na hizi Mambo sijui ya dna hakuna kitu. Mbona mmeiga wazungu English so na huko igeni mazuri.


Mwanamke ukioa kabila lingine ndugu zake ukipata hela za Mana wanajazana hapo sebuleni kwako wanawaza namna ya kukula Mana wewe kwao Ni mbolea kustawi mbaya zaidi wakistawi faida hawaleti kwenu wanapekeka kwa kabila lao jamani.
Chukulia mjukuu wa shemeji yako aliyestawi kwa mbolea yako hatomkumbuka mjukuu wako ama hata akiwa kitengo fulani hawezi msaidia amesahaliana Ila mkiwa kabila moja ama majirani unakuta mnakumbukana jinsi walivyoishi wazee wenu.




Wanaume tusifanye maamuzi due to emotions influenced inatugharimu mno
 

Mahakama imeeleza kuwa uamuzi wa kiasi halisi kinacholipwa lazima ufanywe kwa kuzingatia njia na hali ya maisha ya baba. Mawasilisho na viambatanisho vinadhihirisha kuwa kabla ya kifo cha marehemu alikuwa akitoa kiasi kilichoombwa kutokana na uwezo na hadhi yake. Marehemu alikuwa baba mzazi wa watoto walioitwa.

Mahakama pia imesema kuwa Mwombaji ametaja biashara nyingi kuwa ni ushahidi wa mapato yanayotokana na biashara inayohusishwa na mirathi, hata hivyo watu aliyowaomba matunzo mbele ya mahakama ni wasimamizi wa mali za marehemu.

Mapato yanayotokana na mirathi ya marehemu si mali ya walalamikiwa pekee bali ni mali ya mirathi ambayo imeshughulikiwa mbele ya Mahakama ya Mirathi. Waliyohojiwa wangekuwa baba mzazi wa watoto Mahakama ingewashikilia vinginevyo.

Kwa kuwa hakuna ubishi kwamba mhojiwa kwa nafasi yake ya wasimamizi wamewajibika kuwakimu watoto mahitaji ya msingi, wanapaswa kuendelea na malezi ya watoto kulingana na uwezo na nafasi zao.

Pia, suala la pili la uamuzi ni suala la malimbikizo na amri inayowataka walalamikiwa kutoa matunzo kwa watoto waliotajwa hadi watimize umri wa miaka 18. Ni ukweli kwamba Sheria ya Mtoto ilitungwa ili kuhudumia ustawi wa mtoto. Hata hivyo, tangu awali ni lazima ieleweke kwamba usimamizi wa mali ya marehemu sio jukumu la kudumu.

Kutokana na maelezo ya pande zote, hakuna ubishi kuwa katika shauri la mirathi namba 39 la mwaka 2019 walalamikiwa waliotajwa waliteuliwa kuwa wasimamizi wa mirathi ya marehemu Dk. Reginald Abrahaman Mengi.

Kwa mujibu wa kifungu cha 109 cha mirathi na usimamizi wa Sheria ya Mali majukumu ya wasimamizi ni kukusanya na kusambaza mali za marehemu kwa warithi halali. Jukumu hilo linaisha mara baada ya wasimamizi kuwasilisha hesabu. Mapato ambayo mwombaji anaomba kutunza watoto wake hadi watimize umri wa miaka 18 yakitoka katika mirathi ya marehemu ambapo walalamikiwa ni wasimamizi tu na sio wamiliki.

Kesi ya uthibitisho ni mbele ya mahakama kuu kwa hivyo mahakama ya watoto sio mahakama inayofaa kwa mwombaji kuomba maombi haya. Kadhalika, mahakama hii haiwezi kuwaamuru walalamikiwa kama wasimamizi wa mali za marehemu walipe malimbikizo kutokana na jinsi marehemu alivyokuwa akitunza watoto wake enzi za uhai wake.

Marehemu alikuwa akitoa mahitaji ya watoto wake kwa vile alikuwa baba mzazi wa watoto waliotajwa, na njia na namna zake zilifanikisha mipango yake. Waliohojiwa si wazazi wa watoto, wao ni walezi tu na wasimamizi wa mali za marehemu.

Zaidi ya hayo, kwa kuwa kuna kesi zinazoendelea za mirathi ambazo zote zinalenga kuhakikisha mirathi ya marehemu inagawiwa kwa haki kwa warithi halali, ni vyema mwombaji kupeleka maombi yake mbele ya mahakama ya mirathi na siyo mahakama ya watoto.
Popoo mbili zavuka mto!!
 
Mali zake ni yeye.. alafu emu unapoandika tumia logic usiandike andike tu mradi umeandika... Ni sawa wewe leo ufe alafu watu waseme hauna hati miliki ya mali zako umenipata tafakari tena alafu uje
Mali za Mengi haziwezi kuwa Mengi, kwani mali zinaweza kujiemdesha zenyewe bila msimamizi? (either mmiliki, wafanyakazi au wasimamizi wa mali); no mali ni kitu kimoja na msimamizi ni kitu kingine. Mtu akifa hawezi tena kumiliki, bali umiliki ujamishiwa kwa beneficiaries wake kama mke, watoto nk., na endapo ameandika wosia halali tjen wosia utafuatwa; ila kama ameandika wosia unaovunja sheria za nchi (mfano kuwaengua watoto wake wa kuzaa kwenye urithi bila sababu) , au kuandika wozia wakati ni mgonjwa na ‘dishi’ limeyumba, maana yake wosia huo ni batili, na mahakama itaamua nani asimamie mali (katika kipindi cha mpoto) na kugawa mazao ya mali husika kwa wanufaika wengine kwa viwango vya haki, wanufaika hao ndio kama Jacky na watoto wake. Shida ni pale wanufaika wanapodai mazao zaidi ya yaliyopatikana, kisa muhusika alipokuwa hai aliweza kutimiza kiwango hicho chanmazao ya mali kwa usimamizi wake, anasahau kwamba msimamizi wa mwanzo alikuwa baba mzazi na alikuwa na ujanja na njia zake za kipekee za kuhakikisha mali zinatoa mazao makubwa zaidi, wasimamizi wa sasa hawana ujanja na njia za Mengi, hivyo watagawa mazao kwa kadri yanabyopatikana ili kulinda mtaji / mali zisikate kwa starehe za mdangaji mmoja tu.
 
Sheria ya Tz haitambui ndugu kama mrithi rasmi wa mirathi endapo kama mke/mume,watoto,na wazazi wa marehemu wapo hai na ndio wenye haki ya kurithi mali otherwise marehemu mwenyewe aandike wosia na kugawia mali hao ndugu zake.

Tunadekeza sana ndugu kwenye kurithi mali ndio maana wengine wanaweka makalio chini kusubiria ndugu zao wafe wapate kurithi mali za bure.
Wanampora mama mjane hadi aje apewe haki yake mahakamani unakuta nyumba 1 imebaki kati 3, magari hayafai, yaani kila kitu kimeharibika, bank washafilisi, kuna haja gani ufe uache mali? Zaidi unwaongezea msongo wa mawazo kwa kuzoea kuishi kitajiri wana baki kuishi kimaskini, umaskini unauma mkuu.
 
Sawa huoni tabu wanayo sumbuana nayo kwa sasa. Maisha hatupangiani ila kwenye kuambiana ukweli tunaambiana. Wanawake wengi chanzo cha matatizo na migogoro
Nakataa mkuu, mfano kwa hii kesi mwenye kosa muoaji, ndugu au muolewaji?
 
Back
Top Bottom