Maoni yangu kuhusu Vita ya Urusi Kama Magharibi Au NATO watalazimika kuhusika moja Kwa moja

Maoni yangu kuhusu Vita ya Urusi Kama Magharibi Au NATO watalazimika kuhusika moja Kwa moja

Ikitokea kupigana NATOAMERICA vs Russia si ajabu tukatumia saa moja tu vita vikaisha.

Sababu:
1. Mmoja akiwahiwa kuhackiwa satelaiti zake michezo unaisha.
2. Mmoja akiwahiwa kupigwa sehemu nyeti, hataweza kujibu..

Intelligences za nchi zote ziko lakini.

Naomba isitokee
 
Nimepitia mijadala kadhaa ya vijana mbali mbali nimeona Tatizo ama lipo katika syllabus tunayotumia kuwafundishia masuala ya kidipomasia ya mataifa mbali mbali ,vijana wengi sana hawana ufahamu Kabisa , vita wanaijadili kama Mpira kwamba yeyote anaweza kupigwa, Vita inajadiliwa kama hadithi za abunuasi , vita imejadiliwa Kwa mzaha sana , watu wanakurupuka tu humu,kwanza nataka mjue Urusi iko vizuri sana kijeshi tena kwenye rank za kidunia yupo namba mbili nyuma ya Marekani , lakini leo hii akiingia vitani hata na China ambaye yuko namba tatu atapigwa kwasababu ya uchumi wake mdogo, vita ni bajet yako kijeshi unavyo wekeza kwenye technology ya silaha na udadisi (intelligence). Na Muda katika kupigana vita ya mataifa makubwa hauwi week moja Au mbili ni miezi zaidi ya minne mpaka saba! Hapa lazima uwe vizuri kiuchumi ili uweze kuendesha mambo yote mawili Kwa wakati mmoja , Yaan vita iendelee huku shughuli zako za kiuchumi zisikwame!

Vijana tumekosa kujisomea maandiko mbali mbali na kudadis kupitia makala na scientific research mbali mbali .

Kuna comments moja niliiona sehemu kijana anasema eti alisema ''China itategea kipindi ambacho US ametingwa na uvamizi fulani wa nchi kubwa nyingine, alafu yeye ndo atatumia muda huo kuivamia Taiwan na ataichukua kwasababu kwasasa China yupo mbali sana kijeshi''
Nilimuelewesha mambo mengi sana akaonekana kukubaliana namimi,

Hata hapa JamiiForums sikuwa Mwanachama Nina miezi Kama minne ninejiunga ila napitia masuala kadhaa ya wachambuzi wa siasa zetu Kama kijana Au Mdogo wangu Pascal Mayalla ana makala nyingi sana hapa JamiiForums Kama wangekuwa wanawalipa wana makala basi angepata namba kuna wengine Kama Kiranga Kalamu1 Mag3 sijaona wakichambua masuala haya ya kimataifa na ningetegemea kuona mtizamo wao katika haya

Basi nawaambia kwamba

Watu wanaibeza sana US katika nyanja za vita, US hawana gwaride kuonyesha vifaa vyao ila vita vikianza utaona mengi ambayo macho hayajawahi kuona... Au Kama inafanyika inafanyika katika namna ambayo ni Siri sana !

Pia hatupaswi kuipuuza Urusi katika nyanja za kijeshi, lakini ni upuuzi kudhani Urusi inaweza mess up na Washington na Moscow ikabaki kama ilivyo... tunakosea sana! Hakuna Muungano ulikuwa unatisha kama USSR wadogo ninyi wengi humu !
Hakuna Taifa lilikuwa linatisha Kama Iraq ya Sadam Hussein! Au UMOJA wa waarabu chini ya Sadath wa Misiri. Lakin walikwama sehemu moja tu intelligence na uchumi…

Us kwa uchumi wake na teknolojia lazima Urusi itakuwa katika hali ngumu Kwa Urusi kusema iingie vitani nayo ibaki salama!!

Hata Asia ina safari ndefu kujifunza kutoka America na Ulaya kuanzia military technology,


Nitaendelea kwanini tunapaswa Kukataa vita! Maana nilivyoandika hapa kuna watakaosema natetea maovu Au vamizi za US kwingine Hapana nakemea sana kama nilivyokemea Afghanistan, LIBYA na sasa Nakemea Uvamizi wa Urusi Kwa Ukraine!!


Mimi Dr. Lwaitama
Hivi Bakressa akikuattack atakushinda kwa sababu uchumi wako ni mdogo?


Nauliza tu usichukie.
 
Naona kama Uzi haujashiba!Kwa Tambo ulizoanza nazo basi nikajua Uzi utakuwa na content ila nimekuwa disappointed!
Unasema uzi haujashiba wakati unaona kabisa bado kuna mwendelezo unakuja,kweli bado tuna safari ndefu sana kama Taifa
 
Lakini, pamoja na vikwazo hivi, wewe unadhani wao pia hawatatetereka. Unadhani dunia haitaanza kujiuliza kwa nini mfumo wa biashara uhodhiwe na nchi moja au kundi la nchi? Unadhani huu hautakuwa mwanzo wa kuuliza maswali juu ya mfumo huu?
Hapa umeonesha unazi wako na mahaba kwa Urusi bila kuukubali ukweli uliopo.

Kwani unadhani Dunia haijawahi kujiuliza kuhusu mfumo wa uchumi uliopo mpaka baada ya hivi Vita?...

Marekani Kama kubwa la Ubeberu, ndiyr kinara wa uchumi kwa Sasa, ana ushawishi mkubwa kwenye taasisi/mifuko yote ya kifedha achilia mbali wa kidiplomasia, na Dunia inatambua hilo hivyo hakuna wa kujiuliza kuhusu hilo.
 
Hapa umeonesha unazi wako na mahaba kwa Urusi bila kuukubali ukweli uliopo.

Kwani unadhani Dunia haijawahi kujiuliza kuhusu mfumo wa uchumi uliopo mpaka baada ya hivi Vita?...

Marekani Kama kubwa la Ubeberu, ndiyr kinara wa uchumi kwa Sasa, ana ushawishi mkubwa kwenye taasisi/mifuko yote ya kifedha achilia mbali wa kidiplomasia, na Dunia inatambua hilo hivyo hakuna wa kujiuliza kuhusu hilo.
Heshima mkuu 'Proved'.

Hapana, usinielewe hivyo. Binafsi sina kabisa unazi wowote na Urusi; kwani Urusi yenyewe ilishatumbukia kwenye mfumo huo huo wa uchumi wa dunia, kwa hiyo hakuna tofauti yoyote kwenye mfumo kati ya huo unaotawaliwa na Marekani, akiwa kinara na washirika wake wengine, ambao sasa silaha yao kuu katika vita, hasa na hivi viinchi vidogo vidogo kama Korea Kaskazini, Zimbabwe, Venezuela ni kuwapiga kwa kuwawekea vikwazo vya uchumi. Hii sasa ndiyo silaha ya hawa wakubwa, kuwanyoosha hawa wengine.

Nadhani hujaelewa vizuri hoja ninayojaribu kuiwasilisha hapa kuhusu hii silaha ya vikwazo vya kiuchumi ambayo sasa ndiyo inayotumika sana.
Maana yangu ni kwamba, nchi za dunia lazima zitaanza kujiuliza juu ya swali hili. Kwa nini ziwe tegemezi katika haya maswala kwa nchi moja na washirika wake wachache katika kuendesha mfumo mzima wa uchumi wa dunia?

Ni sawa kabisa kulinganisha hili swala na watu kuanza kujiuliza na kukataa kutawaliwa (ukoloni). Baada ya maswala hayo kuwepo, ukoloni ukapigwa vita, waliokuwa na makoloni bila kupenda wakayaachia.

Sasa wewe unadhani watu wataacha kujiuliza kwa nini sarafu ya nchi moja ndiyo iwe msingi wa uhai wa uchumi wao?

Unadhani watu wataacha kujiuliza kwa nini mabenki ya nchi za upande mmoja ndiyo yawe na uamzi wa wapi pesa zielekezwe?

Huu ni mwanzo tu, mambo hayawezi kubadilika kwa siku au wiki moja. Hayo unayoyasema kuwa kinara wa uchumi duniani, hilo ni swala la mpito tu, leo ni huyo, kesho atakuwepo mwingine.

Nisome vizuri unielewe mkuu wangu 'Proved'.
 
IRAQ labda ilikua inaogopewa na IRAN na SYRIA labda
Kwamba US akiingia vitani na RUSSIA yale majengo marefu pale DC nakwengineko yatabakia kama yalivyo!!?
US ndio anatapatapa hv kuelekea mwisho wake
Wewe nakubaliana na mleta Mada Iran ilikuwa tishio
 
Kwanza Shikamoo Join the chain ya CHADEMA inaendeleaje!

Naona CHADEMA mmeshika msimamo kwamba mnasimama na Urusi nauliza Mbona mkitoa mifano ya democracy mnatolea ya USA, na mnaposhambuliwa mnaenda USA si Urusi?
huo msimamo wa Cdm na Urusi ni wa Yeriko peke yake
halafu hii inaingiaje?
 
Kwanza Shikamoo Join the chain ya CHADEMA inaendeleaje!

Naona CHADEMA mmeshika msimamo kwamba mnasimama na Urusi nauliza Mbona mkitoa mifano ya democracy mnatolea ya USA, na mnaposhambuliwa mnaenda USA si Urusi?
Mkuu, sidhani kama huo msimamo ni wa chama.. Itakuwa ni maoni binafsi ya watu wachache.
Kuunga mkono udikteta kwa sababu yoyote ile lzm uwe kiazi!
 
Kama kweli wewe ndiye Lwaitama basi nina uhakika umeandika haya kwasababu mmeamua kama chama kushabikia mashoga na ushoga mkionhozwa na yule jamaa wa Ubelgiji.

Unapozungumzia uchumi,kwani uchumi utasaidia nini kwenye vita kati ya Urusi na Marekani!? Au unadhani watapigana kama Urusi anavyopigana na Ukraine?

Vita kati ya miamba hao viwili haitakuwa ndefu hadi ihitaji uchumi mkubwa. Wala haitachukua miezi saba kama unavyodhani. Huwenda vikaweka historia mpya ya vita vilivyotumia muda mfupi zaidi duniani. Huenda ikachukua saa kadhaa vita kumalizika na kuacha athari isiyoelezeka. Kuna uwezekano wa nchi kama si dunia kurudi zama za giza. Silaha zitakazotumika nizamaangamizi. Itakuwa nani atawahi kumfikia mwenzake. Na akikuwahi hatakupa nafasi yakujibu wala kutubu. Atakuangamiza.

Huo uchumi haotakusaidia mbele ya silaha hizo za maangamizi.

Sent from my SM-G5500 using JamiiForums mobile app
Mkuu ulichokisema ndo uhalisia wa vita vya kisasa tatizo huyu lwaitama1 amechambua haya mambo ya vita vya karne hii kwa kuangalia technology na facts za kizamani za kutumia mapanga, visu, gobole, farasi, bunduki na mabomu ya kutifua ardhi , ambapo hiyo technology ndo ilikuwa inaweza kutumia muda mrefu mkipagana kwenye battle field face to face.

Au kama siyo hivo basi amechambua kwa kuangalia uwezo wa majeshi yetu ya Africa yanayojivunia kumiliki AkA47 na mizinga, hapo ndo vita inaweza ikaenda miezi hiyo aliyoitaja au hata miaka.

Ila sasa tukirudi kwenye full scale war inayohusisha miongoni mwa nchi hizi nazo enda kuzitaja.
Russia
USA
CHINA
UK
GERMANY
N.KOREA
IRANI
ISRAEL
FRENCH
INDIA na n.k
basi usitegemee kama kuna vita ya miezi hapo.
Mfano ikitokea battle ya USA Vs Russia, halafu wote wakatumia full scale war, kama vita wakianza leo jumatatu basi kufikia Jumatano vita itakuwa imeisha kabisa na hizo nchi zinakuwa zimebaki either magofu au historia katika ulimwengu huu.

Haya mapigano waliyo/wanayopigana Urusi, NATO na Marekani kwenye nchi mbalimbali duniani kama iraq, libya, syria,chenchen, Afghanistan na sasa Ukraine siyo full scale war bali ni special military operation tu.

Na ndo maana ukiondoa ujinga wetu wa ki afrika kama wa huyo mleta mada, mataifa mengi ya ulaya kwa kutambua uhalisia wa Vita vya kisasa yanaogopa na hayataki kabisa kuingia vitani na nchi inayomiliki nukes na hata hao wenye nukes nao wanaombea isitokee migogoro itakayo walazimu wao kutumia hizo nuclear weapons.

Mwisho; naomba nimalize kwa kuuliza maswali mawili kwa mleta mada lwaitama1

Swali namba moja: Just imagine, kama bomu la nukes la 1945 lililopigwa japan liliweza kuteketeza mikoa mikubwa miwili (Hiroshima na Nagasaki) na kuua watu zaidi ya elfu20 kwa mpigo na bado likaacha athari zinazo athiri hadi leo hii vipi leo currently advanced nuclear bombs zikianza kutua kwenye uso wa ardhi unadhani kipi kitatokea na itachukua muda gani kuona hayo matokeo?

Swali namba mbili; unadhani nikwanini mpaka leo japan, south korea na USA hawathubutu hata kuikoromea north korea kijeshi zaidi ya kulia lia tu licha ya north korea kutest mambovu hatari yanayo angukia hadi sehemu ya bahari ya japan ambaye ni mwanachama wa G7 na rafiki wa USA?

Unadhani kwanini Rais(D. TRUMP) wa taifa kubwa kama USA alikubali kutoka white house mpaka kwenda Singapore kwaajili tu yakufanya mazungumzo na bwana mdogo kabisa wa taifa linalosemakana ni masikini Mr Kim jung Un(kiduku)?

Nawasilisha.
 
Nimepitia mijadala kadhaa ya vijana mbali mbali nimeona Tatizo ama lipo katika syllabus tunayotumia kuwafundishia masuala ya kidipomasia ya mataifa mbali mbali ,vijana wengi sana hawana ufahamu Kabisa , vita wanaijadili kama Mpira kwamba yeyote anaweza kupigwa, Vita inajadiliwa kama hadithi za abunuasi , vita imejadiliwa Kwa mzaha sana , watu wanakurupuka tu humu,kwanza nataka mjue Urusi iko vizuri sana kijeshi tena kwenye rank za kidunia yupo namba mbili nyuma ya Marekani , lakini leo hii akiingia vitani hata na China ambaye yuko namba tatu atapigwa kwasababu ya uchumi wake mdogo, vita ni bajet yako kijeshi unavyo wekeza kwenye technology ya silaha na udadisi (intelligence). Na Muda katika kupigana vita ya mataifa makubwa hauwi week moja Au mbili ni miezi zaidi ya minne mpaka saba! Hapa lazima uwe vizuri kiuchumi ili uweze kuendesha mambo yote mawili Kwa wakati mmoja , Yaan vita iendelee huku shughuli zako za kiuchumi zisikwame!

Vijana tumekosa kujisomea maandiko mbali mbali na kudadis kupitia makala na scientific research mbali mbali .

Kuna comments moja niliiona sehemu kijana anasema eti alisema ''China itategea kipindi ambacho US ametingwa na uvamizi fulani wa nchi kubwa nyingine, alafu yeye ndo atatumia muda huo kuivamia Taiwan na ataichukua kwasababu kwasasa China yupo mbali sana kijeshi''
Nilimuelewesha mambo mengi sana akaonekana kukubaliana namimi,

Hata hapa JamiiForums sikuwa Mwanachama Nina miezi Kama minne ninejiunga ila napitia masuala kadhaa ya wachambuzi wa siasa zetu Kama kijana Au Mdogo wangu Pascal Mayalla ana makala nyingi sana hapa JamiiForums Kama wangekuwa wanawalipa wana makala basi angepata namba kuna wengine Kama Kiranga Kalamu1 Mag3 sijaona wakichambua masuala haya ya kimataifa na ningetegemea kuona mtizamo wao katika haya

Basi nawaambia kwamba

Watu wanaibeza sana US katika nyanja za vita, US hawana gwaride kuonyesha vifaa vyao ila vita vikianza utaona mengi ambayo macho hayajawahi kuona... Au Kama inafanyika inafanyika katika namna ambayo ni Siri sana !

Pia hatupaswi kuipuuza Urusi katika nyanja za kijeshi, lakini ni upuuzi kudhani Urusi inaweza mess up na Washington na Moscow ikabaki kama ilivyo... tunakosea sana! Hakuna Muungano ulikuwa unatisha kama USSR wadogo ninyi wengi humu !
Hakuna Taifa lilikuwa linatisha Kama Iraq ya Sadam Hussein! Au UMOJA wa waarabu chini ya Sadath wa Misiri. Lakin walikwama sehemu moja tu intelligence na uchumi…

Us kwa uchumi wake na teknolojia lazima Urusi itakuwa katika hali ngumu Kwa Urusi kusema iingie vitani nayo ibaki salama!!

Hata Asia ina safari ndefu kujifunza kutoka America na Ulaya kuanzia military technology,


Nitaendelea kwanini tunapaswa Kukataa vita! Maana nilivyoandika hapa kuna watakaosema natetea maovu Au vamizi za US kwingine Hapana nakemea sana kama nilivyokemea Afghanistan, LIBYA na sasa Nakemea Uvamizi wa Urusi Kwa Ukraine!!


Mimi Dr. Lwaitama
Mimi kwakweli sikubaliani na hiyo hoja..kama Marekani wangekuwa vizuri kama unavyosema, waliwahi kuingia vitani na Vietnam, nini kilitokea? Walichemsha vibaya sana. Na tena walikuwa wanasaidiwa na ufaransa na nchi zingine za ulaya. Juzi tu alikuwa huko Afghanistan, amefanya nini? Baada ya miaka kama 20 hakuna lolote la maana Ali achieve. Kama alishindwa huko ndo ataiweza urusi? Marekani ameishia kuwanyanyasa waarabu tu. Urusi sio level yake. Kwa kuthibitisha Hilo, hakuna mahali marekani yupo anapigana, urusi akaingia akaendelea kubaki. Wiki 2 tu zilimtosha kumfurusha mmarekani hapo Syria.
 
Waweza ishusha Urusi ktk nyanja zoote ujuazo eg uchumi sijui nini lakini usije thubutu kufanya hivyo kwenye vita na hili wakubwa kuliko wewe wanalijua ndo maana hata wao walianza na vikwazo na wakasema Urusi haiwezi kudumu vitani ndani ya mwezi cha ajabu muda unavyozidi kwenda ndivyo mashambulizi mazito yanazidi fanywa na Urusi na sasa hesabu zimegoma hata propaganda ya kwamba Urusi watu wanalala njaa haziwezekani tena kila nchi muda si mrefu itaanza kutetea maisha ya watu wake badala ya porojo za US.

Kuna watu wanaikosoa Russian kwakuwa ni undemocratic kitu ambacho ni kweli lakini wakumbuke kuwa nchi zote duniani zilizoingia mapigano na NATO pona yao ni kusaidiwa na urusi kama si hivyo hiyo nchi lazima eteketee hivyo ni nchi nyingi sana zilikuwa ni makoloni zilipata uhuru kwa msaada wa AK47 hata Julius Malema aliwahi sema hili.

Kikubwa ktk vita ni mipango na siyo kukariri uchumi kwani ilikuwaje Israel akazishinda nchi zaidi ya 5 kwenye vita?
NATOA ONYO BILA KUJALI UNA UCHUMI MKUBWA KIASI GANI USIJE VAMIA URUSI UKIAMINI UCHUMI UTAKUOKOA UTAKUFA KATIKATI YA MANOTI YAKO NA YASIKUSAIDIE CHOCHOTE.
Urusi kusaidia wengine haihalalish kuvamia sovereign nation , hata mm nlikuwa shabiki mkubwa wa Putin ila nimemuona kenge kwa huu uvamiz
 
Ninakusikitikia sana mkuu 4by94, kwa kukosa ufahamu wa mambo ya dunia kama haya.

Sitapoteza wakati wangu zaidi hapa kufafanua chochote nilichokwishakiandika humu kwa maana naona huna uwezo wa kuelewa kilichoandikwa.
Unauliza kama NATO alishavamia nchi yoyote (ya ulaya), kwani ni ulaya pekee ndiko kuna nchi? Hii inaonyesha wazi huna ufahamu wa kutosha juu ya mambo haya.
Hapo kwanza nicheke , kwan tunazungumzia mataifa ya ukanda gan ? mara hii ushaanza uliza kama hamna mataifa sehemu nyingine ? Naamini umeelewa hoja yangu ila ndo utimu unakutoa ufahamu , mataifa ya mashariki ya Ulya sio wajinga kumwaga damu kujiunga na WEST , Urusi anafanya maovu mengi kwenye uchumi na siasa za majirani zake , ova
 
Ninakusikitikia sana mkuu 4by94, kwa kukosa ufahamu wa mambo ya dunia kama haya.

Sitapoteza wakati wangu zaidi hapa kufafanua chochote nilichokwishakiandika humu kwa maana naona huna uwezo wa kuelewa kilichoandikwa.
Unauliza kama NATO alishavamia nchi yoyote (ya ulaya), kwani ni ulaya pekee ndiko kuna nchi? Hii inaonyesha wazi huna ufahamu wa kutosha juu ya mambo haya.
mjomba tuliza akili hoja zinakuelemea tyr , huelewek unaandika nn , ebu kumbuka mada ni ulaya ya mashariki
 
Back
Top Bottom