Maridhiano ya CCM na CHADEMA Ndiyo Kawaida ya Vyama vya Siasa Duniani Ilivyo?

Sijaona kipya cha kujibu, ila sasa ni kuzungushana tu.
 
Sijakata tamaa popote, diyo maana nipo hapa, lakini siyo kuwa na matumaini kwa kinachoonekana hakipo. CHADEMA kama hakuna zaidi ya haya yanayoonekana katika hii miezi iliyopita, hakuna matumaini huko tena. Lakini hiyo siyo kukata tamaa, ni kueleza tu ukweli unavyojipambanua.

Utakuja hapa unieleze tena kwamba kutakuwepo na Katiba Mpya waliyoipigania sana CHADEMA kabla ya chaguzi zijazo? Kwa mfano mmoja tu, unaoonyesha kuwa tayari wamepangwa na kupanguka.
 
EEeeh!
Mwishowe najaribu kuepa kujibu chochote toka kwako, kwa sababu tulishakubaliana kuhusu swala la "muda kusema."

Maridhiano ya Mandela huwezi kamwe kuyalinganisha na yale ya Tsvangilai. Hayo ya Tsvangi. ungeyafananisha na ya Raia na Mwai kidogo yangeendana.
Kwa maana hiyo basi, kama hayo ndiyo matumaini ya CHADEMA, na kwa kweli ulishaeleza wewe mwenyewe hapa, kwamba hiyo ndiyo ile "win-win", hapa nitakubaliana na wewe. Lakini kwa kufanya hivyo ni kama CHADEMA wamekubali kwamba hawana uwezo wa kuwaondoa CCM madarakani, jambo ambalo siamini kuwa ni kweli.
 
Nadhani wewe umekwishajiondoa kwenye kushiriki majadiliano kwa uelewa unachoshiriki. Imebaki tu kuingiza vimaneno tu.
Kwa hiyo ninakuweka pembeni hadi hapo utakapotuliza akili ujadili kwa utulivu wa akili na kuachana na mihemko.
 
Kwa hiyo tugeuze gia tuwajadili akina "Mdee" kutosamehewa kuwa ishara ya nini?
Hayo yaliyokwishawahusu huko mahakamani na kuendelea kwao bungeni tuchukulie kuwa ni kawaida tu?
 
Nilijuwa huko kichwani kuna kitu.

Lakini, huoni mwisho wa siku ANC walishika hatamu?
Yale maridhiano hayakuwa ya ANC kujisalimisha kwa makaburu kwa njia yoyote ile.

Mikutano imeruhusiwa, leo Rais anahudhuria mkutano wa CHADEMA, kesho katiba Mpya na Tume Huru. CHADEMA wame kuwa wanatumia confrontational politics na hazijalipa, na Wala wananchi hawakuwaunga mkono, so wamaeamua kutumia approach nyingine kupata wanachokitaka.
 
Dalili zinaonyesha hivyo, lakini ni busara tusubiri muda uzungumze.

Dalili gani?. Leo Mh Mbowe kamwambia Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM live kuwa CCM iliiba uchaguzi 2020. Sasa Hapo utsema hiyo kauli ni kujisalimisha au?
 
Heshima sana mkuu 'Econonist'.
Lakini samahani sana, kama bado unasubiri Katiba Mpya kabla ya mwaka kesho 2014?
"Tume Huru"?; labda, siwezi kukataa moja kwa moja, lakini mbona "Uteuzi" wa Mwenyekiti wa Tume unafanyika wakati huu, wewe hudhani sasa ndiyo ingekuwa wakati mzuri kabisa kwa Samia angalau kuonyesha dalili njema za maridhiano? Kwa nini wakati huu muhimu, ndipo anapofanya mambo ambayo hakutegemewa kuyafanya?
 
Maridhiano ya Mandela huwezi kamwe kuyalinganisha na yale ya Tsvangilai.
Mpaka hapa umeshafeli, maridhiano ni maridhiano kusema Mandela ni tofauti ilihali Chadema wamepitia matatizo Yale Yale waliyopitia ANC sijui kipi unaona tofauti? Kama kesi Chadema wamepewa, members 400 so far wameachiwa Toka gerezani Bado wengine zaidi ya 600!! Alafu unasema haifanani?

Zaidi ya 70% ya post za kuchaguliwa kuanzia TAMISEMI Hadi uchaguzi mkuu zilichukuliwa mezani yaani bila kupingwa. Sasa Ina tofauti Gani na kupora haki ya kuchagua kama sauzi ya makaburu?

Wapinzani wengi wameuawa kuanzia Mawazo mpaka Saanane je Ina tofauti Gani na sauzi ya makaburu?

Embu jaribu kuwa objective, ushabiki wa vyama usitutoe ufahamu.
 
Dalili gani?. Leo Mh Mbowe kamwambia Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM live kuwa CCM iliiba uchaguzi 2020. Sasa Hapo utsema hiyo kauli ni kujisalimisha au?
EEEEeeeh, Heeeee.
Bado ninacheka wakati nikiandika kuhusu hayo uliyoandika hapo juu!
Kwa hiyo hapa Mbowe kampa za uso Mh. Rais, ambaye ni Mwenyekiti wa Chama mwenzake?
Samia mwenyewe anafurahi sana kuwa mbali na kila jambo la Magufuli kwa wakati huu. Kwa hiyo kusema hayo hakumnyimi raha hata kidogo. Kusema kweli ni kama kumwongezea sifa na kuaminika, hata katika kundi ambalo hastahiri kuaminiwa.
 
Kwani kusudi kuu la haya maridhiano ni madhira ya utawala uliopita au mbinu za Chadema kui ondosha CCM toka kuanzishwa kwake kuonekana kugonga mwamba ?
 

Rais kashaahidi kuunda Tume hivi karibuni. Ina maana kabla ya uchaguzi wa 2025, katiba mpya itakuwa imepatikana. CHADEMA wanatumia strategy ya kudai kikubwa ili wapate kidogo au zaidi. So kudai katiba mpya ni mlango wa kudai mambo mengi zaidi.
 
Rais kashaahidi kuunda Tume hivi karibuni. Ina maana kabla ya uchaguzi wa 2025, katiba mpya itakuwa imepatikana. CHADEMA wanatumia strategy ya kudai kikubwa ili wapate kidogo au zaidi. So kudai katiba mpya ni mlango wa kudai mambo mengi zaidi.
Nimekuelewa, kwamba sasa hivi CHADEMA wanapambania tume huru, katba hata wao wanajuwa haiwezekani.
 
Je, umewahi ona mbuzi ana noa kisu cha kumchinja yeye mwenyewe ?

Nakuelewa, ila lazima ujue CHADEMA wanadai hivyo vitu wakijua CCM hata vitoa kirahisi, lakini ndio mwanzo wa kuitoa CCM madarakani. Yani dai vikubwa ili angalau upate vichache. Yani dai milioni kwanlengo la kupata laki tano.
 
Nimekuelewa, kwamba sasa hivi CHADEMA wanapambania tume huru, katba hata wao wanajuwa haiwezekani.

Something like that in reality. So wanadai katiba mpya, ili kipindi Cha mzozano wakuabliane kwanza kuwa na Tume huru na mambo Kama hayo wakati Katiba mpya inajadiliwa
 
Nakuelewa, ila lazima ujue CHADEMA wanadai hivyo vitu wakijua CCM hata vitoa kirahisi, lakini ndio mwanzo wa kuitoa CCM madarakani. Yani dai vikubwa ili angalau upate vichache. Yani dai milioni kwanlengo la kupata laki tano.
Wataalamu wa vita wanasema" unapo panga kumshambulia adui kwa mbinu hizi nae adui anapanga mashambulizi makubwa kwa ajili yako kwa mbinu zake".

Asante kwa muda wako ulio nipatia mkuu.
 
ANC walipigana wakachukua nchi, CHADEMA inaonekana kilichobaki ni kupigana kupewa fursa za kujiunga na hao wanaopambana nao. Sasa kama huoni tofauti hiyo, sina uwezo zaidi wa kuielezea tofautti hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…