Mbunge Mstaafu na Mtu Maarufu anahitaji Mchango wa matibabu, wewe unadhani uta survive vipi?

Mbunge Mstaafu na Mtu Maarufu anahitaji Mchango wa matibabu, wewe unadhani uta survive vipi?

Kwanza alivunjiwa nyumba,, ikabidi ajenge ingine
Pili hela ikatumika kwenye kampeni na ubunge hakupata,
Tatu ameugua kila wiki cost milioni 4,,
Lazima atepete tu
Ruge alipigwa 6M kila siku clouds media na kiburi chao chote ilifikia mahali walinyoosha mikono juu wakaomba wa TAG ubavu kwa wananchi!
 
Nimejiuliza hili swali sana si kwa nia mbaya. Kwa nia njema kabisa. Prof Jay. Joseph Haule amekuwa Mbunge kwa miaka 5 akilipwa mamimilioni ya pesa. Baada ya kumaliza kipindi chake amelipwa mamilioni mengine ya kiinuna mgongo.

Leo ameumwa na kulazwa kwa mwezi mmoja anadai achangiwe. Je yule mswahili ambaye anapata mshahara wa tsh 400,000 kwa mwezi ana mke na watoto. Hana malupulupu, hana mbele wala nyuma. akiumwa inakuaje?

Twende mbele na kurudi nyuma. Joseph Haule si mtu wa kuchangiwa pesa ya matibabu. ni kutaka kutumia umaarufu wake vibaya. sisi watanzania tufikie hatua tuwe makini na watu wenye kufikiri kwa kina. Huyu bwana alipokuwa Mbunge miaka 5 aliwahi fikiria nini kuhusiana na gharama za matibabu?

Kama wenzie sasa hivi hawajali maumivu wanayopata watanzania wa kipato cha chini pengine kwa kudhani hayawahusu. But ipo siku pia nao yanaweza kuwakuta ni vyema kujipanga kwa mambo ambayo ukiwa mbunge na usipokuwa mbunge yanaweza saidia taifa hili.

Tuchangini wenye mahitaji ya kweli kweli ndugu zanguni. Prof J ana weza hata uza moja ya nyumba zake au lake. Ila wewe mwenzangu ukiumwa hutoweza jitibia wala kuchangiwa na watu sababu hufahamiki na huna cha kuuza.
Mie sitoi hata mia
 
Acha uchawi, na we ukiumwa sema watu wakuchangie, wasipokuchangia basi wakikuchangia ni vema.
kuchangia ni hiari tuu alafu pia ni ile tuu kuonyesha ile love kwamba mko pamoja naye katika kipindi hiki cha matatizo nadhan hamna alolazimishwa hata familia yake haikutaka achangiwe
Kama watu wanavyokuleteaga matunda ukiumwa its the same to this
 
Nchi yetu bado ni masikini sana hatuwezi kuacha kuishi kwa kuchangiana. Hata hao mnaodhani wana pesa nyingi kimsingi ni za kawaida tu. Watu walioyapatia maisha ni wachache sana, ni familia fulani fulani tu. Wengi tunawaona wametoboa lakini nyuma yao kuna utitiri wa majukumu yanayotokana na familia ndugu jamaa na marafiki ambao bado ni masikini.

Ukiona nchi ambayo unahitaji kuwa na mipesa mingi ili upate huduma nzuri za kijamii jua hiyo nchi bado masikini wa kutupwa. Acha tuchangiane ndugu. Yeyote akiletwa mbele ya jamii na ikathibitika anahitaji msaada wanaoguswa acheni wachange.
Kutoboa bongo ni ngumu sana kwa sababu bado tunaishi kijamaa. Huwezi kuwa unacho ndugu wasilete shida zao na lazma uwatatulie kiungwana tu.

Watu wanahisi ukiwa Mbunge ndio tajiri hawajui deepdown mambo yakoje! Jamaa pia hakukaa vizuri kwenye ubunge kama ambavyo wengine wamepiga term zaidi ya 3 mtu ana hela ndefu kweli kweli! Kama kujiwekeza kawekeza sana tayari.

Naimani angepata nafasi ya kuhudumu walau term 2 angekuwa pazuri zaidi
 
Watu wanajisahau sana, kuna magonjwa hata uwe na hela kama Diamond Platinumz lazma utembeze bakuli tu! Utapambana wee ila hela inayotoka ni kubwa kuliko inayoingia yani!

Imagine upigwe invoice ya 6M kila siku kwa week tu uweze kulipa 42M hata kama una billion 1 bank utaweza kukimbizana na hizo charges kwa muda gani?

Kila mwezi ulipe 168M utakaa muda gani ukikaza sana miezi mitatu tu lazma uombe poo!😂

Maana ikunbukwe ukiwa hospitali kuna wengine nao wanategemea mfuko wako huo huo waishi magari yaendeshwe uje kutazamwa hospitali.
Kuna Kocha mmoja juzi uingereza Wamemchangia £60,000 kwa ajili ya cancer ya ubongo ya mke wake. Mashabiki wa Crystal palace wamechanga. Sio kwamba huyu Kocha hana mshahara mkubwa ila kuna magonjwa mkuu hata kama una Hela ni gharama kuyatibu.

Hizi Issue za Figo kupigwa tu Laser Hospitali Nzuri hapa Tanzania unaambiwa milioni 12, Hapo bado Hela nyengine za kitanda na mambo mengine madogo madogo, na Hapo uombe Mungu isirudie kama Unarudi Rudi hospitali na Ugonjwa unakupelekesha muda Mrefu ndo Hapo unaona mtu anatembeza Bakuli.
 
Bima ya afya imekaa kitapeli sana hasa hii ya NHIF!

Magonjwa yote critical na yanayohitaji care kama za Dialysis wameyaondoa sababu yana gharama kubwa ila wameacha malaria ambayo kila mtu ana mudu!

Kawaida ya bima inatakiwa kundi la watoto na vijana libebe watu wazima wenye matatizo Mengi ila hali ni tofauti! Watoto wana options nyingi kuliko watu wazima ambao ndio wako Prone to sickness!
Hizi bima zimekaa kiwiziwizi tu, mimi nadhani kila mtu angekuwa na akaunti yake ya bima ambako fedha anayokatwa iingizwe huko na the only way anaweza kuitumia ni kwenye matibabu tu, kwa maana ya kwamba mtu anaweza ku accumulate fedha ikamfaa siku akiwa na uhitaji wa matibabu ya gharama ya juu kabisa kuliko hii ya kupimiwa kiwango cha tiba wakati fedha ni yako mwenyewe
 
Hizi bima zimekaa kiwiziwizi tu, mimi nadhani kila mtu angekuwa na akaunti yake ya bima ambako fedha anayokatwa iingizwe huko na the only way anaweza kuitumia ni kwenye matibabu tu, kwa maana ya kwamba mtu anaweza ku accumulate fedha ikamfaa siku akiwa na uhitaji wa matibabu ya gharama ya juu kabisa kuliko hii ya kupimiwa kiwango cha tiba wakati fedha ni yako mwenyewe
Kiongozi sawasawa kabisa NHIF ipo kiwiziwizi mie mwenyewe muhanga nilichangia miaka mitano baada ya kutumbuliwa na KAYAFA bima ikakoma wana utaratibu mbovu sana eti mpaka uchangie miezi 120 yani miaka 10 mfurulizo ndio unakidhi kigezo cha kutibiwa maisha yote.

Ndugu yetu prof' J baada ya ubunge kukoma na bima ikakoma labda km angetumikia vipindi viwili vya ubunge angekidhi kigezo na masharti ya bima kutibiwa maisha yote. Kutoa ni moyo sio utajiri tumchangie prof' J amefanya kazi kubwa sana ya kutuburudisha na kukuza muziki wa kizazi kipya.
 
Mkuu dunia hailingani.

Usipotumia AKILI dunia hi, utajikuta unatumika mpaka mwisho wa Maisha yako.

Hivi hujawahi kusikia msemo kuwa, wewe ukiwa huna gari unaombewa upate ila Kiongozi wako wa kidini akitaka gari ANACHANGIWA😀

Imagine,

Mwanasiasa anahitaji Support yako:

Utatunga nyimbo utamwimbia sana, na kumsindikiza akachukue fomu ya kugombea.

Utaondoka nyumbani kwako, utaenda kwenye mikutano yake ya kampeni kumpa support.

Siku ya KURA utasimama JUANI siku nzima kumpigia kura.

Ukishampigia kura inabidi usubirie kituoni kulinda kura ili asiibiwe.

Akiibiwa inabidi uandamane upigwe mpaka atangazwe kuwa yet ndio mshindi.

Pamoja na kulipwa mabilioni, akiugua Ni lazima achangiwe.

Watanzania Ni WAKARIMU sana, na Kuna watu weshajua hili na wananufauka nalo kill siku.

Hasa Wanasiasa na Wasanii.
Kuna mwanasiasa na mwanasiasa! Binafsi ningezisikia ni yule mbunge chotara wa kuitwa Azan Zungu ningefungua nyuzi hata 50 kuhamasisha apambane na hali yake sababu ni mtu wa hovyo asiejali utu!

Ila kwa Prof. Jay huo utakuwa ni ukosefu wa utu maana jamaa hana baya kabisa! Hajawahi kuropoka utumbo na ni mtu asie na noma na wananchi!
 
Nakumbuka kulikuwa na ofc nafanya Kaz moja Kati ya maboss wa hyo kampuni aliuguwa figo michango ikachagwa na jama Ni doni tu nae siku moja nikasikia majungu kutoka kwa kijna wa boss akisema tunamchangia mtu ambae anajenga nyumba dsm tegeta .. kweli watu wanachangishana
Huyo Dogo mxenge kweli aisee figo iacheni ikiamua kuleta kirambasi ujue kama huna hela watu wapange taratibu za mazishi tu
 
Aahaah wapi mkuu, dogo wake wakishirikiana na mke wake walikiri mzigo wa matibabu umekuwa mkubwa hivyo wanahitaji huruma za watanzania wanyonge waweze kufanikisha hilo zoezi la jamaa kupewa matibabu..

Figo isikie mkuu, ikiwa comprimized sana inasababisha MOF, so guess what will be next?? Hapo ni coma then caput..
Mzigo unafika 4M kwa week mzee! Unahitaji kuwa na serious investment kukabiliana na hilo Gap!

Angekuwa kwenye Ubunge isingekuwa shida sana. Maana wabunge wenzie wangemchangia sana na hata Serikali ingegharamia matibabu yake.
 
Mleta mada unazifahamu gharama za dialysis kweli?Tumuombee tu mwenzetu...Na acha watu wenye Moyo wa kutoa wamchangie....achana na hii kampeni
 
Ngoja siku figo ifeli ndy akili ikukae sawa

Unamkumbuka Ruge mtahaba? Bakuli zilivyo pitishwa?
Ruge alikuwa anapigwa 6M daily jamaa wakawa wamepiga kimya ilipofika mzigo umegonga 650M ilibidi wafunguke tu kuwa mziki mnene jamani tunaomba mlioguswa tusaidiane😂!

Hao ni Clouds Media Group pamoja na viburi vyao vyote.
 
Use Antibiotic when necessary and let it be the last options bro…

Pia unaweza kuwa na good lifestyle ila unakuta vyakula tunavyokula hasa hawa broilers, mayai, maziwa unakuta yana antibiotic residues kama zote…

Sidhani kuna mfugaji ambaye yuko tayari ku discard maziwa, mayai kisa ametoka kutibu mifugo yake..

Public health is still a big proble kwetu waafrika kwa ufupi tumejawa na ubinafsi sana kutokujali afya za walaji.
Dah kumbe hata haya ma broilers na maziwa and all that yana chemical za ajabu?
 
Acha kabisa hio moment ya kusomewa mkeka wanaitwa wazee kwenda kuchukua taarifa za deni! Lazma warudi mwengine mkono kiunoni mwengine anaongea na simu 😂huku akipuputa jasho!


Naonaga pale Mloganzila mgonjwa anaporuhusiwa ndugu wanavyofanya vikao pale chini vya michango ya kulipa bili ndio mgonjwa atoke.
Hao ndugu wenyewe ukiwaangalia wengi hata nauli ya mwendo Kasi ya kimara ni shida, wamekauka midomoo.. Sasa Kuna huyo mkuu wa msafara yeye anapiga simu kwa ndugu wa mbali na kile kitecno triple line.
Kuna binti mmoja aliambiwa akalipie elfu kumi na sita ili apigwe x Ray.
Aliruka hatua kumi na sita huku akilalamika ashamchungulia daktari kwa elfu ishirini bado alipie x-ray ndio alipie dawa? Kwani waganga wa jadi wameisha?
 
Back
Top Bottom