Mimi ni Mkristo mlokole, nimeanza kukosa Imani na ukristo nahisi Uislam ndiyo dini ya kweli

Mimi ni Mkristo mlokole, nimeanza kukosa Imani na ukristo nahisi Uislam ndiyo dini ya kweli

Nilimsikia nabii mkuu na mtume mkuu dr Geordavie kwamba yeye anafanya mambo makuu kuliko Yesu! Sababu yeye anatoa hela na misaada ya fedha na mitaji wakati Yesu hakutoa fedha wala mitaji. Waumini walishangilia na kuweka hela miguuni mwa mtume mkuu!
Yani ni maigizo kweli kweli mkuu.
Kuna muda mambo yanayoendelea kanisani ni bora walevi bar.
Kwaya zimejaa uzinzi, wachungaji na manabii nao pia, mavazi na uimbaji utadhani uko fiesta.
Mahubiri siku hizi 99% ni toa ndugu, na yanamfaidisha mchungaji anakula bata dubai na kuishi kama elon musk.
Ukiwauliza, majibu ni Mungu anaangalia moyo.
Wakati imeandikwa kilicho ndani mwako kitajidhihirisha nje.
Hao akina geodavie wanajiita manabii kila sku kuna nabii mpya.
Ukweli ni kwamba siku hizi watu hawaendi kanisani kuabudu bali wanataka kuwa part of a community tu.
 
Napenda sana ibada ,naamini kupitia ibada mambo mengi yanaweza kuwa sawa! Napata shida kidogo na Imani yangu ya ukristo ,miaka ya 1980 ---1990 ibada ilikuwa nzuri sana kokote utakakoenda kusali na kanisa lolote utakaloingia Ibada zilikuwa na nguvu halisi ya mungu ,hapakuwa na makorombwezo Wala mbwembwe kama Sasa! Huwa navurugwa sana nikiingia kanisani mambo mengi yamebadilika! Kanisa la Sasa imekuwa sehemu ya disco ,dance na mitindo ya hovyo ya mavazi,wanawake wanavaa nguo ambazo hata kwenye baadhi ya bar hawavai na wachungaji wako busy na mapato na matumizi, mahubiri asilimia tisini ni fedha na mipasho ! Nimechoka na miujiza ya zana kama uganga ,kanisa la Leo mchungaji anaamini lazima abebe zana ndio apande madhabahuni ,ukristo unabadilika Kila mwaka ,sura ya kanisa sio Ile ya 1990 ,2000,Kila mwaka kanisa linavaa sura nyingine,wachungaji wetu wanavita kubwa ya kugombea waumini kiasi hawana ushirikiano Tena ! Ni maadui na hawana maombi ya pamoja Tena kama zamani ,Kila mchungaji yaonekana kama ana mbingu ya kwake ,Kuna kundi wanajiita mitume na manabii na Kuna kundi la maaskofu na wachungaji ,maaskofu na wachungaji wanahisi wao nao wanambingu Yao ambayo mitume na manabii hawataenda ! Na mitume na manabii pia wanaona wachungaji na maaskofu hawana nguvu ya mungu Tena! Hizi ni dalili mbaya sana kwa miaka 20 ijayo ya ukristo, mpaka Sasa asilimia 70 waislam wako sawa na unaweza kuwaelewa ! Lakini wakristo wamefeli kabisa , naikubali sana ibada ya hija na Ile ya kuchinja waislamu wanaungana Duniani kote kwa ajili ya Allah! Lugha Yao inakuwa Moja na kauli Yao ni thabiti kabisa ,wanavaa vizuri sana wanapokuwa kwenye ibada na hata ,huwezi kuyaona mapaja ya mwanamke msikitini yakiwa nje sijui kama nitaweza kuuvumilia ukristo kwa miaka michache ijayo mungu aturehemu !
Nimegundua we unachukulia dini Kama timu ya kushabikia. Unaona man u imeanza kufungwa unahamia man city...ukimaliza kuruka ruka hizi dini utafika conclusion kuwa zote ni man made zimeundwa na binadamu kwa ajili ya binadamu.
 
Napenda sana ibada ,naamini kupitia ibada mambo mengi yanaweza kuwa sawa! Napata shida kidogo na Imani yangu ya ukristo ,miaka ya 1980 ---1990 ibada ilikuwa nzuri sana kokote utakakoenda kusali na kanisa lolote utakaloingia Ibada zilikuwa na nguvu halisi ya mungu ,hapakuwa na makorombwezo Wala mbwembwe kama Sasa! Huwa navurugwa sana nikiingia kanisani mambo mengi yamebadilika! Kanisa la Sasa imekuwa sehemu ya disco ,dance na mitindo ya hovyo ya mavazi,wanawake wanavaa nguo ambazo hata kwenye baadhi ya bar hawavai na wachungaji wako busy na mapato na matumizi, mahubiri asilimia tisini ni fedha na mipasho ! Nimechoka na miujiza ya zana kama uganga ,kanisa la Leo mchungaji anaamini lazima abebe zana ndio apande madhabahuni ,ukristo unabadilika Kila mwaka ,sura ya kanisa sio Ile ya 1990 ,2000,Kila mwaka kanisa linavaa sura nyingine,wachungaji wetu wanavita kubwa ya kugombea waumini kiasi hawana ushirikiano Tena ! Ni maadui na hawana maombi ya pamoja Tena kama zamani ,Kila mchungaji yaonekana kama ana mbingu ya kwake ,Kuna kundi wanajiita mitume na manabii na Kuna kundi la maaskofu na wachungaji ,maaskofu na wachungaji wanahisi wao nao wanambingu Yao ambayo mitume na manabii hawataenda ! Na mitume na manabii pia wanaona wachungaji na maaskofu hawana nguvu ya mungu Tena! Hizi ni dalili mbaya sana kwa miaka 20 ijayo ya ukristo, mpaka Sasa asilimia 70 waislam wako sawa na unaweza kuwaelewa ! Lakini wakristo wamefeli kabisa , naikubali sana ibada ya hija na Ile ya kuchinja waislamu wanaungana Duniani kote kwa ajili ya Allah! Lugha Yao inakuwa Moja na kauli Yao ni thabiti kabisa ,wanavaa vizuri sana wanapokuwa kwenye ibada na hata ,huwezi kuyaona mapaja ya mwanamke msikitini yakiwa nje sijui kama nitaweza kuuvumilia ukristo kwa miaka michache ijayo mungu aturehemu !
Sasa unatupa taarifa au unatupa habar
 
Nikushukuru kwanza kwa kulitambua Hilo. Ila nikushauru kitu kimoja kabla hujaamua kuhamia kwa waislamu. Chunguza vizuri dhehebu la waadventista wasabato utagundua kitu
Yale yale ya kuabudu siku wewe muache aende akawe muislam then akaonje joto la jiwe,watu wanakimbilia favours za ajabu mimi nina experience na hili jambo.

Mke zaidi ya mmoja sijui kutoa talaka na vitu kama hivyo imani iliyojengwa rohoni haiachwi kizembe zembe hivi kuna cha ziada unafikiri anakotaka kuhamia hakuna wanaotaka kutoka?,wapo huko sababu wanajua wanafanya nini sasa kama mtu anafanya kwa ajili ya fulani huyo apewe nafasi
 
Yesu Hana kanisa ,kanisa linaongozwa na mchungaji Kila muumini ana mchungaji wake ,mchungaji akipotoka kanisa lote linapotoka !
Kichwa cha kanisa ni Kristo, kwahiyo kiongozi ni Yesu na siyo Mchungaji.

Wakolosai 1:17
Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.

Wakolosai 1:18
Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.

Wakolosai 1:19
Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote
ukae;


Soma pia:

Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
Efe 5:23‭-‬24 SUV

 
Sio kweli ila ukristo sio baba yangu Wala mama yangu
Kama kweli we ni mkristo Unajua ni wapi kwa kupata majibu!ila kama upoupo tu unataka mambo yaende unavofikilia hutoacha kuhamahama ibada za mwanadamu,hata huko uislam Kuna mambo ukikuta tofauti utahama,mwisho utapotea mazima
 
Ulikua mkristo wa kanisa yani wa kujiandikisha namaanisha. Uliwakuta wazazi ni wakristo tu na wewe ukaingia wala hukupata nafasi ya kumtafuta wewe binafsi niseme haukuwa wa kristo wewe. Huyu kristo ukimjua hakuna namna unayodhani unaweza kuachana nae.
Umejibu vema sana mkuu...

Nakazia, Ukimjua Kristo hata dhambi haiwezi kukutenganisha nae:

Rum 8:35‭, ‬38‭-‬39 SUV
Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Mleta mada anzia hapohapo ulipo kumtafuta Kristo Upya.
 
shida sana.Mungu atusaidie tu mambo ni mengi muda mchache,thtabaki wenye vifua vikubwa tunaweza kupambana na mawimbi.kwa mfano huna sadaka unaenda kukaa siti ya mbele kabisa kuonesha hauendi church kwa ajili ya kutoa bali kumwonba Mungu.
 
Kama alivyokutana na Saulo basi Bwana na akutane nawe. Nakuombea neema yake ikufunike. Usilale mauti kamwe kabla hujakutana nae.
Kanisa la kihuni Hilo
20231004_211324.jpg
Screenshot_20231004-211001.jpg
 
Back
Top Bottom