Hukumu iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu, ya mjane wa bilionea wa madini, Bilionea Msuya, Miriam Steven kusomwa leo.
Miriam pamoja na mshtakiwa mwenzake, Revocatus Everist Muyella, maarufu kama Ray, wanakabiriwa na shtaka la mauaji ya kukusudia, wanadaiwa kumuua kwa kumchinja, Aneth Elisaria, mdogo wa marehemu bilione Msuya.
Hukumu hiyo inatarajiwa kusomwa na Jaji Edwin Kakolako, ambayo ndiyo itaamua hatima yao kama wana hatia au lah. Kama watakutwa na hatia hukumu ni kunyongwa hadi kufa.
Watuhumiwa wamekuwa mahabusu kwa nane na leo ndio hatima yake, je, nini kitatokea leo Mambo yatakuwaje? Nini itakuwa hukumu ya kesi hii? Mke wa Msuya na mwenzake watakutwa na hatia au lah?
Mjane wa Bilionea Msuya alikuwa anatetewa na Wakili Peter Kibatala.