Mkataba wa Yanga na Sport Pesa waingia mdudu baada ya Yanga kutambulisha mdhamini mpya

Mkataba wa Yanga na Sport Pesa waingia mdudu baada ya Yanga kutambulisha mdhamini mpya

Umepanic tayari.......soma tena bandiko la Sportpesa ujue nini kimeandikwa, Simba ana husika vipi hapo. Viongozi wenu walitakiwa wawe makini na mkataba.
Wanakua wakali utafikiri nyoka koboko injinia anapigiwa simu kuulizwa povu linamtoka aiseee
 
So unataka kusema hadi SportPesa wanatoa hili tamko ni kwamba hawambui mipaka yao? Sentensi ya mwisho imesema:
'SportPesa reserves its rights to seek compensation and recourse from the relevant authorities for the damages caused'
Hii issue kwakweli sijailewa bado! Labda niulize, ni kitu gan kilisababisha Simba kukatakiwa na Caf kutumia jezi zenye nembo ya sportpesa hapo nyuma?
 
Hii issue kwakweli sijailewa bado! Labda niulize, ni kitu gan kilisababisha Simba kukatakiwa na Caf kutumia jezi zenye nembo ya sportpesa hapo nyuma?
CAF wana mdhamini wa michuano 1XBet hivyo kutakuwa na mgongano wa maslahi..
 
Sportpesa yupo sahihi. Alinunua nafasi ya kifuani kwenye jezi official ya yanga sports club kwa timu zote na mashindano yote hata match za kirafiki.

Tofauti na simba, mbet amenunua nafasi ya kifuani kwa senior timu tu ya wanaume ila kwa mashindano yote. Simba queens na under18 simba inaweza tafuta sponsor mungine.
Na Simba queen pia kanunua juzi juzi Tu hapa
 
Mkuu, kwenye mkataba EVERY WORD COUNTS…!!!
Kila neno lina maaana KUBWA SANA kwani linaweza kufanya mkataba ukavunjika kijinga sana au ukasimama vizuri sana
Na ndio advantage wanayoweza kunufaika SportPesa kisheria katika hilo

Kwasababu bonus always ni reward isiyokuwa na ulazima
 
Hersi kaingiza watu choo cha kike wache wakojoe huku wamechuchumaa
 
Hii issue kwakweli sijailewa bado! Labda niulize, ni kitu gan kilisababisha Simba kukatakiwa na Caf kutumia jezi zenye nembo ya sportpesa hapo nyuma?
Katika mashindano yoyote, anayepewa kipaumbele kuchagua mdhamini ni mwenye mpira (TFF, CAF au FIFA kutegemea na ngazi ya mashindano). Chama cha soka kinaanza kwanza kuchagua mdhamini, baada ya hapo timu zinaweza kuleta wadhamini wao kwenye jezi ili mradi biashara wanayofanya haishindani moja kwa moja na biashara ya mdhamini wa mashindano.

Kujibu swali lako, Simba haikutakiwa kuitumia SportPesa katika jezi zao kuanzia ngazi ya makundi ya CAF competitions (hapa ndipo inahesabika ligi imeanza) maana tayari ligi hiyo mmoja wa wadhamini ambaye ni 1Xbet anafanya biashara kama ya SportPesa. Kwa hiyo kwa kuwa SportPesa tayari alikuwa ameingia mkataba na Simba, aliheshimu utaratibu wa mdhamini wa ligi ya CAF ila kwa makubaliano kwamba SportPesa aridhie mbadala wa nembo itakayokaa katika jezi, na kwa pamoja wakakubaliana itumike Visit Tanzania

Mwaka huu kwa maelezo ya taarifa hiyo iliyotoka ya SportPesa, Yanga walipeleka ombi SportPesa kutaka kuweka mdhamini huyu mpya, lakini SportPesa wakakataa na kupendekeza waweke Visit Tanzania, ila Yanga wakapuuza na kuendelea na utaratibu wa huyu mdhamini na kama ulivyoona wamemtangaza na kumtumia
 
Kuna siku nimesema humu kuwa uongozi wa Said na Gsm una Mambo mengi ya kijuaji na ujinga mwingi..., Ndani ya miaka miwili tiyali timu imeshaingia kwenye migogoro ya kimkataba 3...
1.Morrison
2.Fei
3.Sportpesa, ujuaji umezidi kwa viongozi wa yanga matokeo yake hakuna mdhamini au mtu mwenye pesa zake akaja kuwekeza yanga. Haya Mambo yanaichafua yanga bana, watu wamewekeza muda mrefu afu kanakuja kajinga Kama Said kanafanya Mambo kitoto hivi?. Upuuzi kabisa..
 
Tusitete upuuzi wa viongozi Kama huu, tunamlalamikia fei kuheshimu mkataba vipi sisi timashindwa kuheshimu mkataba wa sportpesa?. Tusiww wapuuzi kiwango hiki haifai na ni ujinga kuona viongozi wanakiuka mikataba na kuwatetea.
Basi mi naona sportpesa kakurupuka
 
Huna uelewa wowote na hilo ulisemalo.

Nionyeshe wapi nimesema sport pesa hana mamlaka na Yanga?. Tumia akili kusoma na kuelewa kwanza bandiko la mtu kuliko kukurupuka kujibu usichokielewa.

MSAADA WAKO
Hatua za awali kila club inajitegemea kwa kila kitu ndio maana wanaenda na jezi zao za ligi.

Kuanzia makundi CAF inatoa pesa kwa clubs. Ili kufanya hivyo inatafuta mdhamini. Kama mdhamini wa club anafanya biashara sawa na wa caf ndipo sheria za caf zinaitaka club hiyo kutovaa jez za mdhamini huyo.

PUNGUZA NONGWA, NI SHIDA ZAKO TU
Duh. We kweli umeshindikana
 
Kitengo cha Sheria cha Yanga kina mapungufu mengi kwasababu walitakiwa kuliona hili wakati wanasaini mkataba na Sportpesa. Hata hivyo Yanga wapo sahihi kwasababu ukiweka kwenye mizani kesi za mikataba ya kibiashara mara nyingi huwa inaisha kistaarabu ili kulinda image za pande zote. Ukisoma vyanzo mbalimbali ni kwamba Yanga walitarajia reaction hii ya Sportpesa na walishafanya calculation zao na kupata mlango wa kutokea.
 
Wachezaji kutosajiliwa ndio inapoteza maana ya mashindano?

Unaelewa maana ya mashindano?
Qualifications za kucheza mapinduzi ni zipi? nitajie mashindano official ambayo mchezaji anaweza cheza bila kusajiliwa na club!
 
Kitengo cha Sheria cha Yanga kina mapungufu mengi kwasababu walitakiwa kuliona hili wakati wanasaini mkataba na Sportpesa. Hata hivyo Yanga wapo sahihi kwasababu ukiweka kwenye mizani kesi za mikataba ya kibiashara mara nyingi huwa inaisha kistaarabu ili kulinda image za pande zote. Ukisoma vyanzo mbalimbali ni kwamba Yanga walitarajia reaction hii ya Sportpesa na walishafanya calculation zao na kupata mlango wa kutokea.
Mi kweli tishio la backlash ya mashabiki wa Yanga inaweza kuwafanya SportPesa kunywea hata kama kisheria wana madai yenye mashiko. Ila hizo ni mbinu za kihuni na siyo zinazotakiwa kufanywa na professional organisation.
 
Hii ndiyo YANGA SC ya mwendo kasi wa kukurupuka.
 
Kuna siku nimesema humu kuwa uongozi wa Said na Gsm una Mambo mengi ya kijuaji na ujinga mwingi..., Ndani ya miaka miwili tiyali timu imeshaingia kwenye migogoro ya kimkataba 3...
1.Morrison
2.Fei
3.Sportpesa, ujuaji umezidi kwa viongozi wa yanga matokeo yake hakuna mdhamini au mtu mwenye pesa zake akaja kuwekeza yanga. Haya Mambo yanaichafua yanga bana, watu wamewekeza muda mrefu afu kanakuja kajinga Kama Said kanafanya Mambo kitoto hivi?. Upuuzi kabisa..
Kuna taasisi ambayo haina migogoro ya kisheria? issue ya Feisal Yanga kakosea wapi?
 
Tusitete upuuzi wa viongozi Kama huu, tunamlalamikia fei kuheshimu mkataba vipi sisi timashindwa kuheshimu mkataba wa sportpesa?. Tusiww wapuuzi kiwango hiki haifai na ni ujinga kuona viongozi wanakiuka mikataba na kuwatetea.
Mkuu umeusoma mkataba wa Yanga na Sportpesa?
 
Back
Top Bottom