Mkoa wa Pwani watoa Mawaziri watano kwenye baraza jipya; ni bahati mbaya au ndiyo tuseme sasa zamu ya watu wa Pwani?

Kama wana uwezo na ni wa Tanzania ni sawa, tofauti na hapo tusiingie kwenye siasa za kidini na ukabila.

Sisi sote ni wa Tanzania, kikubwa tuangalie uwezo wa mtu na nafasi aliyowekwa, kuhoji wanatokea wapi ni kama uchochezi.
Yah right. Uwezo wa Watanzania wa eneo fulani unabadilika au kuongezeka kutokana na Rais aliyeko madarakani.
 
Sidhani kama regional representation ni kitu official bali kilianzishwa na Mkapa ili apate political support kubwa pande zote za nchi.
Regional Representation ni tunu adimu aliyoitumia baba wa Taifa kujenga umoja na mshikamano.

Tusipo enzi hilo hali ya South Sudan itatunyemelea
 
Hebu tupe idadi ya kanda ya ziwa
Kanda ya kaskazini.
Kanda ya nyanda za juu kusini...

Hizi siasa za kifala, watoto wetu watakuja kutudharau sana
Kanda na mkoa ni vitu 2 tofauti, kanda yaweza kuwa na mikoa zaidi ya 3. Hapa tunaongelea mkoa wa PWANI
 
Hiyo paragraph ya mwisho inafikirisha sanaaa... Unamtoa Mchengelwa na kumuweka Jenista??? Kiukweli sijawahi kuelewa vigezo vya hizi teuzi..
 
Enzi zile sasa
1. Bitteko-home kabisa
2. Kalemani- Wa sebuleni
3. Mabula- wa nyumbani
Achana na hao wa Shinyanga sijataka kuwajumuisha.
Mabula sio mwanza?, sasa Mwanza na chato wapi na wapi au tatizo ni kuongea Kisukuma???
 
Hapa Ingekua Magufuli katoa Mkoa wa Geita Mawaziri watano Mkoa mmoja. Mitandao ingepasuka. Kunaunafiki mwingi sana nchi hii. Wasukuma wapo kabla ya Tanzania na watakuwepo baada ya Tanzania imani yao ni kilimo na ufugaji. Biashara na siasa wamejifunza hivi karibuni.
 
Na asikudanganye mtu mikoa yenye mawaziri au naibu waziri wakazi wake wananufaika kweli labda waziri au naibu waziri awe ajitambui.Mkoa ninaotoka waziri anawakimbiza watumishi usiseme na hakuna kinachokwama, ukikwama unamtwangia simu naye hapohapo anawatwangia simu utaona watumishi wanakimbizana humo ofisini.
 
Kumbe watano tu hakuna kibaya japo wakitoka kanda ya ziwa hata wawili husemwa sana hasa kipindi kile.

Am done for today
Wangekua Kanda ya Ziwa Mkoa mmoja Mawaziri wawili kungenuka hapa. Mfano Mkoa wa Mara hakuna Waziri tangu 2020 siyo issue. Mkoa wa simiyu 1 Shy hakuna Kuna naibu, Mwanza wamepata Waziri kamili awamu hii 1. Mkoa wa Geita 1 Waziri.

Pwani 5
Tanga 3.

Assalamualaikum
 
Ikiwezekana Mchengelwa apewe uwaziri wa fedha kabisa ili apiganie Rufiji na wilaya jirani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…