Morogoro: Tundu Lissu awasha moto, ashangaa mabango ya kupatanishwa yaliyobandikwa nchi nzima

Morogoro: Tundu Lissu awasha moto, ashangaa mabango ya kupatanishwa yaliyobandikwa nchi nzima

Katika Mkutano wake Mkubwa wa hadhara wa Morogoro Mjini leo hii , ambao bila shaka umevunja rekodi ya Mahudhurio , Pamoja na Mambo mengine Tundu Lissu anahoji anayebandika mabango nchi nzima yakiwa na picha yake na ya watu wengine kwamba eti wamepatanishwa , amehojiwa kama wamepatanishwa , wamepatanishwa na nani ?

Anadai kwamba hizo ni propaganda za kichovu , na kwamba anawezaje kupatanishwa huku kukiwa na watu waliouawa , kutekwa na kuumizwa na hatima yao wala habari zao hadi leo hazijulikani ?

Akiongea kwa uchungu , Lissu anadai yeye mwenyewe alitandikwa risasi na hadi leo hakuna yeyote aliyekamatwa , anawezaje kupatanishwa na watu wa aina hiyo , anadai sasa hivi anaitwa CHIBA kutokana na majeraha ya wauaji wake (kwa wasiolewa chiba ni lugha ya mjini ikimaanisha mlemavu wa mguu) ,

amezungumzia kupotezwa kwa watu wengi sana akiwemo Ben Saanane , ambao hawajulikani walipo hadi leo , huku wenye madaraka au vyombo vya dola vikinyamaza , anasema katika hali hii anawezaje kupatanishwa na waliokuwa madarakani unyama huu ukitendwa ? na kwamba ambaye hayupo miongoni mwa watenda unyama huo ni mmoja tu , lakini wengine wote bado wapo , hapa unapanishwaje ?

Lissu anadai Arusha ndio mkoa unaoongoza kwa Mabango ya uongo yaliyopachikwa upatanishi , huku sisi wengine tukidhani lengo lao ni kudanganya watalii ili waone nchi sasa iko shwari.
Pamoja sana kamanda Tundu Antipas Mugway Lissu. Ni kweli aliyewatuma wauaji wako hayupo duniani lakini wauaji na chawa wake bado wanadunda mtaani. Watanzania acheni au kama haiwezekani kuacha punguzeni unafiq, sio jambo zuri.
 
Pamoja sana kamanda Tundu Antipas Mugway Lissu. Ni kweli aliyewatuma wauaji wako hayupo duniani lakini wauaji na chawa wake bado wanadunda mtaani. Watanzania acheni au kama haiwezekani kuacha punguzeni unafiq, sio jambo zuri.
Kamanda anayetaka kuwapa watoto wake uraia wa EU......
 
Lisu akue sasa swala la yeye kupigwa risasi akubali sio ajenda ya taifa ajenga hoja
Mfano mambo ya kodi tozo ufisadi
Cag nk
Au aboost kidogo na mwanafunzi udom walau kwa sasa itambeba
 
Lisu akue sasa swala la yeye kupigwa risasi akubali sio ajenda ya taifa ajenga hoja
Mfano mambo ya kodi tozo ufisadi
Cag nk
Au aboost kidogo na mwanafunzi udom walau kwa sasa itambeba
Wala yeye hakusema ni ajenda ya kitaifa
 
Katika Mkutano wake Mkubwa wa hadhara wa Morogoro Mjini leo hii , ambao bila shaka umevunja rekodi ya Mahudhurio , Pamoja na Mambo mengine Tundu Lissu anahoji anayebandika mabango nchi nzima yakiwa na picha yake na ya watu wengine kwamba eti wamepatanishwa , amehojiwa kama wamepatanishwa , wamepatanishwa na nani ?

Anadai kwamba hizo ni propaganda za kichovu , na kwamba anawezaje kupatanishwa huku kukiwa na watu waliouawa , kutekwa na kuumizwa na hatima yao wala habari zao hadi leo hazijulikani ?

Akiongea kwa uchungu , Lissu anadai yeye mwenyewe alitandikwa risasi na hadi leo hakuna yeyote aliyekamatwa , anawezaje kupatanishwa na watu wa aina hiyo , anadai sasa hivi anaitwa CHIBA kutokana na majeraha ya wauaji wake (kwa wasiolewa chiba ni lugha ya mjini ikimaanisha mlemavu wa mguu) ,

amezungumzia kupotezwa kwa watu wengi sana akiwemo Ben Saanane , ambao hawajulikani walipo hadi leo , huku wenye madaraka au vyombo vya dola vikinyamaza , anasema katika hali hii anawezaje kupatanishwa na waliokuwa madarakani unyama huu ukitendwa ? na kwamba ambaye hayupo miongoni mwa watenda unyama huo ni mmoja tu , lakini wengine wote bado wapo , hapa unapanishwaje ?

Lissu anadai Arusha ndio mkoa unaoongoza kwa Mabango ya uongo yaliyopachikwa upatanishi , huku sisi wengine tukidhani lengo lao ni kudanganya watalii ili waone nchi sasa iko shwari.
Tulishaandika mara kadhaa humu JF, kitu pekee kilichobadilika ni "mtindo (style)" tu ya uongozi.

Badala ya vurugu nyingi, makelele na kuumiza watu moja kwa moja, sasa kinachofanyika ni kutumia lugha laini tu, ya kupoza na kusahaulisha, huku malengo yakiwa ni yale yale ya tokea mwanzo.

Tena matokeo ya hii lainisha yatakuwa ni mabaya zaidi, kwa sababu hata baadhi ya wapambanaji watachanganyikiwa akili na kuachana na mapambano ya kuikomboa Tanzania toka kwa mkoloni huyu CCM.
 
Mbowe na Maridhiano : Siasa

Erthyrocyte ,imhotep ,TL: Harakati [emoji1787]
Maridhiano ndiyo hayo yanaenda kulikomboa Taifa kwa mfano Katiba Mpya sio ya CHADEMA pekee tumelilia marekebisho ya HAKI Jinai nalo linafanyiwa kazi.
 
Kwa mara ya Kwanza na muunga Mkono Lissu. Ukiondoa propaganda zingine Haijalisihi, sababu zangu zitajulikana mbeleni. Walakin, Sijamsikia Mbowe akiwa na mtazamo huo. Kulikoni? au miye sina Taarifa!

Kitaeleweka....tafuteni mahojiano ya Heche ya hivi karibuni.
 
ila mabango hata mimi wananikera sana..eti unakuta bango mjini katikati ya miji inabandikwa ..amejenga shule(x), amejenga madaraja(x), barabara (x)......, hizo gharama za kuyatengeneza na kuyabandika si ghali sana?...nawaza kwa sauti sana..hivi ccm wao wanawazaga vitu gani kwenye vichwa vyao??..ina maana akili zao wao wameziweka rikizo wanatumia akili za mihemko tu muda wote?
Sa100 anaogopa kusimama mbele ya wananchi, anategemea hayo mabango yamsaidie. Sa100 bila speech ya kuandikiwa hawezi kuongea hata kwa dk 15.
 
Back
Top Bottom