Mshahara umetoka, nyongeza ipo lakini lazima ucheke tu

Mshahara umetoka, nyongeza ipo lakini lazima ucheke tu

Wewe huwezi kuwa Mtumishi, nakataa huwezi kuwa.

Elfu 9000, ni sawa na 9,000,000 ni kweli umeongezewa hiyo pesa.?
Unataka nikuonyeshe saraly sleep ,me napokea mshara wa 1,350,000, nimeona kilichoongezwa akizidi elf 9,000
 
Bora huyo Me nimeongezwa elf 9000, ujinga mtupu,nieli ya magufuri mala 100, Maana kwa Magufuri mfumuko wa bei ulizibitiwa, Sasahivi majanga matupu huu ni upuuzi,Samia katuzalau wafanyakazi
yaani sijaelewa bado rais kimempata nini mpaka akatufanyia hiki alichofanya, ila poa tuu maisha yenyewe tunapita tuu haya
 
Kamwe aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Pamoja na sifa na tambo zote walizofanya serikali kuhusu kuongeza mishahara wameishia kuongeza elfu 20,000?

Ikiwa ni muda mchache toka bank ya NMB kunipa notification ya mshahara kuingia na kufanikiwa kuona kilichoongezeka. Nimepigwa butwaa kuona tambo zote zile increment haizidi 20K!

Nadhani Sasa ni muda wa watumishi wa umma kujitambua na kuacha kushoboka na serikali. Serikali ime-inflate gharama za maisha kwa kiwango kikubwa but then haina efforts za kuboresha maslahi.

Maamuzi ya namna hii yanapunguza morali ya kazi na kushusha uadilifu. Tutegemee uzembe makazini na kuongezeka ubadhirifu.

Serikali imeshindwa kusimamia utumishi wa umma hususani kwenye suala la maslahi.
MAMA ANAUPIGA MWINGI SANA CCM OYEEE
 
Maana yake ni kwamba hiyo 23.3% nyongeza ya mshahara waliyoahidiwa watumishi wamedanganywa.

Manake Serikali hii sio ya kuiamini tena kwenye chochote itakachokisema.

Ongezeko lililotamkwa kimahesabu haliwezi kuwa ni elf20 tu,ni uongo uliotukuka sana,labda waje waseme kama tamko lilikosewa au mahesabu yamepigwa kimakosa.

Rais ataanza kuwa sio wa kuaminika kama Waziri Mkuu,hili ni doa kubwa sana kwake,kama hakuwa na uwezo wa kuongeza huo mshahara kwa kiwango alichokitamka bora hata angesema ukweli,uongo uongo hauna mwisho mzuri kwake.

Hii ni aibu kubwa sana kwa utawala wa awamu ya sita
 
Dah.. Bora niendelee kupiga forex tu!

Nikitengeneza $10 kila siku kwa mwezi nina kama kilo 6!

Watumishi poleni..


Bora Magu hakuongeza kabisa mshahara ila vitu havikuwa bei juu namna hii!

Sasa hiyo 20 inamsaidia nini mtu ambae garama za maisha zimepanda kwa kasi namna hii?
 
Ni kupunguza matumizi yasiyo na ulazima

Hivi Elfu 20/mwezi unaipunguzia nini? Wafanyakazi wa Tanzania hawana hitaji lisilo la lazima, mshahara wenyewe hata wiki 2 hautoshi na hilo ni kula, pango, umeme, nauli labda na vocha, sasa hapo anapunguza nini ?
 
Back
Top Bottom