Msipotoshe kuhusu Papa na ndoa za jinsia moja

Msipotoshe kuhusu Papa na ndoa za jinsia moja

Papa Francis amewaruhusu mapadre kuwabariki wapenzi wa jinsi moja, yakiwa ni maendeleo makubwa kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja na mahusiano mengine ya kijinsia wanaofahamika kama LGBT katika Kanisa Katoliki la Roma.

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki la Roma amesema makasisi wanapaswa kuruhusiwa kuwabariki wapenzi wa jinsi moja na wanandoa "isiyo ya kawaida", kwa misingi ya hali fulani.

Lakini Vatikani ilisema baraka hazipaswi kuwa sehemu ya taratibu za kawaida za Kanisa au zinazohusiana na miungano ya kiraia au harusi.

Iliongeza kuwa inaendelea kuiona ndoa kuwa kati ya mwanamume na mwanamke.

Papa Francis aliidhinisha waraka uliotolewa na Vatican kutangaza mabadiliko hayo siku ya Jumatatu.

Vaticani ilisema inapaswa kuwa ishara kwamba "Mungu anawakaribisha wote", lakini hati hiyo inasema makuhani lazima waamue kwa msingi wa kesi baada ya kesi.

Akitambulisha andiko hilo, Kardinali Víctor Manuel Fernández, ambaye ni msimamizi wa Kanisa, alisema kwamba tamko jipya limebakia kuwa "imara kwenye fundisho la kimapokeo la Kanisa kuhusu ndoa".

Lakini aliongeza kuwa kwa kuzingatia "maono ya kichungaji" ya Papa" ya "kupanua" ombi la Kanisa Katoliki, miongozo mipya inawaruhusu mapadre kubariki uhusiano ambao bado unachukuliwa kuwa wa dhambi.

Watu wanaopokea baraka "haifai kuhitajika kuwa na ukamilifu wa kimaadili wa awali", kulingana na tamko hilo.

Katika Kanisa Katoliki, baraka ni maombi au ombi, ambalo kwa kawaida hutolewa na mhudumu, akimwomba Mungu ambariki mtu au watu wanaobarikiwa.

Kardinali Fernández alisisitiza kwamba msimamo huo mpya hauhalalishi hadhi ya wapenzi wa jinsia moja mbele ya Kanisa Katoliki.

NB: Hii ni taarifa ya BBC: Lakini kumbukeni BBC wanatetea dhehebu la Anglican ambalo suala la ushoga ama ndoa za jinsia moja ni kawaida kwa Waingereza. Papa alichosema ni kwamba watu wenye ndoa za jinsia moja ni wenye dhambi kama wengine, isipokuwa wakija kanisani kwa kutubu basi wabarikiwe kama binadamu wengine wenye dhambi wabarikiwe ili wajirudi.
upuuzi mtupu!!!....wewe unafikiri angetangaza waziwazi?...lazima azunguke,,,,ni kama kumtongoza msichana unaempenda sana,hauwezi kumwingia direct,MUNGU alipolipoa SODOMA na GOROMA,kwa ajili ya ushoga mbona hakuwabariki???badala yake akawaua wote???,,,,wewe uliyeandia huu ujumbe ni waleale,,,kimsingi mimi nilikuwa mkatoliki lakini sitaki tena!!,,,kumbe yule papa kabla ya huyu alikataa shinikizo la kundekeza ushoga ndo manake akaachia ngazi,,sasaivi UGANDA kuna shinikizo kubwa kuhalalisha usenge!! shetani yupo kazini!!!...kanisa litaanguka vibaya sana,waumini weingi watahama hasa afrika!!
 
Sijataka hata kusoma......!!!! Napita zangu tu bhana.
 
Nadhani kanisa lina mkono mrefu sana,huyo papa ataondolewa soon
 
Even satan himself is not a gay, he approached naked Eve instead of naked Adam!!
By Robert Mugabe
 
Kiukweli sasa ukatoliki umekuwa mwingine sio tunaoujua kwa misimamo. Huyu papa huyu anaajenda yake mpya.
 
Wakristo wanachekesha sana Yani mnahangaika kupaka paka Rangi Maneno wakati msimamo wa papa wenu ni ubariki ushoga Kwa waumini wote wa kanisa katoliki na hafichi huo msimamo.Juzi tu hapa papa kamfukuza kasisi wa kimarekani vatcan kisa anapinga ushoga,maoni yangu ndugu wakristo msikilizeni kiongozi wenu mkitaka Kuoana madume Kwa madume msisite kwenda kanisani kubarikiwa na jumapili mwende kanisani na mabwana Zenu(waume Zenu)
 
Low mind wameibeba iyo habari kicwa kichwa na kudhani pope karuhusu ndoa ya jinsia moja
 
Papa Francis amewaruhusu mapadre kuwabariki wapenzi wa jinsi moja, yakiwa ni maendeleo makubwa kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja na mahusiano mengine ya kijinsia wanaofahamika kama LGBT katika Kanisa Katoliki la Roma.

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki la Roma amesema makasisi wanapaswa kuruhusiwa kuwabariki wapenzi wa jinsi moja na wanandoa "isiyo ya kawaida", kwa misingi ya hali fulani.

Lakini Vatikani ilisema baraka hazipaswi kuwa sehemu ya taratibu za kawaida za Kanisa au zinazohusiana na miungano ya kiraia au harusi.

Iliongeza kuwa inaendelea kuiona ndoa kuwa kati ya mwanamume na mwanamke.

Papa Francis aliidhinisha waraka uliotolewa na Vatican kutangaza mabadiliko hayo siku ya Jumatatu.

Vaticani ilisema inapaswa kuwa ishara kwamba "Mungu anawakaribisha wote", lakini hati hiyo inasema makuhani lazima waamue kwa msingi wa kesi baada ya kesi.

Akitambulisha andiko hilo, Kardinali Víctor Manuel Fernández, ambaye ni msimamizi wa Kanisa, alisema kwamba tamko jipya limebakia kuwa "imara kwenye fundisho la kimapokeo la Kanisa kuhusu ndoa".

Lakini aliongeza kuwa kwa kuzingatia "maono ya kichungaji" ya Papa" ya "kupanua" ombi la Kanisa Katoliki, miongozo mipya inawaruhusu mapadre kubariki uhusiano ambao bado unachukuliwa kuwa wa dhambi.

Watu wanaopokea baraka "haifai kuhitajika kuwa na ukamilifu wa kimaadili wa awali", kulingana na tamko hilo.

Katika Kanisa Katoliki, baraka ni maombi au ombi, ambalo kwa kawaida hutolewa na mhudumu, akimwomba Mungu ambariki mtu au watu wanaobarikiwa.

Kardinali Fernández alisisitiza kwamba msimamo huo mpya hauhalalishi hadhi ya wapenzi wa jinsia moja mbele ya Kanisa Katoliki.

NB: Hii ni taarifa ya BBC: Lakini kumbukeni BBC wanatetea dhehebu la Anglican ambalo suala la ushoga ama ndoa za jinsia moja ni kawaida kwa Waingereza. Papa alichosema ni kwamba watu wenye ndoa za jinsia moja ni wenye dhambi kama wengine, isipokuwa wakija kanisani kwa kutubu basi wabarikiwe kama binadamu wengine wenye dhambi wabarikiwe ili wajirudi.
Nilikuwa nataka kuandika uzi kama huu ila nikasema ngoja nipitie kwanza nione kama utakuwepo maana najua JF kuna watu wenye akili na wanaojua kusoma na kuelewa kilichoandikwa.

Watu wengi hawajaelewa tamko la papa Francis. Wamekimbilia ku judge tu ila hawajasoma hata tamko lenyewe.

Wamekimbilia tu kuanzisha nyuzi kiholela ila hata ukimwambia aweke hapa quote ya papa aliposema amebariki ndoa za jinsia moja atabaki kukutukana tu na kufokafoka bila hoja.

Asante mkuu kwa kuniwahi kuleta huu uzi.
 
Watu waache upotoshaji Yesu mwenyewe aliwabariki hadi makahaba.
 
1703000148719.png


Nashangaa kuna upotoshwaji mkubwa sana unaendelea kwamba karuhusu ndoa, NO !! suala la ndoa bado litaendelea kuwa kati ya mwanaume na mwanamke

Alichosema ni kwamba karuhusu makasisi kuyabariki kitakatifu mahusiano ya wapenzi wa jinsia moja,

Tujue utofauti wa ndoa na mahusiano
 
Nashangaa kuna upotoshwaji mkubwa sana unaendelea kwamba karuhusu ndoa, NO !! karuhusu kuyabariki kitakatifu mahusiano ya wapenzi wa jinsia moja,

Tujue utofauti wa ndoa na mahusiano
Wanakuja Wapagani, wafia dini na wasiokula kitimoto waliosheheni tabia za umbea & usengenyaji, unafki, uzinzi, wizi, ufisadi, uasherati, uchoyo, uhayawani, LGBTQIA ila wao ndiyo wa kwanza kuwanyoshea vidole wengine.
 
View attachment 2847270

Nashangaa kuna upotoshwaji mkubwa sana unaendelea kwamba karuhusu ndoa, NO !! suala la ndoa bado litaendelea kuwa kati ya mwanaume na mwanamke

Alichosema ni kwamba karuhusu makasisi kuyabariki kitakatifu mahusiano ya wapenzi wa jinsia moja,

Tujue utofauti wa ndoa na mahusiano
Kwa hiyo unaona sawa hata hilo la kubariki?
 
View attachment 2847270

Nashangaa kuna upotoshwaji mkubwa sana unaendelea kwamba karuhusu ndoa, NO !! suala la ndoa bado litaendelea kuwa kati ya mwanaume na mwanamke

Alichosema ni kwamba karuhusu makasisi kuyabariki kitakatifu mahusiano ya wapenzi wa jinsia moja,

Tujue utofauti wa ndoa na mahusiano
Una bariki kitu kisicho halali so what?
 
Nimeacha kwenda kanisani muda sasa, kama peponi nitapimwa kwa imani na matendo yangu. Kufungamana na hizi taasisi zilizopotoka nadhani si sahihi. Nitabaki kuwa mkristo huru
 
Back
Top Bottom