Cheua sumu mkuu,imejaa sana kifuani kifuani kwako
 
Habarini za jioni?

Tuendelee kufata taratibu sahihi zilizowekwa na wizara ya afya.

Kiukweli kifo cha corona ni cha dhihaka kabisa. Kama utakufa na corona (sikuombei) basi jua ni kifo cha ovyo sana.

Maiti yako itatengwa kama mdudu na hutapata heshima zote.

Ndugu zako hawatapata nafasi ya kutoa heshima za mwisho wala kukuona tena.

Inawezekana usiswaliwe udumbukizwe shimoni kama mzoga na kufukiwa.

Siku za nyuma kidogo niliangalia kipande cha video jinsi Itali watu wanavyomwagwa kwenye shimo dah!inasikitisha.

Pia nimeona kipande cha video huko twitter kikionyesha maiti ya mtu aliefariki na corona wakidai ni mwananyamala. aisee ni hatari kwa kweli nimeweka link
Aisee Mungu atujalie mwisho mwema na tuendelee kuchukua hatua sahihi kujilinda na kuwalinda tuwapendao.
 
Si COVID-19 tu, ni karibu magonjwa yote ya kuambukiza.
 
Kifahari umesema wewe..

Ila marehemu akizikwa kwa heshima si kuna yale maombi? Pengine yatasaidia kitu huko kwa sir God
kwani akizikwa vipi ndio unakatazwa kumuombea hayo maombi
 
Exposing a dead body to me siyo heshima, mwili uzikwe au uchomwe, I stand to be corrected
 
kwani akizikwa vp ndio unakatazwa kumuombea hayo maombi
Akizikwa na jiji utamuaga vipi?
Ushawahi ona waislamu wakienda kuzika? Na vipi wakristo ile ibada ya kumuaga marehemu?
Hebu acha kujifanya kama huelewi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…