Kwa vile tumeamua hatuwezi kuweka nchi yetu kwenye "lockdown" kutokana na watu wengi kutegemea kuendesha maisha yao kwa kufanya kazi zinazo walazimisha watoke majumbani, ni vizuri serikali ikaweka sheria ambazo zinaweza kusaidia kupunguza maambukizi ya corona.
Sheria moja ambayo napendekeza na nchi ambazo zimeshambuliwa vikali na janga hili wanaanza kutumia, ni watu wote wakitoka nje ya nyumba zao wavae masks/barakoa. Mtu ambae hatovaa mask/barakoa alipishwe faini.
Masks/barakoa sio lazima hiwe ya kutupa kila siku kwani inaweza kuleta gharama kubwa kwa wananchi; mtu anaweza kushonesha na akafua jioni. Ikiwezekana serikali igawe masks/barakoa za vitambaa bure kwa wananchi hili watu waendelee na miangaiko ya kila siku kama kawaida.
Wale ambao watapata dalili za corona yani homa kali, kukooa, na kushindwa kupumua watabaki majumbani au kwenda hospitali kama watazidiwa zaidi.
Mwenyezi Mungu aendelee kutulinda na janga hili, lakini ni muhimu nasisi tuchukue hatua za kujikinga.