Mufti sheikh Zuberi aitisha maombi ya siku tatu kwa Waislamu wote kuombea mvua

Makadirio yanakuwa based kwenye percentage, unaweza kuniambia hiyo siku TMA iliweka asilimia ngapi ya uwezekano wa mvua kunyesha?
 
IKINYESHA YA MADHARA HATA HATUOMBI IPUNGUE. IKICHELEWA NDO TUNAOMBA Mmmmh.MUNGU TUHURUMIE
 
IKINYESHA YA MADHARA HATA HATUOMBI IPUNGUE. IKICHELEWA NDO TUNAOMBA Mmmmh.MUNGU TUHURUMIE
Ungekuwa umeshawahi kuhudhuria katika maombi ya namna hiyo ungetupa ushuhuda kuwa WAOMBAJI huwa wanajinyenyekeza kimaombi kuwa ikinyesha iwe ya heri, baraka na isiyoleta "nakama".....
 
Hao watu wa jngwani hawana sana na shida ya mvua kama sisi, kwani wao wana uwezo wa kununua chakula sehemu yoyote duniani, wana matunda ya aina zote kwa mwaka mzima wana maji ya kutosha na teknolojia ya kuyasafisha maji ya bahari kuweza kutumiwa kwa mahitaji ya wanadamu na wanyama na mimea. Na hiyo ni kutokana na dua ya nabii Ibrahim aliyomuomba Allah katika Quran 14:37
Mola wetu Mlezi! Hakika mimi nimewaweka baadhi ya dhuriya zangu katika bonde lisilo kuwa na mimea, kwenye Nyumba yako Takatifu, ewe Mola wetu Mlezi, ili washike Sala. Basi zijaalie nyoyo za watu zielekee kwao, na waruzuku matunda, ili wapate kushukuru.
Kutokana na hiyo dua hao watu wa jangwani wanaishi maisha ya raha kuliko sisi tuliyokuwa tunaishi karibu na maziwa ya maji, mito na ardhi zenye rutuba. Hivyo wenzako wakiwa katika imani ya mafundisho yao si vizuri kuwakejeli, kama nawe una mchango wa kuleta mvua utoe si wakati wa kubezana, mwisho wa siku kila mtu atanufaika na imani yake.
 
tuliwaambia humu kuwa imani ni jambo zito na lenye nguvu kulko wafikilivyo, nazani mmeona wenyewe mvua ilvyofunguka baada ya viongoz wa imani kuomba, kwahiyo tunavyowaambia humu matatizo ya kijiografia yanaweza kutatuliwa kwa njia za imani muwe mnaelewa, acheni ubishi wakipumbavu

sisi watu weusi ni watu wa kiroho, haijalishi unaabudu ktk dini/imani gani hiyo aitoshi kukutenga na nguvu zako za kiungu..we are the strongest race in spirituality issues.

aibu kwenu mlinipinga kuhusu hili jambo
 
Unatumia nguvu kubwa sana kwa Jambo lililo dhahiri kabisa....kwani naye hakusema "jisaidieni nami niwasaidie"?!!

Chanjo hazijaanza jana kwa maneno yako pia ni kumkosea Mungu Muumba kuwachanja watoto wetu kule RCH.....
“Jisaidie nami niwasaidie “haitakiwa kujisaidia vitu Nusu nusu
Yaani sawasawa na mtu aliyeenda kwa mganga wa kienyeji kutafuta msaada kapewa hirizi wakata huo huo kasimama kwenye madhabau ya Bwana anaomba msaada na hirizi ikiwa mwilini mwako.
Mungu ajibu Maombi kama hayo. Chagua kimoja kuwa Moto au baridi na siyo kuwa vuguvugu
 
Mbele ya Chifu Mkuu Hangaya ,maombi na dua za mchungaji Anthony Lusekelo ,Mufti Sheikh Zuberi na maaskofu wa TEC zimejibu.....mvua imeanza huko Mwanza......🙏🙏

Yetzer ha-tov
Shavua Tov
 
Mvua tayari imeanza kunyesha, maombi ya nini tena?
Kwa kawaida huwa wanasubiri hadi ianze kidogo kisha ndio wanafanya maombi
Kwanza mnafanyaje maombi wakati huu ni msimu wa mvua na mnajua fika kuwa itanyesha tu hata kama imechelewa kuanza??
 
Kwa kawaida huwa wanasubiri hadi ianze kidogo kisha ndio wanafanya maombi
Kwanza mnafanyaje maombi wakati huu ni msimu wa mvua na mnajua fika kuwa itanyesha tu hata kama imechelewa kuanza??
Hivi nchi hii haijawahi kutokea mvua kutonyesha kwa kipindi kirefu mno kufikia VIONGOZI wa dini na jadi kufanya maombi ili ije mvua?!!!

Nikiwahi kuhadithiwa pale jangwani baada ya maombi tu mvua ilimwagika.......

All and all tunapaswa kumuomba Mungu Mwenyezi kipindi chote Cha raha na shida.....na anayefanya miujiza ni Mungu tu kazi yetu kuomba muda wote......
 
Msisahau kuombea walioko magereza wanateseka sana tena wengine hawana hatia
 
Kama unandugu yupo Kanda ya ziwa ..

Muulize , utashangaaa


Haka Kamama yan
Madokta wenzako pale Bugando mbele ya Chifu Mkuu Hangaya wameshuhudia mvua kunyesha baada ya maombi ya Maaskofu wa TEC ,huyo Mufti Zuberi na baba Mchungaji mtumishi Anthony Lusekelo.....🤣🤣
 
Swali lako la 1 jibu langu ni hapana haijawahi kutokea.

Swali la 2 kuhusiana na jangwani mi sijawahi kusikia wala kushuhudia labda ilikuwa 19kweusi kabla sijazaliwa hivyo hiyo taarifa siitambui.

Hapo mwisho nna swali mkuu, unaposema tunapaswa una maana gani?? Hiyo tunapaswa ni kwa mujibu wa nani?? Au wewe??
 
Kutoona ,kutokusikia haina maana ya kwamba tukio HALIKUTOKEA...ndipo hapo mtu makini anatakiwa aulize kwa WENGINE ili ajiridhishe na si kung'ang'ana tu na kile akijuacho.......


Mwishoni nimesema tunapaswa(kwa kuwa mimi ni binadamu) na mapungufu yangu ya kibinadamu haina maana ninayo peke yangu.....joto linatuathiri sote ama peke yangu tu?!! Ukame na ukosefu wa maji unatuathiri sote ama peke yangu tu?!!

Mwisho wa siku pale nguvu zangu zinapoishia hujiegemeza kwenye matumaini na kwangu matumaini yako kwa MUUMBA MBINGU NA NCHI.....ama nakosea mkuu?
 
Mbele ya Chifu Mkuu Hangaya ,maombi na dua za mchungaji Anthony Lusekelo ,Mufti Sheikh Zuberi na maaskofu wa TEC zimejibu.....mvua imeanza huko Mwanza......🙏🙏

Yetzer ha-tov
Shavua Tov
Haaaa
Kuna watu walianza kuomba mvua kunyesha kabla ya hata ilo Tamko.
Mi nilianza kuomba Mvua kabla ya ilo Tamko na Maombi yangu yakajibiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…