Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Mabeberu adii lini kwenye mambo yetu brazaj, ? ifikie hatua basi ya kufrahia juhudi zetu ata kidogo.

Hata kama mmoja kafariki ila mhimbili wamefanya kitu. Na pia wamejifunza
Mawazo kama yako ni hatari na yenye ubinafsi mkubwa. Unaonaje kama wangejifunzia kwako? Au ni mkuki kwa nguruwe tu? By the way beberu ni nani? Au ni yeyote aliyekutangulia hata kwa ujuzi tu?
 
Muhimu haikuwa kutenganisha, muhimu ilikuwa wataishi baada ya kutenganishwa! Mimi siku ya kwanza kutenganishwa nilisema hilo si fanikio fanikio ni kuona watoto hao wanaishi, nilisema hivyo baada ya madakitari kukimbilia kwenye vyombo vya habari na kujisifu kuwa wamefanikiwa! Madakitari hawakuwa na sababu ya kuharakisha kujisifu, wangeweza kusubiri mpaka wamepona majeraha ya oparesheni, kusingekuwa na tatizo.

Umeandika vyema sana mkuu. Tatizo letu kubwa kama watanzania ni kutojua haki zetu. Kwetu tatizo ni lako wala si kwa mwingine. Ndiyo maana tunachezewa katika yote. Katiba, tozo, rushwa, kutowajibika, maonevu, nk ni mwendelezo wa ule uswahili swahili tu.
 
Kama kawaida yetu, jibu rahisi mwachie mungu. Nakwambia waafrica kuona mbingu tusahau maana tunamsingizia mungu mambo mengi sana.
Hiyo ndiyo mitanzania sasa katika ubora wake. Ndiyo maana hata ya kina Ben, Azory, Sanane, Lijenje nk kaachiwa Mungu.

Ya katiba, uwajibikaji, tozo, rushwa nk yote kaachiwa Mungu.

Ya kwamba katika Tanzania ya Kaisari kaachiwa Kaisari.

Maajabu ya Mussa.
 
Kitaalam bado wangekuwa na uwezekano mkubwa wa kufariki wakiwa watu wazima, kama ilivyotokea kwa wale mapacha wawili wa Iringa; Maria na Consolata.

Hivyo upasuaji ulikuwa haukwepeki.

Kwa hiyo mkuu ni heri kuwa wamefariki wakiwa wadogo kuliko kama wangalikuja kuwa wakubwa? Kwani wewe unadhani ilikuwa heri ufe lini mkuu?

Haki ipi tunastahili sisi kuihoji kwa mitazamo kama hii?
 
Tatizo kubwa la watanzania ni mihemko. Leo wengi watalaumu ila baada ya wiki 2 hakuna atakayefuatilia tena hili swala. Inabidi tubadirike haswa tuwe na muendelezo.
Na ukitaka kujua tatizo ni kubwa lawama za jf ni kidogo ila mitandao mingine ni matusi matupu kwa dr's uelewa wa watanzania bado ni mdogo sana.
 
wana jf punguzeni ujuaji
Ujuaji ni nini mkuu? Kwa mawazo yako tunayo hakuna kuhoji lolote kweli? Au ni mawazo yako kuwa ya kaisari tumwachie kaisari? Au kuwa yote tumwachie Mungu?
 
Kama mzazi inaumaa saana ..naenda washtaki iyo hospital. Na mbwembwe zote zile mapicha picha Nini.. halafu watotowamefariki..! Huu Ni uduwanzi..
 
Some time take it as blessings in disguise.

Baadhi ya changamoto natural ni heri kufa kuliko kuendelea kuishi Kwa taabu
Kwani blessings in disclosure utazijuaje basi mkuu? Hudhani kuwa kutaka uwajibikaji katika mambo yote across the board kutatuvusha?
 
Tatizo kubwa la watanzania ni mihemko. Leo wengi watalaumu ila baada ya wiki 2 hakuna atakayefuatilia tena hili swala. Inabidi tubadirike haswa tuwe na muendelezo.
Na ukitaka kujua tatizo ni kubwa lawama za jf ni kidogo ila mitandao mingine ni matusi matupu kwa dr's uelewa wa watanzania bado ni mdogo sana.

Ninakazia: Tatizo kubwa la watanzania ni "ujinga." Haijulikani haki zetu ni zipi na nini cha kufanya. Ndiyo maana tupo tulipo.
 
Kwamba pacha wa pili naye hatunaye? Inasikitisha. Kwani kulikuwa na haja gani ya operation hii? Kama uwezo wetu ungali hautoshi, kwa nini kujimwambafy bure juu ya maisha ya wengine? Kwanini tusingeomba usaidizi wa beberu kwenye masuala nyeti kama haya ya maisha ya watu? Kwa hakika Muhimbili tunastahili maelezo ya kina kutoka kwenu.
mijitu mingine mnatia hasira, mnaropoka ropoka tu.
sas unatak madaktari wawazuie wasife kwan wao ni miungu???
itoshe kusema madaktari wetu wamejitahidi, wabongo em kueni bc na tabia ya kuappreciate! leo mnawakebehi wataalam wetu alafu badae unapeleka mtambi wako hospitali ukatibiwe, nenda bac huko ulaya na marekan unapopasifia !

IDIOT!,FOOL!
 
mijitu mingine mnatia hasira, mnaropoka ropoka tu.
sas unatak madaktari wawazuie wasife kwan wao ni miungu???
itoshe kusema madaktari wetu wamejitahidi, wabongo em kueni bc na tabia ya kuappreciate! leo mnawakebehi wataalam wetu alafu badae unapeleka mtambi wako hospitali ukatibiwe, nenda bac huko ulaya na marekan unapopasifia !

IDIOT!,FOOL!
Umeandika kama ling"ombe tu. Haki ipi itatelekelezwa katika nchi ya mang'ombe kama wewe? No wonder tupo tulipo.

Nakazia: IDIOT!,FOOL!
 
Fundi gereji anajifunzia gereji huko huko bahati mbaya huu ni ukweli mchungu .
Mungu katujaalia maarifa so ni lazima tuyatumie. Unafikiri Dr mzuri alianza tuu kuwa mzuri? Pitia pitia machapisho jinsi tiba ya kaswende walivyogundua huko ubeberuni ...iliwachukua muda gani na waliharibu/walipoteza watu kiasi gani mpaka kufanikiwa
Waonaje wakajifunzie kwako mkuu? Au ni mwendelezo ule ule wa mkuki kwa nguruwe?
 
Waonaje wakajifunzie kwako mkuu? Au ni mwendelezo ule ule wa mkuki kwa nguruwe?
Kuwa muwazi kwa nafsi yako, hili lianzie kwako fuatilia chanzo cha vifo vya hao mapacha, utakuwa umetenda haki kwako na kwa watanzania wengine. Bila kufanya utafiti hapa hakuna tutakachofanya titaishia kulaumu tu.
Ukifuatilia inaweza kuwa ni mwisho kwa mapacha wa aina hiyo kufariki wakitenganishwa. Ukiishia kulaumu leo niamini hili litaendelea kama kawa.
 
Kuwa muwazi kwa nafsi yako, hili lianzie kwako fuatilia chanzo cha vifo vya hao mapacha, utakuwa umetenda haki kwako na kwa watanzania wengine. Bila kufanya utafiti hapa hakuna tutakachofanya titaishia kulaumu tu.
Ukifuatilia inaweza kuwa ni mwisho kwa mapacha wa aina hiyo kufariki wakitenganishwa. Ukiishia kulaumu leo niamini hili litaendelea kama kawa.

Si sahihi kujifunza kwa gharama ya maisha ya wengine.

Mgonjwa adai fidia TMJ, Hindu Mandal

Mkuki kwa nguruwe haitapata kuwa suluhu katika jamii iliyostaarabika.
 
Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kuwatenganisha. Wangeachwa hivyo hivyo waendelee na maisha yao ingekuwaje. Two in one is allowed. Msitafutie ujuzi kwenye maisha ya watu enyi watu.


YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI
Mfia dini umecomment.
 
Si sahihi kujifunza kwa gharama ya maisha ya wengine.

Mgonjwa adai fidia TMJ, Hindu Mandal

Mkuki kwa nguruwe haitapata kuwa suluhu katika jamii iliyostaarabika.
Imeshatokea kulaumu haisadii nakuhakikishia haikuwa mara ya kwanza kwa dr's kufanya oparesheni hiyo so kujifunzia haipo hapo. Lazima kuna mmoja au wawili katika team walishawahi kufanya hizo oparesheni ndo maan nakwambia fuatilia ujue chanzo cha kifo ni nini? Na sio siri japo haiwezi kuwekwa public.
 
Imeshatokea kulaumu haisadii nakuhakikishia haikuwa mara ya kwanza kwa dr's kufanya oparesheni hiyo so kujifunzia haipo hapo. Lazima kuna mmoja au wawili katika team walishawahi kufanya hizo oparesheni ndo maan nakwambia fuatilia ujue chanzo cha kifo ni nini? Na sio siri japo haiwezi kuwekwa public.
Kulaumu? Kwanini unasema kulaumu? Kulaumu maana yake nini?

Kwanini usiuone kama ushauri wa bure? Kwani lipi jipya? Kuzidiwa ujuzi, uzoefu, uwezo nk mbona ni jambo la afya tu?

Mgonjwa adai fidia TMJ, Hindu Mandal

Mzaha mzaha hutumbua usaha.
 
Kwamba pacha wa pili naye hatunaye? Inasikitisha. Kwani kulikuwa na haja gani ya operation hii? Kama uwezo wetu ungali hautoshi, kwa nini kujimwambafy bure juu ya maisha ya wengine? Kwanini tusingeomba usaidizi wa beberu kwenye masuala nyeti kama haya ya maisha ya watu? Kwa hakika Muhimbili tunastahili maelezo ya kina kutoka kwenu.
Mkuu hata haya yanatokea kwingine.
Umesahau yule aliyewekewa moyo wa nfguruwe marekani na wakasema operation imefanikiwa halafu baada ya majuma.kadhaa akafa.
Unless vifo viwe vimetokana na uzembe ambao tunausikia mara kwa mara na kubahatisha
 
Back
Top Bottom