Mwenge wa Uhuru upo kwa faida ya nani?
Aanze na jipu la posho za wabunge. Hizi zinanikera yani mbunge kila siku laki tatu wakati hiyo ni posho ya mwezi ya polisi. Hapo bado mwalimu hana posho ya mwezi.
 
Aanze na jipu la posho za wabunge. Hizi zinanikera yani mbunge kila siku laki tatu wakati hiyo ni posho ya mwezi ya polisi. Hapo bado mwalimu hana posho ya mwezi.

Hilo nalo ni neno, wabunge wa ccm watakazimika kuungana na upinzani wakati huo ukifika maana watakuwa wamekasirika na kuamua kuikomesha serikali kwa kufanya kazi za upinzani
 
Hakuna namna utafutw nami nasema ufutwe unaeneza aman, upendo, ukimwi na umaskini.
 
Hivi Katiba ya Warioba na Katiba pendekezwa si zilitaja Mwenge kama TUNU ya Taifa? Mnataka presidaa akiuke katiba aliyoapa kuilinda?!
 
Mwenge hauewezi kufuitwa nduguzanguni bavicha,mnajichosha bure tu,

litakua ni tusi kwa nyerere,hakuna rais yuko tayari kubeba lawama hizo,
tusubiri 2050 mkikamata madaraka labda
 
Mwenge hauewezi kufuitwa nduguzanguni bavicha,mnajichosha bure tu,

litakua ni tusi kwa nyerere,hakuna rais yuko tayari kubeba lawama hizo,
tusubiri 2050 mkikamata madaraka labda


Ishu sio bavicha/chadema/ukawa ni maslahi ya taifa zaidi.

Kinachosemwa hapa ni kwamba yale mambio ya nchi nzima ndo yasiwepo ila maazimisho sio mbaya yakawepo.

Pesa mingi sana inapotea kwene haya maazimisho na watu wanasumbuliwa sana kwa michango.
 
JPM .... unaenda kushindwa.Body language ya Balozi Sefue akitoa maelekezo yako pale Muhimbili inaonesha ......ni ile ile.Tafakari na uchukuwe hatua au utanyanyuwa mikono kabla ya Xmas ya 2016.
 
hilo litochi
linaleta watoto wa mitaani
ukimwi
linafuja pesa za kutosha
ni ubadhirifu wa hali ya juu lingewekwa kwenye makumbusho ya taifa period
:hand:
 
ila mwenge ni moja ya national symbols huwezi kuufuta kirahisi kama watu wanavyodhani ina hadhi sawa na katiba offcource zote ni national system swala la kuufuta ni gumu sana labla atafute namna nyingine ya kuukimbia huo mwenge with low cost
 
Mwenge hauewezi kufuitwa nduguzanguni bavicha,mnajichosha bure tu,

litakua ni tusi kwa nyerere,hakuna rais yuko tayari kubeba lawama hizo,
tusubiri 2050 mkikamata madaraka labda

huu si muda wa mapokeo tena ya mababu zetu jpm futilia mbali hilo dude halina maana hapa nchini.
 
Kuna mambo ambayo yanatumia kiasi kikubwa cha fedha na yakianza huwa sio ya siku moja,
Kama mwenge wa uhuru kwa sasa hauna faida ila unakuwa na bajeti kubwa inayogharibu kiasi kikubwa cha fedha ambapo hupelekea kuwachangisha fedha mpaka watumishi wa umma.
Kwa nini usifutwe badala yake zionekane sikuku na safari ndizo zinazomaliza fedha?
 
Hapa zimefutwa sherehe za uhuru kwa kuwa ndio ziko jirani kabisa, subiri muda wa mbio za mwenge ukikaribia, ndio tutajua kama atazifuta au laa! Kuulizia mbio za mwenge November wakati huwa zinaanza May sidhani kama utapata jibu, subiri April april huko ndio utajua
 
Ukubwa wa bajeti ya Mwenge wa Uhuru ipo kwenye componet gani?
 
Mwenge wa Uhuru karibu mwamashimba, uwachome walanguzi wote, uwachome mafisadi wote, uwamulikie wazalendo wote
 
Leo kwa mara nyingine mbio za mwenge zimeanza tena Tanzania, na safari hii mwenge umewashwa huko Dole Zanzibar kuendeleza ile adhma ya taifa letu changa kuwa "sisi tumekwisha kuwasha mwenge na kuuweka Kilimanjaro". Mwenge huu ulipowashwa mara ya kwanza na kuwekwa kwenye kilele cha Kilimanjaro na Nyirenda, ulikuwa uwe ishara ya matumaini, upendo, na umoja wa Taifa letu.

Matukio ya hivi karibuni hasa baada ya muasisi wa mwenge huo kufa, kuna kila dalili kuwa tunachokimbiza sasa hivi ni kivuli tu cha mwenge ule kwani miale ile ya mwanzo ya mwenge wetu wa uhuru imeanza kuzimika na inaonekana ikififia kila mwaka mpya ujapo. Mwenge huu sasa umekuwa ni alama ya watu wachache kujiangazia wao na familia zao huku sisi wengine tukiendelea kubakia gizani. Hakuna kitu kinachoonesha kufifia kwa mwenge huo kama suala la mikataba ya nishati, madini, ununuzi wa rada, ndege ya rais, n.k Zaidi ya yote kwa wanafunzi waliokwama Ukraine, mwenge huu kwao tayari umezimika ( a little strech there, but why not try..??)

Je kuna matumaini ya kurejesha nuru yake tena? Je kuna haja ya kuuwasha tena ili uendelee "kuwamulika" wabadhirifu, wazembe maofisini, wala rushwa magendo n.k ? Au tuamue kuuzima tu, ili kila mtu ajiwashie mshumaa wake yeye mwenye na wale wenye uwezo wawashe vibatari, chemli, na taa za umeme! ?

huu mwenge kweli tunasababu ya kuendelea kuukimbiza?


Hakuna haja ya kuwa na mwenge kwakua umekua ukiwashwa na wala haukusaidia kufika malengo ya kumulika maovu na kuleta matumaini. Mwanga wa Mwenge ni ishara, lakini ishara hii inaligharimu taifa muda na fedha.
 
Mwenge hauewezi kufuitwa nduguzanguni bavicha,mnajichosha bure tu,

litakua ni tusi kwa nyerere,hakuna rais yuko tayari kubeba lawama hizo,
tusubiri 2050 mkikamata madaraka labda

Kwani Nyerere ndio mwenye nchi?
 
Nakupongeza sana rais Magufuli kwa jitihada zako za wazi za kudhibiti matumizi ya hovyo ya fedha za serikali, mfano mzuri kuokoa mabilioni ya shilingi zilizopangwa kufujwa katika maazimisho ya uhuru, naomba sasa ukomeshe mbio za mwenge.
 
Back
Top Bottom