Mwenye historia ya Nabii Mwamposa kabla ya kuanza huduma yake

Mwenye historia ya Nabii Mwamposa kabla ya kuanza huduma yake

Wee mtu gani kila unaemuombea anapona hakuna mtu mwenye uwezo kama huo katika dunia tokea ilivyoumbwa mpaka leo juzi nilienda kwa mwamposa nikaenda kwa wale watumishi wanaomsaidia mwamposa nikawaambia kuwa nina ndugu yako alizaliwa kilema namtaka nimelete kwa nabii mwamposa ili apone apate kutembea wakasema sawa mlete acha na simu tutakupigia wee mavi ya pimbi kila nikiwatafuta kesho kesho mara sijui huku mara sijui vile mpaka leo kimya kiwapigia wananiznungusha nikaamini hapa kuna magumashi sana ni kiini macho tu
Simkubali mwamposa ila pia sikubali uzushi kwahiyo uache uongo
 
Kama ni Mkristo na unasoma Biblia vipawa vipo na vimetajwa. Mimi kutokuwa navyo hakusababishi visiwepo. Au mimi kutoamini hakusababishi visiwepo. Biblia haijabadilika hata kidogo. Kosoa utendaji wake but si Vipawa. Kama kuna sehemu anakosea kibiblia ainisha hapa.
Kipawa? Ule ni uganga tu kama uganga mwingine. Kwa wakristo Kipawa kipo ndani ya mtu sio mafuta/keki Wala kutoa fedha Ili uombewe/appointment na Mtume!!
 
Acha kukariri..unaikumbuka story ya naamani yule jemedari?
Unaikumbuka habari ya nyoka wa shaba?
Unakumbuka yule kipofu aliyepakwa tope?
Unafahamu wafalme walikua wakipakwa mafuta kwaajili ya upako wa kuwa wafalme?


Kama unaamini hizo story kwanini usiamini la mafuta na maji ya upako?

Ndugu tofautisha doctrine imani na revelation mafunuo. Doctrine ya mkristo ni kuliamini jina la Yesu Kristo na kuliitia pale inapobidi kwa kukesha na kuomba.

Revelation ni mafunuo ya muda mfupi. Kwa mfano Yesu alipompaka matooe yule kipofu ilikuwa revelation ya muda mfupi sio imani au doctrine. Imani Ni muda wote wa ukristo ila mafunuo ni kwaajili ya muda huo pekee. Ndio maana humuoni Yesu akimpaka matope kipofu mwingine maana ilikuwa kwa wakati na kwa kusudi maalum.

Sasa manabii wa Leo wanatumia mafunuo na kuyanya imani. Yani watu waache kuliitia jina la Yesu Kristo na kuhangaika na mafuta na maji, ukiuliza wanakwambia mbona Yesu alifanya hivi. Njia moja ya kumjua Nabii wa uongo ni pale anapotumia mafunuo kama msingi wa imani.
 
regardless mkuu as long as watu wanafungulia maswahibu yao na wanatoa ushuhuda baada ya kujibiwa shida zao sioni shida kabisa... hata huko katholic kuna maji ya baraka nayo yapo tu brother so i believe that Man ever

Believe in God not Mwamposa.
 
regardless mkuu as long as watu wanafungulia maswahibu yao na wanatoa ushuhuda baada ya kujibiwa shida zao sioni shida kabisa... hata huko katholic kuna maji ya baraka nayo yapo tu brother so i believe that Man ever

Shida sio kufunguliwa , je unafunguliwa na Nani? Nguvu gani inakufungua?
 
naomba unithibitishie ni mganga yupi wa Kienyeji ambaye amemponya mtu akajitokeza hadharani na kusema ameponywa na mganga Fulani? au unaongelea hawa wanasiasa wanaotoa kafara ya ufumbaji wa macho wapiga kura? au?

Kwa kifupi hakuna Mganga wa Kienyeji yeyote ambaye anaweza kuponya Ugonjwa .. Yeye atatibu ila hawezi kumponya.. Mwenye uwezo wa Uponyaji ni Mmoja tu naye niyule aliyempa uhai huyo mganga na huyo Mgonjwa tu ambaye Ni Mungu.

Mbona unajicontradict. Kwa hivyo kwa Mwamposa hakuna uponyaji ni uganga. Maana anatumia maji na mafuata Wala sio mamlaka ya Jina la Yesu Kristo. Jina la Yesu Kristo lina nguvu haliitaji maji Wala mafuta.
 
Sasa kama hawaponi kazi ya mafuta uliyoyataja ni ipi? Na huo uchawi unatumika kwenye nini?
Hayo mafuta ukipaka kiganjani ukaoneshea watu ukasema kwa jina la Inamankusweke anguka,watu wataanguka,uchawi wa mazingaombwe,nasikia wanatapika nyembe na shanga huko,kakobe alikuwa aliwaambia wafuasi wapate mafua na wanapata
 
Maelezo Yako yanafikirisha na yanaweza kuwa kweli.Ila ningetamani nabii asimwage baraka kama njugu Bali awatafutie watu njia ya kuingia ufalme wa Mungu ambalo ndio tatizo kubwa kwa wengi

Kwa jinsi watu wanavyofurika kwenye mikutano ya injili, akawa anapiga injili ya wokovu na kuwaambia watu waache dhambi, watubu na kuongoza sala ya toba. Mungu angeiponya Tanzania na mambo mengi
 
Mimi Kila siku nasikia wale ambao wanataka kumrudia Mungu anawaombea na akimaliza anawambia nendeni kwenye dhehebu lolote lilokaribu yako na muone mchungaji ili uendelee kuishi kiriho sasa Mkuu yeye anazunguka nchi nzima atawabatiza wangapi?

Hiyo anafanya Kama regesha. Sham ili usishtuke.
 
Ile ni ajali na uzembe wa watendaji lakini huwezi ukasema kuwa hilo limetokea kisa ni mtumishi ndiyo kaua au mafuta ndiyo yameua

Hiyo ni dalili mbaya kwanini asioneshwe Kama nabii? Kwamaba kesho Kuna ajali itatokea? Mna macho lakini hamuoni.
 
Ndugu tofautisha doctrine imani na revelation mafunuo. Doctrine ya mkristo ni kuliamini jina la Yesu Kristo na kuliitia pale inapobidi kwa kukesha na kuomba.

Revelation ni mafunuo ya muda mfupi. Kwa mfano Yesu alipompaka matooe yule kipofu ilikuwa revelation ya muda mfupi sio imani au doctrine. Imani Ni muda wote wa ukristo ila mafunuo ni kwaajili ya muda huo pekee. Ndio maana humuoni Yesu akimpaka matope kipofu mwingine maana ilikuwa kwa wakati na kwa kusudi maalum.

Sasa manabii wa Leo wanatumia mafunuo na kuyanya imani. Yani watu waache kuliitia jina la Yesu Kristo na kuhangaika na mafuta na maji, ukiuliza wanakwambia mbona Yesu alifanya hivi. Njia moja ya kumjua Nabii wa uongo ni pale anapotumia mafunuo kama msingi wa imani.
Kutumia mafuta mfululizo pia ni doctorine na msingi wa imani

Kasome

Yakobo 5:14​

Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
 
Back
Top Bottom