Naomba ushauri: Mwanamke wangu ameniomba nimsomeshe kwao wamekwama kipesa

Naomba ushauri: Mwanamke wangu ameniomba nimsomeshe kwao wamekwama kipesa

Uone ajabu sana, pamoja na haya maneno kuntu ya wabobezi wa mapenzi humu jf, bado mwamba atakaidi mawazo yao, atampeleka udom/udsm, atalipa ada, atatoa upkeep.

..baada ya miaka mitatu, kilio na kusaga meno.
 
Mchumba hasomeshwi utakuja kujiua wewe kwa aibu akishakupiga chini. Mke mwenyewe kusomesha ni hatari ndio maana anaenda na mimba.
Ondoa hizo emotional reasoning tumia kichwa
 
Habari mkuu...wanaowasomesha halaf wanakumbana na mambo ya ajabu huwa wanaanziwa hivihivi...
Yaani sio kuwa manzi anakua waruwaru tokea mwanzo, hapana, huwa inatokea baada...
Panya huwa anategwa kwa vitu vitamu anavyopenda...
Anyway, unaweza msomesha kama unahela ya ziada ila its a gamble, na sio jukumu lako
 
Mwaibile,soma comment zote kwa umakini .Kuna la kujifunza.Kama utafanya maamuzi kwa kutumia kichwa cha chini huna wa kumlaumu ,na usilete mada humu ya kulialia baada ya kusalitiwa
 
Mkuu ushawahi kata gogo huku unalia?
Unaoga huku unalia?

Unaangalia timu yako pendwa bar iwe simba au yanga huku unalia?

Sasa jaribu
Uone
Hawa paka wa bangladesh atakavomaliza anakugeukaje[emoji16]
 
Yan nipo njia panda mkuu huyu binti saiv ndo anataka kuanza chuo yan first year nimekuwa nae kwenye mahusiano tangia yupo anasoma advance ila mimi nimempita sana kiumri na kimaisha naifahamu familia yao haiko sawa kiuchumi sasa juzi alikuja kunitembelea mjengoni kwenye maongezi ndo akaniomba hivyo ninacho mpendea ni msikivu sana kwangu na mtiifu sana na siyo mtu wa kuomba hela kabisa hili ndo lililo nivutia tangia mwanzo ndo nikawa nae hadi leo sasa limekuja hili la kuomba nimsomeshe ndo nipo njia panda hapa
Jichanganye miaka 3 sio mingi lazima urudi humu unalialia kwa kusalitiwa...hata angekua mke nae hasomeshwi
 
Ukitulea swali kama hili outomatic tutakushauri kuwa mchumba hasomeshwi ...... ngoja nikushauri ivii ..... kama hutojali mtafte mwanasheria andikisha neni ... mta andikishana nini mtajua nyie ila lazma uthibitisho flani uwepo kama mlikubaliana kwa mandishi kisheria ....utanishukuru badaye
halafu akiachika na kukimbiwa atamfanya nini?
 
Back
Top Bottom