Naombeni wazo la Biashara kwa mtaji wa kati ya Milioni 2-3 kwa Dar es Salaam

Naombeni wazo la Biashara kwa mtaji wa kati ya Milioni 2-3 kwa Dar es Salaam

Daaah sijui nisemeje ila nipo tayari kukupa sapport kwa kazi zote ulizo orodhesha hapo maana nishawahi kufanya.

Hivo ukianza tu kama utahitaji kijana ambaye mwaminifu na anajitambua nipo hapa na nitafanya kwa ubunifu wa hali ya juu aisee.

Sapport pia kwenye capital ipo ila tu kama location ikawa nzuri nipo tayari kabisa
Shukran mkuu 😁😁
 
Mawazo yako ni kama yangu. Hizi biashara zinafanywa na watu wengi sana na ni wengi wanakwama kwa sababu location nzuri karibu zote zina watu. Angejaribu kufikiria kitu kingine ambacho watu wengi hawafanyi. Kama ana utaalamu mzuri kwenye kuchagua viatu na mavazi (hasa ya kike) anaweza kujaribu kuweka goli sehemu.
Shukran mkuu
 
Banda la chips pasua kichwa, inventories nyingi tena makorokoro madogo madogo. Usimamizi mkali na mauzo yanaweza onekana ila faida ikakosa au ukawa unajipunja kipimo. Kwanza mwanamke na biashara ya chips utatumia nguvu nyingi kwa huo mtaji.

Hiyo ya transactions huwa naona ni ya kukuzia awareness tu kama una biashara nyingine hapohapo. As long as hulipi kodi kuanzisha hiyo biashara, otherwise gharama za uendeshaji ni kubwa huku faida ni kidogo na chances za hasara ni kubwa hasa kwa unayeanza. Ukiitaka hiyo uwe na uwakala wa mabenki pia.

Hiyo ya maziwa angalau. Ila zote tatu zinategemea location zaidi. Location ni muhimu kuliko maelezo
Ahsante sana
 
Uza uchumi
Auze uchumi gani tena?
20240427_151033.jpg
 
Hiyo ya M pesa mchawi location tu na kwa wadada naona inawafaa sana haina mishkeli mingi.

Japo wadau wameipiga vita sana ila kwa mimi ningeichagua hiyo.

Chipsi zina mambo mengi na ni lazima utafute mtu wa kukusaidia, uendeshaji wake ni gharama lakini pia inahitaji sana umchunge mfanyakazi wako, tofauti na mpesa ambayo unaifanya mwenyewe.
 
Back
Top Bottom