HIMARS
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 70,791
- 98,334
Tumia akiliDsm Dodoma naweza kulipa hiyo 59,000 iwapo itatumia saa 1 sawa na ndege vinginevyo hata 35,000 sitoi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tumia akiliDsm Dodoma naweza kulipa hiyo 59,000 iwapo itatumia saa 1 sawa na ndege vinginevyo hata 35,000 sitoi
Kwani mwananchi wa hali ya chini anasafiri kutafuta nini?Hizo bei ziko juu sana kwa Mwananchi wa hali ya chini.
Lengo lao ni kuihujumu tu hiyo treni bila shaka. Maana nauli ikiwa chini, mabasi yao yatakosa abiria.View attachment 2440365
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.
Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.
Sababu Dar Moro kwa basi ni masaa 4-5Nini wewe Dar to Moro 24,000 kwa lipi sasa.
Huna akiliIkizidi sanaa iwe 15,000/=na isitumie zaidi ya sa moja na nusu Dar_Moro
Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
Watanzania ni watu wa kulalamikaKama ni saa
Yaan ushakalili kwamba Bei ya tren ni ndogo kuliko basi..haiko hivyo inadepend na huduma unayopewa.leo hii Azam marine wanachaji 25000 had 30000 Kwa usafir Zanzibar.. Kwa mwendo wa saa moja na nusu. NeNda mwanza hadi ukerewe masaa matatu hadi manne, nauli haizid 8000/ Kwa Meli.
Wadanganyika ndiyo zetu kudanganywaKwahiyo huo sio usafiri wa Wamachinga waliokuwa wakipiga Vigelegele Nderemo Vifijo na Hoihoi kwenye hotuba za Mwendazake.
Ila si lazima kupanda.Mhuu mradi utakufa kabla ya kuanza. Hapo Abood lazima achekelee sana. Mtu alipe 2.5x ya nauli basi kwa kisa gani? Upuuzi mtupu
Mwendo kasi imekufa lini? Unajua inaingiza kiasi gani kwa siku?Hakuna sehem usafiri wa treni ni nafuu. Kifo cha mwendokasi ni matokeo ya nauli ndogo hivyo kushindwa kuleta magari mengi na huduma kuwa mbovu.
Hata wanaofanya biashara za daladala nauli ni ndogo ndio maana uwekezaji hafifu.
Tuanze kuishi kwenye uhalisia.
Tuondokane na dhana ya umasikini ni ufahariKwahiyo huo sio usafiri wa Wamachinga waliokuwa wakipiga Vigelegele Nderemo Vifijo na Hoihoi kwenye hotuba za Mwendazake.
Hi iD zamani ilikuwa yaitwaje?Inatumia umeme wa wapi?
Ujue ATC inajaza pamoja na bei zao kuwa kubwa?Kwamba sababu ya mwendo gharama imeongezeka au uhalali unauelezea vipi ? Operation Cost ya hii kitu ni kiasi gani ?
Na wakiingia watu watano ukapeleka dude tupu si ni hasara kuliko kuongeza behewa nyingine hata tisa na kupeleka watu lukuki...
Ofcourse wanaweza kuongeza behewa la presidential na wakachaji hata milioni kumi kama kuna wateja kama wewe mtapatikana
Nitumie akili kusafiria? AuTumia akili
Na hilo mkalitazameniHoja hii ikimfikia huyo mnayemwita "mama yenu", atawajibu kwa kusema:
"Watanzania mlizoea vya bure".
Sio lazima ndiyo. Na watakuwa wengi watakaoona hakuna ulazima.Ila si lazima kupanda.
Ile ni bora liende. Zile huduma zimefikia standard? Matarajio ni kuwa na mradi wa kusukumana? Hali ya mabasi ikoje?Mwendo kasi imekufa lini? Unajua inaingiza kiasi gani kwa siku?
Aisee duh... , hii ni hatari bin balaa kwahio unadhani huo mkopo hata wasipopata hata sumni wewe, mimi na wananchi wote hatutalipa ?Usiangalie running costs tu. What about investment cost? Analipa nani huo mkopo?
Hilo behewa ni kiasi gani? Reli imejengwa kw gharama gani.
Duh aisee hii ni hatari sana..., hivi unajua kuna kipindi ulikuwa unaweza kutoka Birmingham UK mpaka London kwa Pound moja ? (Hio ni system kama aliyokuwa anafanya Fast Jet / Budget Airlines) kuliko kwenda bodi tupu ni bora ukachukua watu kwa bei ndogo (ingawa mule ndani pia kuna watu wanatoa pesa zaidi)...Tafuta mji wowote mfano London kwenda Manchester kwa basi na treni, then tuongee. Taarifa zipo kwenye mtandao