Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

View attachment 2440365
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.
Yaani mtu alipe 60k kwenda Dodoma?!
 
Mkuu nenda na kwenye mabasi check zile free riders zilikuwaje. P
Aisee duh... , hii ni hatari bin balaa kwahio unadhani huo mkopo hata wasipopata hata sumni wewe, mimi na wananchi wote hatutalipa ?

Unajua kitu economy of scale ? ukisema uweke laki laki, watu wakapanda wanne kwa wiki huo mkopo ndio utalipa ? au useme elfu 30 na train kujaa kila wakati ipi ina afadhali ?

Pili Unajua kwanini Train nyingi hata UK zimeshindwa kubinafsishwa kwa faida ? Sababu hii ni huduma kuna sehemu sio profitable kwenda ila kuna watu wanaishi na inabidi wafikiwe hivyo inapelekea hata serikali kutoa ruzuku (kwa private companies ili wanende huko) au kuamua ku-renationalize baada ya privatization (impact ya usafiri kama vile ilivyo umeme na maji ni kubwa) hivyo profit kwa jamii sio monetary pekee

Duh aisee hii ni hatari sana..., hivi unajua kuna kipindi ulikuwa unaweza kutoka Birmingham UK mpaka London kwa Pound moja ? (Hio ni system kama aliyokuwa anafanya Fast Jet / Budget Airlines) kuliko kwenda bodi tupu ni bora ukachukua watu kwa bei ndogo (ingawa mule ndani pia kuna watu wanatoa pesa zaidi)...

Pia ndio maana nikasema hivi unajua Tube System inayobeba commuters kila siku kwenda makazini n.k. isingeweza kufanywa na mabasi (virtually impossible) na huko tunakokwenda sio ajabu mji kama Dar mtu anakaa Morogoro anafanya kazi Dar kwahio huu usafiri kwake ukawa hata mara mbili kwa siku kwenda na kurudi...
Pamoja na kuwa ni huduma baadhi ya maeneo lakini nauli ni kubwa kuliko mabasi na serikali inatoa ruzuku. Mkuu kwenye hii bei, na uwekezaji haviendani. Serikali itatoa ruzuku. Lakini vyovyote vile treni lazima iwe ghali kulipia hizi trillioni. Vinginevyo, tutazalisha kila siku ili tulipie deni la SGR
 
Mkuu nenda na kwenye mabasi check zile free riders zilikuwaje. P

Pamoja na kuwa ni huduma baadhi ya maeneo lakini nauli ni kubwa kuliko mabasi na serikali inatoa ruzuku. Mkuu kwenye hii bei, na uwekezaji haviendani. Serikali itatoa ruzuku. Lakini vyovyote vile treni lazima iwe ghali kulipia hizi trillioni. Vinginevyo, tutazalisha kila siku ili tulipie deni la SGR
Let's get back to basics..., Initial investment ya mkopo utalipa tu, hata iweje..., kwahio hapo cost inayobaki ni operation cost ambayo ni on-going... (kumbuka price isipokuwa rafiki na watu wana alternative utakuwa unasafiri bodi tupu)

Kwa sehemu ya abiria wachache nenda na basi kwenye abiria wengi train ni chaeper sababu inachukua wengi kwa wakati mmoja hence kupunguza unit cost, pia kwa mizigo ndio cheaper zaidi hasa ukiongeza na gharama za uharibifu wa barabara...

Tatu kwenye miji mikuu ambapo kuna traffic congestion train inakuwa rahisi kwa mtu kuwahi kufika (kuzalisha mali) kwahio ni faida kwa nchi huyu mtu kuweza kumtoa point A mpaka point B..., na sio ajabu mtu akafanya kazi Dar akakaa Morogoro kwahio huyu mtu huenda hii isiwe one-off safari kwenda kumuangalia bibi bali ni everyday cost...; Kwahio kama wanaweza wakapatikana watu wa kujaza mabasi 6 kwanini kusiwe na train moja kwa bei bei ya chini ya basi ili wote hao waweze kuwahi makazini ?
 
Ilitakiwa mwanza to dar iwe 50k tu isizidi hapo, nasio huo upumbavu walio andika hapo wa dar to bahi
 
Hii nchi ya ajabu sana. Wenzao hizo tren wanaweka bei chini ili mtu aishi moro lakini anafanya kazi kila siku anaenda na kurudi. Sasa wenyewe nauli kubwa utafikiri sio kitu cha Umma.

Ona usafiri wa ndege ilibidi waiue fast jet ili wakabe wateja. Lakini wateja bado wakashindwa bei wayolikuwa wanapandia fast jet ilikuwa nafuu mara mbili kuliko ya Umma.

Miccm ina tamaa kukimbilia kushibisha matumbo yao. Hapo tayari kuna miccm imeshapanga safu ya watumishi kulifisadi huo mradi. Hapo hata tiket fek za baadhi yao tayari ziko kuchapwa
 
Baada ya kukamilika kwa reli ya kisasa ya umeme ya SGR, Leo yametolewa mapendekezo ya Nauli ili wadau waweze kuchangia maoni yao juu ya nauli hizo. Mkutano wa Kupokea Maoni ya Wadau kuhusu Nauli za Abiria kwa Treni za Reli ya Kisasa SGR utafanyika tarehe 19 Disemba, 2022 ukumbi wa Anatorglo - Dar es Salaam.

Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu imekamilisha tayari kwa kuanza safari tukutane mji kasoro bahaari.

1670576337506.png
 
Hapa au hii ni kutaka kuwaonyesha wananchi kwamba kuendesha huu mradi ni garama kubwa au wananchi kutumia treni ni anasa.

Yaani kwenda Dodoma -60,000/-!.

Treni kwa waliostaarabika huko ni usafiri wa garama nafuu sana sisi unaenda kuonekana ni anasa.
Kama Moro Ni elfu24 basi Dodoma angalau iwe elfu50
 
Running cost ya hii kitu ni kiasi gani ?

Navyojua mimi economy of scale kama inajaza watu wengi kuliko mabasi, na inatajaa sio kutembea tupu basi bei inaweza kushuka maradufu kuliko basi na bado pesa ya uendeshaji na chenji ikapatikana...

Wasisahau hii ni huduma na sio mradi wa kujitajilisha..., ni yuleyule mlipa tozo ndio anakamuliwa na huku
It's a matter of time kabla hujanielewa na suala la umeme wa Bwawa la Nyerere pale nilipokuambia tena na tena kwamba mnaosubiri umeme wa bei rahisi, MNAJIDANGANYA...

Na ile siku, kabla sijaamua kukuacha uendelee na fantasies zako, ulikuwa unatumia hoja hizo hizo "umeme ni huduma"... economies of scale!
 
View attachment 2440365
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.
Sasa ni zamu ya walamba asali na ambao hawafi
 
Hakuna sehem usafiri wa treni ni nafuu. Kifo cha mwendokasi ni matokeo ya nauli ndogo hivyo kushindwa kuleta magari mengi na huduma kuwa mbovu.
Hata wanaofanya biashara za daladala nauli ni ndogo ndio maana uwekezaji hafifu.
Tuanze kuishi kwenye uhalisia.
Kwa siku unajua wanaingiza sh ngapi?
 
Back
Top Bottom