Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Ndoto tunazoota na tafsiri zake

wataalam wa ndoto humu ndani hawapo.Maana hakuna hata mmoja kaongea kwenye ndoto niliyopost
 
Mi naota sana niko darasani wkt mi nishamaliza chuo/shule miaka kadhaa iliyopita,ndoto hii inamaanisha nini mkuu Christine Ibrahim?
 
Ndoto yenyewe iko hivi..
"Nilikuwa nimekaa pembeni ya barabara, mara nikaona kundi la watu wengi japo si sana wakikimbia katika mstari, nikajiridhisha kwamba wako kwenye marathon yaani mashindano ya mbio nami nikaamua kujiunga nao kukimbia.
Watu hao walikuwa wengi wao ni watu ninao wafahamu, wengi tunashirikiana mambo mbalimbali hapa mtaani kwetu. Mazingira ya bara bara pia nilikuwa nayafahamu ni mazingira ya mkoani kwetu Tanga.

Tulivyokuwa tunakimbia mimi niliachwa nyuma yaani tulitengeneza mstari mrefu lakini mimi nilikuwa mtu wa mwisho japo niliingilia katikati. Katika barabara hiyo ambayo ilikuwa ni ya vumbi tulifika sehemu ambapo kulikuwa kuna daraja refu kiasi na tulivyofika tulikuta lile daraja limevunjika. Lakini pamoja na kuwa daraja lile lilikuwa limevunjika lilikuwa limejengwa upya kwa mfumo hatarishi kidogo, kulikuwa na kamba zimepitishwa pamoja na vipande vya mbao vidogovidogo mpaka mwisho hivyo linaruhusu watu kupita kwa njia moja tu. Chini ya daraja kulikuwa kunamaji mengi yaliyokuwa yakipita na niliyasikia yakivuma.

Wakati tukiwa tunavuka kwenye hilo daraja ilikuwa tayari imefika jioni yaani kulikuwa na giza kiasi, watu wote wakaingia kuvuka na kufanya chain ndefu ambapo mimi nilikuwa wa mwisho. Nilipokuwa nataka kuingia kwenye hicho kidaraja ili nivuke ilitokea ajali, daraja lile la vipande vya mbao lilivunjika na watu wote kuangukia kwenye maji isipokuwa mimi tu kwasababu nilikuwa nyuma na nilikuwa bado sijaingia kwenye kile kidaraja. Niliwasikia watu wakilalamika na wengine wakijitahidi kujiokoa.

Nikaona kumepambazuka yaani mwanga nilikuwa nauona kama asubuhi vile, mimi nilikuwa juu kwenye ukingo wa mto, mto ulikuwa na kina kirefu na maji yalikuwa chini sana japo yalikuwa mengi. Niliwaona baadhi ya watu wamekaa katikati ya ule mto kwenye kisiwa cha mawe na baadhi wameweza kusogea mpaka pembezoni mwa ule mto nikiwa nawatazama. Mimi nilikuwa nawatupia kamba na wakiidaka basi nawavuta wanapanda juu ya ile kamba mpaka juu halafu wanaokoka, nilifanya hivyo kwa watu kadhaa. Baadae nikaona kama watu wameongezeka mahali pale niliwaona viongozi wa kidini na kisiasa, tulipeana mkono wa pole.

Wakati naendelea kuokoa watu ghafla mimi nikaanguka mpaka chini ya ule ukingo japo sikutumbukia majini lakini sasa nilikuwa chini na pembezoni mwa ule mto, niliwaona watu wengi wakiwa kule juu pamoja na wale watu nilio waokoa. Nami nikawa naomba msaada wa kutupiwa kamba ili nitoke kule chini ya mto, cha ajabu ni kwamba wale nilio waokoa walikuwa mstari wa mbele kunicheka na nilipata hasira sana ila sikuwa na jinsi zaidi ya kuwasihi waniokoe lakini hakuna hata mmoja aliye nisaidia.

Baadaye kuna mtu aliweza kunisaidia nadhani ni katika wale walio kuja kutoa pole na na kumbuka wakati napanda ile kamba yenye mafundo kwa nguvu kuna walio nishangilia lakini pia kuna walio nicheka...."
Ndoto yangu iliishia hapo baada ya kuamshwa na alarm ya simu kwamba natakiwa nijiandae kwenda kazini.

Wadau naomba mwenye utaalamu wa ndoto anitafsirie je hii ndoto ina maana gani au ni kiashiria gani katika maisha yangu?

Ahsante.
 
Upo katika vita kubwa ya mafanikio.

GET RICH OR DIE TRYN'..!
 
Huo msafara ni maandamano ya UKUTA, kukatika kwa daraja ni mfano wa maji ya kuwasha na mabomu ya machozi. Viongozi wa dini na siasa walotumbukia mtoni ni viongozi wa ukawa ambao watachakaa kwa maji ya kuwasha, ila una bahati kwakuwa ni mmoja wa watu ambao watatoa msaada kipindi cha mabomu.
USHAURI: Andaa vyombo vya uokozi kwa tukio la September mosi.
 
Huo msafara ni maandamano ya UKUTA, kukatika kwa daraja ni mfano wa maji ya kuwasha na mabomu ya machozi. Viongozi wa dini na siasa walotumbukia mtoni ni viongozi wa ukawa ambao watachakaa kwa maji ya kuwasha, ila una bahati kwakuwa ni mmoja wa watu ambao watatoa msaada kipindi cha mabomu.
USHAURI: Andaa vyombo vya uokozi kwa tukio la September mosi.
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
ifatilie tu mkuu huenda ni mind made! ambayo imesababishwa na mawazo yako
 
Ndoto yenyewe iko hivi..
"Nilikuwa nimekaa pembeni ya barabara, mara nikaona kundi la watu wengi japo si sana wakikimbia katika mstari, nikajiridhisha kwamba wako kwenye marathon yaani mashindano ya mbio nami nikaamua kujiunga nao kukimbia.
Watu hao walikuwa wengi wao ni watu ninao wafahamu, wengi tunashirikiana mambo mbalimbali hapa mtaani kwetu. Mazingira ya bara bara pia nilikuwa nayafahamu ni mazingira ya mkoani kwetu Tanga.

Tulivyokuwa tunakimbia mimi niliachwa nyuma yaani tulitengeneza mstari mrefu lakini mimi nilikuwa mtu wa mwisho japo niliingilia katikati. Katika barabara hiyo ambayo ilikuwa ni ya vumbi tulifika sehemu ambapo kulikuwa kuna daraja refu kiasi na tulivyofika tulikuta lile daraja limevunjika. Lakini pamoja na kuwa daraja lile lilikuwa limevunjika lilikuwa limejengwa upya kwa mfumo hatarishi kidogo, kulikuwa na kamba zimepitishwa pamoja na vipande vya mbao vidogovidogo mpaka mwisho hivyo linaruhusu watu kupita kwa njia moja tu. Chini ya daraja kulikuwa kunamaji mengi yaliyokuwa yakipita na niliyasikia yakivuma.

Wakati tukiwa tunavuka kwenye hilo daraja ilikuwa tayari imefika jioni yaani kulikuwa na giza kiasi, watu wote wakaingia kuvuka na kufanya chain ndefu ambapo mimi nilikuwa wa mwisho. Nilipokuwa nataka kuingia kwenye hicho kidaraja ili nivuke ilitokea ajali, daraja lile la vipande vya mbao lilivunjika na watu wote kuangukia kwenye maji isipokuwa mimi tu kwasababu nilikuwa nyuma na nilikuwa bado sijaingia kwenye kile kidaraja. Niliwasikia watu wakilalamika na wengine wakijitahidi kujiokoa.

Nikaona kumepambazuka yaani mwanga nilikuwa nauona kama asubuhi vile, mimi nilikuwa juu kwenye ukingo wa mto, mto ulikuwa na kina kirefu na maji yalikuwa chini sana japo yalikuwa mengi. Niliwaona baadhi ya watu wamekaa katikati ya ule mto kwenye kisiwa cha mawe na baadhi wameweza kusogea mpaka pembezoni mwa ule mto nikiwa nawatazama. Mimi nilikuwa nawatupia kamba na wakiidaka basi nawavuta wanapanda juu ya ile kamba mpaka juu halafu wanaokoka, nilifanya hivyo kwa watu kadhaa. Baadae nikaona kama watu wameongezeka mahali pale niliwaona viongozi wa kidini na kisiasa, tulipeana mkono wa pole.

Wakati naendelea kuokoa watu ghafla mimi nikaanguka mpaka chini ya ule ukingo japo sikutumbukia majini lakini sasa nilikuwa chini na pembezoni mwa ule mto, niliwaona watu wengi wakiwa kule juu pamoja na wale watu nilio waokoa. Nami nikawa naomba msaada wa kutupiwa kamba ili nitoke kule chini ya mto, cha ajabu ni kwamba wale nilio waokoa walikuwa mstari wa mbele kunicheka na nilipata hasira sana ila sikuwa na jinsi zaidi ya kuwasihi waniokoe lakini hakuna hata mmoja aliye nisaidia.

Baadaye kuna mtu aliweza kunisaidia nadhani ni katika wale walio kuja kutoa pole na na kumbuka wakati napanda ile kamba yenye mafundo kwa nguvu kuna walio nishangilia lakini pia kuna walio nicheka...."
Ndoto yangu iliishia hapo baada ya kuamshwa na alarm ya simu kwamba natakiwa nijiandae kwenda kazini.

Wadau naomba mwenye utaalamu wa ndoto anitafsirie je hii ndoto ina maana gani au ni kiashiria gani katika maisha yangu?

Ahsante.
katika maandamano mwiko kabisa kukaa nyuma lazima utaumia au kukamatwa na polisi kwa sababu utakuwa hujui kinachoendelea tar 1/9 utaniona siku hiyo
 
Pole sana! Maana yake ni hii! Marathon ni maisha ambayo hata wewe yanakuhusu ndio maana baadae na wewe uliingia kwenye msululu, ila inaonekana kuna lifestyle au tabia fulani ambayo inaonekana ni ya kawaida na watu wameizoelea ktk maisha ila inagharimu sana maisha na inaletaga majanga makubwa sana kwa watu! Ingawa na wewe huwa unawasaidia wanaopatwa na majanga yanayotokana na tabia hiyo lakini inaonekana na wewe uko kwenye msululu huo huo itakuja kukucost na waliokutangulia wanaweza wasikusaidie katu! Inawezekana msaada unaweza ukatoka kwa watu wengine mfano viongozi wa Dini nk! Hebu kagua mahusiano yako! Kazini nk! Usiamini sana watu pia kuna magonjwa! Ahsante!
 
Mimi siku kama 8 zimepita nimeota nakimbia tuko wawili na mwingine ni kama wa kike hv ila sikumuelewa,na nyuma yetu kulikua na watu si wengi sana wala wachache sana kama wanatukimbiza na tukawa tunaogopa tunazidi kukimbia,lakini mpaka wakatupata na nikaona tena kama hawana time na sisi tukawa tunakimbia wote,na sikujua tuliishia wapi tena.sijui ni nini kile

Hiyo itakua bangi!
 
Jamani mi nimeota leo saa nane na dk 35 hivi, nasali sana, yaani kwa kiingereza, kama kuna kitu kibaya nakikemea. Baadae tena kikaja kikanikaba na kama kinaingia mwilini, so muda huo huo nikawa macho na nikafungua TV Joshua prayer for distance people, kila nikiomba mwili unasisimka vile. Ndoto gani hii jamani
 
Back
Top Bottom