Ni lini Rais Samia ataanza ziara kusikiliza kero za Wananchi?

Ni lini Rais Samia ataanza ziara kusikiliza kero za Wananchi?

Aangalie wabunge bungeni wanasema nini. Hao ndio wanawakilisha shida za wananchi.
Sijasema rais atembelee kijiji, bali nauliza atajuaje kuwa kama watumishi wake wanafanya kazi kiufasaha, mfano kama si kuingia mitandaoni asingejua kuwa huku mitaani vitendo vya ujambazi vimeudi.
 
Mlishakataa utawala wa majimbo huo ndio ungekuwa mfumo sahihi kwa nchi kubwa kama hii na sio huo wa kutaka Rais azurure vijijini akikagua kama shule zina vyoo au zahanati zina maji.

Tanzania in vijiji na mitaa zaidi ya 16,000 Hata Rais akiamua kila siku kufanya kazi ya kutembelea vijiji angalau 3 hawezi kuvimaliza kwa miaka 10 ya utawala wake.
Tanzania ni kubwa mkuu wangu ukikaa tu officen huwezi kupata yote kwa usahihi...
 
Mamaa mamaa mama huyo mamaa mama huyo mamaa mama.
Ye ni kuteua tu na kutumbuana sijui km kuna kazi zingine za kufanya.
 
Zile ziara za mwendazake zilikuwa za kujijenga kutawala zaidi ya miaka 10.
Na alishafaulu kuteka "wafuata mkumbo wengi pasipo kufikiria!" Genge la wapumbavu waliokaririshwa midundo wasioijua... wamecheza wee mwishowe wanataka kuingia kwenye mzinga wa nyuki na makelele yao....
 
wanyonge si mnyongwe tu
Ni jambo zuri Raisi kutembelea wananchi wake mikoani siku moja moja kukiwa na sababu ya msingi. Wakuu wa mikoa na wilaya ni wasaidizi wa raisi wa moja kwa moja ndio wenye wajibu wa kusikiliza na kutatua kero za kila siku zinazowakabili wananchi. Mhe. Raisi SASHA halazimiki kujihusika moja kwa moja kusikiliza na kutatua kazi zilizo chini ya wasaidizi wake!
 
Hao uliowataja sio wakuwaamini japo wanakuwa ni wateule wako kama raisi!!!! Lakini mjuba alikuwa mpambanaji san aisee ile kuingia front mwenyewe sio mchezo na ndio ilileta heshima kwa watumishi wake... Ni vizuri mama nae akawa anatembea kuangalia watendaji wake wanafanya kama anavyoagiza au ndo somjo na wao
Hapa ndipo mnapothibitisha kuwa ccm haifai, yaani kazi zote afanye rais hii nchi siyo duka la mangi.
 
Kwani huko alikoenda uganda na kenya hakuna mabalozi aje na huku kwetu dabaga tumwone kila siku tunamwona kwenye Tv tu
Swali kama hili akiuliza mtu ambaye ana uwezo wa kujisajili jamii forum, huwa sijibu.
Lakini angeuliza mwanangu junior ningejibu.
 
Kwahiyo Mama hatakiwi kwenda kwa wananchi? Ila ikifika wakati wa Uchaguzi Mkuu ndio aende sio? Washauri wa Mama Oyeeeeeeeee!!!!
Kuna kwenda kwa wananchi na kushinda kwa wananchi, mnachotaka wafuasi wa kichaa ni mama kushinda kwa wananchi, anunue mahindi,mapapai agawe laki tano tano.
Huyo atakuwa kiongozi au kichaa?

Kama kwenda kwa wananchi anaenda na ndiyo maana kaongea na wazee wa Dar es salaam kwa niaba ya wazee. Au unataka wananchi gani?
 
Rais wetu anakwepa, majukumu yake. Basi ingekuwa kutumia watendaji wake hata huko nje asingeenda, angeacha waziri wa mambo ya nje amwakilishe. Kwani majukumu ya Waziri wa mambo ya nje ni nini?
Katiba inatoa haki ya wananchi kusikilizwa na Rais wao. Si migogoro au Kero zote uweza kutatuliwa na wakuu wa wilaya au Wakuu wa mikoa. Mfano kuna mgogoro ulishawahi tokea, halmashauri iliona vyema kubadili eneo litumike kama makazi. Hivyo viwanja viligawiwa kwa wananchi na wananchi walijenga.
Wizara ikaibuka ikasema hapana, eneo libaki kama hifadhi. Mkuu wa mkoa nae akawa upande wa wananchi.
Nakumbuka ilibidi Rais kuingilia kwani hata hao watendaji wa wizara kidogo wapingwe na wananchi walipojitokeza eneo husika.

Pia kuna migogoro baina ya maeneo ya jeshi na raia, mara nyingi uhitajika kauli ya Rais kama Amiri Jeshi Mkuu. Si hayo tu ni mengi kivyovyote Rais hawezi kukwepa majukumu akasingizia ana wawakilishi. Hatukatai kuwa na wawakilishi, na wanasaidia mengi.

Ila ajue kama mama hawezi acha kila jambo dani ya nyumba kutatuliwa na dada wa kazi. Kuna watoto wakorofi hawatomsikiliza dada au kumtii mpaka wasikie sauti ya mama. Huu ni mfano tu.

Wakuu wa mikoa wapo ila kutokana na utendaji na kanuni za kiutumishi kuna maeneo wanakwama.
Mfano kuna mama alikwamishwa malipo ya haki ya kijana wake kulipwa ambaye alifariki akiwa kazini. Katika kufatilia kote shida ilikuwa wizara ya fedha, walimsumbua yule mama miaka 9 bila kupewa haki ya kijana wake huyu mama alikuwa mzee kaachiwa wajukuu. Na aliishi mikoani.

Mkuu wa mkoa akashughulika na hii kesi ila Wizarani
wakawa wanazingua pamoja na kuwepo kwa mawasiliano lukuki.
Mkuu wa mkoa hawezi mwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya fedha.

Kivyovyote kuna mengi ambayo Rais anatakiwa apate muda wa kuwasikiliza wananchi. Asikwepe kijanja. Kama vipi abaki ikulu kukaa tu kwani wawakilishi anao kila mahala. Tujue moja.
Hata marais wote walio pita waliwasikiliza wananchi. Atakuwa Rais wa pekee kukwepa kinamna majukumu yake. Kwanza ukiwasikiliza wananchi, unaelewa nini kinaendelea katika mfumo mzima wa utawala. Wakati mwingine wasaidizi udanganya kwa manufaa yao.
Kwamba unanambia rais anajua hayo yote akiwa barabarani kila siku akinunua mahindi na mapapai?
Dikteta anayetaka kutawala milele ndiyo huwa na hizo tabia ili kupata popularity.
Rais anayejielewa anakutana na wananchi lakini hawezi akawa anashinda barabarani kila siku kufanya propaganda.
 
Japokua hayati alikua anaendesha nchi kibabe, lakini kuna baadi yamambo aliyafanya yalitupendezea hata sisi wananchi wanyonge tunaoshi chini ya dola moja kwa siku,

ziara za sehemu mbalimbali kusikiliza kero za wananchi zilitufariji sana,

kwa heshima na taadhima tunakuomba mama yetu, Amiri jeshi mkuu, President material mweshimiwa Rais samia suluhu uanze ziara za kusikiliza kero za wananchi wako wanyonge na kuzitafutia ufumbuzi


tunakupenda sana

asante sana

mitano tena[emoji113]

Tuwe uchumi wa kati chini halafu tuendelee na tabia za banana republic? No taasisi; no watendaji; no mgawanyo wa madaraka? Rais anahudumia wanyonge wasiopungua milioni 40 moja kwa moja? Huo ni UONGO mkubwa.
 
Ule ulikuwa usanii tu. Wewe unaamini Rais anaweza kumaliza kero kwa kumsikiliza mtu mmoja mmoja kwenye mkutano wa hadhara?
It send a message. Kwamba Tltunawaangalia nyie wote, mkizingua, utatenguliwa.

Ni kitu kizuri alichoanzisha Magufuli. Uwajibikaji.
 
Mleta uzi nakuunga mkono.
Rais wa Tanzania lazima aijue Tanzania, ndani nje. Yeye si Rais wa dar au dom au zenj pekee.

Lazima akashuhudie changamoto za watu wake kwa kuwatembelea na kuongea nao. Huo ndio uongozi. Kuwa Rais wa nchi kubwa kama hii si kazi ya lelemama.

Msidanganye hapa kwamba asubirie dom au dar taarifa za wananchi wake. Hawezi kufika kila sehem lakin lazima awe na utaratibu wa kutembelea huko mawilayani. Lasivyo yale yaleee. Kwamba alikuwa Rais mzuri ila wasaidizi wake wamemuangusha
 
Kwaiyo ye akitaka kuja huku chini aje kuomba kura tu si ndiyo?
Mkuu, ndo wanavyotaka.

Ikikaribia uchaguzi au wakati wa kampeni ndo eti tuanze kumuona mara anaenda Sikonge, mara Liwale mara Songwe. Kwasasa hawataki. Wanataka wawe wanamlisha matango pori. Bosi kila kitu kiko shwari Rombo kumbe hamna lolote

Au wanamuonea huruma kuwa atakuwa anachoka?

Aende akashuhudie watu wake wanavyoishi hukoooo
 
Kuna kwenda kwa wananchi na kushinda kwa wananchi, mnachotaka wafuasi wa kichaa ni mama kushinda kwa wananchi, anunue mahindi,mapapai agawe laki tano tano.
Huyo atakuwa kiongozi au kichaa?

Kama kwenda kwa wananchi anaenda na ndiyo maana kaongea na wazee wa Dar es salaam kwa niaba ya wazee. Au unataka wananchi gani?
Sina uhakika kama una uelewa na ulichochangia.
 
Mfumo wa uongozi uheshimiwe , Kila nafasi ina umuhimu wake, kama Kila Jambo tukimwachia rais atatue , tutalemaza viongozi wengine , watakosa ubunifu na uthubutu wa kufanya maamuzi yaliyo ndani ya uwezo.
Rais kama kocha kazi yake kubwa Ni kupanga timu yake vizuri, kuhakikisha nani anafaa kucheza namba fulani ,nani anazingua abadilishwe. So ukiona kocha anataka kuingia uwanjani anakuwa na tatizo, maana siyo majukumu yake na mwisho timu lazima imshinde,
Kuna majukumu mengi sana makubwa ya kitaifa ambayo rais anapaswa kuyatimiza.Hayo Ni mengine sio lazima kuyafanya
 
Tatizo ni kwamba watz sio waaminifu ndo sababu unaona mjuba alikuwa front!!! Hawa wateule wengi usipo wafatilia ni ujanja ujanja tu huko uraiani mkuu
Hapa ndipo mnapothibitisha kuwa ccm haifai, yaani kazi zote afanye rais hii nchi siyo duka la mangi.
 
Mambo gani makubwa unayodhani zaid ya kuwatumikia wananchi. Kuingia mikataba ya Gesi au? Rais ni Rais wa watu si Rais wakusafiri bila kuona tija ya safari zake. So unataka azurure mitaa ya Karen, Mombasa, Kasarani na si mitaa ya nchi yake! Ha ha ha!
We kenge kweli kuwatumikia wananchi ni kupi? Huko ikulu au kwenye ziara za nje anawatumikia mbwa au

Kazi ya Rais sio kufanya unavyotaka wewe
 
Back
Top Bottom