Ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu?
Ningependa nimjue mwanzisha mada kwanza, kabla ya kukomenti.
 
Ungeweka na 5. Inawezekana washambuliaji wakatoka cdm yenyewe katika mpambano wa kugombea mgombea urais wao 2020.
6. Washambuliaji kutoka huko huko cdm ili kuichonganisha serikali na wananchi?
Hili suala ni gumu sana linachohitaji ni kusubiri uchunguzi wa vyombo vya usalama tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa kabisa, wahenga wamenena ukitaka kumulika nyoka anzia miguuni. Lakini si lazima nyoka awe miguuni, maana yake ni kuwa ukianza kumulika mbali na kwa kutembea utamkanyaka nyoka na atakung'ata.
Kwa hiyo kama maadui wa Lissu wako CDM na ndiyo wanaomtibu akilala kitandani kwa matibabu itakuwa ndiyo kwaheri Baba wa CDM. Atakata kauli moja kwa moja.
 
Kwa haraka haraka watu watasema CCM inahusika, ila ukiangalia katika jicho la upelelezi unawezaona kuwa Lissu alitaka kuuliwa aidha na watu wenye mapenzi na nchi hii, chadema yenyewe ili kumfachua Magufuli, pamoja na baadhi ya maadui zake ambao pia yeye anadhani kuwa ni marafiki zake. Ujasusi ni kitu kinachotumia intelijensi sana ila kwa bahati mbaya watu hawafikirii au kuona mbali, matokeo yake wanakuja na hoja za kijinga kwa kunyoshea vidole wasio na hatia. My guess and knowledge inaniambia kwamba hapa CCM wala haiusiki.
Asante.Ni kama vile umeamua kujipofusha ila usione ukweli.Ata mwanangu wa chekechea anajua nani ni mtuhumiwa.
Ni kama vile Ronaldo apewe penati bila kipa golini alafu akaamua kupaisha.
Wahenga walisema "Common things occurs commonly".
 
Ujinga mtupu,nadharia haitakiwi kuonesha upande wako ila tu uhalisia wa nadharia yenyewe ili kila mtu achague mojawapo kati ya hizo na aweze kiwa muumini wa nadharia hiyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bahati mbaya watanzania hatuna muda wa kufikiri kutokana na chuki na kuichoka serikali yetu.

Jana nimemwambia jamaa yangu siamini kuwa serikali ilitaka kumuua Lissu, yani hadi urafiki umeisha..

Tatizo tuna jazba sana, na hatutulii katika maamuzi.

Siamini kabisa kwamba kama nina visa na Juma, na mtaa mzima wanajua, naweza kumuua, mana ntakuwa first suspect.

Icpokuwa, naamini kuwa kuna watu nlio na chuki nao wanaweza utumia uhusiano wetu mbovu to their advantages....

Ndo mana wahenga walisema mchawi mpe mwanao akulelee... Mana hata akilogwa na mwngne wote tutajua ni yeye tu... Hvyo lazima atamtibu...

<> semper fi <>
 
At the end of the day umeonesha unatetea upande gani na upo chama gani!! Ukweli kunasiku utajulikana tu na kuna watu wataaaibika!!
Kweli kabisa, sababu humo humo kwenye chama chao kuna "Power Struggle", ya chini chini, na wachunguzi walitegemea kitu sio kama hiki ila chepesi zaidi, naamini kabisa wanaohusika na na hili tukio ni wenyewe...
Mke au Mume akifa, uchunguzi waanza kwao, wanandugu na marafiki, simple...
 
Nasema "alietaka kumuua" kwa sababu ukiangalia yale matundu ya risasi upande wake wa gari utajua kuwa hawa watu hawakutaka kumtishia tu. Walidhamiria kumuua.

Niungane na Watanzania wenzangu kumuombea Tundu Lissu dua/sala ili apone kikamilifu, Amin.

Nimejiuliza maswali mengi kuhusu shambulio hili la kipekee kwa mbunge (sijui kama kulikwishatokea shambulio jingine kama hili), hapa Tanzania.

Yafuatayo ni malumbano ya kifikra ndani ya nafsi yangu kuwa ni nani hawa waliotaka Tundu Lissu afe. Maoni yako yanahusika, tafadhal.

Nimefikiria wahusika katika dhana 4. Nitazichambua hizi dhana moja moja.

Dhana zenyewe ni hizi. Washambuliaji ni:

1. Vichaa fulani tu. (Random act)

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.

3. Serikali yenyewe

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.


1. Vichaa fulani tu. (Random act)
Hii inawezekana lakini inakinzana na taarifa za kuwa Lissu alikuwa anafuatiliwa na magari kwa kipindi kirefu. Huu mpango ulisukwa na pia walijua wanaemtaka hadi kumfuata mpaka nyumbani kwake. Sidhani hii ilikuwa ni Random Act. Dhana hii ni potofu.

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.
Hii inawezekana kabisa. Wengi walimshutumu Lissu kwa kupinga sera zote za serikali (mimi nikiwa mmojawao). Kuna watu walikwenda mbali zaidi na kusema wanataka serikali iwaruhusu wamuue. Ndio maana kuna umuhimu wa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu hawa.

Katika demokrasia watu tunashambuliana vikali kwa hoja na sio kwa kuumizana au kuuana. Kama hii itathibitika, basi kuna umuhimu wa kuwapatia ulinzi wanasiasa machachari wanaoibua hisia kali.

Kuna uwezekano mkubwa dhana hii ni sahihi.

3. Serikali yenyewe
Kuna watu mitandaoni wanadhani ni serikali yenyewe ndio imeunda hii mbinu ya kumuua Lissu ili awaondolee kelele. Wengi wanasema Lissu amefichua siri nyingi za serikali kufikia kuwa tishio kwa hii serikali.

Kwa maoni yangu huu ni upuuzi. Serikali hii inakubaliwa na watanzania wengi. Hoja karibuni zote alizotoa Lissu dhidi ya serikali zinaweza kujibiwa kirahisi sana. In fact, baadhi ya shutuma za Lissu zinaipaisha serikali kwa Watanzania. Kelele za Lissu zinaweza kuwa baraka (blessing) kwa CCM ifikapo 2020. Kumuua Lissu kutajenga hisia za uonevu na kuwaonea huruma CDM ifikapo uchaguzi mkuu. Serikali haiwezi kufanya kosa hilo.

Kwa hiyo dhana hii ni potofu

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.
Hii dhana inahusisha watu wanaoichukia serikali (sio lazima wapinzani, inaweza kuwa watu wa nje) wanaotaka kumuondoa Rais Magufuli madarakani ifikapo 2020 kwa kuihusisha serikali yake na mauaji ya Lissu.

Serikali ya Magufuli imeathiri maslahi ya watu wengi sana wa ndani na wa nje. Akiendelea hivi hivi ana uhakika kabisa wa kupita ifikapo 2020. Sasa utaitoaje hii serikali madarakani ifikapo 2020. Jenga chuki kwayo.

Kama nilivyoeleza kwenye dhana namba 3, watu wakiamini kuwa serikali imemuua Lissu kinyama basi watawaonea huruma CDM na kuichukia CCM. CDM watachukua dola ifikapo 2020.

Je ni nani hawa wanaotaka kufanya unyama kama huu na kuisingizia serikali ya CCM (false-flag attack)?

Nina dhana nyingine 2 au 3 hivi (mfano, internal politics within CDM) lakini ni za pembeni sana na uwezekano wake ni karibu na sifuri. Kwa sasa hayo ndio malumbano yanayoendelea kichwani mwangu.

Please tell me I am not crazy.
MLETA MADA! Mimi binafsi najaribu kutafakari ili jambo/tukio na bado sijapata jawabu! Kuna chapisho flani nililisoma humuhumu JF, kama siku nne zimepita, kuhusiana na kambi mbili ndani ya chama ila nilibaki na wasiwasi kuhusu hilo chapisho na mtu aliyezungumziwa kuwa katika kambi inayokujaa juu au kupata umaarufu ndani ya chama ni huyu aliyeshambuliwa kwa risasi! Sasa, baada ya tukio la shambulio la jana, akili yangu imenifanya nikumbuke Kifo cha Marehemu CHACHA WANGWE kilichosababishwa na ajali ya gari, nimekumbuka tukio la Mh. ZITTO KABWE kuvuliwa uanachama, Beni saanane kupotea na mengine mengi hapa nchini. Haya matukio yanatokea baada ya kuonekana kuwepo kwa kambi moja kutaka kulinda maslahi yake dhidi ya kambi nyingine. Tunaliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina ili tupate ukweli wa ili jambo. Haiwezekani watu wetu ambao ndiyo tunaowategemea watusemee sisi wananchi ambao hatuna nafasi ya kusemea waumizwe na kuuwawa kiholela! Wahusika wasakwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.
 
Kwani ambao wamempeleka mahabusu lissu mara saba hawajulikani???

Kwa nini asipelekwe mahabusu kama anahoja ya kujibu? hata mara mia anaweza kupelekwa. Hiyo sio hoja. Kuvaa kofia ya uwakili haina maana vyombo vya dola visimhoji kwa kosa analosemekana ametenda au anatenda. Tuache kuwa na mihemuko isiyo na tija. Tundu Lissu is a great man. hata mimi nampenda. Hicho kilichomtokea si sawa. Watu waliofanya hivyo watajulikana tu. Tuviamini vyombo vyetu. Vitafanyakazi. Vitaibua maovu hayo. Tuwe na subira.
 
Ongezea Bashite...Jana alikuwa wapi na mbona hakupost kitu instagram... Acheni kuzunguka mbuyu...Nissan patrol nyeupe????hakuna MTU binafsi anatumia magari mabovu..chunguza mtaani kwako...Lissu anabounce back tutampa ulinzi magari hata kumi na atafukua siri zote hakuna kuacha kitu
 
Bahati mbaya watanzania hatuna muda wa kufikiri kutokana na chuki na kuichoka serikali yetu.

Jana nimemwambia jamaa yangu siamini kuwa serikali ilitaka kumuua Lissu, yani hadi urafiki umeisha..

Tatizo tuna jazba sana, na hatutulii katika maamuzi.

Siamini kabisa kwamba kama nina visa na Juma, na mtaa mzima wanajua, naweza kumuua, mana ntakuwa first suspect.

Icpokuwa, naamini kuwa kuna watu nlio na chuki nao wanaweza utumia uhusiano wetu mbovu to their advantages....

Ndo mana wahenga walisema mchawi mpe mwanao akulelee... Mana hata akilogwa na mwngne wote tutajua ni yeye tu... Hvyo lazima atamtibu...

<> semper fi <>
Amlight umenichekesha. jana rafiki yangu nusura apewe talaka kwa kusema haamini serikali imemmiminia risasi Tundu.. Mimi mwenyewe siamini kabisa na wala sifichi hisia zangu. Umiminiaji wa risasi wa aina ile ni mtindo wa Zamadani. Serikali kama inania ya kumwondoa Lissu si kwa kumfatilia na gari mchana kweupe na kummiminia risasi! hivi masikio hayasikii na macho hayaoni? Lissu anaweza kuwa na maadui wengi tu kama wakili wa kujitegengemea. Mara ngapi tunasikia watu wanaua kwa vile wamenyimwa haki mahakamani? wameshindwa kesi "on technicalities ground"? sasa anayenyimwa haki akiwa na roho ndogo na stress ya ajabu anaweza kufanya nini? kuna scenario nyingi. Lakini No! No! No! hiyo sio kazi ya Serikali. Tuache kuipaka matope serikali jamani; Tumelogwa?
 
Back
Top Bottom