Ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu?
Mkuu

Tujiulize

Ishu ya lisu kupigwa risasi ilikuwa ya mtu Binafsi au ya system ya vipepeo wa nchi HII!!?

Kama ilikuwa ya system ni vigumu kujileta coz atamwamini Nani!!?

Madam hajamhakikishia usalama wake Binafsi kama mhanga!!

NADHANI katiba mpya itasimamia vyama vyote viwe salama kuepusha haya!!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA""!!
Kwa hiyo katiba mpya itakaa mlangoni kwa lissu kumlinda????
 
Hiyo namba 4 inaweza kuwa sawa...kuna watu sasa hivi ni maswahiba ndani ya chama tawala na upinzani
 
Nasema "alietaka kumuua" kwa sababu ukiangalia yale matundu ya risasi upande wake wa gari utajua kuwa hawa watu hawakutaka kumtishia tu. Walidhamiria kumuua.
Huu uzi na taarifa na muujiza wake utadumu kwa miaka 1000Mbele
 
Nasema "alietaka kumuua" kwa sababu ukiangalia yale matundu ya risasi upande wake wa gari utajua kuwa hawa watu hawakutaka kumtishia tu. Walidhamiria kumuua.

Niungane na Watanzania wenzangu kumuombea Tundu Lissu dua/sala ili apone kikamilifu, Amin.

Nimejiuliza maswali mengi kuhusu shambulio hili la kipekee kwa mbunge (sijui kama kulikwishatokea shambulio jingine kama hili), hapa Tanzania.

Yafuatayo ni malumbano ya kifikra ndani ya nafsi yangu kuwa ni nani hawa waliotaka Tundu Lissu afe. Maoni yako yanahusika, tafadhal.

Nimefikiria wahusika katika dhana 4. Nitazichambua hizi dhana moja moja.

Dhana zenyewe ni hizi. Washambuliaji ni:

1. Vichaa fulani tu. (Random act)

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.

3. Serikali yenyewe

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.


1. Vichaa fulani tu. (Random act)
Hii inawezekana lakini inakinzana na taarifa za kuwa Lissu alikuwa anafuatiliwa na magari kwa kipindi kirefu. Huu mpango ulisukwa na pia walijua wanaemtaka hadi kumfuata mpaka nyumbani kwake. Sidhani hii ilikuwa ni Random Act. Dhana hii ni potofu.

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.
Hii inawezekana kabisa. Wengi walimshutumu Lissu kwa kupinga sera zote za serikali (mimi nikiwa mmojawao). Kuna watu walikwenda mbali zaidi na kusema wanataka serikali iwaruhusu wamuue. Ndio maana kuna umuhimu wa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu hawa.

Katika demokrasia watu tunashambuliana vikali kwa hoja na sio kwa kuumizana au kuuana. Kama hii itathibitika, basi kuna umuhimu wa kuwapatia ulinzi wanasiasa machachari wanaoibua hisia kali.

Kuna uwezekano mkubwa dhana hii ni sahihi.

3. Serikali yenyewe
Kuna watu mitandaoni wanadhani ni serikali yenyewe ndio imeunda hii mbinu ya kumuua Lissu ili awaondolee kelele. Wengi wanasema Lissu amefichua siri nyingi za serikali kufikia kuwa tishio kwa hii serikali.

Kwa maoni yangu huu ni upuuzi. Serikali hii inakubaliwa na watanzania wengi. Hoja karibuni zote alizotoa Lissu dhidi ya serikali zinaweza kujibiwa kirahisi sana. In fact, baadhi ya shutuma za Lissu zinaipaisha serikali kwa Watanzania. Kelele za Lissu zinaweza kuwa baraka (blessing) kwa CCM ifikapo 2020. Kumuua Lissu kutajenga hisia za uonevu na kuwaonea huruma CDM ifikapo uchaguzi mkuu. Serikali haiwezi kufanya kosa hilo.

Kwa hiyo dhana hii ni potofu

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.
Hii dhana inahusisha watu wanaoichukia serikali (sio lazima wapinzani, inaweza kuwa watu wa nje) wanaotaka kumuondoa Rais Magufuli madarakani ifikapo 2020 kwa kuihusisha serikali yake na mauaji ya Lissu.

Serikali ya Magufuli imeathiri maslahi ya watu wengi sana wa ndani na wa nje. Akiendelea hivi hivi ana uhakika kabisa wa kupita ifikapo 2020. Sasa utaitoaje hii serikali madarakani ifikapo 2020. Jenga chuki kwayo.

Kama nilivyoeleza kwenye dhana namba 3, watu wakiamini kuwa serikali imemuua Lissu kinyama basi watawaonea huruma CDM na kuichukia CCM. CDM watachukua dola ifikapo 2020.

Je ni nani hawa wanaotaka kufanya unyama kama huu na kuisingizia serikali ya CCM (false-flag attack)?

Nina dhana nyingine 2 au 3 hivi (mfano, internal politics within CDM) lakini ni za pembeni sana na uwezekano wake ni karibu na sifuri. Kwa sasa hayo ndio malumbano yanayoendelea kichwani mwangu.

Please tell me I am not crazy.

==============================
Baada ya michango mingi iliyowekwa hapa kuna dhana niliyoigusia tu (Internal politics within CHADEMA) na wengi kuuliza kwa nini sikuifafanua. Hapa chini naiongeza ingawaje mwanzoni sikuipa kipaumbele.

Dhana ya 5.
Maadui wa ndani wa CHADEMA walitaka kumuua Lissu ili watimize malengo 3 yafuatayo.

1. Lissu aondoe ushindani katika uchaguzi ujao wa Uenyekiti.

2. Lissu aondoe ushindani katika uteuzi ujao wa mgombea urais ifikapo 2020.

3. Lissu atumiwe kama kafara ili kuipa CHADEMA mvuto na kuonewa huruma na kuichukia serikali katika uchaguzi wa 2020.
Suspect namba moja ni wewe mtoa mada maana uchambuzi wote unaonyesha unavyotaka kupoteza ushahidi wakati ushahidi haufutiki.
 
Kat
Kwa hiyo katiba mpya itakaa mlangoni kwa lissu kumlinda????
Katiba Mpya itasimamia haki zote za watu na wanasiasa watoapo maoni yao hata kama ni mwiba kwa serikali iliyoshika hatamu!!

Hoja za kisiasa zitajibiwa kisiasa na sio kwa Risasi!

Pia Rais aliepo madarakani atapunguziwa madaraka hataweza kumziba mdomo yeyote kwa njia yeyote ile kama ilivyo Sasa!!

Nachelea tena:-

"Rasimu ya Warioba irudi mezani Sasa iwe Katiba Mpya"!
 
Habari za ujenzi wa taifa wanajamvi.

Shambulizi la Tundu A. Lissu Lilitokea kipindi ambacho kulikuwa na mvutano baina ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Hayati John Joseph Pombe Magufuri na mwanasiasa huyo Nguli Tundu Lissu.

Shambulizi hili lilitugawa watanzania mara mbili kama si mara tatu, yaani wanaokubali madai ya Tundu Lissu ambae ndiye aliyeshambuliwa (wote tunatambua madai yake) na wale wanaopinga kuhusika kwa aliyekuwa Rais wa JMT John Magufuri.

Binafsi kinachonifanya nipingangane na madai ya mshambuliwa ambae ametuhakikishia Watanzania kuwa JP Magufuri ndiye mhusika namba moja wa shambulizi hilo.

Sababu kuu ya kupinga hilo ni kuwa, Selikali ya awamu ya sita(6) chini ya Rais shupavu Samia Suluhu Hassan ilianisha uovu wote ambao ulifanywa na Rais aliyepita sasa hili la kushambuliwa kwa Tundu lissu mbona liwe gumu kusemwa hadharani ili watanzania tuujue ukweli na wahusika wa shambulio.

Namaanisha waliobeba silaha hatari na kwenda kumshambulia Mbunge asiye armed wala asiye na hatia wanyooshwe na mkono wa sheria kama ilivyofanyika kwa wahusika wa uovu mwingine, mfano aliyekuwa Dc wa Hai.

Mheshimiwa Tundu Lissu amejenga chuki kubwa sana na Hayati JPM akimfananisha na Nduli Idd Amin huku akidai Taifa la Tanzania lilipata ahueni baada ya kufariki kwa aliyekuwa Rais huyo, hayo yote ni kuamini kuwa washambulizi walitumwa na JPM jambo ambalo ni wrong100%.

NB: Mimi si sukuma gang.


Nawasilisha



Sent from my STK-L21 using JamiiForums mobile app
 
Mmemuuliza Mbowe vizuri? Mana Dr Slaa alisema Mbowe ana tabia ya kuteka na kuua watu wake. Interview ipo mitandaoni, akitolea mfano wa mwenyekiti wa CHADEMA wa Temeke alivyonusurika kuuawa na gaidi mbowe
 
Habari za ujenzi wa taifa wanajamvi.
Shambulizi la Mheshimiwa Tundu A. Lissu Lilitokea kipindi ambacho kulikuwa na mvutano baina ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Hayati John Joseph Pombe Magufuri na mwanasiasa huyo Nguli Mh Tundu Lissu. Shambulizi hili lilitugawa watanzania mara mbili kama si mara tatu, yaani wanaokubali madai ya Mh Tundu Lissu ambae ndiye aliyeshambuliwa (wote tunatambua madai yake) na wale wanaopinga kuhusika kwa aliyekuwa Rais wa JMT John Magufuri.

Binafsi kinachonifanya nipingangane na madai ya mshambuliwa ambae ametuhakikishia Watanzania kuwa JP Magufuri ndiye mhusika namba moja wa shambulizi hilo. Sababu kuu ya kupinga hilo ni kuwa, Selikali ya awamu ya sita(6) chini ya Rais shupavu Dr Samia Suluhu Hassan ilianisha uovu wote ambao ulifanywa na Rais aliyepita sasa hili la kushambuliwa kwa Tundu lissu mbona liwe gumu kusemwa hadharani ili watanzania tuujue ukweli na wahusika wa shambulio, namaanisha waliobeba silaha hatari na kwenda kumshambulia Mbunge asiye armed wala asiye na hatia wanyooshwe na mkono wa sheria kama ilivyofanyika kwa wahusika wa uovu mwingine, mfano aliyekuwa Dc wa Hai.
Mheshimiwa Tundu Lissu amejenga chuki kubwa sana na hayati JPM akimfananisha na Nduli Idd Amin huku akidai Taifa la Tanzania lilipata ahueni baada ya kufariki kwa aliyekuwa Rais huyo, hayo yote ni kuamini kuwa washambulizi walitumwa na JPM jambo ambalo ni wrong100% .


Nb: mimi si sukuma gang


Nawasilisha



Sent from my STK-L21 using JamiiForums mobile app
Ungeweka na facts zinazofanya umkingie kifua dictator Jiwe ili zichambuliwe otherwise na wewe ni Sukuma gang mlinda 'legacy'.
Ushahidi wa mazingira unaonyesha ushiriki wa Jiwe kwenye mpango mzima wa jaribio lililofeli la kutaka kumuua nduli Jiwe, serikali(CCM) haina uhakika na reputations kama watalisanua hivyo wameamua bora waendeleze 'mute' iliyowekwa na utawala wa dictator Jiwe kuhusu hilo shambulio.
 
Ungeweka na 5. Inawezekana washambuliaji wakatoka cdm yenyewe katika mpambano wa kugombea mgombea urais wao 2020.
6. Washambuliaji kutoka huko huko cdm ili kuichonganisha serikali na wananchi?
Hili suala ni gumu sana linachohitaji ni kusubiri uchunguzi wa vyombo vya usalama tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Bashite na cyprian msiba le mutuzi na wenzao ndiyo wanajua shambulio lote nenda kawaulize usitumie nguvu kuwasingizia chochote chadema
 
Nasema "alitaka kumuua" kwa sababu ukiangalia yale matundu ya risasi upande wake wa gari utajua kuwa hawa watu hawakutaka kumtishia tu. Walidhamiria kumuua.

Niungane na Watanzania wenzangu kumuombea Tundu Lissu dua/sala ili apone kikamilifu, Amin.

Nimejiuliza maswali mengi kuhusu shambulio hili la kipekee kwa mbunge (sijui kama kulikwishatokea shambulio jingine kama hili), hapa Tanzania.

Yafuatayo ni malumbano ya kifikra ndani ya nafsi yangu kuwa ni nani hawa waliotaka Tundu Lissu afe. Maoni yako yanahusika, tafadhal.

Nimefikiria wahusika katika dhana 4, nitazichambua hizi dhana moja moja.

Dhana zenyewe ni hizi, washambuliaji ni:

1. Vichaa fulani tu. (Random act).

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali.

3. Serikali yenyewe.

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu.


1. Vichaa fulani tu. (Random act)
Hii inawezekana lakini inakinzana na taarifa za kuwa Lissu alikuwa anafuatiliwa na magari kwa kipindi kirefu. Huu mpango ulisukwa na pia walijua wanaemtaka hadi kumfuata mpaka nyumbani kwake. Sidhani hii ilikuwa ni Random Act. Dhana hii ni potofu.

2. Raia wenye chuki na Lissu kwa kuikalia kooni serikali
Hii inawezekana kabisa. Wengi walimshutumu Lissu kwa kupinga sera zote za serikali (mimi nikiwa mmojawao). Kuna watu walikwenda mbali zaidi na kusema wanataka serikali iwaruhusu wamuue. Ndio maana kuna umuhimu wa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu hawa.

Katika demokrasia watu tunashambuliana vikali kwa hoja na sio kwa kuumizana au kuuana. Kama hii itathibitika, basi kuna umuhimu wa kuwapatia ulinzi wanasiasa machachari wanaoibua hisia kali.

Kuna uwezekano mkubwa dhana hii ni sahihi.

3. Serikali yenyewe
Kuna watu mitandaoni wanadhani ni serikali yenyewe ndio imeunda hii mbinu ya kumuua Lissu ili awaondolee kelele. Wengi wanasema Lissu amefichua siri nyingi za serikali kufikia kuwa tishio kwa hii serikali.

Kwa maoni yangu huu ni upuuzi. Serikali hii inakubaliwa na watanzania wengi. Hoja karibuni zote alizotoa Lissu dhidi ya serikali zinaweza kujibiwa kirahisi sana. In fact, baadhi ya shutuma za Lissu zinaipaisha serikali kwa Watanzania. Kelele za Lissu zinaweza kuwa baraka (blessing) kwa CCM ifikapo 2020. Kumuua Lissu kutajenga hisia za uonevu na kuwaonea huruma CDM ifikapo uchaguzi mkuu. Serikali haiwezi kufanya kosa hilo.

Kwa hiyo dhana hii ni potofu.

4. Watu wenye chuki na serikali (false-flag attack) ili waisingizie serikali uovu huu
Hii dhana inahusisha watu wanaoichukia serikali (sio lazima wapinzani, inaweza kuwa watu wa nje) wanaotaka kumuondoa Rais Magufuli madarakani ifikapo 2020 kwa kuihusisha serikali yake na mauaji ya Lissu.

Serikali ya Magufuli imeathiri maslahi ya watu wengi sana wa ndani na wa nje. Akiendelea hivi hivi ana uhakika kabisa wa kupita ifikapo 2020. Sasa utaitoaje hii serikali madarakani ifikapo 2020. Jenga chuki kwayo.

Kama nilivyoeleza kwenye dhana namba 3, watu wakiamini kuwa serikali imemuua Lissu kinyama basi watawaonea huruma CDM na kuichukia CCM. CDM watachukua dola ifikapo 2020.

J,e ni nani hawa wanaotaka kufanya unyama kama huu na kuisingizia serikali ya CCM (false-flag attack)?

Nina dhana nyingine 2 au 3 hivi (mfano, internal politics within CDM) lakini ni za pembeni sana na uwezekano wake ni karibu na sifuri. Kwa sasa hayo ndio malumbano yanayoendelea kichwani mwangu.

Please tell me I am not crazy.

==============================

Baada ya michango mingi iliyowekwa hapa kuna dhana niliyoigusia tu (Internal politics within CHADEMA) na wengi kuuliza kwa nini sikuifafanua. Hapa chini naiongeza ingawaje mwanzoni sikuipa kipaumbele.

Dhana ya 5.
Maadui wa ndani wa CHADEMA walitaka kumuua Lissu ili watimize malengo 3 yafuatayo;

1. Lissu aondoe ushindani katika uchaguzi ujao wa Uenyekiti.

2. Lissu aondoe ushindani katika uteuzi ujao wa mgombea Urais ifikapo 2020.

3. Lissu atumiwe kama kafara ili kuipa CHADEMA mvuto na kuonewa huruma na kuichukia serikali katika uchaguzi wa 2020.
Hivi unahangaika nini wakati mwenyewe yupo?

Nenda kamuulize. Mnapenda kupoteza muda na nguvu kwa mambo ya kipuuzi.

Kwahiyo ukijua alietaka kumuua unapata nini?

Tafuta kujua namna ya kupiga pesa.
 
Hii issue haita kaa iishe....

Ila kuna siku wahisani wa kimataifa ambao wanatupa misaada wakisema jamani Serikali chukueni hatua za mwanzo.....

Basi itakuwa siku mbaya sana kwa Bashite... Ndiye atakuwa wakwanza kuhojiwa...
 
Kwakatibayetu mkuu wa kaya akiamua kukumaliza huchomoki.
Ukichomoka ujue hausiki kwa namna yoyote kwasababu anakila kitu kinacho hutajika.
 
Back
Top Bottom